other blog

Jumanne, 1 Septemba 2015

Watanzania .. tuamini tunachokiamini .. maneno ya mtu mmoja yasitupotoshe lowasa anatosha .. na inaonekana dhana ya kufeli alikuwa nayo slaa wakati akiwa mlezi wa ccm B na sasa tumepata kiboko atakayetengeneza chadema ya kweli yeye inamuuma padre na siasa wap na wap ..........


Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA,
Dr. Slaa akiwa kwenye mkutano na
waandishi wa Habari katika ukumbi wa
Hoteli ya Serena.
Slaa: Watanzania wana kiu ya
kujua kwanini amekuwa kimya
kwa muda mrefu sasa licha ya
harakati za kisiasa kuendelea.
Muda utakaotumika ni saa moja,
hakuna muda mrefu sana.
Ameamua kufanya hayo kwa kuwa
imefika mahali ukweli lazima
usemwe na upotoshwaji
ukomeshwa. Namna pekee ya
kufanya hivyo ni kutoka
hadharani na kuusema ukweli.
Sote tunafahamu kuwa hana tabia
ya kuchenga mambo, mengi
yamesemwa na watu tofauti,
kwenye mitandao, magazeti na
viongozi wake!
Hana ugomvi na kiongozi yoyote,
kwa kuwa siasa sio ugomvi. Kama
binadamu wa kawaida hana chuki
wala hasira na binadamu
mwingine yoyote!
Iwe wazi kuwa katika Taifa kuna
misingi ambayo inaongoza taifa.
Inapofika mahali taifa
linaongozwa kwa msingi ya
propaganda na upotoshwaji
matokeo yake ni vurugu kubwa
katika taifa. Yeye amekataa hayo
yote!
Anasema kuwa YEYE hakuwa
likizo kama inavyosemwa na
viongozi wake! Atafafanua kwa
kifupi!
Kilichotokea ni kuwa aliamua
kuachana na siasa, tarehe 28 Julai
2015, majira ya saa tatu usiku,
baada ya kuona yanayofanyika
ndani ya chama chake
hayamridhishi.
Mtangulizi wa shuguli ambaye
anatoka kwenye kampuni ya
mahusiano ya umma
anamtambulisha Dr. Willibrod
Slaa.
Anasema kuwa kwa muda mrefu
Slaa amekuwa alama ya harakati
za ukombozi dhidi ya makucha ya
mkoloni mweusi.
anaongeza kuwa Dr. ataongea kwa
muda kisha kuruhusu maswali
kutoka kwa waandishi,
anamkaribisha!
Kinachosemwa ni kuwa Dr. Slaa
alishiriki tangu mwanzo kwenye
mchakato. Anasema ni kweli
alishirii kwenye majadiliano,
akaweka msingi na msimamo
wako. Kuna wakati wengi
wanashinda kutokana na wingi
wao, wewe unayeamini katika
misingi inabidi uachie ngazi.
Azam TV wameanza matangazo
kupitia kipindi chao cha KITUO
CHAKO CHA UCHAGUZI, wako LIVE
sasa... Bado uchambuzi wa safari
ya Kisiasa ya Dr. Willibrod Slaa
unaendelea.
Tumepelekwa moja kwa moja
kutoka Hoteli ya Serena
Mtangulizi wa shuguli ambaye
anatoka kwenye kampuni ya
mahusiano ya umma
anamtambulisha Dr. Willibrod
Slaa.
Anasema kuwa kwa muda mrefu
Slaa amekuwa alama ya harakati
za ukombozi dhidi ya makucha ya
mkoloni mweusi.
anaongeza kuwa Dr. ataongea kwa
muda kisha kuruhusu maswali
kutoka kwa waandishi,
anamkaribisha!
==========================
Slaa: Watanzania wana kiu ya
kujua kwanini amekuwa kimya
kwa muda mrefu sasa licha ya
harakati za kisiasa kuendelea.
Muda utakaotumika ni saa moja,
hakuna muda mrefu sana.
Ameamua kufanya hayo kwa kuwa
imefika mahali ukweli lazima
usemwe na upotoshwaji
ukomeshwa. Namna pekee ya
kufanya hivyo ni kutoka
hadharani na kuusema ukweli.
Sote tunafahamu kuwa hana tabia
ya kuchenga mambo, mengi
yamesemwa na watu tofauti,
kwenye mitandao, magazeti na
viongozi wake!
Hana ugomvi na kiongozi yoyote,
kwa kuwa siasa sio ugomvi. Kama
binadamu wa kawaida hana chuki
wala hasira na binadamu
mwingine yoyote!
Iwe wazi kuwa katika Taifa kuna
misingi ambayo inaongoza taifa.
Inapofika mahali taifa
linaongozwa kwa msingi ya
propaganda na upotoshwaji
matokeo yake ni vurugu kubwa
katika taifa. Yeye amekataa hayo
yote!
Anasema kuwa YEYE hakuwa
likizo kama inavyosemwa na
viongozi wake! Atafafanua kwa
kifupi!
Kilichotokea ni kuwa aliamua
kuachana na siasa, tarehe 28 Julai
2015, majira ya saa tatu usiku,
baada ya kuona yanayofanyika
ndani ya chama chake
hayamridhishi.
Kinachosemwa ni kuwa Dr. Slaa
alishiriki tangu mwanzo kwenye
mchakato. Anasema ni kweli
alishirii kwenye majadiliano,
akaweka msingi na msimamo
wako. Kuna wakati wengi
wanashinda kutokana na wingi
wao, wewe unayeamini katika
misingi inabidi uachie ngazi.
Baada ya Edward Lowassa
kukatwa na CCM Dodoma,
Mshenga wake alimpigia simu na
kuuliza nini kifuate baada ya
tukio la dodoma. Akamuambia
wawasiliane na mwenyekiti
Freeman Mbowe, Gwajima nae
akafika kwenye kikao hicho.
Msimamo wa Slaa ni kuwa ni
lazima kumsikiliza mtu kabla ya
kuamua nini cha kufanya.
chadema ni cham cha siasa na
hakiwezi kumkataa mtu yeyote
kujiunga na chama.
