other blog

Jumatatu, 26 Desemba 2016

MDADA AFARIKI GAFLA KANISANI ROMBO AKIWA ANAPAMBA KANISANI..

kwenye picha ni mdada aliyefariki gafla baada ya kuanguka juu ya jukwaaa kanisani mdada

aliyetambulikana kwa jina la CATHERIN ELIGI MANG'ORO alianguka kwenye aliteleza na kuanguka kwenye jukwaaa wakati akiwa anapamba jukwaa kwa ajili ya misa takatifu ya christmass.. dada huyo alipata ajali hiyo katika kigango cha kwamaksau kilichopo PAROKIA YA KENI ....ROMBO MKOANI KILLIMANJARO..

wadau walisaidiana ili kukimbiza hospitalini lakini huhudi zao pamoja na daktari hazikuzaa matunda.. DADA CATHERIN ametuachia pengo kubwa alikuwa mhitimu wa chuo kikuu msubiri ajira pasipo hata kufarahia matunda ya elimu yake mungu kamuita kwenda kumuandalia makao huko mbinguni.. tunaamini dada yetu aliaga akiwa anafanya  kazi ya kanisa basi na mbinguni ataendelea na kazi hiyohiyo ya kumsifu mungu..

tuliobaki mim na ww tumkumbuke mungu kila wakati kwani hatujui saa wa siku atakayojuja mwana wa mungu tumsifu mungu daima hekaluni

DADA YETU CATHERIN TULIKUPENDA ILA MUNGU KAKUPENDA ZAIDI ..MUNGU AKUREHEMU UPUMZIKE KWA AMANI.         AMINA

Alhamisi, 22 Desemba 2016

Ndalichako asitisha ajira za waalimu wa sanaa yaani arts kwa ngazi ya sekondari kama ulikuwa unasubiria ajira mkuu anza kufanya vitu vingine.

WAZIRI wa Elimu, Sayansi,
Teknolojia na Ufundi,
Profesa Joyce Ndalichako,
ametoa masharti mapya ya
ajira za ualimu nchini, huku
akisema Serikali haitaajiri
walimu wa masomo ya sanaa
(arts) kwa kuwa wapo wa
kutosha.

Akizungumza mjini Dodoma
jana wakati akifungua
mkutano mkuu wa mwaka wa
Wakuu wa Shule za Sekondari
Tanzania (TAHOSSA), Profesa
Ndalichako, alisema Serikali
kwa sasa haiwezi kuajiri
walimu wa masomo hayo
kwa kuwa inataka kuajiri
walimu wa masomo ya
sayansi na hisabati ambao
idadi yao ni ndogo.
“Pamoja na uamuzi huo mpya,
ajira za walimu wapya wa
masomo ya sayansi nazo
zimebadilika kwani wale wote
waliohitimu ualimu wa sayansi
na hisabati, wanatakiwa
watume vyeti vyao kabla ya
kupangiwa kituo cha kazi.
Kuhusu wale walimu wa
‘arts’, kule tuna walimu wa
ziada ambao tutajaribu
kuwapanga kutokana na shule,
kwani wengi walikuwa
wamepangwa shule moja.
Kwahiyo, tutaangalia utaratibu
wa kuwapanga kulingana na
mahitaji,’’ alisema Profesa
Ndalichako.
Akizungumzia suala la ubora
wa elimu nchini, Profesa
Ndalichako aliwataka walimu
wakuu hao kuhakikisha
wanasimamia ubora wa
elimu kwa kuwa wao ndio
wanaowaandaa wanafunzi
kabla hawajaenda vyuoni.
“Vilevile pelekeni takwimu
sahihi za wanafunzi waliopo
katika shule zenu kuisaidia
Serikali katika kupanga bajeti ili
iweze kutoa fedha sahihi.
“Hapa kuna kimbembe, yaani
wakati mwingine huwa
najifanya nimepoteza takwimu
ya shule fulani, nikiziomba na
kutumiwa, zinakuwa ni tofauti
na zile za mwanzo.
“Hili nawaomba mkalisimamie
ili iwe rahisi kwetu kupanga
bajeti yenye tija,’’ alisema.
Kuhusu ujenzi wa maabara
katika shule za sekondari,
waziri huyo alisema kwamba
kutokana na nyingi
kukamilika, Serikali itatoa
vifaa vya maabara kuanzia
Januari mwakani baada ya
kuwa vimeingia nchini
kutoka vilikoagizwa.
Awali, akisoma risala ya
walimu hao, Rais wa
TAHOSSA, Bonus Nyimbo,
aliiomba Serikali itoe waraka
wa kupiga marufuku
matumizi ya simu kwa
wanafunzi shuleni kwa kuwa
zimekuwa zikichangia
kushuka kwa ufaulu kwa
baadhi ya wanafunzi.
“Ili kuboresha elimu,
tunaiomba Serikali itoe waraka
wa kupiga marufuku matumizi
ya simu kwa wanafunzi kwani
simu nyingi tunazozikamata
tunakuta mule hakuna
taaluma,’’ alisema Nyimbo.
Kwa upande wake,
Mkurugenzi wa Global
Education Link, Abdulmalik
Molel, ambaye pia kampuni
yake ilipewa tuzo ya heshima
katika kuendeleza elimu
nchini, alisema ni jukumu la
kila mmoja kutimiza wajibu
wake ili kuiendeleza elimu ya
Tanzania.
“Kila mmoja anapaswa
kutimiza wajibu, wazazi,
walezi na walimu, waambieni
wanafunzi wasiwe na
‘expectation’ (matarajio)
makubwa kwani wanapokuwa
na matarajio hayo, wakienda
vyuo vikuu wanakuwa
wasumbufu,” alisema.
Wakati hayo yakiendelea, juzi
taarifa ilitolewa jijini Dar es
Salaam na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Elimu, Sayansi,
Teknolojia na Ufundi,
Maimuna Tarishi, ikisema
kwamba, walimu wahitimu
wa masomo ya sayansi na
hisabati waliohitimu shahada
na astashahada mwaka 2015,
wanatakiwa kuwasilisha
nakala za vyeti vya elimu ya
sekondari vya kidato cha nne
na sita na taaluma ya ualimu
kwa uhakiki.
Pamoja na hayo, hivi
karibuni Serikali ilitangaza
kusitisha ajira zote nchini ili
kukabiliana na wimbi la
watumishi hewa.
Sambamba na uamuzi huo,
nyongeza za mishahara kwa
watumishi wa Serikali nazo
zilisimamishwa ili
kukabiliana na watumishi
hao hewa ambao walikuwa

