other blog

Jumatatu, 19 Oktoba 2015

MWADADA NOREEN KAHAYA...EAGLEFM


Msanii wa muziki wa Reggae, Jhikolabwino
Manyika 'Jhikoman' akipiga gitaa mbele ya
waandishi wa habari muda mfupi baada ya
mkutano ulioongelea tamasha la 'Karibu
Music Festival 2015'. Kulia ni Meneja
Uvumbuzi wa Serengeti Breweries
Limited, Attu Mynah. Picha na Said Hamis
Dar. Wadau wa muziki nchini, Afrika
Mashariki na dunia nzima kwa ujumla
watapata fursa kujumuika pamoja na
kubadilishana uzoefu wa kazi zao
katika tamasha la pili la muziki
maarufu kama ‘Karibu Music Festival’
litakalofanyika mapema mwezi ujao
huko Bagamoyo.
Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya
‘Fahari ya Tanzania’ linalennga kukuza
muziki wa Kiafrika na kuonesha
tamaduni za Kiafrika kwa dunia nzima
kupitia jukwaa la muziki
litakalokutanisha wanamuziki kutoka
sehemu mbalimbali duniani.
Akizungumza na waandishi wa habarI
leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari
Maelezo mwakilishi wa Karibu Music
Festival, Ernest Biseko alisema
Tamasha hilo mwaka huu
litahudhuriwa na wanamuziki
wakubwa akiwemo mkongwe Papa
Wemba, Sarabi Band, H-Art The Band,
Yuzzo & Frontline Band.
Biseko alisema kuwa, wasanii toka
Tanzania ni pamoja na Jhiko Manyika
(Jhikoman) na band yake ya
Afrikabisa, Tomgwa Ensembe, mshindi
wa shindano la vipaji la BSS mwaka
2008, Misoji Nkwambi, Ze Spirit, Isha
Mashauzi, Damian Soul na bandi yake,
Juma Nature, Msafiri Zawose na band
yake.
“Pamoja na kwamba lengo kubwa ni
kukuza muziki wa Kiafrika na
tamaduni zake pia tunataka liwe
tamasha pekee Afrika Mashariki
kukuza uchumi na kuleta maendeleo
kwa watu wake ndio maana biashara
na maenesho ya bidhaa mbali mbali ni
sehemu ya tamasha hili,” alisema
Biseko.
Naye mwakilishi wa wanamuziki
watakaoshiriki katika tamasha hilo,
Jhikolabwino Manyika maarufu kama
Jhikoman ambaye pia ni msanii
maarufu wa miondoko ya Reggae
nchini alisema mashabiki wa muziki
watarajie kuona wasanii wote
wakitumbuzia bila kutumia CD
‘playback’.
Jhikoman alisema kuwa kupitia
tamasha hilo anatarajia kupata nafasi
ya kujifunza kutoka kwa bendi
nyingine jinsi ya kukuza kazi zao na
kudumisha urafiki utakaoleta manufaa
katika kazi yake.
Tamasha hilo litaanza kwa matembezi
kuashiria uzinduzi wake na pia
kutakuwa na mafunzo mbali mbali
yenye mlengo wa kuwasaidia wadau
wa muziki kufahamu mambo mbali
mbali kwenye maswala ya kiutawala
na jinsi ya kujitangaza, mambo ya hati
miliki, ngoma za asili, kupiga ngoma,
na mengineyo.
Kiingilio katika tamasha hilo ni
Sh2,500 kwa watoto, watu wazima
watakaonunua tiketi zao kabla ya
tamasha itakua ni Sh 5,000 na kwa
wale watakaonunua getini itakua Sh
7,000 na kwa watu maalumu (VIP)
tiketi zitauzwa kwa Sh 30,000.

MABERE GODLUCK SPORT EAGLFM..... Messi ajipa matumaini


Mshambuliaji wa Azam, Ramadhan
Singano ‘Messi’
Dar es Salaam. Mshambuliaji wa
Azam, Ramadhan Singano ‘Messi’
amesema kuwa hakatishwi tamaa na
kitendo cha kutopata nafasi kwenye
kikosi cha kwanza cha timu hiyo na
ana uhakika atapata nafasi hiyo ndani
ya kipindi kifupi kijacho.
Singano aliyejiunga na Azam msimu
huu akitokea Simba, amekuwa hana
nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha
timu hiyo kutokana na ushindani
mkubwa uliopo kwa washambuliaji
mbalimbali waliosajiliwa na klabu
hiyo.
Miongoni mwa washambuliaji
wanaowania namba naye ni, Kipre
Tchetche, John Bocco, Farid Mussa,
Didier Kavumbagu na Allan Wanga
walioifanya Azam iwe moja ya timu
zenye safu kali ya ushambuliaji
kwenye ligi.
Singano aliliambia gazeti hili jana
kuwa si jambo la kushangaza kwa
mchezaji kutopata nafasi ya kuanza
kwenye kikosi cha kwanza kwani ni
jambo inategemeana na matakwa ya
kocha.
“Mwenyezi Mungu ndiye kila kitu
katika maisha na yeye ndiyo
kampangia kila mwanadamu riziki.
“Nafurahia maisha hapa na ingawa
bado sijapata nafasi ya kucheza
kwenye kikosi cha kwanza mara.
Naendelea kufanya mazoezi na
naamini Mungu atanisaidia kupata
nafasi muda siyo mrefu,” alisema
Singano.

GODLUCK MABERE EAGLEFM ON SPORT...


Mshambuliaji wa Mbeya City, Haruna
Moshi ‘Boban’
Mbeya. Wakati Simba ikiibuka na
ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya
City, imebainika kuwa Wekundu hao
wa Msimbazi waliingia uwanjani
wakiwaza namna ya kumkaba kiungo
wao wa zamani Haruna Moshi ‘Boban’.
Simba waliingia mchezo wakiwaza
Boban angeingia na jipya gani,
baadaye waligundua kiungo huyo
hawatishi kwani ameongeza uzito kiasi
cha kushindwa kuendana na kasi ya
mechi huo uliochezwa Uwanja wa
Sokoine.
Hiyo ilikuwa mechi yake ya kwanza
kwa Boban ya Ligi Kuu Bara msimu
huu baada ya kuchelewa kujiunga na
kikosi hicho na alifanya mazoezi siku
moja kabla ya mechi hiyo na kocha wa
City, Meja Mstaafu Abdul Mingange
kuamua kumtumia.
Wachezaji waliowahi kucheza naye
Boban akiwa Simba, akiwamo kocha
msaidizi, Seleman Matola na nahodha
wa timu hiyo, Musa Hassan ‘Mgosi’
walimwelezea Boban kuwa ni mchezaji
mzuri, ila kwa sasa anahitaji kuongeza
juhudi katika mazoezi kwani
anaonekana kuwa mzito kutokana na
mwili wake kuongezeka uzito.
“Boban nimemwona, ni mchezaji
mzuri, kikubwa anachopaswa
kukifanya kwasasa ni kuongeza
mazoezi, maana amekuwa na mwili
mnene, ila kiuwezo bado anaonekana
yupo fiti na anaweza kukubadilishia
matokeo muda wowote,” alisema
Matola.
Naye Mgosi alisema, “namfahamu
Boban, si mchezaji wa kubezwa
unapocheza naye, anaweza kukuliza
muda wowote, ila kwa sasa bado
hajapata mchezaji ndani ya Mbeya
City ambaye anaweza kumwelewa kwa
haraka uchezaji wa Boban ama nini
anataka anapokuwa uwanjani.
“Boban siyo mchezaji wa
kukimbiakimbia, jinsi anavyocheza
ndivyo hivyo hivyo, anavyoweza
kukufunga bila kutarajia, ila
namshauri aongeze mazoezi apunguze
mwili na atawasaidia Mbeya City kama
watamtumia vizuri,” alisema Mgosi.
Kocha mkuu wa Simba, Dylan Kerr
naye alisema kuwa amepata taarifa za
Boban kuwa ni mchezaji hatari na
anapaswa kuchungwa katika mechi
hiyo japokuwa hajawahi kumuona
akicheza.
“Tunashukuru tumeshinda mechi hii
na kupata pointi tatu, Mbeya City siyo
timu mbaya na wamecheza kwa
kiwango cha juu, ila hawajapata bahati
ya kutufunga.”

