other blog

Ijumaa, 16 Desemba 2016

Serekali inajua alipo ben saanane.. Lisu aomba watumie vyombo vyao vya ulinzi kumsaka.. CCM ni lini mtatupa uhuru.. We want lema alive.. And max wa jf akiwa huru....tumechoka

Mwanasheria Mkuu wa Chadema,
Tundu Lissu, akizungumza na
waandishi wa habari, Dar es Salaam
jana kuhusu kupotea kwa msaidizi
wa mwenyekiti wa chama hicho, Ben
Saanane. Kulia ni Ofi sa Habari,
Tumaini Makene na Katibu Mkuu
wa Baraza la Vijana (Bavicha), Julius
Mwita.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka Serikali kutumia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kumtafuta msaidizi wa mwenyekiti wa chama hicho, Bernard Saanane , ambaye ametoweka katika mazingira ya kutatanisha zaidi ya mwezi mmoja sasa. Chadema imesema Serikali ndiyo yenye uwezo pekee wa kiufundi kujua na kuamuru mashirika ya simu kueleza mawasiliano yake ya mwisho yalivyokuwa. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema katika siku za karibuni, Saanane amekuwa akiongoza kampeni kwenye mitandao ya kijamii, kuhusu kuhakikiwa kwa shahada za uzamivu (PhD) kwa baadhi ya viongozi. Mwanasheria huyo wa Chadema, alisema wakati fulani Saanane alitumiwa ujumbe wa maneno kupitia simu yake ya kiganjani akitishiwa kuacha kuikosoa Serikali. “Nanukuu maneno aliyotumiwa: “Ben Saanane unachokitafuta ndani ya Serikali hii utakipata, kwa elimu na uwezo wako hatukutarajia ungefikia hatua ya ajabu kwa namna ulivyofikia, hujiulizi kwanini upo huru hadi muda huu. “You are too young to die. Tunajua utaandika na hili, andika lakini the next post hutaandika ukiwa na uhuru wa kutosha, andika but your days are numbered. “Unajua kuna rafiki yako alipuuza na hutaki kuandika kuhusu yeye, labda kwa kuwa alitangulia, andika Ben, andika sana, ongea, sema lakini utajikuta mwenyewe na chatu,” alinukuu Lissu. Alisema: “Katika miezi ya hivi karibuni watu ambao wamekuwa wakiikosoa Serikali kupitia mitandao ya kijamii wamekuwa wakikamatwa na watwambie kama wanamshikilia Ben Saanane ili tujue. “Serikali ndiyo yenye udhibiti wa mipaka yetu kuanzia baharini, nchi kavu, mipaka yetu ya anga na hata katika bandari, hivyo ituambie,” alisema Lissu. Aidha mbunge huyo wa Singida Mashariki alisema yeyote anayefahamu taarifa za Saanane azitoe hadharani katika vyombo vya habari, polisi na hata katika vyombo vingine vya Serikali. Aidha Lissu alisema taarifa za kupotea kwa Saanane wamezifikisha ngazi za kimataifa na wataendelea kuzisambaza ili dunia nzima ijue. Akizungumzia kuhusu taarifa ambayo imesambaa katika mitandao ya kijamii kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe anajua aliko Saanane, alisema: “Mara ya mwisho Ben amewasiliana na mwenyekiti Novemba 14 mwaka huu akiwa Dodoma na huwa hawaongozani, bali Ben anafanyia kazi zake makao makuu ya chama.”

Jumatatu, 12 Desemba 2016

Nafazi za kazi serikalin wizara ya afya. Jinsia wazee walemavu na watoto.. Omba mapema...

