other blog

Alhamisi, 12 Novemba 2015

NAFASI YA KAZI HALMASHAURIYA WILAYA YA NGORONGORO MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 20 NOVEMBA 2015

HALMASHAURIYA WILAYA YA
NGORONGORO
NAFASI YA KAZI
Halmashauriya Wilaya ya
Ngorongoro imepokea kibali cha
Ajira Mbadala chenye Kumb.
Na.CB.170/371 /01 /'H’/77 cha
Tarehe 01 Septemba 2015.
Mkurugenzi Mtendaji we
Halmashauri yo Wilaya ya
Ngorongoro anawetangazia
Wananchi wote wenye sifa
kutuma maombi ya kazi kwa
kuzingatia vigezo na maelezo
yaliyo kalika Tangazo hili.
DEREVA DARAJA II (NAFASI 01)
SIFA
• Awe na Elimu ya kidato cha
nne (lV).
• leseni daraja C ya uendeshaji
pamoja na uzoefu kuendesha
magari kwa muda usiopungua
miaka mitatu (3) bila kusababisha
ajali.
• Mwenye cheti cha majaribio yo
Ufundi daraja Ia II.
NGAZI YA MSHAHARA
Kwe kuzingolia viwango vya
mishahara vya Serikali ngazi yo
Mshahara yo TGOS A kwa mwezi.
Majukumu ya Kazi
• Kuendesha magari ya
Halmashouri.
• Kuhakikisha gari na vyamba
vyake vipo katiko hali nzuri wakati
wote na kufanya uchunguzi wa
gari baada ya safari ili kugundua
ubovu unaohitaji matengenezo.
• Kufanya matengenezo madogo
madogo katika gari.
• Kutunza na kuandika daftari To
salari "Logbook" kwa safari zote.
MASHARTI YA JUMLA KWA
WAOMBAJI
• Mwombaji awe Raia wa
Tanzania.
• Mwombaji awe na umri kati ya
miaka 18 hodi 40.
• Barua zoIe ziandikwe kwa
mkono no ziambatane na nyaraka
zifualaza:-
• Maelezo binafsi (CV)
• Nakala za vyeti kidato cha 4 au
6, na cheti cha kuzaliwa.
• Picha ndogo moja (Passport
size) ya hivi karibuni.
• Transcript, "Testimonial",
Provisional Result au statement of
Result havitakubaliwa.
JINSI YA KUTUMA MAOMBI
Barua zote ziwe na anuani ya
mwombaji na namba ya simu
(kama ipo na zitumwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji,
HaImaShauri ya WiIaya ya
Ngorongoro,
S.LP. 1,
LOLIONDO
Tareheyo Mwisho yo kupokea
maombi ni tarehe 20/11/2015 saa
tisa na nusu (9:30) alasiri.
John K. Mgalula
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
NGORONGORO

Jumamosi, 7 Novemba 2015

Walimu Manyara



Mwenyekiti wa Chama cha Walimu nchini
(CWT) mkoani Manyara, Qambos Sulle.
Mirerani. Walimu mkoani Manyara
wametakiwa kujipanga ili wapate
huduma za fedha kwenye Benki ya
Walimu ambayo imepata leseni.
Benki hiyo inatarajiwa kuanza
kuwahudumia walimu na wananchi
wakati wowote kuanzia sasa.
Mwenyekiti wa Chama cha Walimu
nchini (CWT) mkoani Manyara,
Qambos Sulle aliyasema hayo wakati
akizungumza kwenye siku ya mwalimu
ambayo ilifanyika katika Mji Mdogo wa
Mirerani wilayani Simanjiro juzi.
Qambos alisema walimu ni wengi na
mishahara yao inapopitia kwenye
benki nyingine huwatengeneza faida
wamiliki wa benki hizo, hivyo
wanapaswa kutumia benki yao ili
iwanufaishe.
“Benki yetu pindi ikishaanza shughuli
zake tutazungumza na Serikali ili tuwe
tunapitisha mishahara ya walimu,
kwani watumishi tutakaowaajiri
tutawalipa kupitia makato ya benki,”
alisema.
Alisema huu ni wakati sahihi kwa
walimu kufaidi matunda ya jasho lao
kwa kuwa kupitia benki hiyo
watajiongezea kipato na kufanya
shughuli nyingine za maendeleo.
Akizungumza katika siku hiyo ya
mwalimu, Katibu wa CWT wilayani
Simanjiro, Abraham Kisimbi alisema
walimu wanapaswa kushughulikiwa
mahitaji yao ili waweze kutekeleza
majukumu ipasavyo.
Katibu wa CWT mkoani Manyara, Nuru
Shenkalwa alisema kwa sasa walimu
wengi ni vijana ambao wanajua haki
zao na wanasoma hadi mitandao,
tofauti na walimu walioanza kazi
miaka ya 1980 wanaotarajia kustaafu.
“Walimu wengi wa zamani walikuwa
wanategemea kusoma magazeti mawili
yaliyokuwapo, lakini hivi sasa kuna
hadi mitandao, hivyo walimu vijana
wanatambua namna ya kudai haki zao
za msingi,” alisema Shenkalwa.