GUDLACK MABERE ON SPORT. EAGLEFM... Ubonge ‘nyanya’ wamtesa Boban Wakati Simba ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City, imebainika kuwa Wekundu hao wa

POSTED BY MABERE GODLUCK EAGLEFM... KATIKA SPORT


Mshambuliaji wa Barcelona, Neymar da
Silva Santos Junior (wa pili kushoto)
akiwania mpira na beki wa Rayo Vallecano
Nacho (kushoto) na kiungo Diego Llorente
wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Hispania
uliozikutanisha timu hizo kwenye Uwanja
wa Camp Nou, Barcelona. Barca ilishinda
5-2. Picha na AFP
Madrid, Hispania. Real Madrid na
Barcelona zimeng’ang’ania kileleni
mwa La Liga wakati Cristiano Ronaldo
akiweka rekodi Real ikishinda 3-0 dhidi
ya Levante, huku Neymar akifunga bao
manne wakati Barca ikichapa Rayo
Vallecano 5-2.
Real imeutumia vizuri uwanja wake
Bernabeu, wakati Ronaldo akivunja
rekodi ya Raul akifunga mabao 324
katika misimu yake saba aliyocheza
kwa miamba hiyo ya Hispania.
Barca ilitumia vizuri wenyeji wake,
huku safu yao ya ulinzi ikionyesha
kupwaya na kuhitaji uwezo wa binafsi
wa Neymar kusawazisha kutoka
nyuma kabla ya kuifunga Rayo
iliyocheza soka zuri la kushambulia
kwenye Uwanja Nou Camp.
Miamba hiyo ya Hispania
inayosumbuliwa na majeruhi sasa
zinaongoza ligi zikiwa na pointi18
katika michezo nane, huku Real
ikiongoza kwa tofauti ya mabao.
Villarreal iliyokuwa ikishikiria usukani
kwa muda, imeporomoka hadi nafasi
ya tatu, kabla ya mechi yake ya jana
dhidi ya Celta Vigo, wakati Atletico
Madrid inayoshika nafasi ya tano
itacheza na Real Sociedad.
Marcelo alifunga bao la kwanza la Real
katika dakika 27, wakati alipobadilisha
pasi na Ronaldo na kupiga shuti
lililompata kipa Ruben wa Levante.
Ronaldo alifunga bao la pili dakika tatu
baadaye kwa shuti la mbali lililojaa
wavuni , na kumaliza ukame wake wa
kutokufunga katika michezo minne
iliyopita ya ligi.
Naye Jese akiingia akitokea benchi
aliifunga bao la tatu dakika nane kabla
ya filimbi ya mwisho na kuhakikishi
ushindi 3-0, wakati Real ikijiandaa na
mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa
Kundi A dhidi ya Paris St Germain.
Barca yatakata
Barca ilimkosa nyota wake Lionel
Messi na nahodha wake Andres
Iniesta, wakati Javi Guerra alipofunga
bao la kuongoza kwa Rayo katika
dakika15.
Ivan Rakitic na Luis Suarez awali
alishindwa kumfunga Tono wakati
alipokutana uso kwa uso na kipa huyo
wa Rayo, lakini Barcelona ilisawazisha
dakika 22, kupitia Neymar kwa
mkwaju wa penalti.
Mbrazil huyo amechukua jukumu la
kuibeba timu hiyo baada ya
kukosekana kwa Messi, alidondoshwa
tena kwenye eneo la hatari dakika 13
na kufunga penalti yake ya pili.
Neymar alifunga bao la tatu dakika 69
na kupachika la nne dakika 70 kufanya
matokeo kuwa 4-1, magoli hayo
yanamfanya Neymar kuwa mchezaji
mwingine wa Barca mbali ya Messi
kufunga idadi hiyo ya magoli tangu
Samuel Eto’o alivyofanya hivyo 2008.
Neymar alitegeneza bao la tano kwa
kupiga krosi nzuri iliyomaliziwa na
Suarez na kuhitimisha kalamu hiyo ya
mabao 5-2.
Jozabed alitumia vizuri kutumia
udhaifu wa mabeki wa Barca kufunga
bao la pili kwa Rayo katika dakika ya
86.
“Neymar amekuwa katika kiwango
kizuri tangu kuanza kwa msimu huu,”
alisema Luis Enrique. “Wakati
anapoingia katika eneo la hatari
hakuna wa kumzuia.”
Sevilla inayojiandaa kucheza na
Manchester City katika Ligi ya
Mabingwa Jumatano, imelazimishwa
sare 1-1 na Eibar, wakati Valencia
ikipata ushindi mnono wa mabao 3-0
dhidi ya Malaga.

POSTED BY PINDA ..EAGLEFM

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
Dar es Salaam. Waziri Mkuu Mizengo
Pinda, jana alitumia Ibada ya Shukrani
iliyofanyika katika Parokia ya
Hananasifu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar
es Salaam, kumshukuru Mungu kwa
kumwezesha kulitumikia Taifa kwa
zaidi ya miaka 15 na kuwaomba
Watanzania wamsamehe kwa
matamshi aliyoyatoa akiwa kiongozi,
huenda yaliwakwaza baadhi yao.
Pinda ambaye amekuwa Waziri Mkuu
kwa miaka minane na miezi tisa,
Waziri kwa miaka miwili na nusu na
Naibu Waziri kwa miaka mitano,
alisema anasikia fahari kumaliza
uongozi wake kwa furaha na amani.
Moja ya kauli tata zilizowahi kutolewa
na kiongozi huyo iliyozua sintofahamu
ni ile ya Juni 29, 2013 katika ukumbi
wa Bunge mjini Dodoma alipoviagiza
vyombo vya dola kuwashughulikia kwa
kuwapiga wale watakaokataa kutii
amri wakati wakifanya vitendo vya
uvunjifu wa amani.
Kauli nyingine tata ni ile ya mwaka
2009 baada ya kuwaeleza wanaoua
watu wenye ulemavu wa ngozi
(albino) pamoja na vikongwe hawana
budi kuuawa kwa kuwa wakisubiri
mahakama kuwahukumu, watakuwa
wanakosea.
“Katika ibada hii ya shukrani,
nimemuomba Mungu anisamehe kwa
matamshi niliyoyatoa nikiwa kiongozi
yanaweza kuwa yaliwaudhi watu bila
mimi kujua.
“Uwaziri Mkuu ni kazi ngumu yenye
changamoto nyingi. Nitakuwa mtu wa
ajabu nisipomshukuru Mungu kwa
uongozi wake katika kipindi chote
hicho tangu nikiwa naibu waziri hadi
kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu,”
alisema.
Pinda alisema katika utumishi wake
kwa umma amejifunza mambo mengi
lakini kikubwa zaidi ni kujua jinsi ya
kuishi na watu.
Katika hatua nyingine, Abate Thadei
Mhagama wa Abasia ya Hanga,
aliwataka waumini nchini wazidishe
maombi kwa kufunga na kuomba kwa
siku sita zilizobaki kabla ya kufanyika
kwa Uchaguzi Mkuu.
“Ninawaomba waumini wote tuzidishe
sala ili nchi iendelee kuwa na amani
na upendo, tumwombe Mungu pia
atuwezeshe kupata viongozi
aliowandaa kwa yeye kwa maana ya
rais, wabunge na madiwani,” alisema
Mhagama.
Alisema uchaguzi wa mwaka huu ni wa
aina yake kwani demokrasia imekuwa
miongoni mwa Watanzania.
“Sote ni mashahidi, tumeona kwenye
mikutano kila mgombea akija sote
tunajaa huko. Hii ni kwa sababu
hatujui yupi ni yupi, ndiyo maana
nasisitiza kuwa tumuombe Mungu
atuletee yule ambaye amemuandaa
yeye,” alisisitiza.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya
Baraza la Walei katika parokia hiyo,
Arbogasti Warioba alisema:
“Sote tunatambua kuwa kazi
aliyoifanya Waziri Mkuu Pinda ilikuwa
ngumu, misafara ilikuwa ni mingi na
wakati mwingine ilikuwa ya mwendo
mkali, lakini Mungu alimtetea na
kumlinda hadi leo yuko salama.
Tunakushukuru pia kwa ushirikiano
ulioendelea kutuonyesha wakati ukiwa
madarakani na tunakuombea uendelee
kuwa na ucha Mungu katika maisha
yako ya uraiani.”

