other blog

Alhamisi, 24 Septemba 2015

Njia bora na sahihi kwa vijana kujiwekea akiba kwa sababu ya maisha ya kesho..hii hapa..imeandaliwa na mwandishi wa rombo wasonga mrombo


Taifa lenye akiba ya kutosha na
uchumi imara linakuwa na uwezo
katika kujiletea maendeleo na hata
kustahimili majanga yoyote
yanapotokea. Nguvu hiyo inatokana na
uwezo mkubwa wa akiba na mtaji
iliyowekezwa kwenye miradi
mikubwa.
Mtu kuweka akiba, ni muhimu sana
kama vile ilivyo kwa taifa. Saikolojia ya
matumizi ya fedha inaonyesha kuwa
mtu hupenda kutumia sasa kuliko
kusubiri baadaye ambapo ingeongeza
faida na thamani zaidi.
Fedha ni kitu ambacho kipo tu kwa
muda kama mtu aliyekuwa nayo sasa
akishindwa kuidhibiti leo, kesho
hatakuwa nayo. Suala mtambuka hapa
ni je, kwa nini niweke akiba au
niwekeze kwa jambo lingine?
Ningependa nizungumzie juu ya njia
mbalimbali za kuweka akiba ambapo
zikitumika zinaweza kukuletea faida
kwa karne hii, japo kiuhalisia kwa
Waafrika kuweka fedha ni tatizo sugu
kwa walio wengi. Hali kama hii
inatokana na uwezo mdogo wa
kudhibiti fedha kwa mitindo ya kisasa
na kibiashara pia. Elimu juu ya jambo
hili haijafika au haijakaa vizuri katika
upande wa ubongo iliyo wazi kwa
mazingira ya hapa nchini.
Zipo njia ambazo ni nzuri zikitumika
kwa kuweka akiba kwa faida
zitaongeza maendeleo ya wengi. Njia
hizo ni:
Moja, ni kununua fedha za kigeni.
Mara nyingi fedha za kigeni mfano
Dola za Marekani, Euro, Pound ya
Uingereza na fedha kutoka Bara la Asia
kama vile za Saudi Arabia, huwa
zinapanda thamani ukilinganisha na za
Tanzania.
Mfano, ulinunua Dola moja ya
Marekani Novemba, mwaka jana kwa
Sh1,300. Mwaka huu unaiuza kwa
Sh2,100. Ukipiga hesabu umepata
faida ya Sh800. Kama ulinunua Dola
10,000, leo hii ikiziuza una faida ya
Sh1 milioni, na kadhalika.
Mtindo wa kununua dola kwanza
unapunguza kubeba lundo la fedha
nyingi, inakuzuia kuitumia bila
sababu, hivyo kuendelea kuwa akiba,
kukulinda na kukuwezesha uwe na
faida pale mfumuko wa bei
unapoongezeka na inaweza kukusaidia
iwapo itakulazimu usafiri nje ya nchi.
Ukisafiri nje ya nchi itakufanya
usitumie fedha nyingi za kununua za
kigeni kwa gharama kubwa.
Pili, ni simu benki. Huu ni mfumo
ambao upo sana siku hizi eneo la
Afrika Mashariki. Siku hizi kampuni za
simu zimewezesha mtu kuweka akiba.
Huduma imeboreshwa zaidi kwa
kuweza kuzihamishia kwenye akaunti
za benki, kulipia huduma na bidhaa au
kuzitoa katika nchi nyingine kulingana
na aina ya fedha za eneo husika.
Hii inamuwezesha hata kama mtu
akiwa mbali na benki na kuwa na
uwezo wa kuokoa muda kwa kutumia
pesa alizoweka kwenye simu yake kwa
kuzitoa kwa wakala aliye karibu naye.
Vilevile, kwa kutumia simu waweza
kuvuta fedha kutoka kwenye akaunti
yako ya benki na kuziingiza kwenye
simu yako na kuwa huru kuzitoa ili
kuzitumia eneo lolote kwa kutumia
mawakala.
Siku hizi pia kwa kutumia akiba
kwenye simu unaweza kupata huduma
nyingine kupitia simu hiyo kama vile
kununua umeme, kulipia bili ya maji,
matibabu, king’amuzi na hata tiketi za
kuingia kwenye michezo ya soka au
tamasha. Mtu aweza kudunduliza
fedha kidogokidogo kwenye simu yake.
Tatu, kuweka akiba kwa kutumia benki
na taasisi nyingine za kifedha. Hii
husaidia sana kuhamasisha huduma za
kuweka akiba kwa malengo kama vile
kumsomesha mtoto au amana.
Uwekaji wa fedha za namna hiyo pia
huweza kusaidia kuwa na fedha za
kukabili dharura na kuwa na mitaji
mikubwa ya kibiashara na hatimaye
kuleta maendeleo makubwa
yaliyokusudiwa.
Nne, ni kumkopesha mtu na kurudisha
kwa riba. Siku hizi aina hii ya
ukopeshaji imeenea sana, hasa mijini
na vyuoni. Hii imetokana na watu
kuzidi kukua sana kiuelewa,
wamebadili mwelekeo kutoka
kumkopesha mtu pasipo riba hadi
kuwa na faida.
Watu wameerevuka na kufahamu
kuwa fedha ya mwezi au wiki hii ni
tofauti na ya mwezi au wiki lijalo.
Tatizo lililopo ni kwamba hakuna
maandishi ya kukopeshana kwa walio
wengi kwa sababu za kujali utu. Lakini
ukweli ni kwamba wanadamu wengi
wana tabia ya kubadilika. Kama huna
maandishi ya kukopeshana itakuwa
vigumu kupata fedha zako pale
anapokuwa si mwaminifu.
Tano, ni kuwekea bima mali zako na
biashara yako. Hii ni njia ambayo ni
muhimu sana maana hakuna mtu
anayeweza kuzuia majanga ambayo ni
ya asili au ya kawaida, hivyo bima
hasaidia sana siku ukipata ajali ya
biashara kwa kuibiwa au kuungua.
Sita, ni kununua vitu kama nyumba,
ardhi na vifaa vya gharama vyenye
kudumu muda mrefu. Hivi waweza
kuviuza baadaye kwa bei ya juu.
Maendeleo ya mtu mmojammoja ni
mafanikio ya taifa. Taifa lenye akiba ya
kutosha kwa kawaida linakuwa imara
na wananchi wenye akiba kwa njia
mbalimbali kama nilivyoorodhesha, ni
watu wenye maisha ya uhakika.
Dharura zote wanaweza kuzikabili na
hapa ndipo pia mitaji mikubwa ya
biashara inatokea. Kuweka akiba ni
jambo la msingi, tuanze leo kuweka
akiba. MPENZI MSOMAJI KAMA UMEGUZWA NA MAKALA HAYA TUANDIKIE KWENDA EMAIL HII kimarioerasmi@gmail.com