Wakaweka vijana kuchunguza nini
wanataka hao wanaotaka
kujiunga na chama!
Slaa akataka kwanza Lowassa
atangaze kutoka kwenye chama
chake alichopo, kisha atangaze
anakwenda kwenye chama gani.
Atumie nafasi hiyo ya mkutano
huo ajisafishe na tuhuma zote
ambazo amekuwa akituhumiwa
na watu.
Chadema ni cham ambacho kwa
muda mrefu kimejijenga kwa
msingi, na ni lazima wapokee mtu
ambaye hawezi kukichafua chama
chao.
Lowassa hakutangaza kujitoa,
wala kujisafisha hadi kwenye
mkutano ambao uliandaliwa na
chadema. Slaa hakuhudhuria ule
mkutano.
Kwenye kila jambo kuna jambo la
kuzingatia. Mtu anayejiunga
popote anakuja kama mtaji au
kama mzigo? Lowassa anakuja
chadema kama asset au liability?
Ijulikane, suala sio urais! Mpaka
siku hiyo Slaa hakuwa amechukua
fomu ya Urais kwenye chama
chake. Slaa hakuwa anamzuia
Lowassa kugombea urais
chadema. Alitaka mgombea
mwenye sifa na uwezo wa kukitoa
Chama cha Mapinduzi.
Hakutamka popote kuwa anataka
kugombea, hata 2010
hakugombea, aliombwa
kugombea! Urais wake binafsi
hauwezi kuikomboa nchi bila
mchango wa jamii nzima.
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Suala la adha Lowaasa ni msizo au
mtaji halikujibiwa hadi siku ya
mkutano tajwa. Wakataka kujua
anapokuja anakuja na akina nani,
ni wafuasi wa aina gani; vijana wa
bodaboda, vijana wasio na ajira
au watu waliosombwa tu, au
wanakuja kwenye mapambano?
Jibu lilikuwa ni kuwa tungepata
wabunge 50 na wenyeviti wa CCM
mkoa wasiopungua 22, wenyeviti
wa CCM wilaya 88. Slaa akakiri
kuwa kama ni hivyo kutakuwa na
tetemeko (la kisiasa).
Wakahitaji majina ya hao
waliotajwa kwa kuwa walikuwa
kwenye mchakato wa kupitisha
majina kwenye chama. KAtibu
mkuu makini huwezi kuchukuwa
watu usiowajua. Hakuna jina
nililopewa mpaka tarehe 25.
Tarehe 25 wakamfata na
kumuambia aitishe Kamati Kuu
ya chama. Akakubali lakini
akatahadjharisha kuwa hajapata
majina na hajapata jibu kuwa
Lowassa ni asset au liability.
Lakini akaitisha kikao kwa kuwa
ni jukumu la kikatiba la katiba.
Mwenyekiti akapiga simu,
anasikia kuwa hajaridhika. Tangu
2004 Slaa hajawahi kugombana na
mwenyekiti wake, isingekuwa
sawa kama wangetofautiana
kwenye kikao rasmi.
Wakakutana na Mwenyekiti,
Gwajima, Lissu na wakajadiliana
mpaka saa 9 mchana. Maneno
kuwa alikuwa anakubaliana na
mpango huo tangu mwanzo SI
KWELI!
Mkutano ukashindikana. Wdau
wakasema waende nyumbani kwa
Lowassa, Slaa akakataa wakaenda
Kamati kuu.
Kikao kikafanyika hadi saa 12
jioni. Ikaundwa kamati ndogo ya
kumshawishi Slaa. Akakataa!
Akaandika barua ya kujiuzulu kwa
kamati, Prof. Safari akaichana
barua yake. Akaandika barua
nyingine kwa Makamu-Zanzibar,
makamu akamuambia kuwa haya
mambo yamepangwa,
asijisumbue!
Wanasema siasa ni mchezo
mchafu, yeye anaaamini kuwa
siasa ni sayansi! Asubuhi ya
kesho akaandika barua,
wasichojua ni kuwa kujiuzulu
hakuhitaji barua. Maneno
yakazuka kuwa Slaa hajaandika
barua!
Upotoshwaji ukaendelea kuwa
Slaa atazungumza na waandishi
wa habari, wengine wakasema
amefungiwa, amefungiwa na
mkewe na kadhalika! Ukweli ni
kuwa alikuwa na Lissu, Gwajima
na Mbowe tangu asubuhi.
Maamuzi aliyoyafanya yanatokana
nadhamiri yake!
Josephine nae ni mwanaharakati,
ana sababu ya kuwa na uchungu.
Alipigwa mwaka 2011 wakati
wengine walijificha! Propaganda
hizo tumeshazisoea!
Kama kuna mwenye ushahidi wa
propaganda hizi aje, audited
report zipo! Josephine halipwi na
chama! Watu wanasema kuwa Slaa
analipwa mil. 7, yeye ameendelea
kula mihogo na maharage kama
walivyoahidi mwaka 2010.
Wana uchungu na harakati!
Kikubwa katika harakati ni
credibilty, jina la chama
kilichojengwa kwa muda mrefu
kisichafuliwe kwa namna yoyote!
Mwanasiasa yoyote hataki
kuchaguliwa, na Slaa nae hataki
kuchaguliwa!
Wanasema kuna maslahi mapana
ya taifa, ni nani anayapima?
Lazima kuwe na kipimo cha
kuapima hayo maslahi badala ya
kutegemea mtazamo wa mtu!
Anafafanua suala la liability sasa!
Wamekuwa waongo kwa kuwa
hakuna kipengele hata kimoja cha
madai ya Slaa kimetekelezwa.
Alisema wabunge waje kabla ya
kura ya maoni ya CCM, kuja
baada ya hapo ni kutafuta
kichaka cha kujificha!
Watanzania wameijenga Chadema
kwa damu yao, rasilimali zao!
Watu hawawezi kukimbilia
kirahisi wakati sio wasafi,
akiwemo Sumaye na wengine.
Nani hajua kama Sumaye ni
fisadi? Kwa muda mrefu Slaa
haongei na Sumaye kwa kuwa
alimtuhumu kwa ufisaidi.
Sumaye ni mtu ambaye
wanahabari walidai kuwa Sumaye
alisema kuwa atahama chama