POSTED BY VUMILIA NKYA A.K.A VEN DA CLASSIC....EAGLEFM... Magufuli: Asiyefanya kazi


Mgombea urais wa CCM, Dk John
Magufuli akihutubia mkutano wa kampeni
wilayani Misungwi, Mwanza jana. Picha na
Mpigapicha Wetu
Magu/Misungwi. Mgombea urais wa
CCM, Dk John Magufuli amewataka
wananchi kujipanga kufanya kazi kwa
sababu Serikali yake haitavumilia
watu wavivu.
Akihutubia mkutano wa kampeni
katika Uwanja wa Shule ya Msingi
Misungwi jana, Dk Magufuli alisema
hata vitabu vya dini vimeelekeza
kwamba asiyefanya kazi na asile, hivyo
wanaoahidi vitu vya bure
wanawadanganya Watanzania.
“Tujipange kufanya kazi, hata
maandiko ya vitabu vitakatifu
yanasema, asiyefanya kazi asile…
Misungwi nitaibeba kwa nguvu zangu
zote nikichaguliwa,” alisema.
Pia alisema nyumba za tembe ambazo
zinaahidiwa na wagombea wenzake
kwamba zitaondolewa ndani ya siku
100 ni uongo hivyo wasisikilizwe, bali
atakachofanya ni kuhakikisha bei ya
vifaa vya ujenzi inapungua na
ameanza na saruji.
Alisema anatambua kuwa wilaya hiyo
inakabiliwa na tatizo la maji na
kuwaahidi wananchi kulishughulikia
na wasimsumbue mbunge wao na
kwamba anapoahidi kutoa Sh50
milioni kila kijiji nchini watu
wanamshangaa lakini Serikali ina
fedha, nyingine zilikuwa zinatafunwa
na mafisadi.
“...Ndiyo maana baada ya kusikia
nimetangazwa mengine yakakimbia…
hivi sasa wanasema Serikali haijafanya
chochote wakati wengine wamezeekea
humu mpaka wakang’oka meno na
kuwekewa ya bandia, mbona
hawakuondoka muda wote?” alihoji Dk
Magufuli.
Mgombea huyo huku akichomeka
lugha ya Kisukuma kila mara, alisema
ujenzi wa barabara ya Usagara –
Kisema ukikamilika, malori yatakuwa
hayaruhusiwi kuingia katikati ya mjini
wa Mwanza. Aliahidi kufufua viwanda
vya kuchambua pamba ili kuleta
mabadiliko ya kweli.
Dk Magufuli aliahidi kufufua kilimo
cha pamba kwa kuhakikisha mkulima
anapata pembejeo na kunufaika na zao
hilo na kwamba, haiwezekani pamba
ilimwe Tanzania Ulaya wavae nguo
mpya halafu Watanzania waletewe
mitumba.
Hata hivyo, mgombea huyo akiendelea
kutoa ahadi sauti za wanawake
zilisikika zikimtaka kuzungumzia
samaki kazi ambayo ndiyo
wanayoitegemea kiuchumi, hivyo
akalazimika kutamka kuwa atafuta
ushuru unaoonekana kuwa kero.
“Nitafufua Chuo cha Kilimo Ukiriguru
na kutumia wataalamu wake
kuboresha kilimo cha pamba,”
alisema.
Mgombea ubunge Jimbo la Misungwi,
Charles Kitwanga alisema kuna sifa ya
Dk Magufuli ambayo haijatajwa nayo
ni ubunifu, kwani alianzisha mfuko wa
kujenga barabara kwa fedha za ndani
hali iliyowashangaza wafadhili.
“Hizi barabara tunazotaja kama siyo
yeye zisingekuwapo, mnakumbuka
wafadhili walikuwa wanakataa
kutukopesha, akaanzisha mfuko wa
kujenga barabara mpaka wafadhili
wanauliza fedha zitakapopatikana,
akawaambia tunazo,” alisema.
Kitwanga alimwomba mgombea huyo
kuwajengea hospitali ya wilaya na
kiwanda cha kusindika nyanya, zao
linalolimwa kwa wingi.
Akiwa Magu, Dk Magufuli alisema
endapo atachaguliwa, ataubadilisha
mji huo kwa kutatua kero sugu ya maji
na kujenga barabara zinazozunguka
mji huo. Alisema atatumia uwezo wake
wote kuhakikisha kilimo cha pamba
kinakuwa bora ili bei ya zao hilo
ipande na kuwanufaisha wakulima.
Akihutubia umati wa watu kwenye
Viwanja vya Sabasaba jana, Dk
Magufuli alisema: “Natambua kwamba
Magu shida yenu kubwa ni maji,
mmekuwa mkitaabika kwa muda
mrefu, huku Ziwa Victoria likiwa
limewazunguka.
“Kwa kutambua kwamba maji ni
muhimu kwa binadamu, hapa Magu
lazima mpate maji na tayari Kampuni
ya Cowi inafanya upembuzi yakinifu
kuhakikisha maji yanafika,
wakikamilisha tu suala la maji kufika
Magu niacheni mimi...”
Dk Magufuli alisema anataka kuona
Magu inabadilika na kwamba
ameahidi kujenga barabara
zinazozunguka mji huo na kuunganisha
wilaya jirani.
Alisema amezaliwa na kulima pamba
pamoja na kufuga, hivyo ni mtoto wa
mkulima na mfugaji na kwamba
atatumia uzoefu wake kuhakikisha bei
ya pamba inakuwa juu. “Nafahamu
kwamba bei ya pamba kwa sasa
imeshuka, lakini mimi ni mtoto wa
mkulima na mfugaji, pamba
naifahamu vizuri, nataka tutengeneze
mazingira mazuri kwa wakulima wa
pamba ili iwe bora,” alisema Dk
Magufuli.
Aliwataka wakazi wa mji huo, kula
fedha za watu wanaowahonga ili
wawachague, akisema hizo ni fedha
zao ambazo walizichuma kwa kutumia
ufisadi.
“Nyie mkipewa fedha kuleni, kwani
kula ni kwa mafisadi kulala kwa
Magufuli,” alisema na kuongeza kuwa
akichaguliwa, atakuwa rais wa watu
wote, kwa kuwa maendeleo hayana
chama.
Aliahidi kufuta ushuru ambao
umekuwa ukiwasumbua
wafanyabiashara ndogondogo
sambamba na kupunguza kodi za vifaa
vya ujenzi ili bei ya vifaa hivyo
ipungue na kuwawezesha wananchi
kununua na kujenga nyumba bora.
Imeandikwa na Aidan Mhando, Midraji
Ibrahim na Twalad Salum