Haya libabu la arsenal hii Ndoa ya Arsene Wenger yavunjika Ndoa ya kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na mke wake, Annie iliyodumu kwa miaka mitano imevunjika


Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na
mkewe Annie
Strasbourg, Ufaransa. Ndoa ya kocha
wa Arsenal, Arsene Wenger na mke
wake, Annie iliyodumu kwa miaka
mitano imevunjika baada ya miezi
kadhaa ya uvumi.
Habari za kimahakama mjini
Strasbourg zilieleza jana kuwa wawili
hao wenye binti wa miaka 18,
wamekuwa hawaonekani pamoja
tangu mwaka 2013.
Wenger, mwenye umri wa miaka 65 na
mkewe, Annie 59 wamefikia mwafaka
wa kugawana mali.
Mara kadhaa, kocha huyo alikiri kuwa
shinikizo kubwa la kazi kwenye klabu
hiyo ya London Kaskazini
limesababisha matatizo kwenye ndoa
yake.
Nyaraka za kimahakama zilionyesha
kuwa wawili hao walitengana Juni
mwaka huu.
Hata hivyo, nyaraka hizo zimeeleza
kuwa si talaka kamili, bali
wametengana kisheria, jambo
linalomaanisha kuwa wana jukumu la
kuendelea kuwa pamoja.
Wawili hao walifunga ndoa Desemba
2010 baada ya uhusiano wa muda
mrefu, lakini wamekuwa si wenye
furaha kwa muda sasa.
“Wamegawana mali na rasilimali,
wamefikia mwafaka wa kutengana.
Mwaka 2008, kocha huyo alieleza
dhamira ya kuacha soka ili kuwekeza
nguvu kwenye ndoa.
Alisema: “ Miaka kumi iliyopita,
nilimweleza mke wangu (Annie),
‘Anipe miaka mitano zaidi katika soka
inatosha’, lakini hadi leo ninaendelea
na kazi.
“Ni vigumu kuwa na muda wa kutosha
kukaa pamoja kwa sababu ya ratiba
ngumu ya masuala ya soka. Kuna
wenzetu wanaondoka Jumatatu na
kurudi Ijumaa
“Ninasafiri kikazi, lakini tatizo si kiasi
gani cha muda ninaotumia mbali ya
familia yangu, bali ubora wa muda
ninaotumia na familia yangu.
“Nikizingatia hilo, kuna madhara.
Familia inakosa ubora wa huduma
wanazostahili nikiwa nyumbani, kwani
ninafikiria mchezo unaofuata.”
Aliongeza: “Mke wangu anapenda
kuangalia soka, anaona mechi za
Arsenal akiwa nyumbani . Siyo shabiki,
lakini anapenda michezo. Ni kwa kuwa
hakuwa na chaguo.”
-

Watu 41 wakamatwa kwa kutishia amani kwenye kampeni Watu 41 wakiwamo wanawake tisa wamekamatwa mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya vurugu katika


Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya,
Ahmed Msangi.
Mbeya. Watu 41 wakiwamo wanawake
tisa wamekamatwa mkoani hapa kwa
tuhuma za kufanya vurugu katika
maeneo mbalimbali wakati wa
kampeni zinazoendelea kuwanadi
madiwani na wabunge.
Kamanda wa polisi mkoani hapa,
Ahmed Msangi amesema hayo leo
alipozungumza na waandishi wa
habari kuhusu tathimini ya matukio ya
uchaguzi.
Amesema tangu kampeni zilipoanza
matukio 30 ya uhalifu yalifanyika
yakiwahusisha wanaume 32 na
wanawake tisa.
Amesema tukio moja kati ya hayo
lilimhusisha Aman John ambaye
amefikishwa kortini na kupatikana na
hatia iliyosababisha alipe faini ya
Sh30,000.
“Kesi nane kati ya matukio hayo zipo
mahakamani zikiwa katika hatua
mbalimbali lakini kesi tatu majalada
yapo ofisi ya wanasheria wa Serikali
wakati kesi zingine 19 zinapelelezwa,’’
amesema.
Amesema waliokamatwa
wametuhumiwa makosa mbalimbali
yakiwamo ya kuchana mabango ya
wagombea wa Urais, Ubunge na
Udiwani.
‘’Wengine wamekamatwa kwa makosa
ya kung’oa bendera, kuharibu mali,
kufanya fujo, kujeruhi, kuingilia
mkutano, kutishia kuua kupigana
hadharani na wizi’’ amesema kamanda
huyo

Kipindupindu chaendelea kunyonga watu dar.. Kipindupindu chaendelea kuua D’Salaam Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa ugonjwa wa kipindupindu imeongezeka na kufikia 17 baada ya


Watoto wakicheza katika jalala eneo la
Bugando Mwanza, mazingira ya namna hii
ni hatari kwa afya zao.
Dar es Salaam. Idadi ya watu
waliopoteza maisha kwa ugonjwa wa
kipindupindu imeongezeka na kufikia
17 baada ya watu wengine wawili
kupoteza maisha jana.
Hata hivyo, idadi ya watu
walioripotiwa kuugua ugonjwa huo
tangu ulipuke katika Jiji la Dar es
Salaam Agosti 17, imefikia 2,000.
Ofisa Habari wa Manispaa ya Temeke,
Joyce Msumba alisema kuwa jana
walipokea wagonjwa wapya saba na
kati yao, mmoja ameshafariki dunia.
Msumba alisema wagonjwa wengi
hawatoki katika Manispaa hiyo bali
wapo wanaotoka eneo la Buguruni
katika Manispaa ya Ilala na
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
mkoani Pwani.
Alisema tayari wameshatoa taarifa
kwa maofisa wa afya wa wilaya zao ili
wafuatilie hali katika familia zao.
Mganga Mkuu wa Manispaa ya
Kinondoni, Victorina Ludovick alisema
wamepokea wagonjwa wapya 31 idadi
inayofanya watu waliolazwa katika
kambi ya ugonjwa huo kufikia 38.
Dk Ludovick alisema wagonjwa wengi
wanatoka maeneo ya Buguruni,
Vingunguti, Jangwani, Ilala,
Mchikichini, Tabata na Kigogo.
Alisema kuendelea kusambaa kwa
ugonjwa huo kunatokana na wakazi
wengi wa maeneo hayo kutozingatia
kanuni za afya wanazofundishwa na
wataalamu.
“Magari ya matangazo yanapita katika
mitaa yao kila siku kutoa elimu na
kuwahamasisha kunawa mikono kwa
sabuni baada ya kutoka chooni,
kuchemsha maji ya kunywa na
kuzingatia usafi wanapoandaa
vyakula,” alisema Ludovick
Alisema maofisa afya wanaendelea na
kazi ya kukagua mazingira
wanayofanyia kazi wafanyabiashara
wa vyakula na matunda ili kuwabaini
wanaokiuka agizo la kuacha kufanya
biashara hiyo hadi ugonjwa huo
utakapokwisha.

Idd kwa waislamu wengine imewasababishia kifo Mamia ya mahujaji wafariki katika mkanyagano Makka Watu wasiopungua 717 wamekufa, huku wengine 816 wamejeruhiwa leo jirani na mji mtakatifu wa Makka


Watu wasiopungua 717 wamekufa,
huku wengine 816 wamejeruhiwa leo
jirani na mji mtakatifu wa Makka
walikokwenda kuhiji ikiwa ni sehemu
ya utekelezaji wa moja ya nguzo
muhimu katika Imani ya dini ya
Kiislamu, maofisa Saudi Arabia
wathibitisha.
Kwa mujibu wa Baraza la Taasisi na
Jumuiya za Kiiislam nchini, kati ya
mahujaji 2,000,000 waliokwenda Saudi
Arabia mwaka huu, 1,500 wanatoka
Tanzania.
Japokuwa Msemaji wa Baraza hilo,
Shekhe Rajabu Katimba amesema
hakuna vifo vilivyokwisharipotiwa hadi
sasa toka Makka, taarifa zisizo rasmi
kutoka huko zinasema Mtanzania
mmoja amekufa na mwingine
amejeruhiwa baada ya kutokea
mkanyagano.
Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji
la BBC, katika maafa hayo, mahujaji
wengine wasiopungua 816
wamejeruhiwa katika eneo la Mina.
Vifo hivyo vimetokea ikiwa ni siku
chache kupita baada ya kutokea jail
nyingine ambapo winchi lilianguka na
kuua watu 109 katika msikiti ambapo
kulikuwa kukifanyika ibada ikiwa ni
maandalizi ya kuelekea sikukuu ya leo.
Haya ni maafa makubwa zaidi kutokea
katika sikukuu ya Eid Al Hajj baada ya
kupita takribani miaka 25. Kwa mujibu
wa Kurugenzi ya Wizara ya Usalama
wa Raia nchini Saudi Arabia, maafa
hayo yametokea kati ya saa sita
(majira ya Afrika Mashariki) katika
makutano ya mitaa namba 204 na 223
wakati mahujaji hao wakipanda ngazi
kuelekea jengo la ghorofa tano ambalo
limeuzunguka mnara, maarufu kwa
jina la Jamarat Bridge. “Tukio hilo
limetokea baada ya mahujaji
kuongezeka ghafla wakielekea kwenye
mnara,” taarifa ya wizara iliongeza.