Magufuli afuta safari


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dk John Pombe Magufuli
Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dk John
Pombe Magufuli amefuta safari zote za
nje ya nchi kuanzia leo hadi hapo
maamuzi mengine yatakapotolewa.
Dk Magufuli ameagiza shughuli zote
zinazotakiwa kufanywa nje ya nchi
zifanywe na kusimamiwa na
mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania
nchi za nje.
Uamuzi huo wa rais ameutoa Ikulu
jijini Dar es Salaam katika kikao
kilichojumuisha watendaji
mbalimbali wa serikali wakiwemo
Makatibu wakuu, Manaibu Makatibu
wakuu, Gavana wa Benki Kuu na
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA).
Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu kwa
vyombo vya habari ruhusa ya safari
nje ya nchi inaweza kutolewa kwa
jambo la dharura ambalo hata hivyo
jambo hilo lazima lipate kibali cha
Katibu Mkuu Kiongozi.
“Badala yake rais ametaka ziara nyingi
zielekezwe kwenda vijijini ili
kuwawezesha watendaji kujua na
kutatua kero za wananchi” imesema
taarifa hiyo.
Katika kikao hicho, rais ameelekeza pia
mambo kadhaa ambayo watendaji hao
wanapaswa kuyasimamia, kuyawekea
mikakati na kuyapanga vizuri ili
yasimamiwe mara moja na Baraza la
Mawaziri atakaloliteua.
Mambo hayo ni pamoja na kuanza kwa
mikakati ya kuhakikisha wanafunzi
wote wanaanza kupatiwa elimu ya
bure kuanzia Januari mwakani.
Taarifa hiyo imetaja jambo la pili kuwa
ni suala la uratibu wa mikopo ya
wanafunzi wa elimu ya juu ambapo
ameagiza lifanyiwe kazi na mipango
yake ikamilike kwa ajili ya utekelezaji
mzuri zaidi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, rais
amemuagiza Kamishna wa TRA
kusimamia kwa makini zoezi la
ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha
kero ndogo ndogo zinazowakabili
wananchi zinaanza kushughulikiwa
mara moja.
Ameitaka TRA kukusanya mapato toka
kwa wafanya biashara wakubwa na
wakwepa kodi bila kuogopa mtu wala
taasisi yoyote na kusisitiza kuwa
hakuna mwenye mamlaka ya
kubatilisha maamuzi hayo zaidi yake.
Dk Magufuli ametaka usimamizi
mzuri katika suala la manunuzi ya
umma ambalo amesema limekuwa
likitumika vibaya na kuwa mwanya
wa maofisa wasio waaminifu kuiibia
serikali kwa kuongeza bei za bidhaa
na huduma tofauti na bei halisi ya
manunuzi.