POSTED BY RIZIKI MALYA EAGLEFM Lowassa: Nimejiandaa


Mgombea urais wa Chadema, Edward
Lowassa akihutubia mkutano wa kampeni
uliofanyika kwenye Uwanja wa
Rwandanzovwe, Nzovwe mjini Mbeya
jana. Picha na Emmanuel Herman
Mbeya/Mbarali. Mgombea urais wa
Chadema, Edward Lowassa amesema
amejiandaa na yupo tayari
kuwaongoza Watanzania akiwa rais wa
awamu ya tano.
Akizungumza kwenye Uwanja wa
Ruanda Nzovwe- Mbeya Mjini, Lowassa
alisema: “Ninatosha, nitumeni kwa
kura zenu… nipeni kura za kutosha
niwatumikie.”
Lowassa ambaye alisema anasikia deko
kutokana na wingi wa watu, alisema
misamaha ya kodi kwa sasa ni Sh1.6
trilioni na kwamba atahitaji Sh1.3
trilioni kati ya hizo kwa ajili ya elimu
itakayolipiwa na serikali kuanzia
chekechea hadi chuo kikuu.
Alirejea kusema kuwa katika serikali
yake hakutakuwa na michango ya
elimu, maabara wala madawati.
Akizungumza kabla ya kumkaribisha
Lowassa, Mwenyekiti wa Chadema,
Freeman Mbowe alisema viongozi
waliokuwa CCM akiwamo Lowassa,
wamejiunga na chama chao kwa kuwa
kina misingi imara.
Akizungumzia suala la upigaji kura,
alisema siku sita zilizobaki ni muhimu
kwa Watanzania kufanya uamuzi na
kusisitiza kuwa kuna kila sababu ya
kubakia kwenye vituo vya kura baada
ya kupiga kura huku akidai kwamba
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),
haiko huru.
Sumaye
Akihutubia mkutano huo, Waziri Mkuu
mstaafu, Frederick Sumaye alimtaka
Waziri wa Uchukuzi, Harrison
Mwakyembe kuwasomea wananchi wa
Mbeya, ripoti ya Richmond kuona
kama Lowassa anahusika.
“Lowassa hahusiki, alijiuzulu kwa ajili
ya kuwakoa wao na wao wanaendelea
kuilipa Richmond kwa mgongo wa
Dowans wakati Lowassa hayupo,”
alisema.
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph
Mbilinyi alisema tatizo kubwa kwa
wakazi wa jimbo lake ni maji hasa
katika vijiji vya Uyole na Mwakibete na
kusema kuna kila sababu ya kuvuta
maji kutoka Ziwa Nyasa hadi Mbeya ili
kukabiliana na tatizo hilo. Alisema
matatizo mengine ni hospitali na
huduma za afya akitaka wapatiwe
mashine za x-ray, CT Scan na umeme
wa uhakika.
Ilivyokuwa mchakamchaka
Kabla ya mkutano huo, Jiji la Mbeya
lilitawaliwa katika hekaheka za
mapokezi ya Lowassa kuanzia asubuhi
huku wakazi wakianza kufurika
kwenye uwanja huo tangu saa mbili
asubuhi.
Jiji lilitawaliwa na pilipika za
bodaboda na bajaji zenye bendera za
Chadema katika maeneo mengi
hususan Barabara Kuu ya Mbeya-
Zambia kuanzia Kabwe, Mwanjelwa,
Mafiati, Soweto na Mama John
ulikofanyikia mkutano huo.
Wafuasi wa mgombea huyo
walionekana wakirandaranda maeneo
mengi ya jiji hilo wakiwa wamevalia
sare za Chadema huku wakipiga deki
Barabara Kuu ya Mbeya - Zambia.
Muda mfupi kabla ya mkutano kuanza,
wafanyabiashara walifunga maduka
kwenda kusikiliza sera.
Wachuuzi wa vyakula na vinywaji
walihamishia biashara zao kwenye
mkutano huo tangu usiku wa kuamkia
jana na wengi walionekana kufurahia
uamuzi wao kutokana na biashara
waliyofanya.
Mmoja wa wauza chipsi, John Antony
alisema: “Aisee si unajua tena kufaa
kufaana, leo kuna neema kubwa kwetu
ndiyo maana leo tumehamishia
biashara yetu uwanjani.”
Mbarali
Katika mkutano wa Mbarali, wafuasi
wa CUF na Chadema walizua tafrani
wakati wakimsubiri Lowassa katika
Uwanja wa Mpira, Rujewa.
Tafrani hiyo ilizuka baada ya
mgombea wa CUF, Gamdust Haji
kufika na gari lake kisha kushuka na
wafuasi wanaomuunga mkono kwa
kumbeba juujuu na kumpeleka jukwaa
kuu, jambo ambalo liliwakera wafuasi
wanaomuunga mkono mgombea wa
Chadema, Liberatus Mwang’ombe na
kutaka kumuondoa kwa nguvu.
Polisi wazima rabsha
Baadhi ya mashuhuda walisema
kulikuwa na kundi la wafuasi
wanaomuunga mkono mgombea wa
CUF na kundi la mgombea wa
Chadema ambao walikuwa
wakilumbana huku kila upande
ukitaka mgombea wao ndiye anadiwe
na Lowassa kwa wananchi.
“Unajua hawa watu walishindwa
kuafikiana nani agombee ubunge
kupitia yale makubaliano yao Ukawa,
kitu ambacho kila chama kilisimamisha
mgombea wake,” alisema mmoja wa
wakazi wa Rujewa mjini, Athumani
Mwakitalima.
Akizungumzia suala hilo, Haji alisema:
“Ni kweli nimefanyiwa vurugu,
wamevunja vioo vya gari langu,
wakitaka niondoke kwenye mkutano
huo eti sina haki ya kushiriki na
kumsikiliza mgombea wangu wa urais.
Nimetoa taarifa polisi na kuna watu
wamekamatwa.”
Aliwalaumu viongozi wa kitaifa
walioambatana na Lowassa kwamba
hawakutaka kuuliza sababu za yeye
kutowapo mkutanoni hapo na badala
yake kumnadi Mwang’ombe akisema
hawakutenda haki.