endapo Lowassa atateuliwa, leo
akageuka!
Leo anamsafisha Lowaasa,
dhambi haisafishwa kwa dhambi.
Anakumbusha jina la Mr. Zero
(jina la utani la Sumaye).
Chama kimepokea makapi, na
katibu alitahadharisha kuwa
chama hakipokei makapi! Hakuna
ambaye alijitoa kwa hiari, wengi
walikuja baada ya kukatwa.
Wenyeviti wengi ni mzigo,
akiwemo Msindai.
Anangoja ajibu amlipue hadharani
kwa kuwa alikuwa mwenyekiti wa
kamati ya bunge hesabu za
serikali z mitaa.
Siku aliyoambiwa aitishe kamati
kuu aliuliza majina, akaambiwa
anakuja chizi! Chizi ni nani, hata
nyie hamumjui! Anaitwa chizi kwa
kuwa ni mwizi wa kura ndani ya
CCM.
Kuna haja gani ya kushindana
kama tunampango wa kuiba kura
pia. Wakamtaja Guninita, nani
asiyemjua udhaifu wake? Hawezi
kuandika hata ukurasa mmoja wa
ripoti, amehama vyama mara
kadhaa!
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Viongozi wa Chadema wamepata
kigugumizi, waseme nani
ameongeza thamani kwenye
chama?
Najua maneno ya kuwa ni lazima
kuiondoa CCM kwanza hata
ikibidi tuweke mkataba na
shetani, mimi ni padre wa Kanisa
Katoliki! Kuwaondoa CCM kwa
namna yoyote hakuleti
maendeleo. CCM itaondolewa kwa
program siriaz, sio kutumia watu
wale wale!
Lazima tujue nini kilifanya
Watanzania waamini chadema,
kwa kuwa waliamini wana misingi
isiyoyumba na uadilifu. Leo
tunasimamia uadilifu?
Wanasema mwenye ushahidi
aende mahakamani. Kama
tusingewatuhumu Mramba na
Yona wasingefikishwa kizimbani.
Chadema imefungwa mdomo kwa
kisingizio cha ushahidi!
Ni bora kukaa kimya kuliko
kupotosha. Anasema nukuu ya
biblia kuhusu wapotoshaji!
Inapofika mahali unapoambiwa
hakuna mwenye dhambi ni
makosa, dhambi haisahihishwi
kwa dhambi nyingine! CCM
wamekuwa waoga, wamewalea
watu hawa kwa muda mrefu!
Kwa Wafrika choo ni neno baya,
kwa wazungu choo ni rest room!
Choo cha Kitanzania huwezi
kukihamisha ndani ya chumba
cha kulala na ukakiita choo,
huwezi kulala kwa kuwa kitanuka,
tena zaidi!
Ufisadi ilikuwa ajenda iliyowapa
umaarufu CHADEMA, leo
wamewachukua. Waanweza kuwa
na ujasiri wa kukemea ufisadi?
Mwaka 2008 Slaa alikuwa bungeni
wakati wa sakata la Richmond,
anafahamu kwa uzuri
anachokimaanisha. Bahati mbaya
waandishi hawasomi makaratasi,
na wabunge wa CCM pia.
Lowassa hatuhumiwi kwa habari
ya Richmond pekee!
Lowassa aliambiwa na Slaa aache
kulalamika, atangaze uhalali au
uharamu wa Richmond, anamtaka
aseme hao 'wakubwa' ni akina
nani? Ni afadhali sifa yake
iharibike kuliko kusema uongo.
Ni aheri kupotea kwenye siasa za
dunia kuliko kusimamia uongo!
Msingi wa kwanza wa Richmond:
Ili uelewe ni lazima urudi kwenye
taarifa ya Kamati ya Mwakyembe,
Slaa alifuatwa asubuhi ya siku ile
kupewa rushwa, anashuru Sitta na
Mwakyembe wajitokeze!
Akamuuliza mtoa rushwa kama
anatoa m.500 kwa mbunge,
atakuwa nazo ngapi? Aliwaambia
Sumaye na Lowassa kuwa rushwa
ni jambo linaloanzia kifuani
kwanza. Mwanzo wa jambo hili ni
taarifa ya Baraza la Mawaziri la
10.2.2006. Kamati ya mwakyembe
iliangalia faili la kikao kile kisha
kuandika ripoti!
Suala hili lilianzia wakati wa
utawala wa mkapa kutokana na
dharura ya umeme nchini,
wakawasiliana na kampuni moja
ya Amerika Kaskazini kwa suluhu
ya muda mfupi ya umeme.
Serikali ya Kikwete ikapokea lile
suala. Wakaruhusu mpango
uendelee, ila kwa kufuata sheria.
Hiyo ilikuwa kauli ya Baraza la
Mawaziri!
Wakati auala lile linaamuliwa,
Lowassa alikuwa Waziri Mkuu! Na
ndie mwenye mandate ya
maamuzi ya Serikali, iweje leo
akane kuhusika?
Taarifa ya Mwakyembe
inapotoshwa! Taarifa ilitaka
Waziri Mkuu ajipime, au bunge
limjadili na kumchukulia hatua.
Lowassa akakimbia kwa kuwa
alijua Bunge lingemfukuza kazi!
Waliioomba tenda walikuwa 26,
waliorudisha walikuwa 8. Kamati
ya Tathmini ikaona hakuna
anayefaa hata mmoja! Waziri
Msabaha akaagiza taarifa ile
ifutwe na tathmini ifanyike upya,
mara ya kwanza, ya pili, ya tatu
na ya nne. Jeuri wa Msabaha
ilitoka wapi?
Baraza likaamua baadaye tenda
iliyopewa kwa kampuni ya kwanza
ifutwe! Lowassa alishiriki!
TANESCO wakatoa ushauriwa wao,
Mamlaka husika ikatafute
internatonal tender ya kununua
turbine!
Lowassa akaingilia mchakato
dakika za mwisho, akamuagiza
katibu muhtasi wake!
Kwanini Lowassa, kwa kuwa
anagombea urais, rais
asiyeaminika hawezi kuchaguliwa!
Lowassa alishawahi kumuita Slaa
kuhusu habari ya Meremeta, na
kumuambia kuwa taarifa yake
inaiaibisha Serikali! Kampuni ya
jeshi imewahi kutengeneza gari,