Imeandaliwa na ben mrosso kutoka dodoma

Jumatatu, 19 Desemba 2016

Chuo cha serikali za mitaa kimetoa harufu ya ufisadi wa ngono....Waziri ataka Bodi Chuo cha Serikali za Mitaa kushughulikia malalamiko

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), Mhe.George Simbachawene, ameiagiza bodi ya chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo mkoani Dodoma (LGTI), kuyafanyia kazi malalamiko ya vitendo vya rushwa ya ngono katika idara ya taaluma na mitihani. Mhe.Simbachawene ametoa agizo hilo tarehe 25 Novemba, 2016, wakati alipokuwa akizungumza na wanafunzi pamoja na uongozi wa chuo hicho wakati wa mahafali ya nane ya chuo hicho. Amesema katika moja ya maeneo ambayo hajaridhishwa nayo, idara ya mitihani ambayo imekuwa ikilalamikiwa na wanafunzi juu ya urasimu uliopo hasa wakati wa wanafunzi wanapo hitaji matokeo yao. Aidha, Waziri Simbachawene amesema malalamiko mengi yamekuwa katika idara hiyo kwa kipindi kirefu lakini uongozo wa chuo hicho umeendelea kulikalia kimya bila kuchukua hatua. "Naiagiza bodi ya chuo kuhakikisha kuwa idara hii inachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kuifumua na kuiunda upya kwani malalamiko haya yamekuwa ya muda mrefu watu wanaohusika na idara hii wamekuwa na ukilitimba wa hali ya juu mwanafunzi anapotaka kupata matokeo ya mitihani yake ni atazungushwa kama nini," amesema Mhe.Simbachawene. Amesema hali hiyo imekuwa ikiashiria uwepo wa vitendo vya rushwa mbaya ya ngono kati ya wahusika wa idara ya mitihani na wanafunzi wa kike lakini pia wanafunzi wa kiume kudaiwa fedha. "Naomba mlifanyie kazi suala hili haraka sana kwani haya malalamiko mimi ninayo kwa mda mrefu lakini na shangaa uongozi mmekaa kimya hali ambayo imefikia hatua hata kama mwanafunzi kalipia ada ya hosteli lakini bado atazungushwa hadi muhusika mwentee apende utazani anaomba bure,"amesema. Aidha aliongeza kuwa kitu kingine ambacho anautaka uongozi wa chuo hicho kukifanyia kazi ni namna ya matumizi ya fedha za chuo kwani kumekuwepo na upotevu wa fedha lakini hakuna hatua zilizochukuliwa kwa waliohusika. "Fedha za chuo zimeibiwa na wahusika wapo hadi hii leo lakini hakuna kilichuuliwa naomba wahusika wasimamishwe haraka ili uchuguzi ufanyike na hatua zingine kuchukuliwa kwa wahusika," alisema. Hata hivyo amesema kuwa kuna kila sababu ya serikali kutengeneza utaratibu ambao utakuwa unatumika katika kuwaajili wanafunzi wanaomaliza katika chuo hicho ambao wanataaluma ya utumishi katika mamlaka za serikali a mitaa. "Serikali inatumia takribani bilioni 8.3 kwajili ya kuendesa chuo hichi kilamwaka lakini wanafunzi wanapotoka hapa wanakosa kazi hali ambayo si sahihi kutokana na uwezkezaji huo unaofanywa na serikali kwa mwaka kwani hata ujenzi wa chuo hiki umeghalimu sh. bilioni 36.5 hivyo ni lazimu wahitimu hawa tuwatumie ipasavyo,"alisema Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya chuo hicho Prof. Suleiman Ngware alisema kuwa maagizo yote yaliyotolewa na Waziri atayafanyika kazi haraka iwezekanvyo na wahusika wote watachukuliwa hatua. "Mheshimiwa Waziri yote uliyoagiza tutayafanyia kazi na hatua kali zitachuliwa kwa wahusika wote bila ya kumuonea mtu," amesema Prof. Ngware.