NAFASI YA KAZI WIZARA YA
AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA , WAZEE NA WATOTO
Wizara YA Afya , Maendeleo
ya Jamii, JiNSIA , Wazee , na
Watoto imepeta kibali cha
mpango wa ajira ya dharula
kwa wataalamu wa fani za
tabibu na wauguzi mpango
huu utaendeshwa chini ya
mradi kwa ufadhili wa fedha
mfuko wa cdc, award no.
5U2GGHOO1062-03
kwa muda wa miaka miwili
mradi utaajiri watumishi
m192 ambao watafanya kazi
katika wilaya mbalimbali
zenye uhaba wa watumishi
wa kutoa huduma za afya
hasa kwa waathirika wa
wenye virus ivy UKIMWI .
watumishi hawa watalipwa
mshahara na stahiki nyingine
kwa kufuata tarabitu na
kanuni za serikali. Watumishi
wanao takiwa ni
- TABIBU
WASAIDIZI
(NAFASI 95)
wenye ngazi ya
astashahada
(CERTIFICATE IN
CLINICAL
MEDICAL)
- WAUGUZI
(nafasi 97 )
wenye ngazi ya
astashahada
(CERTIFICATE IN
NURSING AND
MIDIWIFERY)
Wizara inakaribisha maombi
ya kazi kutoka kwa
watanzania wenye sifa
zilizotajwa hapo juu , wawe n
vitu vifuatavyo
- Cheti cha
kumaliza  kidato
cha nne
- Cheti cha
taaluma
aliyosomea
kutoka kwenye
chuo
kinachotambulika
na serikali
barua ya
maombi
ionyeshe wilaya
unayotaka
kupangiwa
- Maombi
yatumwe kwa
KATIBU MKUU,
WIZARA YA AFYA,
MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, NA WATOTO,
6 SAMORAL MACHEL
AVENUE,
S.L.P 9083
11478, DAR ES SALAAM,
TANZANIA.
ORODHA YA HALMASHAURI
ZA WILAYA NA IDADI YA
WATUMISHI
WALIOPENDEKEZWA
ARUSHA
NA MKOA HALMASHAURI TABIBU WAUGUZI JUMLA
1 arusha Arusha CC 3 3 6
2 dar es salaam Ilala MC 3 3 6
Temeke MC 3 3 6
Kinondoni MC 3 3 6
3 dodoma dodoma MC 2 3 5
4 geita Geita DC 2 2 4
5 iringa mufindi DC 3 3 6
Iringa MC 2 2 4
6 kagera bukoba DC 3 3 6
Muleba DC 2 2 4
7 kigoma Kigma Ujiji MC 2 3 5
8. Kilimanjaro Moshi Dc 3 3 6
9i Lindi Lindi DC 2 2 4
10 Mara Musoms DC 2 2 4
Rorya DC 2 2 4
11 Mbeya Chunya DC 2 2 4
Kyela Dc 3 3 6
Mbarali DC 2 2 4
Mbeya DC 3 3 6
Mbozi DC 2 2 4
Rungwe DC 2 2 4
12 Morogoro Morogoro DC 3 3 6
13 Mwanza Nyamagana DC 3 3 6
Sengerema DC 2 2 4
14 Njombe Njombe DC 2 2 4
Wang’ing’ombe DC 2 2 4
15 Rukwa Sumbawanga DC 2 2 4
Sumbawanga MC 2 2 4
16 Ruvuma Mbinga DC 2 2 4
Songea MC 2 2 4
17 Shinyanga Kahama DC 3 3 6
Shinyanga MC 2 2 4
18 Tabora Igunga DC 2 2 4
Ndega DC 2 2 4
Tabora MC 3 3 6
19 Tanga

Jumamosi, 5 Novemba 2016

Joyce ndelchako afumuka makubwa kuhusu bodi ya mkopo na aamuru kuwa wote walioomba mkopo wapatiwe. shuka nayo hii..