Jumatano, 23 Septemba 2015

Maaaajabu haya .. mtoto mwenye miguu minnee azaliwa rombo ..kijiji cha kitowo


Mpenzi msomaji haya ni maajabu ambayo huwa hutokea kwa nchi za wenzetu lakini leo nishtuka sana na habari hizi ambazo hazijathibitishwa.. ila chanzo kmoja kinasema kwamba mtoto huyo alizaliwa katika zahanati ya kasuruwa.. tarehe 21/03/2014 na hadi sasa mtoto huyo amehamishiwa daresalamu ambako wanaishi wazazi wake ila nyumbani kwao ni kitowo ... habari hizi hazijathibitishwa pindi zitakapo kuwa sawa mtapata hapahapa eaglefm endelea kutufuatilia ili upate ukweli.

Jumanne, 22 Septemba 2015

Kwa vume kunani.. Liewig ajitetea Stand United kuchemsha Wakati uongozi wa Stand United ukiwakingia kifua mashabiki wa timu hiyo kwa kumfanyia vurugu


Kocha wa Stand United, Patrick Liewig
Dar es Salaam. Wakati uongozi wa
Stand United ukiwakingia kifua
mashabiki wa timu hiyo kwa
kumfanyia vurugu kocha, Patrick
Liewig mwenyewe amesema uwezo
wake hauwezi kupimwa kwa mechi
mbili.
Liewig ameiongoza Stand kushinda
mechi moja na kutoka sare mbili tangu
alipojiunga na timu hiyo alijikuta
kwenye wakati mgumu wa kutaka
kupigwa na mashabiki baada ya timu
yake kuruhusu kipigo cha mabao 2-0
dhidi ya Azam wiki iliyopita mjini
Shinyanga.
Akizungumza na gazeti hili jana,
Mfaransa huyo alisema anajiamini na
anaamini yeye ni kocha mwenye
uwezo huku akisisitiza asipimwe kwa
matokeo ya mechi mbili ambazo timu
yake imekwishapoteza tangu kuanza
kwa ligi.
“Nahitaji kupewa muda, timu ya Stand
inajengwa taratibu, mashabiki wawe
na subira endapo wanahitaji mafanikio
kwani naamini ushindi hupo,” alisema
kocha huyo kwa kifupi.
Mwenyekiti wa Stand United, Aman
Vicent alisema kitendo kilichofanywa
na mashabiki wao kinaweza kutokea
katika timu nyingine yoyote ni cha
kawaida katika soka.
“Unajua tulitarajia makubwa
ukizingatia kocha analipwa fedha
nyingi sasa kitendo cha kufungwa
mechi mbili mfululizo kiliwakasirisha
mashabiki na kulazimika kufanya kile
kilichotokea, lakini tumeyamaliza na
tunajipanga kwa mechi zijazo,”
alisema Vicent.
Liewig aliajiliwa kuinoa Stand kama
kocha mkuu miezi michache kabla ya
ligi kuanza, kocha huyo pia aliwahi
kuifundisha Simba huku akiacha
rekodi ya kuwaibua vijana kwenye
timu hiyo.
Naye Mchambuzi wa soka na kocha wa
zamani wa Taifa Stars, Mshindo Msolla
amemtetea kocha huyo raia wa
Ufaransa na kueleza kuwa hastahili
kulaumiwa hivi sasa kutokana na
matokeo ya timu hiyo imepata na
kusisitiza kuwa wachezaji wa timu hiyo
hakuwasajili yeye.
“Liewig hastahili lawama, timu
ameikuta tayari imesajiliwa hivyo
matokeo ya sasa yanawahusu uongozi,
wanachotakiwa kufanya kwa sasa ni
kumpa muda wa kuijenga timu hiyo na
itakapofika kipindi cha dirisha dogo
aachiwe afanye usajili wa wachezaji
anaowahitaji,” alisema Msolla.