POSTED BY DENIC LYAMUYA EAGLEFM


Dar es Salaam. Zimesalia saa 144 za
kampeni ambazo wagombea wa vyama
vyote vya siasa watazitumia kutupa
karata zao za mwisho wakilenga
kupata ushawishi wa mwishomwisho
na hatimaye kunyakua ushindi.
Saa hizo za majeruhi zimesababisha
wagombea urais wa CCM, Dk John
Magufuli, Edward Lowassa wa
Chadema na Anna Mghwira wa ACT –
Wazalendo kujikita katika mikoa “ya
kimkakati” na ile yenye wapigakura
wengi.
Dk Magufuli ndiye aliyefungua pazia la
kampeni Agosti 23 kwenye viwanja wa
Jangwani, Dar es Salaam na kufuatiwa
na Lowassa hapohapo Jangwani kabla
ya Mghwira kuzindua huko Mbagala.
Wagombea hao ambao
wameshazunguka mikoa yote nchini,
watazitumia siku sita zilizobaki kabla
ya siku ya kupigakura kujiwekea
mazingira mazuri ya ushindi.
Akizungumzia mikakati ya mwisho ya
kampeni, Kaimu Katibu Mkuu wa
Chadema, Salum Mwalimu alisema
mikoa yote nchini ni ya kimkakati kwa
chama hicho na Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa), huku akieleza jinsi
Lowassa atakavyohitimisha siku
zilizobaki.
“Kwa sasa, mgombea anaendelea na
mikutano ya kampeni mkoani Mbeya.
Akimaliza huko atarejea Dar es Salaam
kwa ajili ya kufunga kampeni ila
atapita katika mikoa ya Iringa na
Morogoro.
“Tupo katika hatua za mwisho, hivyo
tunaweza kuangalia pia ni wapi
mgombea wetu anaweza kwenda
ukiacha maeneo hayo,” alisema
Mwalimu.
Mjumbe wa kamati ya kampeni ya
CCM, January Makamba alisema
mgombea urais wa chama hicho
atazitumia siku sita zilizobaki kupita
majimbo ambayo aliyaruka katika
baadhi ya mikoa.
“Lengo letu ni kwenda kwenye
majimbo yote, hivyo siku hizi zilizobaki
atapita huko. Kuhusu wapi tutafunga
kampeni zetu tutatangaza siku yoyote
kuanzia leo,” alisema Makamba.
Lowassa jana aliendelea na kampeni
mkoani Mbeya huku Dk Magufuli
akiwa katika Wilaya ya Magu mkoani
Mwanza.
Mikoa ya kimkakati na yenye
wapigakura zaidi ya milioni moja kila
mmoja ambayo huenda wagombea hao
wakaitumia kunadi sera zao za
mwishomwisho ni Morogoro, Tabora,
Dodoma, Kagera, Tanga, Arusha, Mara,
Geita, Kilimanjaro, Kigoma, Shinyanga,
Ruvuma, Mtwara na Simiyu.
Mambo yasiyosikika
Akizungumzia ahadi za wagombea hao,
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama
vya Wafanyakazi (Tucta), Nicolaus
Mgaya alisema wagombea wengi wa
urais wanazungumzia kuongeza
mishahara wafanyakazi, lakini
wanasahau kuzungumzia jinsi
watakavyoongeza marupurupu ya
wafanyakazi hao.
“Hapa nazungumzia kodi ya nyumba,
fedha za usafiri na malipo ya likizo,”
alisema Mgaya alipoulizwa kuhusu
ahadi za wagombea.
Ardhi na Katiba
Pamoja na wagombea hao kuahidi
kutatua migogoro ya ardhi, mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine
(Sua), Profesa Damian Gabagambi
anaona jambo hilo halijatolewa
maelezo ya kutosha.
“Ardhi ni jambo ambalo halijapewa
kipaumbele kwa maana ya kupimwa
na matumizi yake kuidhinishwa na
kulindwa kisheria. Mwingiliano wa
matumizi ya ardhi ni moja ya matatizo
makubwa nchini,” alisema Profesa
Gabagambi.
Alisema wagombea hao hawajagusia
suala la Watanzania kupata Katiba
Mpya, ambayo mchakato wake
ulikwama kabla ya hatua ya Kura ya
Maoni.
“Suala la kusaidia wakulima kupata
masoko ya uhakika halijafafanuliwa
kwa kina wala jinsi ya kuanzisha na
kuendeleza viwanda vidogovidogo kwa
sababu ndiyo vinaajiri wananchi wengi
kuliko vikubwa, ambavyo kila
mgombea anasema atavianzisha
akiingia madarakani,” alisema.
Itikadi
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa
Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu
Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM), Profesa Penina Mlama
alisema hakuna aliyesema akishinda
ataongoza nchi kwa itikadi ipi.
“Tunajua kuwa Wamarekani
wanatumia mfumo wa ubepari na
Mwalimu (Julius) Nyerere alitumia
ujamaa, sasa hawa wa sasa
(wagombea) wanaamini mfumo upi?”
alihoji Profesa Mlama.
Ahadi za Lowassa
Lowassa amekuwa akitumia ahadi ya
elimu bure kuanzia msingi hadi chuo
kikuu kama silaha yake kuu ya kupata
kura kwa wananchi.
“Kipaumbele cha kwanza ni elimu, cha
pili ni elimu na cha tatu ni elimu,”
alisema Lowassa tangu kwenye
uzinduzi wa kampeni zake na
amekuwa akirudiarudia kuhakikisha
kinaeleweka.
Pia, katika mikutano yake mingi waziri
huyo mkuu wa zamani amekuwa
akizungumzia jinsi ya kutatua tatizo la
maji, ambalo linaonekana kuwa kubwa
sehemu nyingi licha ya baadhi kuwa
na vijito, mito na maziwa, akitoa mfano
wa jinsi alivyoshughulikia mradi wa
maji ya Ziwa Victoria, ambao unasaidia
wakazi wa mikoa ya Mwanza, Tabora
na Mara.
“Nitahakikisha maziwa na mito
mikubwa kama Kagera inatumika
kuondoa tatizo la maji,” alisema
Lowassa alipozungumza na wananchi
wa Nkenge, Kagera.
“Kama niliweza kutoa maji Ziwa
Victoria nitashindwa vipi kutoa maji
kutoka Ziwa Tanganyika ili wananchi
mpate maji ya uhakika?” alisema
Lowassa katika mkutano wake wa
kampeni uliofanyika katika Uwanja wa
Mwanga Community Centre, Kigoma.
Lowassa, ambaye amekuwa akiwaita
waendesha bodaboda, wamachinga na
mamalishe kuwa ni marafiki zake,
amekuwa akiahidi kuanzisha benki
maalumu ya kuhudumia wajasiriamali
wadogo.
“Tumetengeza ilani kiboko ambayo
ndani ya miaka mitano Tanzania yetu
itabadilika, lazima tupunguze tabaka
kati ya tajiri na maskini kwa uchumi
wa pamba, chai, dhahabu na gesi kwa
nini tushindwe? Mkitupa ridhaa na
Mungu akikubali, tutakwenda kasi na
tutakuwa na maendeleo,” alisema
Lowassa katika mkutano uliofanyika
mjini Makambako.
Ahadi za Dk Magufuli
Kete kubwa tano za mgombea wa CCM,
Dk Magufuli ambazo amekuwa
akizinadi takriban kila mahali