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya
Juu (HELSB), imeagizwa
kuhakikisha kuwa fedha zote
zilizotengwa kwa ajili ya
mikopo ya wanafunzi
wanaoendelea na masomo
zinapelekwa vyuoni ifikapo
leo.
Agizo hilo lilitolewa bungeni
jana na Waziri wa Elimu,
Sayansi, Teknolojia na Ufundi,
Profesa Joyce Ndalichako
baada ya wabunge mbalimbali
kuomba miongozo kwa Spika
kuhusu kuwapo kwa wanafunzi
wengi waliokosa mikopo kwa
mwaka wa fedha 2016/17.
Mwongozo kwa Spika ulitiliwa
mkazo na Mbunge wa Chalinze
(CCM), Ridhiwan Kikwete
aliyeeleza kuwapo taarifa
kutoka Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM) kuwa
wanafunzi wanataka kugoma
kwa kukosa fedha za mikopo.
Kutokana na miongozo hiyo,
Mwenyekiti wa Bunge, Najma
Giga aliitaka Serikali kutoa
maelezo.
Akitoa kauli ya Serikali, Profesa
Ndalichako alisema fedha za
mikopo kwa ajili ya wanafunzi
zilikwenda vyuoni wiki moja
iliyopita.
“Tatizo lililotokea kwa UDSM
sijui kama walidanganyana au
la lakini hawakujaza fomu.
Serikali haitatoa mkopo kwa
mwanafunzi ambaye hajajaza
fomu. Na waliosaini leo
wataingiziwa fedha zao kwenye
akaunti na vyuo,” alisema.
Kuhusu wanaoendelea na
masomo, Profesa Ndalichako
alisema wanafunzi wote
wanufaika na wanaoendelea na
masomo wataendelea kupatiwa
mikopo kama ilivyokuwa
mwaka uliopita.
Alisema wanafunzi ambao
vyuo vyao vimewasilisha HELSB
taarifa za matokeo, Bodi
imekwishawatumia fedha
vyuoni kwa ajili ya kuwapa
mikopo wanafunzi hao.
Hata hivyo, alisema taratibu za
kuwabaini wanafunzi wenye
sifa zinaendelea na wasio na
sifa wataendelea kuondolewa
kupata mikopo.
Pia, alikiri kuwa ucheleweshaji
wa matokeo ya wanafunzi
wanaoendelea na masomo
umeathiri kasi ya kutuma fedha
vyuoni.
“Wizara yangu imekwishaagiza
vyuo vyote ambavyo
havijawasilisha matokeo ya
mitihani ya wanafunzi wao kwa
mwaka wa masomo uliopita,
kufanya hivyo mara
moja,” alisema.
Ndalichako alisema hadi
kufikia Novemba 3 mwaka huu,
Sh71.042 bilioni
zilikwishatumwa vyuoni kwa
ajili ya wanafunzi wa mwaka
wa kwanza na wanaoendelea
na masomo.
Akizungumzia utoaji wa
mikopo kwa mwaka wa fedha
2016/17, Ndalichako alisema
katika mwaka huo, Sh483
bilioni zimetengwa na
zimelenga kutoa mikopo kwa
wanafunzi 119,012, wanafunzi
93,295 wanaoendelea na
masomo na wa mwaka wa
kwanza 25,717.
Ndalichako alisema katika
mwaka wa fedha 2016/17
wanafunzi 58,010 walidahiliwa
na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU)
na orodha yao iliwasilishwa
HELSB na hadi Novemba 2,
mwaka huu, wanafunzi 21,190
wa mwaka wa kwanza
wamepewa fedha. Kati yao
4,321 ni yatima, 118 wenye
ulemavu na 87 ni waliosoma
sekondari kwa ufadhili wa
taasisi mbalimbali.

Jumapili, 4 Septemba 2016

mh.... hi ni hatari. CCM watashia kuanzisha ukuta .. Nimeamin kwamba wapinzani ndo mafisadi wakubwa... Hongera magufuli.