Sport man RIZIK MALYA leo amekuandalia Martial aing’arisha Man United Mabao mawili ya kinda Anthony Martial na jingine la Juan Mata jana yaliiwezesha Manchester United


Martial alichukua mpira kutoka upande wa
kushoto akakimbia nao kuelekea kwenye
boksi na kumpiga chenga beki mzoefu
kwenye ligi, Martin Skrtel kabla ya
kufunga bao maridadi kabisa.
London, England. Mabao mawili ya
kinda Anthony Martial na jingine la
Juan Mata jana yaliiwezesha
Manchester United kushinda mabao
3-2 dhidi ya Southampton kwenye
mchezo mgumu wa Ligi Kuu England.
Kwa ushindi huo, Man United
imefikisha pointi 13 na kushika nafasi
ya pili ikiwa nyuma ya Man City
ambayo ipo kileleni ikiwa na pointi 15,
huku West Ham ikiwa katika nafasi ya
tatu ikiwa na pointi 12.
Katika mchezo huo uliofanyika
kwenye Uwanja wa St Mary’s, wenyeji
Southampton walitangulia kupata bao
kupitia kwa Graziano Pelle, kipindi cha
kwanza.
Kipindi cha pili, Martial aliyejiunga na
klabu hiyo siku ya mwisho ya usajili,
Septemba 2 kwa ada kubwa akitokea
AS Monaco ya Ufaransa, alifunga
mabao hayo mawili na Mata kuongeza
jingine, huku Pelle akifunga pia la pili
katika mchezo huo.
Mapema, Tottenham au Spurs iliilaza
Crystal Palace kwa bao 1-0 katika
mchezo wa mapema saa 9.30 alasiri
kwenye Uwanja wa White Hart Lane.
Nayo Liverpool ilizuiwa na Norwich
City na kutoka sare ya bao 1-1 katika
mchezo mwingine wa Ligi Kuu kwenye
Uwanja wa Anfield.

Matajiri watano kuibeba Chadema Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema chama chake kina watu watano wenye uwezo wa kiuchumi