anapokwenda tangu alipozindua
kampeni zake ni pamoja na kufuta
utaratibu wa kuwakamata na
kuwatoza ushuru usio na tija
waendesha bodaboda na mama lishe
na kuwabana wafanyabiashara
wakubwa kulipa kodi.
Kutoka Mpanda Vijijini alikoanzia
kampeni za mikoani hadi maeneo
anayoyafikia sasa, Dk Magufuli
amekuwa akipata zaidi shangwe pale
anapowaahidi awananchi kutoa
mikopo ya Sh50 milioni kwa kina
mama na vijana kwa kila kijiji nchi
nzima ili kukuza ujasiriamali na
kusomesha watoto bure kuanzia
darasa la kwanza hadi kidato cha nne.
Amekuwa akianisha mikakati yake ya
kudhibiti ufisadi nchini akiahidi
kuanzisha mahakama maalumu ya
kuwafunga mafisadi, ahadi ambao
imeonekana kumbeba kiasi cha
kutoisahau kila anapofanya mikutano
yake.
Katika kipindi hicho cha takriban siku
58 za kampeni, Dk Magufuli ambaye ni
waziri wa ujenzi, amekuwa akiahidi
kuinganisha nchi kwa kujenga
barabara za lami katika kila mkoa na
hata katika miji mikubwa isiyo na
barabara hizo kwenye mitaa na wiki
iliyopita wakati kampeni zilielekea
ukingoni alisaini mkataba wa ujenzi wa
barabara za juu jijini Dar es Salaam.
Ahadi hizo kubwa zimekuwa
zikisindikizwa na mikakati ya kujenga
Reli ya Kati, ya Kusini kuanzia Bandari
ya Mtwara – Songea – Mbamba Bay
kupitia Mchuchuma na Liganga na ile
ya Kaskazini kwa kiwango cha
kimataifa.
Dk Magufuli ameahidi kuboresha
huduma za afya na kusambaza maji na
umeme vijijini ili usaidie kufanikisha
mkakati wa kuifanya Tanzania kuwa
nchi ya viwanda.
Mghwira wa ACT
Mpaka sasa mgombea urais wa ACT-
Wazalendo, Anna Mghwira amefanya
kampeni katika mikoa mbalimbali Bara
na Zanzibar na ahadi zake kubwa
zikiwa ni kumaliza tatizo la maji, ujenzi
wa barabara, viwanda, migogoro ya
ardhi na elimu.
Upatikanaji wa majisafi na salama
umeonekana kuwa tatizo kuu katika
maeneo karibu mengi aliyozunguka
kufanya kampeni zake. Akiwa kwenye
mikoa ya Kanda ya Kusini na Kaskazini
na Dodoma, Tabora na Pwani aliahidi
kuwa serikali yake itapambana
kuondokana na tatizo hilo, kwa haoni
sababu ya kuendelea hasa ikizingatiwa
kuwa Tanzania ni nchi yenye vyanzo
vingi vya maji.
Akiwa Ruvuma kwenye majimbo ya
Tunduru Kusini na Kaskazini,
mgombea huyo aliahidi kuimaliza kero
ya muda mrefu inayowakabili wakazi
wa Tunduru na vitongoji vyake ya
ukosefu wa barabara iliyodumu kwa
kipindi cha zaidi ya miaka 54 ya
Uhuru, kwa kuhakikisha
inatengenezwa kwa kiwango cha lami.
Alirudia ahadi hiyo akiwa Lindi,
Mtwara, Katavi, Kigoma, Rukwa,
Dodoma na Tabora akisisitiza kuwa
nchi haiwezi kuendelea ikiwa hakuna
barabara zinazoungana na barabara
kuu. Kuhusu viwanda, amekuwa
akihoji ni nani walioviua
vilivyokuwapo?
Akiwa katika mikoa ya Kusini, Mtwara
Lindi Ruvuma, aliahidi Serikali yake
itahakikisha inajenga viwanda vya
korosho ili kuondokana na uuzaji wa
korosho ghafi kunakoipunguzia
mapato Serikali. Katika mikutano yake
aliyoifanya Korogwe na Handeni,
Tanga alisema ACT itawajengea
viwanda vya kusindika matunda ili
kuongeza ajira na pato kwa serikali.
Akiwa Mbulu mkoani Manyara,
aliahidi kujenga kiwanda cha pareto
pamoja na viwanda vidogovidogo vya
usagaji wa mazao ya ngano, dengu na
mahindi yanayopatikana kwa wingi
kwenye maeneo hayo.
Maoni ya wananchi
Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo
Kikuu cha Ruaha (Ruco), alisema ahadi
hizo zinaonekana kuwa nzuri na kujibu
vilio vya wananchi lakini tatizo kubwa
linatokea katika utekelezaji wake
kutokana na mfumo mzima wa
kiuchumi.
Alisema rais yoyote atakayepita ili
atekeleze ahadi za elimu bure, afya na
maji bure atatakiwa kupambana zaidi
na mfumo wa uchumi wa dunia ambao
hauungi mkono sera hizo za kijamaa.
Mkazi wa Kigogo, Salim Juma alisema
ahadi za Dk Magufuli ni nzuri na kwa
utendaji zinaweza kutekelezwa lakini
tatizo lipo kwenye chama chake
ambacho kimekithiri ufisadi na hakipo
tayari kwa mabadiliko hivyo
kupunguza kasi ya utekelezaji.
Dar es Salaam. Zimesalia saa 144 za
kampeni ambazo wagombea wa vyama
vyote vya siasa watazitumia kutupa
karata zao za mwisho wakilenga
kupata ushawishi wa mwishomwisho
na hatimaye kunyakua ushindi.
Saa hizo za majeruhi zimesababisha
wagombea urais wa CCM, Dk John
Magufuli, Edward Lowassa wa
Chadema na Anna Mghwira wa ACT –
Wazalendo kujikita katika mikoa “ya
kimkakati” na ile yenye wapigakura
wengi.
Dk Magufuli ndiye aliyefungua pazia la
kampeni Agosti 23 kwenye viwanja wa
Jangwani, Dar es Salaam na kufuatiwa
na Lowassa hapohapo Jangwani kabla
ya Mghwira kuzindua huko Mbagala.
Wagombea hao ambao
wameshazunguka mikoa yote nchini,
watazitumia siku sita zilizobaki kabla
ya siku ya kupigakura kujiwekea
mazingira mazuri ya ushindi.
Akizungumzia mikakati ya mwisho ya
kampeni, Kaimu Katibu Mkuu wa
Chadema, Salum Mwalimu alisema
mikoa yote nchini ni ya kimkakati kwa
chama hicho na Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa), huku akieleza jinsi
Lowassa atakavyohitimisha siku
zilizobaki.
“Kwa sasa, mgombea anaendelea na
mikutano ya kampeni mkoani Mbeya.
Akimaliza huko atarejea Dar es Salaam
kwa ajili ya kufunga kampeni ila
atapita katika mikoa ya Iringa na
Morogoro.
“Tupo katika hatua za mwisho, hivyo
tunaweza kuangalia pia ni wapi
mgombea wetu anaweza kwenda
ukiacha maeneo hayo,” alisema
Mwalimu.
Mjumbe wa kamati ya kampeni ya
CCM, January Makamba alisema
mgombea urais wa chama hicho
atazitumia siku sita zilizobaki kupita
majimbo ambayo aliyaruka katika
baadhi ya mikoa.
“Lengo letu ni kwenda kwenye
majimbo yote, hivyo siku hizi zilizobaki
atapita huko. Kuhusu wapi tutafunga
kampeni zetu tutatangaza siku yoyote
kuanzia leo,” alisema Makamba.