imehujumiwa na wahuni.
Akamtaka Lowassa amuambie ni
nani aliyehusika?
Akamuita mwingine kwnye
Speaker lounge. Slaa akamuambia
kuwa yeye ni fisadi kichwani,
rohoni mpaka...!
Tunamsifia Lowassa kuwa
an=taleta maji wakti jimbo la
Lowassa halina maji na ufisadi
mkubwa umefanyika kwneye
jimbo hilo. Mnazungumzia shule
za kata wakati wakati hamjua
zimeanza wapi?
Slaa anataja nafasi alizowahi
kushika Afrika. Uamuzi wa
kujenga shule za kata ulifikiwa
mwaka 90 huko Thailand, mpango
huo ukaitwa Education for All, sio
MMES kama unavyoitwa leo!
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Anasoma barua ya Ibrahim
Msabaha kwa Flugence Kazaura,
mkurugenzi wa bodi wa TANESCO!
Mpango ulikuwa kuondoa suala la
umeme mikononi mwa tanesko
kwa kuwa imeshindwa kutekeleza.
Ugomvi wake na Masha ni kwa
kuwa Lowassa alimlaumu Masha
kuingilia mchakato wa serikali,
akawekewa kinasa sauti
chumbani.
Waziri Mkuu haruhusiwi na sheria
kuingilia mchakato wowote wa
tenda.
Kwenye kampuni nane
zilizowasilisha maombi ya zabuni,
Richmond ni kampuni iliyokuwa
mbovu. Ilikuwa ni kampuni ya
steshenari, sio umeme!Wakadai
wana ushirikiano na kampuni
nyingine ya umeme, kampuni
hiyo ikakataa kujihusisha na
Richmond, wala kuzalisha na
majenereta!
Bill Clinton aliwai kukutwa na
kashfa, walitaka kumchukulia
hatua si kwa sababu ya zinaa, bali
kwa kuwa alifanya uongo! Kwa
kuwa alidanganya umma! Hata
sheria za Tanzania zinakataza
kuongopa, hata kesi za uchaguzi
za Slaa zimethibitisha hilo.
Lowassa anadai yeye
alisimamisha tenda, Slaa
anaonesha uthibitisho wa hilo
kwa barua za Lowassa kwenda
kwa Msabaha zinazokanusha hilo,
'Anaisoma'! Waziri Mkuu
aliharakisha mchakato wa tenda,
tofauti na sheria ya PPRA. Barua
imeandikwa miezi mitatu baada
ya mkataba kusainiwa, kwa
maagizo ya Waziri Mkuu.
Tanesko ikaagizwa kusaini
mkataba ambao haikuhusika
kwenye kuujadili! Anaona aishie
hapo... Anaupigia chapuo
mdahalo wa Sitta na Mwakyembe,
anasema Lowaasa nae afike
kuondoa utata na kusema ukweli!
Chadema ni chama kilichotoa
matumaini kwa vijana wengi!
Isifike mahali tukawa washabiki
kama 2005 ambapo watu
waliahidiwa maisha bora,
wakajikaanga kutokana na
ushabiki! Anatoa ushahidi wa
kitakwimu wa mfumuko wa bei...
Slaa ana uchungu kuona chama
alichokijenga, kikifikia hatua ya
kusomba watu kwa mabasi na
malori kisha mkasema mafuriko
hayazuiliki! Hayuko tayari,...
Anakataa kuwa ZEZETA!
Ajenda ya Chadema ni nini,
ilikuwa ni rushwa! Wananchi
waliamini kwa kuwa msingi huo
ndio unakijenga chama!
Sehemu kubwa ya kilichosemwa
Jangwani ni ilani ambayo
ilishaandaliwa tayri, hakuna kipya
kilichosemwa. Kinachomuuma ni
chama makini kuwa kibovu zaidi
ya Chama cha Mapinduzi!
Hatuwezi kujenga maadili tukiwa
na watu wachafu, anaishi na
mwanamke bila kufunga ndoa
kwa kuwa Serikali ya CCM haitaki
afunge ndoa. Kesi yake ililetwa na
mawaziri, waandishi wa habari na
mtu kutoka IKULU. Ndoa
inafungwa na Mungu!
Scotland Yard iliamrisha Lowassa
achunguzwe, inakuwaje leo
tunamtetea? Huu ni ushabiki usio
na vielelezo, Slaa ana ushahidi!
Hakuna ulazima wa kwenda
mahakamani kwa kuwa kesi ya
rushwa ni jinai, ni kesi ya
serikali! Slaa au mwingine hana
locus ya kwenda mahakamani
kwa kesi ya jinai!
Mwakyembe alisema kesi ya jinai
haina mwisho (kama zilizyo za
madai).
chadema iliahidi kusafisha nchi
kwanza endapo itashika dola,
huku maendeleo yakiendelea!
Anasoma barua ya mchakato wa
Richmond kuwa DOWANS.
Kampuni imesajiliwa Costa Rica,
na mwenyekiti asiye na anuani,
simu wala jengo! Siku
iliyosajiliwa, mmiliki alisajili
makampuni mengine 99! Zaidi ya
hayo ana makampuni mengine
zaidi ya 50, DOWANS ni jina tu.
Kampuni haipo!
Dowans sio kampuni halisi huko
Kosta Rika, nchi nzima hakuna
kampuni yenye uwezo wa
kuzalisha umeme kwa kiwango
hicho!
Leo Lowaassa anatuambia
tufunge mdomo, huu ni udikteta!
Anakumbusha sakata lake na
Waziri Marmo...
Mabilioni ya fedha yanalipwa kwa
kampuni ambayo haipo!
Tunapenda ushabiki... Acha sifa
iharibike!
Anasema hataki kuingia kwenye
mambo ya Babu Seya! Vyuo vikuu
vinatumia kesi ya Babu Seya
kama case study. Mtoto mdogo
hawezi kutoa ushahidi
mahakamani, haki inapuuzwa kwa
kuwa mtoto hawezi kutoa
ushahidi!
Kesi ya Ulawiti rais hana
mamlaka nayo, anatoa wapi
kiburi cha kusema kuwa atamtoa?
Aliyeagiza polisi kuingia na polisi
kuingia na mbwa msikiti wa
mwembechai ni Sumaye, akiwa
waziri mkubwa. Leo hii ni mpiga
kampeni wa Lowassa! Leo