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman
Mbowe (mwenye kipaza sauti) akiendesha
harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya
kampeni za chama hicho iliyofanyika Dar
es Salaam juzi. Picha na Said Khamis
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa
Chadema, Freeman Mbowe amesema
chama chake kina watu watano wenye
uwezo wa kiuchumi wanaoweza
kukisaidia chama hicho kuendesha
shughuli zake za kampeni, ikiwa ni
siku 32 kabla ya wananchi kupiga kura
Oktoba 25.
Lakini mwenyekiti huyo wa Chadema
amesema watu hao hawataki
kutangazwa majina yao kutokana na
kuhofia kufuatiliwa na vyombo vya
dola, akisema kitendo hicho ni cha
kushangaza kwa nchi huru kama
Tanzania.
Chadema, ambayo inashirikiana na
NLD, CUF na NCCR Mageuzi chini ya
mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa) iliandaa harambee
hiyo juzi kwenye ukumbi wa Mlimani
City kwa ajili ya kutafuta fedha za
kuchangia shughuli zao za kampeni
zinazoendelea kote nchini.
Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na
takriban watu 800, jumla ya Sh97
milioni zilikusanywa, ikiwa ni fedha
taslimu, michango kwa njia ya simu na
ahadi.
Baada ya kazi ya uchangishaji kuanza,
Mbowe alishika kipaza sauti na
kueleza michango mingine kutoka nje
ya ukumbi huo.
“Wakati tunaendelea na uchangiaji
hapa, nimepokea simu kutoka kwa
rafiki zangu watano wenye uwezo
mkubwa kiuchumi. Wameahidi
kuchangia harambee lakini wanaogopa
kujulikana kwa kuhofia mkono wa
serikali,” alisema mwenyekiti huyo.
“Inasikitisha Mtanzania mwenye uhuru
ndani ya Taifa lake anahofia kuchangia
safari ya mabadiliko kwa sababu ya
kuiogopa Serikali, wakati Serikali
iliyopo imejaa mafisadi wakubwa?
“Unaweza kuona hii ni Serikali ya
namna gani, lakini ningewaomba
niwatie moyo tu ndugu zangu wenye
nia ya mabadiliko, tuwe na ujasiri,
msiogope.”
Sheria ya Gharama za Uchaguzi,
ambayo mwaka huu imeweka kiwango
cha juu cha matumizi ya kila chama
kuwa Sh17 bilioni, inataka uwazi wa
vyanzo vya mapato na matumizi, lakini
ni nadra kwa wafanyabiashara kuweka
bayana michango yao kwa vyama vya
upinzani.
Chadema imekuwa ikinufaika na
michango ya fedha na mali kutoka kwa
mfanyabiashara maarufu nchini,
Mustapha Sabodo, ambaye amekuwa
akitangaza hadharani kila
anapokichangia chama hicho.
Alipoulizwa ni kiasi gani chama hicho
kimepanga kutumia kwenye uchaguzi,
Mbowe alisema ni vigumu kutaja.
“Uchaguzi ni dynamic
(unabadilikabadilika). Hesabu za siku
haziwezi kuwa sawa wakati wote. Kwa
mfano bango la kupinga bao la mkono,
inahitajika sana kwa wakati huu lakini
gharama inaweza kuwa nyingine
wakati wa kusambaza bango jingine,”
alisema Mbowe.
Mkurugenzi wa mipango na uchaguzi
wa CUF, Shaweji Mketo alisema kila
chama ndani ya umoja huo
kinajitegemea kwenye gharama za
wagombea wake kwa ngazi ya
majimbo na udiwani.
“Hakuna tathmini ya pamoja ya
Ukawa...taarifa za gharama kwa CUF
tutaziweka wazi baada ya kukamilisha
majumuisho ya taarifa zote kutoka
majimboni na ngazi ya madiwani,”
alisema Mketo.
Maoni ya wachambuzi
Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),
Dk Alexander Makulilo alisema hofu
kwa wafanyabiashara nchini
imekuwapo kwa muda mrefu.
Alisema ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa
mwaka 2010 iliyoandaliwa na Timu ya
Waangalizi wa ndani wa uchaguzi
mkuu (Temco) inaonyesha TRA
kulalamikiwa na wafanyabiashara kwa
kuchunguza wafanyabiashara
waliokuwa hawaiungi mkono CCM.
Suala la matajiri hao kutotaka majina
yao kutajwa pia lilimgusa
mwanaharakati wa mtandao wa TGNP,
Gemma Akilimali, ambaye alisema
haoni sababu ya kuhofia kuchangia
kwa uwazi ili mradi ni wasafi katika
biashara zao.
“Sabodo ni mfanyabiashara mkubwa
tu na amekuwa akiwachangia
Chadema na CCM waziwazi bila
kuficha na hatujaona lolote likimtokea.
Kwa hivyo hofu zao zinaweza
kutujengea maswali katika uwazi wa
shughuli zao. Hofu iko kwa utayari
wao katika kuchimbuliwa shughuli zao
au vyanzo vya mapato yao.”
Awali kabla ya uchangiaji huo kuanza,
mgombea urais wa Chadema na
Ukawa, Edward Lowassa aliwataka
waalikwa kutoogopa kuchangia
harambee hiyo kwa hofu ya
kufuatiliwa na Mamlaka ya Mapato
(TRA).
“Nawaomba msiogope kuchangia, mtoe
tu kwani mabadiliko haya yanawahusu
wale wanaoyapenda na wasioyapenda.
Tunahitaji mabadiliko haya yafanikiwe
kwa kila hali,” alisema Lowassa,
ambaye aliihama CCM mwishoni mwa
mwezi Julai na kuungana na Chadema
kudai mabadiliko.
“Nawapongeza sana kwa juhudi za
maandalizi yaliyofanyika leo, na inatia
matumaini ya kufanikisha.”
Maombi ya uchangiaji
Akifungua harambee hiyo, Mbowe
alisema mikoa iliyosalia ni mingi kwa
hivyo bado wanategemea zaidi
michango ya wadau katika kufanikisha
kampeni.
Mbowe alisema muda uliobakia ni wa
“vita ya lala salama”, ambayo inahitaji
bajeti ya kutosha ili kufanikisha kufikia
wapiga kura wengi watakaoshiriki
uchaguzi huo.
“Ukichangia harambee hii hautakuwa
umemchangia Mbowe au Lowassa, bali
utakuwa umechangia ufanikishaji wa
kufikia ndoto ya mabadiliko. Utakuwa
umechangia ukombozi wa akina mama
na vijana wa Taifa la Tanzania,”
alisema Mbowe.
“Tangu kuanza kwa kampeni hizi,
Ukawa tumekuwa tukisaidiwa na
Watanzania mbalimbali wenye nafasi
zao, wapo waliotoa usafiri wa magari
ya kufanyia kampeni. Kwa hivyo
tunahitaji sana mchango wako katika
kipindi hiki.”
Chadema pamoja na Ukawa zimekuwa
zikipambana sambamba na CCM
kwenye kampeni za urais na ubunge
na matumizi yao makubwa
yanaonekana kuwa katika gharama za
safari za wagombea, matangazo ya
redio na televisheni, matangazo ya
moja kwa moja ya mikutano yao ya
kampeni, posho za mawakala na vifaa
kama mavazi, bendera, vipeperushi na
mabango.
Akizungumza kwenye hafla hiyo,
mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James
Mbatia, ambaye ni pia ni mwenyekiti
wa NCCR-Mageuzi, aliwataka waalikwa
kuhakikisha wanashiriki kikamilifu
kuchangia harakati za mabadiliko ili
kufanikisha ndoto za kuwakomboa
Watanzania kutoka mikononi mwa
Serikali ya CCM.
Mwingine aliyezungumza na waalikwa
ni mgombea mwenza wa urais, Juma
Duni Haji, maarufu kwa jina la Babu
Duni, ambaye alikuwa kivutio kutokana
na vijembe na misemo anayotoa
wakati akiwa jukwani.
Duni alisema kutoa ni moyo na siyo
utajiri kwani wapo wenye fedha
nyingi, lakini hawana moyo wa utoaji.
Mzee wa Upako aibuka
Baada ya viongozi hao kuzungumza na
kuendesha harambee, Mchungaji
Anthony Lusekelo wa Kanisa la
Maombezi (GRC), Ubungo Kibangu,
alitaka watu kuwa tayari kukubali
matokeo yoyote kwa kuwa ushindi wa
Lowassa au mgombea wa CCM, Dk John
Magufuli utakuwa wa Watanzania
wote.
Baada ya kutoa kauli hiyo, waalikwa
walipiga kelele za kupinga kauli yake
lakini aliendelea kueleza msimamo
wake huku akiwatuliza.
“Tulia, tulia wewe unayepiga kelele,
siasa chafu hazifai na siasa siyo
kumchafua mtu,” alisema.
“Hakuna taasisi inayoweza kuzidi
nguvu ya umma, lakini niseme jambo
kwamba, kwa sasa tuna wagombea
wakubwa wawili ambao ni Dk
Magufuli na Lowassa. Yeyote
atakayeshinda itakuwa ni ushindi kwa
Watanzania, tusiweke nongwa. Mimi ni
kiongozi wa dini nisiyekuwa na itikadi
ya vyama, ninaishi na waislamu na
Wakristo, kwa hiyo ni sawa kwa yeyote
kati yao.”
Lusekelo alisema hana itikadi ya
chama chochote kile na Lowassa ni
rafiki yake kwamuda mrefu, lakini
endapo Dk Magufuli atashinda bado
itakuwa ni sawa kwake.
Mbowe alisema uchangiaji huo
unaendelea kufanyika kwa njia ya
akaunti maalumu za simu za mikononi
na kujaza fomu zilizoandaliwa kwa ajili
ya ahadi za wanachama ukumbini
hapo.