Lowassa jana aliendelea na kampeni
mkoani Mbeya huku Dk Magufuli
akiwa katika Wilaya ya Magu mkoani
Mwanza.
Mikoa ya kimkakati na yenye
wapigakura zaidi ya milioni moja kila
mmoja ambayo huenda wagombea hao
wakaitumia kunadi sera zao za
mwishomwisho ni Morogoro, Tabora,
Dodoma, Kagera, Tanga, Arusha, Mara,
Geita, Kilimanjaro, Kigoma, Shinyanga,
Ruvuma, Mtwara na Simiyu.
Mambo yasiyosikika
Akizungumzia ahadi za wagombea hao,
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama
vya Wafanyakazi (Tucta), Nicolaus
Mgaya alisema wagombea wengi wa
urais wanazungumzia kuongeza
mishahara wafanyakazi, lakini
wanasahau kuzungumzia jinsi
watakavyoongeza marupurupu ya
wafanyakazi hao.
“Hapa nazungumzia kodi ya nyumba,
fedha za usafiri na malipo ya likizo,”
alisema Mgaya alipoulizwa kuhusu
ahadi za wagombea.
Ardhi na Katiba
Pamoja na wagombea hao kuahidi
kutatua migogoro ya ardhi, mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine
(Sua), Profesa Damian Gabagambi
anaona jambo hilo halijatolewa
maelezo ya kutosha.
“Ardhi ni jambo ambalo halijapewa
kipaumbele kwa maana ya kupimwa
na matumizi yake kuidhinishwa na
kulindwa kisheria. Mwingiliano wa
matumizi ya ardhi ni moja ya matatizo
makubwa nchini,” alisema Profesa
Gabagambi.
Alisema wagombea hao hawajagusia
suala la Watanzania kupata Katiba
Mpya, ambayo mchakato wake
ulikwama kabla ya hatua ya Kura ya
Maoni.
“Suala la kusaidia wakulima kupata
masoko ya uhakika halijafafanuliwa
kwa kina wala jinsi ya kuanzisha na
kuendeleza viwanda vidogovidogo kwa
sababu ndiyo vinaajiri wananchi wengi
kuliko vikubwa, ambavyo kila
mgombea anasema atavianzisha
akiingia madarakani,” alisema.
Itikadi
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa
Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu
Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM), Profesa Penina Mlama
alisema hakuna aliyesema akishinda
ataongoza nchi kwa itikadi ipi.
“Tunajua kuwa Wamarekani
wanatumia mfumo wa ubepari na
Mwalimu (Julius) Nyerere alitumia
ujamaa, sasa hawa wa sasa
(wagombea) wanaamini mfumo upi?”
alihoji Profesa Mlama.
Ahadi za Lowassa
Lowassa amekuwa akitumia ahadi ya
elimu bure kuanzia msingi hadi chuo
kikuu kama silaha yake kuu ya kupata
kura kwa wananchi.
“Kipaumbele cha kwanza ni elimu, cha
pili ni elimu na cha tatu ni elimu,”
alisema Lowassa tangu kwenye
uzinduzi wa kampeni zake na
amekuwa akirudiarudia kuhakikisha
kinaeleweka.
Pia, katika mikutano yake mingi waziri
huyo mkuu wa zamani amekuwa
akizungumzia jinsi ya kutatua tatizo la
maji, ambalo linaonekana kuwa kubwa
sehemu nyingi licha ya baadhi kuwa
na vijito, mito na maziwa, akitoa mfano
wa jinsi alivyoshughulikia mradi wa
maji ya Ziwa Victoria, ambao unasaidia
wakazi wa mikoa ya Mwanza, Tabora
na Mara.
“Nitahakikisha maziwa na mito
mikubwa kama Kagera inatumika
kuondoa tatizo la maji,” alisema
Lowassa alipozungumza na wananchi
wa Nkenge, Kagera.
“Kama niliweza kutoa maji Ziwa
Victoria nitashindwa vipi kutoa maji
kutoka Ziwa Tanganyika ili wananchi
mpate maji ya uhakika?” alisema
Lowassa katika mkutano wake wa
kampeni uliofanyika katika Uwanja wa
Mwanga Community Centre, Kigoma.
Lowassa, ambaye amekuwa akiwaita
waendesha bodaboda, wamachinga na
mamalishe kuwa ni marafiki zake,
amekuwa akiahidi kuanzisha benki
maalumu ya kuhudumia wajasiriamali
wadogo.
“Tumetengeza ilani kiboko ambayo
ndani ya miaka mitano Tanzania yetu
itabadilika, lazima tupunguze tabaka
kati ya tajiri na maskini kwa uchumi
wa pamba, chai, dhahabu na gesi kwa
nini tushindwe? Mkitupa ridhaa na
Mungu akikubali, tutakwenda kasi na
tutakuwa na maendeleo,” alisema
Lowassa katika mkutano uliofanyika
mjini Makambako.
Ahadi za Dk Magufuli
Kete kubwa tano za mgombea wa CCM,
Dk Magufuli ambazo amekuwa
akizinadi takriban kila mahali
anapokwenda tangu alipozindua
kampeni zake ni pamoja na kufuta
utaratibu wa kuwakamata na
kuwatoza ushuru usio na tija
waendesha bodaboda na mama lishe
na kuwabana wafanyabiashara
wakubwa kulipa kodi.
Kutoka Mpanda Vijijini alikoanzia
kampeni za mikoani hadi maeneo
anayoyafikia sasa, Dk Magufuli
amekuwa akipata zaidi shangwe pale
anapowaahidi awananchi kutoa
mikopo ya Sh50 milioni kwa kina
mama na vijana kwa kila kijiji nchi
nzima ili kukuza ujasiriamali na
kusomesha watoto bure kuanzia
darasa la kwanza hadi kidato cha nne.
Amekuwa akianisha mikakati yake ya
kudhibiti ufisadi nchini akiahidi
kuanzisha mahakama maalumu ya
kuwafunga mafisadi, ahadi ambao
imeonekana kumbeba kiasi cha
kutoisahau kila anapofanya mikutano
yake.
Katika kipindi hicho cha takriban siku
58 za kampeni, Dk Magufuli ambaye ni
waziri wa ujenzi, amekuwa akiahidi
kuinganisha nchi kwa kujenga
barabara za lami katika kila mkoa na
hata katika miji mikubwa isiyo na
barabara hizo kwenye mitaa na wiki
iliyopita wakati kampeni zilielekea
ukingoni alisaini mkataba wa ujenzi wa
barabara za juu jijini Dar es Salaam.
Ahadi hizo kubwa zimekuwa
zikisindikizwa na mikakati ya kujenga
Reli ya Kati, ya Kusini kuanzia Bandari
ya Mtwara – Songea – Mbamba Bay
kupitia Mchuchuma na Liganga na ile
ya Kaskazini kwa kiwango cha
kimataifa.
Dk Magufuli ameahidi kuboresha
huduma za afya na kusambaza maji na
umeme vijijini ili usaidie kufanikisha
mkakati wa kuifanya Tanzania kuwa
nchi ya viwanda.
Mghwira wa ACT
Mpaka sasa mgombea urais wa ACT-
Wazalendo, Anna Mghwira amefanya
kampeni katika mikoa mbalimbali Bara
na Zanzibar na ahadi zake kubwa
zikiwa ni kumaliza tatizo la maji, ujenzi
wa barabara, viwanda, migogoro ya
ardhi na elimu.