Ijumaa, 16 Desemba 2016

Serekali inajua alipo ben saanane.. Lisu aomba watumie vyombo vyao vya ulinzi kumsaka.. CCM ni lini mtatupa uhuru.. We want lema alive.. And max wa jf akiwa huru....tumechoka

Mwanasheria Mkuu wa Chadema,
Tundu Lissu, akizungumza na
waandishi wa habari, Dar es Salaam
jana kuhusu kupotea kwa msaidizi
wa mwenyekiti wa chama hicho, Ben
Saanane. Kulia ni Ofi sa Habari,
Tumaini Makene na Katibu Mkuu
wa Baraza la Vijana (Bavicha), Julius
Mwita.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka Serikali kutumia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kumtafuta msaidizi wa mwenyekiti wa chama hicho, Bernard Saanane , ambaye ametoweka katika mazingira ya kutatanisha zaidi ya mwezi mmoja sasa. Chadema imesema Serikali ndiyo yenye uwezo pekee wa kiufundi kujua na kuamuru mashirika ya simu kueleza mawasiliano yake ya mwisho yalivyokuwa. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema katika siku za karibuni, Saanane amekuwa akiongoza kampeni kwenye mitandao ya kijamii, kuhusu kuhakikiwa kwa shahada za uzamivu (PhD) kwa baadhi ya viongozi. Mwanasheria huyo wa Chadema, alisema wakati fulani Saanane alitumiwa ujumbe wa maneno kupitia simu yake ya kiganjani akitishiwa kuacha kuikosoa Serikali. “Nanukuu maneno aliyotumiwa: “Ben Saanane unachokitafuta ndani ya Serikali hii utakipata, kwa elimu na uwezo wako hatukutarajia ungefikia hatua ya ajabu kwa namna ulivyofikia, hujiulizi kwanini upo huru hadi muda huu. “You are too young to die. Tunajua utaandika na hili, andika lakini the next post hutaandika ukiwa na uhuru wa kutosha, andika but your days are numbered. “Unajua kuna rafiki yako alipuuza na hutaki kuandika kuhusu yeye, labda kwa kuwa alitangulia, andika Ben, andika sana, ongea, sema lakini utajikuta mwenyewe na chatu,” alinukuu Lissu. Alisema: “Katika miezi ya hivi karibuni watu ambao wamekuwa wakiikosoa Serikali kupitia mitandao ya kijamii wamekuwa wakikamatwa na watwambie kama wanamshikilia Ben Saanane ili tujue. “Serikali ndiyo yenye udhibiti wa mipaka yetu kuanzia baharini, nchi kavu, mipaka yetu ya anga na hata katika bandari, hivyo ituambie,” alisema Lissu. Aidha mbunge huyo wa Singida Mashariki alisema yeyote anayefahamu taarifa za Saanane azitoe hadharani katika vyombo vya habari, polisi na hata katika vyombo vingine vya Serikali. Aidha Lissu alisema taarifa za kupotea kwa Saanane wamezifikisha ngazi za kimataifa na wataendelea kuzisambaza ili dunia nzima ijue. Akizungumzia kuhusu taarifa ambayo imesambaa katika mitandao ya kijamii kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe anajua aliko Saanane, alisema: “Mara ya mwisho Ben amewasiliana na mwenyekiti Novemba 14 mwaka huu akiwa Dodoma na huwa hawaongozani, bali Ben anafanyia kazi zake makao makuu ya chama.”

Jumatatu, 12 Desemba 2016

Nafazi za kazi serikalin wizara ya afya. Jinsia wazee walemavu na watoto.. Omba mapema...