Ajali yafunga barabara kwa saa nne Kibaha Mamia ya abiria waliokua wanasafiri kupitia barabara kuu ya Dar esalam - Morogoro leo wamekwama


Kamanda wa Polisi Pwani, Jafar Mohamed
Kibaha. Mamia ya abiria waliokua
wanasafiri kupitia barabara kuu ya
Dar esalam - Morogoro leo
wamekwama kwa zaidi saa nne katika
eneo la Bamba Kata ya Kongowe mjini
Kibaha baada ya magari matano
kugongana na kisha kuziba barabara.
Katika ajali hiyo abiria watano
wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za
mwili huku wanne kati yao wakiwa
wamevunjika mikono na miguu
ambapo majeruhi wote wamepelekwa
katika hospitali teule ya rufaa ya
Tumbi kwa matibabu.
Kamanda wa Polisi Pwani, Jafar
Mohamed amethibitisha kutokea kwa
tukio hilo na kusema ilitokea majira
ya saa 10.50 alfajiri ya leo na kwamba
barabara ilifunga kutokana na moja ya
magari yaliyogongana kuziba
barabara.
Kamanda Jafar alifafanua kuwa hatua
hiyo ilisababisha mabasi,malori na
magari mengine madogo kushindwa
kuendelea na safari kwa wakati katika
barabara hiyo.
"Ni kweli kuna usumbufu uliotokea
kwa wasafiri wa mikoani hasa wale
waliosafiri na magari yaliyotoka
alfajiri kwenda mikoani katika
barabara hii,” alisema kamanda huyo.
Kamanda huyo amewataja majeruhi
hao kuwa ni Abdul Mashaka
aliyevunjika mkono wa kulia,Juma
Hajji aliyevunjika mguu wa kulia,
Halfani Abdalla aliyevunjika miguu,
Zakaria Ramadhani na Othuman
Omary na wote walipelekwa kutibiwa
hospitali yaTumbi.
Awali Mkuu wa kikosi cha usalama
barabarani mkoani Pwani, Isango Abdi
alisema magariyaliyohusika na ajali
hiyo ni aina ya Fuso, Scania tanker na
Iveco tanker.
Alibainisha kuwa askari walifanikiwa
kudhibiti wizi wa mafuta katika malori
hayo na hivyo uharibu uliotokea ni
majeruhi na magari kuharibika.
Aliongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo
ni dereva wa mojawapo ya lori
Raymond Mtega kuyapita gari zaidi ya
moja bila tahadhari na kufafanua
kuwa dereva huyo ameshakamatwa na
anahojiwa na baadae hatua za kisheria
zitafuata dhidi yake,
Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Bamba
ilipotokea ajali hiyo Amri Mavalla
alisema serikali ya mtaa kwa
kushirikiana na polisi walifanikiwa
kuyaondoa malori hayo yaliyoziba
barabara na saa 2.30 asubuhi magari
yote yaliyokuwa yamekwama eneo hilo
yaliendelea na safari kama kawaida.
-

Jumatatu, 21 Septemba 2015

Fahamu kuhusu historia ya wachaga,chanzo na asili yao pekee kupitia eaglefm na mwandishi wetu malya ..mwandishi wa kitabu cha historia marangu.imeeandaliwa na wasonga mrombo