tunataka kura kwa namna yoyote!
Ni afadhali kutokuwa na rais wa
aina ya mtu huyu! anayesaka kura
kwa kusaka huruma za watu. Slaa
hayuko tayari kuona hilo
linatokea...
Anahitimisha kwa kusema
hajagusa chochote kuhusu ilani
wala mkakati!
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Kama taifa tuna kazi kubwa ya
kuchambua vitu nje ya
shamrashamra, maneno matamu!
Tumeshaumwa na nyoka,
tusilaghaiwe na maneno ya watu
hawa tena!
Utendaji uliotukuka unapimwa
kwa utafiti, sio kwa ukasuku na
kunukuu maneno ya wanasiasa!
Lowassa alipokuwa Waziri Mkuu,
matatizo ya wakulima na wafugaji
yalikuwepo, alifanya nini?
Lowassa aliwahi kubadili mpaka
wa Monduli na Karatu na
kusababisha mgogoro!
Mkampenia wake, Sumaye
alisababisha matatizo ya ardhi
Mvomero, akipora ardhi ambayo
ilitakiwa yajengwe makao makuu
ya Mvomero! Mengine ya Sumaye
ameyaweka kiporo, hisa zake za
kampuni aziweke wazi kama
Sekretarieti ya Maadili
inavyotaka!
Kutotangaza mali kunatosha
kumtoa mtu ubunge! Sembuse
Urais?
==============================
=========================
Ukweli huwa una tabia ya
kuegemea upande, anasemea
speculation kuwa ameisema
chadema peke yake.
Anasema amestaafu siasa, hana
chama lakini bado anabaki kuwa
mtanzania, mtetezi wa wanyonge
na atabaki hivyo! Ataendelea
kuwatumikia watanzania kadiri
ya Mungu alivyomjalia vipawa!
Kama alivyoombwa kugombea
urais 2010!
Anaweza kuwatumikia Watanzania
bila kuwa na chama!
Anasema kuwa hajapata vitisho
kama alivyopata kipindi hiki,
inazidi hata wakati alipotangaza
List of Shame. Rostam ndiye
anafadhili kampeni za urais wa
Lowassa! Anamnukuu vitisho
vyake! anakiri kuwa maaskofu
wamehongwa, Rostam akiwa
anaona, m60-m300!
Anasema hatenda chama
chochote, anasisitiza! Amejitoa
rasmi siasa za vyama vya siasa...
Ataendelea kuwa msimamiaji wa
anachokiamini!
Anawataka watu aliowataja
watoke hadharani, anatoa baraka
za KIMUNGU kwa nchi na watu
wake!
MASWALI!
Swali: Unawammbia nini
Watanzania kuelekea uchaguzi, ni
rais yupi anafaa?
Amesema hana chama, hampigii
kampeni mtu yoyote! Amesema
anafanya uchambuzi wa madhara
ambayo taifa litapata endapo
watamchagua Lowassa, na kwa
kuwa na uzoefu nao kwa muda
mrefu!
Hataki kufanya kampeni yoyote.
Anawaelimisha Watanzania
kuacha ushabiki
utakaowagharimu! Ni watu
wachache wanoweza kumtaja mtu
kwa majina, kuna tofauti ya
wanaotaja ajenda tu na wanaotaja
majina.
Rostam alimuambia kuwa ana
dakika 5 za kuishi, apige magoti
na kusali! Aliweka roho yake
rehani kwa ustawi wa taifa
hili...Anakumbusha ya
Mwembeyanga na namna Usalama
wa Taifa walivyokuwa na tension.
Magazeti mengi yaliogopa hata
kuandika habari, isipokuwa
MWanaHalisi!
Swali: Siasa ingekuwa asset kama
angekuja na wabunge kadhaa.
Angekuja kama asset, mengine
yangesafishika?
Kulikuwa na vigezo viwili, ama
asset na liability, yaani hayo
madhambi yote aliyoyasema.
Baada ya hayo wangefanya
tathmini kama anapokelewa au
hapokelewi. Anatoa mfano wa
Shirikisho la Afrika Mashariki na
nchi zinazotaka kujiunga!
Swali: Waliopokelewa ni makapi.
Je wewe ulikuwa kapi 95?
Anauliza kama watu wanaamini
yeye alikuwa kapi? Tupime
vigezo... Makapi ni watu
waliokataliwa na watu wao baada
ya kuwa wabunge kwa muda
mrefu. CCM wakasema kuwa
hakuwa mwenzao: hakuwa
anahonga, hakuwa anapokea
rushwa na kadhalika!
Kuingia kwa tiketi ya Chadema
ulikuwa ukombozi kwake!
Swali: Umetangaza kustaafu siasa,
una kadi za vyama viwili.
Unazirudisha au unakaa nazo?
Watanzania tuelimika, kadi sio
uanachama. Kadi ni mali ya
mwanachama, unaweza kuichoma,
kuweka kumbukumbu au
vyovyote, sawa na kadi ya ndoa
ambayo hairudishwi hata kama
ndoa itavunjika. Tuulize maswali
ya kujenga.
Swali: Anaoneka baada ya kukosa
urais anamshambulia Lowassa!
Wapi Slaa alichukua fomu ya
Urais, hakuwa na nia na urais
wala hawezi kukasirika. Tuache
ushabiki, tuwe na mtiririko na
kuzingatia hoja! Mwandishi awe
msikivu sana... Ameeleza tangu
mwanzo, hana chuki wala ugomvi
na mtu yoyote!
Chama cha Mapinduzi kilishakuja
kumpa ofa kadhaa kuachia jimbo
la Karatu, akaweka sharti la
mkataba wenye sahihi za watu
watatu; Rais, Slaa na Yesu Kristo.
Swali: Kama wewe uliweza
kuhama, wengine nao hawawezi?
Dr. Slaa hakuwa na uchafu
wowote, tatizo halikuwa kuhama
chama, tatizo ni watu wa aina
gani wanahama chama?
Swali: Unahamasisha uwazi,
mbona wewe umemficha muovu
mmoja?
Silaha haziwekwi zote mezani,
amewaomba anaowatuhumu
wajitokeze!