NAFASI YA KAZI WIZARA YA
AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA , WAZEE NA WATOTO
Wizara YA Afya , Maendeleo
ya Jamii, JiNSIA , Wazee , na
Watoto imepeta kibali cha
mpango wa ajira ya dharula
kwa wataalamu wa fani za
tabibu na wauguzi mpango
huu utaendeshwa chini ya
mradi kwa ufadhili wa fedha
mfuko wa cdc, award no.
5U2GGHOO1062-03
kwa muda wa miaka miwili
mradi utaajiri watumishi
m192 ambao watafanya kazi
katika wilaya mbalimbali
zenye uhaba wa watumishi
wa kutoa huduma za afya
hasa kwa waathirika wa
wenye virus ivy UKIMWI .
watumishi hawa watalipwa
mshahara na stahiki nyingine
kwa kufuata tarabitu na
kanuni za serikali. Watumishi
wanao takiwa ni
- TABIBU
WASAIDIZI
(NAFASI 95)
wenye ngazi ya
astashahada
(CERTIFICATE IN
CLINICAL
MEDICAL)
- WAUGUZI
(nafasi 97 )
wenye ngazi ya
astashahada
(CERTIFICATE IN
NURSING AND
MIDIWIFERY)
Wizara inakaribisha maombi
ya kazi kutoka kwa
watanzania wenye sifa
zilizotajwa hapo juu , wawe n
vitu vifuatavyo
- Cheti cha
kumaliza  kidato
cha nne
- Cheti cha
taaluma
aliyosomea
kutoka kwenye
chuo
kinachotambulika
na serikali
barua ya
maombi
ionyeshe wilaya
unayotaka
kupangiwa
- Maombi
yatumwe kwa
KATIBU MKUU,
WIZARA YA AFYA,
MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, NA WATOTO,
6 SAMORAL MACHEL
AVENUE,
S.L.P 9083
11478, DAR ES SALAAM,
TANZANIA.
ORODHA YA HALMASHAURI
ZA WILAYA NA IDADI YA
WATUMISHI
WALIOPENDEKEZWA
ARUSHA
NA MKOA HALMASHAURI TABIBU WAUGUZI JUMLA
1 arusha Arusha CC 3 3 6
2 dar es salaam Ilala MC 3 3 6
Temeke MC 3 3 6
Kinondoni MC 3 3 6
3 dodoma dodoma MC 2 3 5
4 geita Geita DC 2 2 4
5 iringa mufindi DC 3 3 6
Iringa MC 2 2 4
6 kagera bukoba DC 3 3 6
Muleba DC 2 2 4
7 kigoma Kigma Ujiji MC 2 3 5
8. Kilimanjaro Moshi Dc 3 3 6
9i Lindi Lindi DC 2 2 4
10 Mara Musoms DC 2 2 4
Rorya DC 2 2 4
11 Mbeya Chunya DC 2 2 4
Kyela Dc 3 3 6
Mbarali DC 2 2 4
Mbeya DC 3 3 6
Mbozi DC 2 2 4
Rungwe DC 2 2 4
12 Morogoro Morogoro DC 3 3 6
13 Mwanza Nyamagana DC 3 3 6
Sengerema DC 2 2 4
14 Njombe Njombe DC 2 2 4
Wang’ing’ombe DC 2 2 4
15 Rukwa Sumbawanga DC 2 2 4
Sumbawanga MC 2 2 4
16 Ruvuma Mbinga DC 2 2 4
Songea MC 2 2 4
17 Shinyanga Kahama DC 3 3 6
Shinyanga MC 2 2 4
18 Tabora Igunga DC 2 2 4
Ndega DC 2 2 4
Tabora MC 3 3 6
19 Tanga

Jumamosi, 5 Novemba 2016

Joyce ndelchako afumuka makubwa kuhusu bodi ya mkopo na aamuru kuwa wote walioomba mkopo wapatiwe. shuka nayo hii..