Prof Jay: Vijana ndiyo

Mbunge mteule wa Jimbo la Mikumi,
Joseph Haule, maarufu Profesa Jay
Mbunge mteule wa Jimbo la Mikumi,
Joseph Haule, maarufu Profesa Jay
amesema vijana ndiyo watakaoleta
mabadiliko nchini.
Akizungumza mwanzoni mwa wiki hii,
Profesa Jay, ambaye ni mbunge mteule
wa Jimbo la Mikumi kwa tiketi ya
Chadema, alisema vijana wanatakiwa
kujituma ili kuwa chachu ya
mabadiliko katika taifa lao.
Alisema jambo hilo wanatakiwa
kulifanya sasa bila kujali itikadi za
vyama vyao.
Profesa Jay, ambaye alipata umaarufu
kutokana na kibao chake cha kisiasa
cha “Ndio Mzee”, alisema kukaa
vijiweni na kulalamika hakuwezi kuwa
suluhu ya matatizo yao, hivyo
wakijituma kufanya kazi kwa pamoja
watawezesha Taifa kusonga mbele.
Profesa Jay alisema kuwa na malengo
ni njia mojawapo itakayomwezesha
kijana kujitambua na kujituma katika
kile anachokifanya, ili kutimiza
malengo aliyojiwekea kwa kipindi
mwafaka.
“Ukiangalia vijana maeneo ya vijijini
wanakuwa na malengo ya kuhakikishe
wanafanya mambo kadhaa kama
‘kujenga nyumba yangu ya kuishi
ndipo nioe mke’. Hii ni tofauti na
vijana wengi wa mijini. Naamini hata
wao wakiweka malengo Taifa litasogea
mbele kutoka hapa tulipo,” alisema
Profesa Jay.
Alieleza kuwa kijana yeyote anayeona
ana uwezo wa kufanya mabadiliko
anatakiwa kufahamu kuwa siasa
imeisha na huu ni wakati wa kufanya
kazi.
Alisema kwa sasa mabadiliko ni lazima
ili kuyavuta maendeleo kwani ndiyo
kitu cha msingi zaidi, akibainisha
kwamba ni kwa vijana wote nchini na
si Mikumi pekee.
“Mimi ni kijana nimefikiria kufanya
kazi itakayowakwamua vijana wote
nchini, nathamini uamuzi na namna
walivyoniamini wananchi wa Mikumi
kwa kunipa nafasi niwaongoze, lakini
natambua uwapo wa vijana Tanzania
nzima,” alisema Profesa Jay.
Alisema anachoweza kufanya sasa ni
kuwasaidia wasanii wenzake
kuwasemea na kutafuta njia za
kuwakomboa.
Hata hivyo alisema licha ya kuingia
katika siasa hana mpango wa
kuachana na muziki.
“Wapo wachungaji ambao waliingia
katika siasa hawakuacha kuhubiri,
wapo wafanyabiashara ambao nao
waliingia huko hata nao hawakuacha
biashara zao, kwa upande wangu
siwezi kuacha nitaendelea kufanya
muziki mpaka mwisho wa maisha
yangu,” alisema Profesa Jay.