Jumapili, 30 Agosti 2015

Soma droo ya uefa hapa katika mechi za makundi Man Utd yapeta, Arsenal kwa Bayern Arsenal imetupwa kwa Bayern Munich wakati Manchester United ikipewa vibonde katika mashindano ya


Mshambuliaji wa FC Barcelona, Lionel
Messi akipokea tuzo ya mwanasoka bora
wa Ulaya kutoka kwa rais wa UEFA,
Michael Platini (kulia) baada ya kumshinda
mpinzani wake Cristiano Ronaldo wa Real
Madrid jana wakati kwa kupangwa kwa
ratiba ya Ligi ya Mabingwa UEFA jijinin
Monaco.
Monaco, Ufaransa. Arsenal imetupwa
kwa Bayern Munich wakati
Manchester United ikipewa vibonde
katika mashindano ya Ligi ya
Mabingwa, huku Lionel Messi akitwaa
tuzo ya mwanasoka bora wa mwaka
wa Ulaya.
Katika ratiba hiyo iliyopangwa jana
jijini Monaco inaonyesha Arsenal
inakutana tena na Bayern kwa mara
ya tatu ndani ya misimu minne
mfululizo.
Gunners pia itacheza na Olympiakos
ya Ugiriki na Dinamo Zagreb ya
Croatia.
Manchester United imepangwa
kuchezwa na PSV Eindhoven mechi
itakuwa kimrudisha mshambuliaji
Memphis Depay kucheza na timu yake
ya zamani.
Chelsea imetupwa kwa Porto, klabu
ambayo Jose Mourinho alitwaa taji
lake la kwanza la mashindano hayo
2004.
Manchester City itawavaa mabingwa
wa Serie A, Juventus pamoja na
mabingwa wa Europa Ligi, Sevilla na
Borussia Monchengladbach.
Mabingwa watetezi Barcelona
wakipangwa katika Kundi E, pamoja
naza Bayer Leverkusen, Roma na
BATE.
Barca, ambao wametwaa taji hilo mara
tano katika hisoria ya timu hizo
wataanza utetezi wa nyumbani
wakisaka heshima mpya ya kuvunja
rekodi ya kulinyakua taji hilo mara
nyingi.
Juventus, ambao walicheza fainali ya
msimu uliopita dhidi ya Barca,
wamepangwa katika Kundi D,
sambamba na timu za Manchester
City, Sevilla na Borussia
Monchengladbach.
Katika Kundi A, mabingwa wa
Ufaransa, Paris Saint-Germain
wataumana na mabingwa wa
kihistoria barani Ulaya, Real Madrid
pamoja na timu za Shakhtar Donetsk
na Malmo.
Wakifuzu kwa kishindo katika hatua ya
makundi, Manchester United nao
wamerudi katika fainali hizo kwa kasi
baada ya kukosa mashindano hayo
kwa msimu mmoja.
Man United wametupwa katika Kundi
B wakiwa na timu za PSV, CSKA
Moscow na Wolfsburg ya Ujerumani.
Katika Kundi C, mabingwa wa Ureno,
Benfica watakuwa na mabingwa wa
zamani wa Hispania, Atletico Madrid,
Galatasaray na Astana.
Vinara wa Ligi Kuu England msimu
huu, Manchester City wamepangwa
kuanza mashindano hayo katika Kundi
D, ambalo pia lina timu za Juventus,
Sevilla na Borussia Monchengladbach.
Bayern Munich, ambao ni mabingwa
wa Ujerumani waliocheza fainali ya
Ligi ya Mabingwa 2012 dhidi ya
Chelsea, wamepangwa kuanza
kampeni za msimu huu katika Kundi F
pamoja na timu za Arsenal,
Olympiacos na Dinamo Zagreb.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu
England, wao wamepangwa katika
Kundi G, wakiwa na Porto, Dynamo
Kiev na Maccabi Tel-Aviv ya Israel.
Katika Kundi H, mabingwa wa Urusi,
Zenit, Valencia, Lyon na Gent. Ligi ya
Mabingwa Ulaya msimu huu
inatarajiwa kuanza mwezi ujao.
Katika hatua nyingine, mshambuliaji
wa kimataifa wa Argentina
anayeichezea Barcelona, Lionel Messi
amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa
Ulaya wa mwaka.
Messi ameibuka na ushindi katika tuzo
hiyo akiwabwaga wenzake wawili
Cristiano Ronaldo wa Real Madris na
mshambuliaji mwenzake wa Barca,
Luis Suarez.

By rizik malya ... Logarusic amrejesha Kenya Ivo Mapunda Kocha wa zamani wa Simba, Zdravko Logarusic amempa kibarua kipa wa zamani wa klabu hiyo, Ivo