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya
Juu (HELSB), imeagizwa
kuhakikisha kuwa fedha zote
zilizotengwa kwa ajili ya
mikopo ya wanafunzi
wanaoendelea na masomo
zinapelekwa vyuoni ifikapo
leo.
Agizo hilo lilitolewa bungeni
jana na Waziri wa Elimu,
Sayansi, Teknolojia na Ufundi,
Profesa Joyce Ndalichako
baada ya wabunge mbalimbali
kuomba miongozo kwa Spika
kuhusu kuwapo kwa wanafunzi
wengi waliokosa mikopo kwa
mwaka wa fedha 2016/17.
Mwongozo kwa Spika ulitiliwa
mkazo na Mbunge wa Chalinze
(CCM), Ridhiwan Kikwete
aliyeeleza kuwapo taarifa
kutoka Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM) kuwa
wanafunzi wanataka kugoma
kwa kukosa fedha za mikopo.
Kutokana na miongozo hiyo,
Mwenyekiti wa Bunge, Najma
Giga aliitaka Serikali kutoa
maelezo.
Akitoa kauli ya Serikali, Profesa
Ndalichako alisema fedha za
mikopo kwa ajili ya wanafunzi
zilikwenda vyuoni wiki moja
iliyopita.
“Tatizo lililotokea kwa UDSM
sijui kama walidanganyana au
la lakini hawakujaza fomu.
Serikali haitatoa mkopo kwa
mwanafunzi ambaye hajajaza
fomu. Na waliosaini leo
wataingiziwa fedha zao kwenye
akaunti na vyuo,” alisema.
Kuhusu wanaoendelea na
masomo, Profesa Ndalichako
alisema wanafunzi wote
wanufaika na wanaoendelea na
masomo wataendelea kupatiwa
mikopo kama ilivyokuwa
mwaka uliopita.
Alisema wanafunzi ambao
vyuo vyao vimewasilisha HELSB
taarifa za matokeo, Bodi
imekwishawatumia fedha
vyuoni kwa ajili ya kuwapa
mikopo wanafunzi hao.
Hata hivyo, alisema taratibu za
kuwabaini wanafunzi wenye
sifa zinaendelea na wasio na
sifa wataendelea kuondolewa
kupata mikopo.
Pia, alikiri kuwa ucheleweshaji
wa matokeo ya wanafunzi
wanaoendelea na masomo
umeathiri kasi ya kutuma fedha
vyuoni.
“Wizara yangu imekwishaagiza
vyuo vyote ambavyo
havijawasilisha matokeo ya
mitihani ya wanafunzi wao kwa
mwaka wa masomo uliopita,
kufanya hivyo mara
moja,” alisema.
Ndalichako alisema hadi
kufikia Novemba 3 mwaka huu,
Sh71.042 bilioni
zilikwishatumwa vyuoni kwa
ajili ya wanafunzi wa mwaka
wa kwanza na wanaoendelea
na masomo.
Akizungumzia utoaji wa
mikopo kwa mwaka wa fedha
2016/17, Ndalichako alisema
katika mwaka huo, Sh483
bilioni zimetengwa na
zimelenga kutoa mikopo kwa
wanafunzi 119,012, wanafunzi
93,295 wanaoendelea na
masomo na wa mwaka wa
kwanza 25,717.
Ndalichako alisema katika
mwaka wa fedha 2016/17
wanafunzi 58,010 walidahiliwa
na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU)
na orodha yao iliwasilishwa
HELSB na hadi Novemba 2,
mwaka huu, wanafunzi 21,190
wa mwaka wa kwanza
wamepewa fedha. Kati yao
4,321 ni yatima, 118 wenye
ulemavu na 87 ni waliosoma
sekondari kwa ufadhili wa
taasisi mbalimbali.

Jumapili, 4 Septemba 2016

mh.... hi ni hatari. CCM watashia kuanzisha ukuta .. Nimeamin kwamba wapinzani ndo mafisadi wakubwa... Hongera magufuli.