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameingia katika mzozo mkubwa na Rais John Magufuli, na sasa wameanza Job Ndugai, kumlazimisha Spika wa Bunge, awanusuru, MwanaHALISI linaweza kueleza.
Habari kutoka Ikulu, Ofisi ya Spika na Kamati ya Wabunge wa CCM, zinasema wabunge hao wamejiapiza kuwa Ndugai na Rais Magufuli wamekalia moto.
Sababu kuu inayotajwa ni hatua ya serikali, kwa amri ya Rais Magufuli, kuhoji na kufikisha mahakamani baadhi ya wabunge wa CCM wanaotuhumiwa kuomba rushwa kutoka kwa taasisi wanazosimamia.
Wabunge wa CCM waliofikishwa mahakamani ni Kangi Lugola (Mwibara), Victor Mwambalaswa (Lupa), na Suleiman Sadiq (Mvomero). Wanatuhumiwa kwa kwa kosa la kuomba rushwa ya milioni 30 kutoka kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Gairo ili wampendele katika kukagua hesabu za halmashauri yake mwaka 2015/16.
Mwingine ni Richard Ndassa (Sumve), ambaye anatuhumiwa kwa  kushawishi na kuomba rushwa ya Tsh 30 milioni kutoka kwa Felchesmi Mramba, Mtendaji Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  ili amsaidie kuwashawishi wajumbe wengine wa Kamati ya Mtaji na Uwekezaji kupitisha bila kipingamizi taarifa ya TANESCO kwa mwaka 2015/2016.
Taarifa zinasema kuwa hadi Ijumaa iliyopita, Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) ilikuwa imehoji wabunge wengine 18 wa CCM, na ilikuwa imeshakamilisha taratibu zote za kuwafikisha mahakamani.
Miongoni mwa wabunge hao ni Martha Mlata (Viti Maalumu), Raphael Chegeni (Busega), Margareth Sitta (Urambo Mashariki), Mary Mwanjelwa (Viti Maalumu), Edwin Sanga (Kondoa Mjini). Majina mengine hayakupatikana hadi tunakwenda mitamboni.
Baada ya taarifa za kufikishwa mahakamani wabunge hao kuanza kuenea, kundi la wabunge wa CCM linadaiwa kumzonga Ndugai, wakimtaka awasimamie wabunge wa chama chake, asiruhusu wadhalilishwe.
Watoa habari wetu wanasema wabunge walimweleza Ndugai kuwa kitendo cha serikali kudhalilisha wabunge wa CCM kitaondoa umoja wao wa kutetea serikali, na kitaathiri msimamo wao katika umoja wa wabunge wa chama chao.
“Mweleze rais asitudhalilishe, sisi ni wabunge wa chama chake; asitafute sifa zake peke yake,” mbunge mmoja kijana alinukuliwa akimweleza Ndugai.
Kabla hata Ndugai hajawasiliana na rais kuhusu hoja za wabunge, taarifa zinasema rais mwenyewe alipata taarifa hizo kutoka kwa “vijana wake” ndani ya wabunge hao.
Mtoa habari kutoka Ikulu ameeleza gazeti hili kuwa Rais alipompigia simu Ndugai alizungumza kwa ukali, “hiyo ni mijizi, acha ifungwe tu.”
Gazeti hili lilipohitaji ufafanuzi wa Ndugai kuhusu masuala haya alithibitisha kuwa wabunge wake  wameshahojiwa na TAKUKURU, lakini akagoma kusema alichoambiwa na rais.
“Ni kweli kuna wabunge 18 wameshahojiwa na Takukuru. Hata hivyo, tumeshindwa kuwa na maelezo ya pamoja kwa kuwa kuna wengine wameitwa kama mashahidi, na wengine wamehojiwa kama watuhumiwa,” Alisema.
Alisema kilichotokea ni kwamba wabunge hao wamekuwa wanaitwa kwa nyakati tofauti, kwa sababu tofauti. “Mwingine anaitwa leo anahojiwa kwa tuhuma, mwingine anaitwa kesho kwa ushahidi pengine baada ya kutajwa na mwenzake,” alidokeza.
Baadhi ya wabunge wa CCM wameliambia gazeti hili kuwa kuna kesi zinatengenezwa kisiasa, hivyo wanajipa muda kuliweka sawa suala la tuhuma zinazowakabili.
Hata hivyo, taarifa zinasema wabunge wameikamia serikali, na wengi wao wanajiapiza kuunga mkono hoja za wapinzani kama namna ya kumkomoa Rais Magufuli.
Taarifa hizo hizo zinasema rais mwenyewe baada ya kusikia vitisho vya wabunge wa CCM, amemwambia Ndugai, “kama watatunisha misuli nitavunja bunge, turudi kwenye uchaguzi, tuone watarudi wangapi miongoni mwao.”
Taarifa hizi zinakuja ikiwa ni wiki moja tangu Spika kuahidi kuwa suala hilo litazungumzwa vizuri ndani ya Bunge kwa kuzingatia kanuni wala si mtaani. Source ni mwanahalisi..