POSTED BY ERASMI KIMARIO EAGLEFM Washauri mambo matano




Dar es Salaam. Zikiwa zimebakia siku
sita kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi
Mkuu, Watanzania wameibua mambo
matano yanayoweza kuliepusha Taifa
na vurugu zinazoweza kutokea baada
ya uchaguzi.
Mambo hayo ni pamoja na uwazi wa
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),
pande zinazohusika kuheshimu sheria,
wagombea kuwa wakweli kwa wafuasi
wao, kukaa pamoja kuweka mwafaka
wa kitaifa na NEC kuwa huru.
Mambo hayo yametajwa kukiwa na
mvutano kati ya vyombo vya dola na
viongozi wa vyama vya upinzani
kuhusu suala la wananchi kukaa mita
200 au kwenda majumbani baada ya
kupiga kura.
Tayari Rais Jakaya Kikwete
ameshaagiza vyombo vya dola
kuchukua hatua kali dhidi ya watu
watakaokaidi agizo la kuondoka kituoni
baada ya kupiga kura.
Mbali na mvutano huo, juzi wilayani
Tunduma mkoani Mbeya mfuasi
mmoja wa CCM alimuua kwa
kumchoma kisu mwanachama wa
Chadema, kabla ya yeye kuuawa pia.
Viongozi kukutana
Kutokana na hali hiyo, mhadhiri
kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
(OUT), Emmanuel Mallya alishauri
viongozi wa vyama vyote
vinavyoshiriki uchaguzi huo wakutane
kujadiliana mambo ya kukubaliana
katika kipindi hiki kabla ya kufanyika
uchaguzi huo, Jumapili.
Mallya, ambaye ni Mkuu wa Idara ya
Sayansi ya Siasa chuoni hapo, alisema
kukutana kwa viongozi hao kutasaidia
kuwarejesha kwenye tafsiri ya
uchaguzi wa demokrasia badala ya
kuvutana kwa maslahi yao, hatua
inayoweza kuliathiri Taifa.
“Pili, uwazi wa NEC unahitajika zaidi
katika kipindi hiki, iwaeleze wagombea
kuweka mawakala waaminifu na
ijenge uhusiano mzuri na vyama,
taasisi za kiraia kwani dhamana ya
taifa ipo mikononi mwao na lazima
wanasiasa waongoze Taifa likiwa
salama na siyo walemavu,” alisema
Mallya.
Kufuata sheria
Profesa Gaudence Mpangalla wa Chuo
Kikuu cha Ruaha mkoani Iringa
alisema ili kuepuka vurugu ni
kuhakikisha sheria zinafuatwa.
Alisema ili kufuatwa sheria lazima
wanasiasa wajenge utamaduni wa
kuwa wakweli kwa wafuasi wao.
“Ushindani siyo vita wala uhasama
lakini inaonyesha kundi la vijana
limekosa uvumilivu na walitakiwa
kuelimishwa ukweli, watambue itikadi
zao haziwezi kuwa zaidi ya maslahi au
amani ya Taifa,” alisema Profesa
Mpangalla.
Uwazi wa NEC
Kwa upande wake, Profesa
Mohammed Bakari kutoka Idara ya
Sayansi ya Siasa, Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam(UDSM), alitaja jambo
jingine linaloweza kunusuru amani ni
uwazi wakati wa shughuli za NEC.
Alifafanua kuwa licha ya vyombo vya
dola kujitahidi katika ulinzi, wafuasi
wa vyama vya siasa wanakosa imani
na NEC baada ya kuwazuia wasisubiri
matokeo ya uchaguzi mita 200 kutoka
vituoni, suala ambalo ni tofauti na
maelekezo ya sheria inayowataka
kukaa umbali wa mita 200 kutoka
kituoni.
“Mwaka 2010 walijikusanya kusubiri
kura na waliondoka wakiwa
wameridhika na matokeo lakini kwa
nini NEC izuie na kauli ya Rais
inatumika kama agizo la Amiri Jeshi
Mkuu, kwa hivyo dola lazima itekeleze
wakati kauli zake nyingine
zimeonyesha upendeleo kwa chama
chake, hii ni hatari sana,” alisema.
Vijana waepuke kutumika
Mwenyekiti wa Mtandao wa
Wanawake nchini, Profesa Ruth Meena
aliwataka vijana kuepuka kutolewa
kafara na wanasiasa wenye maslahi
yao ya kuelekea Ikulu.
“Burundi ilipochafuka kina mama,
watoto na vijana ndiyo walioanza
kuumia na machafuko lakini viongozi
walikuwa kwenye ulinzi mkali kwa
hivyo lazima vijana wajitambue itikadi
zao haziwezi kuwa zaidi ya maisha
yao,” alisema.
“Lakini pia wanasiasa wote lazima
wajiandae kupokea matokeo, hakuna
aliyeshinda au aliyeshindwa hadi sasa
na uchaguzi ni sawa na mchezo wa
soka kwani lazima kuna mmoja
atashindwa na mwingine kushinda.”
Vyombo vya habari kutenda haki
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za
Kiislamu Tanzania, Sheikh Rajabu
Katimba alisema mbali na tahadhari
hiyo, Rais hatakiwi kutoa matamko
yanayokinzana na sheria zilizopo huku
vyombo vya habari vikitakiwa kutenda
haki.
“Kama ni haki ya kisheria kulinda kura
umbali wa mita 200 basi Rais Kikwete
anatakiwa kuheshimu hilo na
wananchi watamwelewa.”
“Lakini pia NEC inatakiwa
kuheshimiwa kwa sheria
inazosimamia, wafuasi wa vyama na
wagombea kujiepusha na kauli
zinazovunja sheria za uchaguzi na
mwisho kabisa vyombo vya habari
vitende haki katika kuripoti habari
zake,”alisema Katimba.

Jumatatu, 5 Oktoba 2015

Jifunze kinanda hapa mfano moyo funguka as written by wasonga mrombo


Moyo wangu funguka solfa on piano play try now...

Rais Kikwete ateua


Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete
Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete
amewateua wakuu wapya 13 wa wilaya
na kuwahamisha vituo vya kazi
wengine saba.
Walioteuliwa ni Shaaban Ntanambe
ambaye anakwenda Chato; Thabisa
Mwalapwa (Hanang), Richard
Kasesera (Iringa), Ruth Msafiri
(Kibondo) na Abdallah Njwayo
(Kilwa).
Wengine ni Asumpta Mshama
(Wanging’ombe), Mohammed Utaly
(Mpwapwa), Dauda Yasin (Makete),
Honorata Chitanda (Ngara), Vita
Kawawa (Kahama), Christopher
Ng’ubyagai (Mkalama), Hawa
Ng’humbi (Kishapu) na Mrisho Gambo
(Uvinza).
Wakuu wa wilaya waliohamishwa vituo
vya kazi ni Fadhili Nkurlu ambaye
anatoka Mkalama, kwenda Wilaya ya
Arusha, Wilson Nkambaku
anahamishiwa Arumeru, kutoka
Kishapu, Francis Miti ambaye
anahama Hanang kwenda Monduli na
Jowika Kasunga ambaye anahamia
Mufindi kutoka Monduli.
Wengine waliohamishwa ni Muhingo
Rweyemamu kutoka Makete kwenda
Morogoro; Hadija Nyembo anayehamia
Kaliua kutoka Uvinza na Benson
Mpesya ambaye anahamia Songea
Ruvuma kutoka Kahama.