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameingia katika mzozo mkubwa na Rais John Magufuli, na sasa wameanza Job Ndugai, kumlazimisha Spika wa Bunge, awanusuru, MwanaHALISI linaweza kueleza.
Habari kutoka Ikulu, Ofisi ya Spika na Kamati ya Wabunge wa CCM, zinasema wabunge hao wamejiapiza kuwa Ndugai na Rais Magufuli wamekalia moto.
Sababu kuu inayotajwa ni hatua ya serikali, kwa amri ya Rais Magufuli, kuhoji na kufikisha mahakamani baadhi ya wabunge wa CCM wanaotuhumiwa kuomba rushwa kutoka kwa taasisi wanazosimamia.
Wabunge wa CCM waliofikishwa mahakamani ni Kangi Lugola (Mwibara), Victor Mwambalaswa (Lupa), na Suleiman Sadiq (Mvomero). Wanatuhumiwa kwa kwa kosa la kuomba rushwa ya milioni 30 kutoka kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Gairo ili wampendele katika kukagua hesabu za halmashauri yake mwaka 2015/16.
Mwingine ni Richard Ndassa (Sumve), ambaye anatuhumiwa kwa  kushawishi na kuomba rushwa ya Tsh 30 milioni kutoka kwa Felchesmi Mramba, Mtendaji Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  ili amsaidie kuwashawishi wajumbe wengine wa Kamati ya Mtaji na Uwekezaji kupitisha bila kipingamizi taarifa ya TANESCO kwa mwaka 2015/2016.
Taarifa zinasema kuwa hadi Ijumaa iliyopita, Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) ilikuwa imehoji wabunge wengine 18 wa CCM, na ilikuwa imeshakamilisha taratibu zote za kuwafikisha mahakamani.
Miongoni mwa wabunge hao ni Martha Mlata (Viti Maalumu), Raphael Chegeni (Busega), Margareth Sitta (Urambo Mashariki), Mary Mwanjelwa (Viti Maalumu), Edwin Sanga (Kondoa Mjini). Majina mengine hayakupatikana hadi tunakwenda mitamboni.
Baada ya taarifa za kufikishwa mahakamani wabunge hao kuanza kuenea, kundi la wabunge wa CCM linadaiwa kumzonga Ndugai, wakimtaka awasimamie wabunge wa chama chake, asiruhusu wadhalilishwe.
Watoa habari wetu wanasema wabunge walimweleza Ndugai kuwa kitendo cha serikali kudhalilisha wabunge wa CCM kitaondoa umoja wao wa kutetea serikali, na kitaathiri msimamo wao katika umoja wa wabunge wa chama chao.
“Mweleze rais asitudhalilishe, sisi ni wabunge wa chama chake; asitafute sifa zake peke yake,” mbunge mmoja kijana alinukuliwa akimweleza Ndugai.
Kabla hata Ndugai hajawasiliana na rais kuhusu hoja za wabunge, taarifa zinasema rais mwenyewe alipata taarifa hizo kutoka kwa “vijana wake” ndani ya wabunge hao.
Mtoa habari kutoka Ikulu ameeleza gazeti hili kuwa Rais alipompigia simu Ndugai alizungumza kwa ukali, “hiyo ni mijizi, acha ifungwe tu.”
Gazeti hili lilipohitaji ufafanuzi wa Ndugai kuhusu masuala haya alithibitisha kuwa wabunge wake  wameshahojiwa na TAKUKURU, lakini akagoma kusema alichoambiwa na rais.
“Ni kweli kuna wabunge 18 wameshahojiwa na Takukuru. Hata hivyo, tumeshindwa kuwa na maelezo ya pamoja kwa kuwa kuna wengine wameitwa kama mashahidi, na wengine wamehojiwa kama watuhumiwa,” Alisema.
Alisema kilichotokea ni kwamba wabunge hao wamekuwa wanaitwa kwa nyakati tofauti, kwa sababu tofauti. “Mwingine anaitwa leo anahojiwa kwa tuhuma, mwingine anaitwa kesho kwa ushahidi pengine baada ya kutajwa na mwenzake,” alidokeza.
Baadhi ya wabunge wa CCM wameliambia gazeti hili kuwa kuna kesi zinatengenezwa kisiasa, hivyo wanajipa muda kuliweka sawa suala la tuhuma zinazowakabili.
Hata hivyo, taarifa zinasema wabunge wameikamia serikali, na wengi wao wanajiapiza kuunga mkono hoja za wapinzani kama namna ya kumkomoa Rais Magufuli.
Taarifa hizo hizo zinasema rais mwenyewe baada ya kusikia vitisho vya wabunge wa CCM, amemwambia Ndugai, “kama watatunisha misuli nitavunja bunge, turudi kwenye uchaguzi, tuone watarudi wangapi miongoni mwao.”
Taarifa hizi zinakuja ikiwa ni wiki moja tangu Spika kuahidi kuwa suala hilo litazungumzwa vizuri ndani ya Bunge kwa kuzingatia kanuni wala si mtaani. Source ni mwanahalisi..

Jumatano, 3 Agosti 2016

Mashirika ya kitawa kwa wote mnaotaka kuwa watawa

karibuni wote mjiunge na utawa maisha matakatifu ni maisha ya kazi na sala wanaotaka kuwa mabruda ... waandike barua kwa anuani ifuatayo mkurugenzi , scim brothers, s.l.p 29 Tosamaganga, Iringa. kumbuka kigezo uwe tu hujaoa na pia uwe umehitimu kidato cha nne. pia lipo shirika la mtakatifu carmel lilopo bunju kwa  malezi ya kipadre wote wenye nia mnaombwa kutuma maombi yenu kwa mkurugenzi tz kwa mawasiliano zaidi watumie email carmelitestz@gmail.com na Kwa upande wa masisita soma kibandiko cha mtakatifu consolata missionery kwa malezi ya kisista yaani utawa wa kwanza na pia shirika la mtakatifu charles borromeo

kumbuka mabruda na masista lazima uwe mhitimu wa kidato cha nne. pia uwe hujaoa wala hujazaaa  na kwa upande wa upadre lazima uwe mhitimu wa kidato cha sita na kufaulu uwezo wa kwenda chuo kikuuu ... karibuni utawani tujifunze maisha halisi ya bwana wetu yesu kristo.. Tumsifu yesu kristo .... kwa maelezo zaidi usisite kunipigia simu 0743719830