Ikulu kutamu kwa

Kuna sura inayokinzana katika eneo la
Afrika Mashariki na lile la Kati. Kuna
wakati wanasiasa wanabisha kwenye
eneo hilo. Pia, bado kuna mwangwi
unaosukuma juu ya kile kinachoitwa
‘mabadiliko ya nyakati’.
Wote wanaozunguka eneo hilo
wanavuta subira kujua hatma yake.
Hata hivyo, kwa Rais Paul Kagame wa
Rwanda ni kama vile tayari
amechochea gia. Anajiandaa kukoleza
moto gari lake ili asonge mbele zaidi.
Inawezekana wakati huu anawatupia
macho wenzake. Anaendelea
kuwakodolea tena anawasimanga
moyoni. Lakini bila shaka anaamini iko
siku watafaulu na hatimaye kufuata
mkondo wa kisiasa zake.
Wenzake wanaendelea kupingana
kuanzia kwenye vikao vya Bunge hadi
majukwaa ya wazi ya kisiasa.
Pia, wanaendelea kutumia mifumo
‘dhaifu’ ya kisheria kuendelea
kupenyeza ushawishi wao. Wana kiu
kubwa tena wanaendelea kuwajaza
hamasa wananchi ili waendelea
kusalia madarakani.
Mengi yanaendelea kujitokeza barani
Afrika. Mathalani, Rais Joseph Kabila
wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
(DRC), bado haamini kama atafaulu.
Jaribio lake la awali kulishawishi
Bunge kubadilisha Katiba ili awanie
muhula mwingine wa tatu wa uongozi
lilizua mzozo mkubwa na hata
kusababisha ‘vurumai na kujitokeza
harufu ya kutoweka kwa amani’.
Jaribio hilo sasa ameliweka kando
huku akiendelea kupima kina cha maji
kwa kijiti.
Wale wanaomjua wanasema kuwa Rais
Kabila anachanga upya karata zake.
Wanasema huenda akaibuka
‘kivingine’.
Wanasisitiza kuwa Rais Kabila bado
hajakata tamaa tena anasukumwa na
kile kilichojitokeza kwa Rais Kagame.
Rais Kagame ameidhinishwa na Bunge
kuendelea kuwania madaraka kwa
muhula mwingine wa miaka saba.
Pia, kuna wale wanaamini kuwa, Rais
Kabika inawezekana yupo kwenye
tafakuli kubwa.
Wanaamini kuwa huenda kiongozi
huyo akabadilisha mchezo na
kuwashinda wapinzani wake kwa
kutumia ‘mkakati mgumu’ uliotumiwa
na Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi.
Licha ya kuwa mazingira ya kisiasa
kwa nchi hizo mbili yanabeba sura
mbili zinazotofautiana lakini siasa
hupenda kuazima matukio. Siasa ni
harakati ya kuhodhi madaraka. Daima
siasa ni mchezo wa kuwinda dola.
Inavyoonekana Rais Kabila shauku
yake kubwa ni kufuata mkondo wa
jirani yake Rais Kagame.
Rais Kagame amefunguliwa mlango
kuendelea kusalia madarakani. Bunge
limeidhinisha marekebisho ya Katiba
na hivyo kumpa fungua wa kuendelea
kukalia kiti cha ‘enzi’ kwa utawala wa
Rwanda.
Wenyewe Rwanda wanamsifu
wakisema ni kiongozi aliyebeba
‘mkono wa chuma’.
Rais Pierre Nkurunziza amejitwalia
funguo. Amewapiga chenga wapinzani
wake na kuendelea kushikilia ufunguo
wa kusalia madarakani. Licha ya
kuandamwa na shinikizo kutoka
nyumbani hadi katika duru za
kimataifa, Rais Nkurunziza hakusita
kuendelea na mkakati wake. Aliusuka
mpango na kisha kuutekeleza na sasa
anaushikilia.
Analaumiwa na kushutumiwa na
wengi. Anakosolewa tena anabanwa na
wakubwa wa magharibi.
Hata hivyo, amepuuza hayo yote na
kuendelea na kile kinachotajwa na
wengi ‘ umwamba wa baadhi ya
viongozi wa Afrika kusalia madarakani
kwa kupindisha katiba zao’.
Tayari ameanza kuonja kile wengi
wanakiita joto la jiwe. Mkoloni wake
wa zamani, Ubelgiji ilikuwa nchi ya
kwanza kuuadhibu utawala wake.
Ubelgiji imesitisha baadhi ya misaada
ya maendeleo huku ukionya kuchukua
hatua zaidi katika siku za karibuni
iwapo ukandamizaji kwa makundi ya
wapinzani utaendelea.
Marekani imefuata mkondo. Rais
Barack Obama ametangaza kuing’oa
Burundi kutoka kwenye mikataba yake
ya kibiashara ya AGOA
inayoyawezesha mataifa ya Afrika
kuingiza bidhaa zao katika soko la nchi
hiyo bila ya kulipa kodi.
Mpango huo uliasisiwa wakati wa
utawala wa Rais Bill Clinton
anayetajwa ndiye aliyefufua upya
uhusiano wa karibu baina ya mataifa
ya Afrika na Marekani.
Rais Obama ambaye katika siku za hivi
karibuni amekuwa mstari wa mbele
kuwakosoa viongozi wa Afrika
wanaong’ang’ania kubakia
madarakani, alisema amechukua
hatua hiyo baada ya kushuhudia
kushuka kwa viwango vya demokrasia
katika taifa hilo.
Jinamizi la utamu wa madarakani bado
linaendelea kuzunguka. Rais Kagame
amefaulu kunyosha mstari tena kwa
wananchi wake.
Hata hivyo, wapinzani wake
wanalalamika kwa kile wanadai
kuandamwa na vitisho na wakati
mwingine kuwa hatarini kuuawa.
Ingawa amefaulu kushika ufunguo wa
kuendelea kusalia Ikulu kwa mkono
wa umma, lakini kivuli cha mwisho
wake bado kinatawaliwa na chenga.
Wengi wanaona kuwa, Rais Kagame
‘amejitengenezea’ maadui wengi
kuliko ilivyotarajiwa.
Hali kama hiyo inaanza kulinyemelea
taifa la Congo Brazzaville ambako Rais
Denis Sassou Nguesso ambaye wakati
fulani alipewa sifa kubwa kutokana
mchango wake wa kusaidia kutatua
migogoro ya Afrika. Inaelezwa kuwa
kwa sasa kiongozi huyo anageuka
kinyonga.
Ameanzisha mkakati wa kubadilisha
Katiba ya nchi hiyo ili awanie urais
katika muhula mwingine wa tatu.
Hata hivyo anakabiliwa na upinzani
mkali, lakini mwenyewe anasisitiza
kuwa lazima ajenda yake ipate
uungwaji mkono.
Japokuwa kila mwanasiasa huja na
mwonekano wake, lakini kwa walio
wengi wanahisi kuwa viongozi hao
wanajaribu kucheza kwenye utelezi
mkali huku wakiwa wamevalia suruali
yenye msumari pembeni.