Jumatano, 3 Agosti 2016

Mashirika ya kitawa kwa wote mnaotaka kuwa watawa

karibuni wote mjiunge na utawa maisha matakatifu ni maisha ya kazi na sala wanaotaka kuwa mabruda ... waandike barua kwa anuani ifuatayo mkurugenzi , scim brothers, s.l.p 29 Tosamaganga, Iringa. kumbuka kigezo uwe tu hujaoa na pia uwe umehitimu kidato cha nne. pia lipo shirika la mtakatifu carmel lilopo bunju kwa  malezi ya kipadre wote wenye nia mnaombwa kutuma maombi yenu kwa mkurugenzi tz kwa mawasiliano zaidi watumie email carmelitestz@gmail.com na Kwa upande wa masisita soma kibandiko cha mtakatifu consolata missionery kwa malezi ya kisista yaani utawa wa kwanza na pia shirika la mtakatifu charles borromeo

kumbuka mabruda na masista lazima uwe mhitimu wa kidato cha nne. pia uwe hujaoa wala hujazaaa  na kwa upande wa upadre lazima uwe mhitimu wa kidato cha sita na kufaulu uwezo wa kwenda chuo kikuuu ... karibuni utawani tujifunze maisha halisi ya bwana wetu yesu kristo.. Tumsifu yesu kristo .... kwa maelezo zaidi usisite kunipigia simu 0743719830

Alhamisi, 9 Juni 2016

UMMA KUHUSU KUFUNGWA KWA MUDA WA KUPOKEA MAOMBI YA UDAHILI WA KOZI ZA CHETI, DIPLOMA, DIPLOMA YA JUU NA SHAHADA YA KWANZA KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) UNAORATIBIWA NA BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)

 
Tarehe 3 Juni 2016 ilikuwa siku ya mwisho ya kuwasilisha maombi ya udahili wa kozi za Cheti, Diploma, Diploma ya Juu na Shahada ya Kwanza kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) unaoratibiwa na NACTE.
Baraza linapenda kuwaarifu waombaji udahili wa kozi tajwa hapo juu na umma kwa ujumla kuwa, kwa sasa maombi yote yaliyowasilishwa mpaka tarehe 3 Juni 2016 saa sita usiku yameanza kuchambuliwa kwa ajili ya kuchagua waombaji wenye sifa stahiki. Zoezi la kuchambua waombaji udahili na hatimaye kuchagua waombaji wenye sifa stahiki na waombaji hao kuidhinishwa na mamlaka husika na kutangazwa litachukua muda wa wiki nne (4) kuanzia tarehe 3 Juni, 2016.
Baraza linatambua uwepo wa waombaji wapya na baadhi ya waombaji walioshindwa kuwasilisha maombi yao kupitia mtandao ilipofika tarehe 3 Juni 2016. Waombaji wa namna hii na wengine wanaopanga kuwasilisha maombi yao kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) wanaombwa kuwa na subira mpaka hapo majina ya waombaji waliowasilisha maombi yao kabla ya kufungwa kwa mfumo watakapotangazwa.
Baada ya kutangazwa majina ya waombaji waliochaguliwa, Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) utafunguliwa tena kwa ajili ya kujaza nafasi za udahili ambazo zitakuwa hazijajazwa na waombaji waliowasilisha maombi yao kuanzia tarehe 4 Machi, 2016 hadi tarehe 3 Juni 2016.
Baraza linatarajia kufungua tena Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) kwa ajili ya kozi za Cheti, Diploma, Diploma ya Juu na Shahada ya Kwanza wiki ya mwishoni mwa mwezi wa Sita, 2016.
Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
NACTE
Tarehe: 9 Juni, 2016