Ivo Mapunda
Dar es Salaam. Kocha wa zamani wa
Simba, Zdravko Logarusic amempa
kibarua kipa wa zamani wa klabu hiyo,
Ivo Mapunda (pichani) kwa kukubali
kumsajili katika klabu yake, AFC ya
Leopards ya Kenya.
Mapunda aliliambia gazeti hili jana
kuwa muda wowote atasaini kuichezea
klabu hiyo ya Ligi Kuu Kenya baada ya
kutoswa na Wekundu wa Msimbazi.
Ivo, ambaye alidaiwa kuchukua Sh10
milioni za awali kwa ajili ya kusaini
mkataba mwingine na klabu hiyo
aliachana na klabu hiyo kwa madai ya
viongozi wa klabu hiyo kuwa aligoma
kusaini fomu za usajili.
Kipa huyo mahiri na mzoefu aliliambia
gazeti hili kuwa ameitwa na Logarusic
kwa ajili ya kufanya mazungumzo na
kisha kusaini mkataba.
“Logarusic alinifundisha wakati ule
nikiwa Gor Mahia na alivyokuja Simba
nami nikamfuata, kisha akaondoka na
kujiunga na AFC Leopards na ameniita
ili niende huko,” alisema.
Pia, Ivo aliwataka wachezaji nchini
kuwa makini na mikataba yao na kama
wanashindwa kujisimamia wenyewe
inafaa watafute watu wa karibu wa
kuwasimamia kwani viongozi wengi wa
klabu kubwa ni wajanja wajanja.
“Nawashauri wachezaji wawe makini
kwenye suala la mikataba, wawe
makini kuisoma vizuri mikataba yao
na kama wakishindwa watafute
wasimamizi wa karibu.
“Wachezaji wengi wamekumbana na
matatizo ya mikataba yao na hiyo
inatokana na kutoisoma vizuri
mikataba hiyo na kuielewa ndipo
usaini,” alisema.
Aliongeza: “Viongozi wengi ni wajanja
katika masuala ya mikataba, baadhi
yao siyo wa kweli na kuna masuala ya
bima na mengine muhimu kwenye
mikataba hawayafuti, wanachoangalia
ni kukutumia wakishakuchoka
wanakuacha na mchezaji ukiwa
mkweli kwao wanakuweka pembeni.”
“Mchezaji ukipata timu inakupa
maslahi mazuri iwe nje ya nchi au
hapa nyumbani wewe nenda tu
hakuna haja ya kujishauri kwani mpira
ni biashara.
“Using’ang’anie sehemu moja hata
kama haina masilahi kwako hata kama
unacheza nje na hakuna masilahi na
nyumbani kuna timu imekuita
inalikupa vizuri rudi,” alieleza.
Kuhusu kuachwa na Simba, alisema ni
mizengwe, lakini binafsi hajali kwani
hawezi kukosa timu ya kucheza.
“Kuna maneno mengi yametokea,
naamini ni mizengwe imesababisha
yote haya kwani iliamriwa tukae kikao
cha pamoja mwisho wa siku
nikaambiwa sina ushirikiano.
“Wakati naendelea kuuguza majeraha
kuna kiongozi wa Simba alitumwa
kuniletea fomu za usajili, lakini
hakunitafuta na baadaye nikasikia
amerudisha majibu kwa viongozi kuwa
sionekani na kamati ya usajili ikaamini
bila kuniita ili nijitetee.
Aliongeza: “Nilishangaa sionekani vipi
wakati mimi nipo kila siku na wengi
walifahamu kuwa ninaumwa, lakini
isitoshe hata huyo kiongozi
aliyetumwa kwangu sina mazoea naye
na hata kuhusu masuala ya mimi kuwa
majeruhi hakuwa anafuatilia sasa sijui
alikuwa na lengo gani la kurudisha
majibu kama hayo.”
Alisema hakuwa na haraka ya kusaini
mkata mpya wakati mkataba wake
umebaki miezi michache kwa sababu
alihakikishiwa kuwa ataendelea
kuitumikia timu hiyo msimu ujao.
“Sikuwa na haraka ya kusaini mkataba
mpya baada ya mkataba wangu kubaki
miezi michache kwa sababu sikuwa na
wasiwasi, waliniambia kuwa
wataendelea na mimi, hivyo sikuona
haja ya kusaini mapema kabla ya
mkataba wangu haujaisha na isitoshe
tayari walishanipa kiasi cha fedha,”
alisema kipa huyo aliyewahi kuichezea
pia Yanga miaka michache iliyopita na
baadae kwenda nje ya nchi.
-

Jumamosi, 29 Agosti 2015

Kikwete atahadharisha kauli za uvunjifu wa amani Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amesema baadhi ya kauli zinazotolewa


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya
Kikwete amesema baadhi ya kauli
zinazotolewa na Umoja wa Vyama vya
Upinzani (Ukawa), zinaashiria uvunjifu
wa amani pindi matokeo ya kura
yatakapoanishwa baada ya zoezi la
upigaji kura Oktoba 25 mwaka huu.
Rais Kikwete alisema baadhi ya kauli
hizo zimekuwa zikionyesha wazi
viashiria vya uvunjifu wa amani na
upotoshaji kwa kundi kubwa la vijana
ambao wanapiga kura kwa mara ya
kwanza.
Akizungumza wakati akizindua
Kampeni ya Mama Ongea na Mwanao
jijini Dar es Salaam Rais Kikwete
alisema;
“Wamediriki kusema wazi bila kificho
kwamba patakuwa hapatoshi, hizi ni
kauli zinazoashiria uvunjifu wa amani.
Tunachokisema CCM ushindi kwetu ni
lazima na tutashinda kwa kishindo na
kwenda nginja nginja mpaka Ikulu.”
Kikwete alisema CCM imejipanga
kuhakikisha inapata ushindi katika
Uchaguzi Mkuu ujao na kuongeza
kuwa ili kufanikisha hilo wamepanga
kikosi kazi ambacho kitatembea
nyumba kwa nyumba, chumba kwa
chumba, mtu kwa mtu ikiwa kwa sasa
tayari wameshaanza kufanya kampeni
zao kupitia mtandao ya simu za
mkononi.
Katika hafla hiyo ya kuzindua kampeni
hiyo inayoratibiwa na msanii wa
filamu na Miss Tanzania mwaka 2006,
Wema Sepetu, Rais Kikwete aliwataka
wanawake kaungalia mazuri yote
yaliyofanywa na Serikali ya CCM katika
kumuinua mwanamke.
-

Jumatano, 26 Agosti 2015

LASTECK ALFRED 0 Recomendar DESKTOP VIEW BACK TO TOP Pluijm: Yondani, Cannavaro igeni Kocha mkuu wa Yanga, Hans Pluijm amewataka mabeki Ligi Kuu wakiwamo wa klabu yake, Kelvin Yondani


Kocha mkuu wa Yanga, Hans Pluijm.
Dar es Salaam. Kocha mkuu wa Yanga,
Hans Pluijm amewataka mabeki Ligi
Kuu wakiwamo wa klabu yake, Kelvin
Yondani na Nadir Haroub ‘Cannavaro’
waige aina ya ukabaji wa beki wa
Azam, Pascal Wawa.
Alisema ukabaji wa nguvu na wa
kujiamini wa beki huyo raia wa
Ivory Coast ndiyo unaotakiwa kwa
sasa kwenye soka.
Alisema, “ Wawa (Pascal) ni beki
mahiri na anayetakiwa kuigwa na
mabeki wengine Ligi Kuu, lakini pia na
mabeki wangu Nadir Haroub
‘Cannavaro’ na Yondani (Kelvin) kwa
kuwa beki huyo anakaba kwa nguvu
wakati inapoitajika huku akijiamini.
“Wawa ana nguvu anazitumia nguvu
zake akijiamini na kujua wazi kuwa
anafanya kitu sahihi. Ukabaji wake
unafuata sheria za soka na hata
anavyofanya hivyo na wachezaji
kumlaumu basi ni wazi kuwa
wachezaji hawatambui kuwa anafanya
kazi yake inavyotakiwa.
“ Kizuri anachofanya ni kujiamini na
kujua sheria za soka, pia anatumia
nguvu akijua kuwa hajakosea wala
hatadhibiwa kwa kuwa anafanya kitu
sahihi na kwa muda mwafaka,”
alieleza kocha huyo.
Alisema kuwa ukabaji wa Wawa una
utofauti mkubwa na ule unaofanywa
na mabeki wengine Tanzania.
“Wawa anakaba kwa nguvu kwa
malengo na kujiamini, lakini mabeki
wengi ambao nimekuwa nikiona hapa
wanakaba kwa nguvu bila ya lengo la
kuisaidia timu kimpira zaidi
wanawaumiza wenzao, pia wanakaba
kwa nguvu bila kujiamini na chote
wanachokuwa wanafanya wanaona
kama vile wanakosea na mara nyingi
huwa wanajikuta wakipatwa na hofu
wanapokuwa wakikaba huku waamuzi
wakiwafuatilia kwa umakini,” alieleza.
-