Alhamisi, 9 Juni 2016

UMMA KUHUSU KUFUNGWA KWA MUDA WA KUPOKEA MAOMBI YA UDAHILI WA KOZI ZA CHETI, DIPLOMA, DIPLOMA YA JUU NA SHAHADA YA KWANZA KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) UNAORATIBIWA NA BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)

 
Tarehe 3 Juni 2016 ilikuwa siku ya mwisho ya kuwasilisha maombi ya udahili wa kozi za Cheti, Diploma, Diploma ya Juu na Shahada ya Kwanza kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) unaoratibiwa na NACTE.
Baraza linapenda kuwaarifu waombaji udahili wa kozi tajwa hapo juu na umma kwa ujumla kuwa, kwa sasa maombi yote yaliyowasilishwa mpaka tarehe 3 Juni 2016 saa sita usiku yameanza kuchambuliwa kwa ajili ya kuchagua waombaji wenye sifa stahiki. Zoezi la kuchambua waombaji udahili na hatimaye kuchagua waombaji wenye sifa stahiki na waombaji hao kuidhinishwa na mamlaka husika na kutangazwa litachukua muda wa wiki nne (4) kuanzia tarehe 3 Juni, 2016.
Baraza linatambua uwepo wa waombaji wapya na baadhi ya waombaji walioshindwa kuwasilisha maombi yao kupitia mtandao ilipofika tarehe 3 Juni 2016. Waombaji wa namna hii na wengine wanaopanga kuwasilisha maombi yao kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) wanaombwa kuwa na subira mpaka hapo majina ya waombaji waliowasilisha maombi yao kabla ya kufungwa kwa mfumo watakapotangazwa.
Baada ya kutangazwa majina ya waombaji waliochaguliwa, Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) utafunguliwa tena kwa ajili ya kujaza nafasi za udahili ambazo zitakuwa hazijajazwa na waombaji waliowasilisha maombi yao kuanzia tarehe 4 Machi, 2016 hadi tarehe 3 Juni 2016.
Baraza linatarajia kufungua tena Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) kwa ajili ya kozi za Cheti, Diploma, Diploma ya Juu na Shahada ya Kwanza wiki ya mwishoni mwa mwezi wa Sita, 2016.
Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
NACTE
Tarehe: 9 Juni, 2016

Jumapili, 29 Mei 2016

AJALI MBAYA YATOKEA MAKERERE BARABARA YA KUSHUKA MWIKA ILIYOHUSISHA NOA ITOKAYO TARAKEA KWENDA MOSHI





Mungu ibariki Tanzania mungu iokoe Tanzania .. yatupasa kutubu kila wasaa maana hatujui siku wala saa kitakapo tokea kiama.. AJALI HIYO HAIKUPONYESHA HATA MMOJA WOTE KUMI NA TANO WALIKUFA WENGI WAKIWA NI WA TARAKEA.. CHANZO CHA AJALI HIYO INASEMEKANA KUWA NI HITILAFU YA GARI ILIPOFELI BREAK NA KUSABABISHA KUACHA NJIA NA KUPINDUKA MARA KADHAA .. WALIOSHUHUDIA AJALI HIYO WANASEMA KUWA ABIRIA KUMI NA MBILI WALIAGA DUNIA PAPO HAPO NA WENGINE WATATU WALIFIA KCMC ... YA MUNGU NI MENGI SIFA NA UTUKUFU ZIRUDI KWAKE .. YEYE NDIYE MUUMBA ..YEYE NDO ANACHUKUA APEWE SIFA MILELE...ROHO ZA MAREHEMU WOTE WAPATE REHEMA KWA MUNGU WAPUMZIKE KWA AMANI.

Jumatano, 18 Mei 2016

Marketers, Project Manager, Teachers

Nafasi za kazi ardhi chuo kikuu.. Omba sasa



VACANCY ANNOUNCEMENT
Ardhi University has vacant position in
the Administrative cadre.
The University subscribes to the policy
of an equal opportunity employer and
therefore invites applications from
candidates who are interested to work
in a thriving University environment
and have the requisite skills,
Qualifications and experience for
various positions as indicated below;
Job Title: Insurance Manager (1
Post) Re -advertised)
Required Qualifications:
• Holder of first Degree / Advanced
Diploma in Insurance or a
• Diploma in Business Field plus a
Certificate in Insurance or any other
recognized professional
Insurance qualifications. AND 3 years
post qualification experience in the
Insurance Industry at,
managerial or executive position.
Duties
i. To run a department for handling
Insurance business at Ardhi
University.
ii. To develop competitive quotes, to
prompt of documents promptly, and
proper advice at
the time of claims.
iii. To maintain follow-ups of claims of
their prompt settlement by Insurance.
iv. To develop and nurse relationship
with clients through, physical visits
and various
communication platform.
v. To enhance public awareness of the
Agency through various
communication strategies.
vi. To build support with Institutions in
Tanzania in order to have their
Insurance routed
through ARU’S Insurance Agency.
vii. To maintain an accurate and
complete customer database and
networking with
construction firms in order to solicit
business on engineering for ARU’S
Insurance
Agency.
Duty Station for the advertised post is
Dar es salaam.
GENERAL REQUIREMENTS FOR ALL
APPLICANTS
1. All academic awards should be
from recognized Universities and
Institutions.
2. All applicants with certificates from
foreign Universities should have the
certificates verified by the Tanzania
Commission for Universities (TCU)
3. All applicants must submit signed
application letters accompanied with
the following:
i) Copies of relevant academic and
professional certificates;
ii) Three names and complete
addresses of referees;
2iii) Current CV
4. Age limit: Not above 35 years
5. Applications should reach the
University by using the address below
not later than 5Th May, 2016.
6. Only short-listed applicants will be
contacted.
7. Those applied during the first
advertisement need not to apply
APPLICATION INSTRUCTIONS:
Interested applicants should submit
their applications to the undersigned:
The Deputy Vice Chancellor
(Planning, Finance and
Administration)
Ardhi University
P.O. Box 35176
DAR ES SALAAM

Jumatatu, 25 Aprili 2016

Hatimaye nothern highland teachers college yatoa wahitimu wa ualimu stashahada na astashahada ikiwa ni nahafali ya saba tangu kuanxishwa kwa chuo.






Wanao onekana kwenye picha ni wahitimu wa koxi mbalimbali xa ualimu chuo cha ualimu nothernhighland kilichopo moshi karibu kabisa na uwanja wa ndege moshi . Chuo hiki kinatoa mafunzo ya ualimu diploma ya msingi kwa waalimu ambao wapo kazini pamoja na mafunzi ya ualimu kwa wahitimu wa kidato cha nne wenye ufaulu wa division 3 au mwenye division 4 na amehitimu chuo kinachitambuliwa na serikali anaweza kujiunga na kozi hixo zs ualimu maombi yote yanapatikana hapa www.nacte.co.tz kisha chagua chuo bora cha northern highland kama chaguo la kwanza.. Ni chuo bora chenye bei nafuu na wAalimu mahiri.. Karibuni nyote.

Ijumaa, 8 Aprili 2016

Kimeta, kimeta, kimeta, chatishia Rombo chaua nane user na tarakea, nne kooti na sita mkuu...serikali itangaze tahadhari.


[image_2

Zinazoonekana hapo juu ni nyama za mbuzi ambazo tiyari zimeshaandaliwa kuuzwa kwa wakazi wa eneo la useri..


Leo ni siku ya tisa ambapo ugonjwa hatari wa wanyama ujulikanao kama kimeta kulaza watu wapatao 16.. nikifanya mahojiano ya moja kwa moja na wamama pamoja na wakazi waliothiriwa na ugonjwa huo wa tarakea na useri nawanukuu" tulinunua nyama ya ng'ombe ambayo tiyari ilishapimwa na madaktari na kusema aendelee kuuza lakini cha kushangaza tukasikia wengi waliotumia ile nyama wamekimbizwa hospitalini ilitubidi sis wenyewe tujihami kwa kukimbilia hospitalini na kupewa matibabu haraka na kupata nafuu ..huku tukiambiwa kuwa wenzetu wamekwisha fariki.. nililia sana na kuilaumu serikali kwa,nini watuletee madaktari feki wa mifugo.. bac tunaomba,serikali itangaze hali ya tahadhari ya kula, nyama kwani mpaka sasa sio serikali ya kijiji mpaka wilaya zote zimenyamaza tu. Serikali ituonee huruma.." walimalizia wakazi hao
Mpaka sasa inasemekana watu 16 wameaga dunia kwa kula nyama hiyo ya kimeta Rombo huku serikali ikijitahidi kupita kutangaza ukusanyaji na ulipaji wa kodi kila siku huku suala la kimeta likitupwa nje .. watalipa je kodi kama watakufa kimeta? Serikali piteni na mtangaze tahadhari ya kutokula nyama.. suala la madaktari kuna,wengine hatujui kama walilazimishwa kufanya kazi hiyo inakuwaje huyu anasema uza na mwingine anakuja anasema acha. Mimi nafungasha mikoba yangu na kuondoka kwani sina cha kuwasaidia labda tu taarifa zifike mahali husika maana hii nchi ina wenyewe .. imeandaliwa na wasonga mrombo kutoka wilayani rombo.