Majambazi yauawa Mwanza Polisi mkoani hapa wamefanikiwa kuwauwa majambazi wawili baada ya kutupiana nao risasi kwa zaidi


Kamanda wa Polisi Mwanza, Charles
Mkumbo
Mwanza. Polisi mkoani hapa
wamefanikiwa kuwauwa majambazi
wawili baada ya kutupiana nao risasi
kwa zaidi ya dakika 10.
Majambazi hao ambao walikuwa
wanne wanadaiwa kutaka kufanya
uhalifu kwenye Kisiwa cha
Chembaya kilichopo katika Ziwa
Victoria juzi.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi
Mwanza, Charles Mkumbo majambazi
hao walikuwa wanatumia usafiri wa
pikipiki na kwamba walianza
kutupiana risasi na polisi baada ya
kubaini kuwa wanafuatiliwa na askari
waliopata taarifa dhidi yao.
Akizungumza na waandishi wa habari
leo, Kamanda amesema polisi walipata
taarifa saa 8:00 mchana juzi kutoka
kwa raia wema kwamba kuna kikundi
cha majambazi kinajiaanda kufanya
uhalifu Ziwa Victoria.
“Baada ya Polisi kupata taarifa hizo
walijipanga na kuweka mtego kwenye
eneo la mwalo wa Kisaka uliyopo
katika Kata ya Ilemela,” Kamanda
Mkumbo amesema na kuongeza:
Kwa mujibu wa jeshi hilo, silaha moja
aina ya Shotgun iliyofutwa namba na
kukatwa kitako na mtutu wake
zimepatikana baada ya majambazi hao
kupekuliwa walikutwa na riasi tano.
Kamanda Mkumbo amesema miili ya
majambazi hao imehifadhiwa katika
hospitali ya Rufaa Bugando, jijini
Mwanza.

Je unakumbuka haya mazuri ya lowassa... yaone hapa

Lowassa aendelea kuumbua vigogo
Ingawa Wahenga wana msemo
usemao mgeni njoo mwenyeji
apone kwa mabosi wa mkoa wa
Kigoma hali imekuwa tofauti
baada ya mgeni wao, Waziri
Mkuu Bwana Edward Lowassa
kuwaonjesha joto ya jiwe
hadharani.
Miongoni mwa walioonja
shubiri ya Waziri Lowassa
ni Mkuu wa Wilaya ya
Kigoma, Bw. John Mongella
ambaye bila kutarajia
alijikuta akikatizwa kusoma
ripoti yake yenye kurasa
zaidi ya 10 wakati ndiyo
kwanza amefika ukurasa wa
tatu.
Ripoti hiyo ilianza
kumchafua Waziri Mkuu pale
Mkuu huyo wa Wilaya
aliposema kuwa chanzo cha
kuzorota kwa kilimo cha
kahawa ni ukosefu wa
wataalam wa zao hilo.
Bw. Lowassa akasema hayo ni
mambo ya zamani asiyotaka
kuyasikia katika ziara yake
na badala yake anahitaji
kuona wakuu hao wa wilaya
wakionyesha kwa vitendo
uelewa wao baada ya kupigwa
msasa wa nguvu na Rais
Kikwete kwenye semina
elekezi iliyomalizika hivi
karibuni huko Arusha.
’’John huna taarifa,
afadhali twende kwenye
ziara’’, akasema Bw.
Lowassa na kuinuka
kuendelea na ziara.
Bosi mwingine aliyekumbwa
na kasheshe hilo ni Mkuu wa
wilaya ya Kibondo Luteni
Kanari John Mzurikwao
ambaye naye aliambiwa
ripoti yake ni mbovu.
Waziri Mkuu akazidi
kumuumbua mkuu huyo wa
wilaya kwa kusema kuwa
anashangazwa na utendaji
wake wa kazi kwa vile ni
tofauti kabisa na jinsi
anavyomfahamu.
Akasema inaonekana wakuu
hao wa wilaya hawakuambulia
kitu katika semina elekezi
iliyoendeshwa na Rais
Kikwete hivi karibuni
katika hoteli ya Ngurdoto
iliyopo nje kidogo ya Jiji
la Arusha.
’’Inaonyesha kuwa semina
ile haikueleweka wala
hotuba ya Rais aliyoitoa
mwishoni mwa mwezi uliopita
haikusikilizwa, ndio maana
mambo haya yanajitokeza’’,
akasema Bw. Lowassa.
Kana kwamba hiyo haitoshi,
Lowassa pia akamuibukia
Katibu Tawala wa wilaya ya
Kigoma, Bw. Martin
Mgongolwa na wakurugenzi wa
wilaya hiyo kwa kushindwa
kumsaidia mkuu wa wilaya na
badala yake wakamuandalia
hotuba iliyopitwa na
wakati.
Akasema Mkuu wa wilaya hiyo
bado ni mgeni na anahitaji
msaada wa viongozi wengine
wa wilaya ambao wana uzoefu
na maeneo yao.
’’Mnashindwa kuwasaidia
vijana hawa na mnataka sisi
tuwashambulie bure’’,
akacharuka Bw. Lowassa.
Waziri Mkuu yuko mkoani
Kigoma kwa ziara ya siku
tano akikagua miradi
mbalimbali ya maendeleo.