Kabila la Wachaga linafahamika kwa
wengi kuwa linapatikana mkoani
Kilimanjaro.Kwa asili, Wachaga ni
mchanganyiko wa Wamasai,
Wasambaa, Wataita, Wakamba na
Wakahe.
Wachaga walianza kuhamia kwenye
miteremko ya Mlima Kilimanjaro
kwenye karne ya 17.
Walipofika wakiwa katika vikundi
vidogovidogo waliwakuta wakazi,
wenyeji kwenye Misitu ya Mlima
Kilimanjaro walioitwa ìWakonyingo..
Wenyeji hawa ambao huitwa
Mbilikimo hawakupenda
kuchanganyika na wahamiaji wageni,
hivyo wakahama na kuanzisha makao
yao ya kudumu kwenye misitu
minene iliyopo nchini Kongo.
Watu wengi wanafikiria kwamba
Wachaga wanatokana na asili moja.
Ukweli ni kwamba wamegawanyika
katika himaya 15, wanatofautiana
kwa lafudhi, lugha, rangi na
mwonekano wa miili yao.Wachaga
wapo katika makundi makuu matatu
ya Hai, Vunjo na Rombo.
Wale wanaopatikana eneo la Hai ni
Wasiha, Wamasama,
Wamachame,Wangíuni, Wakibosho,
Wauru na Wamoshi. Kwa wale
wanaopatikana eneo la Vunjo ni
Wakirua, Wakilema, Wamarangu,
Wamamba na Wamwika.
Kutoka eneo la Rombo ni Wamkuu,
Wamashati na Wasseri.
Hadi sasa haijulikani vizuri asili ya
jina Wachaga, ila wanahistoria
wanaeleza kwamba jina hilo
linatokana na neno la Kiswahili
linaloitwa 'Kichaka'.
Inaelezwa kwamba misafara ya
wafanyabiashara iliyokuwa
ikiongozwa na Waswahili pamoja na
Waarabu, walipokuwa wakipita
maeneo ya Vunjo waliwaona wenyeji
wa huko wakiwa wamejenga vibanda
vya kulinda mazao yao yasiliwe na
wanyama waharibifu.
Wakawaita wenyeji hawa kwamba
wanaishi vichakani na kuanzia hapo
wageni wafanyabiashara na
Wamisionari walipokuwa wanakuja
Kilimanjaro walielekezwa na
waongozaji misafara yao kwamba
wanakwenda kwenye nchi ya
ìUchakani,î, wakimaanisha kwamba
kwa watu wanaoishi vichakani.
Hatimaye wageni wakashindwa
kulitamka vizuri neno hili na kuliita
ìUchagani,
Jina hili likawekwa kwenye ramani
na kuitwa nchi ya ìWachaga.î Hivyo
ndivyo wenyeji waliokuwa wakiishi
kwenye Miteremko ya Mlima
Kilimanjaro walivyopewa jina lao.
Wachaga.
Maendeleo ya Wachaga
Maendeleo yao hapo awali yalitokana
na zao la kahawa. Walifanikiwa
kuanzisha vyama vya ushirika na
hatimaye mwaka 1932 walianzisha
Halmashauri ya Wachaga (Chaga
Council) ambayo kwa sasa inatumiwa
na Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.
Halmashauri hii iliongozwa na Mangi
Mkuu ìMshumbue Thomas Marealle
II.
Mwaka 1946, utawala wa Waingereza
uliboresha Baraza la Halmashauri ya
Wachaga. Himaya ndogo za Wachaga
zipatazo 17 (himaya mbili za
Wakahe na Waarusha chini
zilijumuishwa kwenye Tarafa ya
Vunjo) na kuundwa kwa Tarafa tatu
za Hai, Vunjo na Rombo.
Halmashauri ya Wachaga ilijenga
miundombinu na huduma za jamii
ikiwamo kuwasomesha watoto wao
kwenye shule na vyuo mbalimbali
kama Chuo Kikuu cha Makerere,
Uganda.
Halmashauri ya Uchaga ilikuwa na
bendera yake ambayo ipo hadi leo
kwenye Halmashauri ya Wilaya ya
Moshi, yenye nembo tano kuu:
1- Mlima Kilimanjaro uliochorwa
katikati ya bendera ukionyesha
mandhari nzuri ya kilele cha Kibo.
Kilele cha Kibo kinatoa maji safi na ni
kielelezo cha umoja wao.
2- Chini ya kilele cha Kibo, upande
wa kushoto wa bendera kuna
mgomba wenye ndizi. Hiki ni chakula
kikuu cha Wachaga.
3- Upande wa kulia wa bendera ni
tawi la mbuni ukiwa na matunda
yake. Kahawa ni zao lililowaletea
maendeleo.
4- Bendera imezungukwa na
matawi ya 'sale' lenye matawi mawili
(draceana plant). Matawi haya
yamefanya mduara kuzunguka kilele
cha Kibo, mgomba wa ndizi na tawi la
zao la kahawa. Masale ni mmea
unaoheshimiwa sana na Wachaga
wote.
Ni alama ya amani. Masale hutumika
katika sherehe na shughuli zote za
kimila zinazofanywa na Wachaga.
Majani yake ni kijani kibichi
yanayoonyesha jinsi Kilimanjaro
ilivyo na rutuba nzuri inayostawisha
mazao ya kila aina.
5- Juu kidogo ya kilele cha Kibo
yupo chui ambaye amejipumzisha.
Chui ni alama kuu ya mamlaka ya
Wachaga.
Hapo awali kwenye miteremko ya
Mlima Kilimanjaro walikuwepo chui
wengi wa rangi nyeusi lakini
kutokana na ongezeko la watu
pamoja na uharibifu wa mazingira
chui hawa wametoweka.
Sikukuu ya Wachaga
Sikukuu ya Wachaga wote ilikuwa
ikiadhimishwa Novemba 10 kila
mwaka kama kumbukumbu ya siku
ambayo Wachaga wote
walipokusanyika na kumchagua
Mangi Mkuu baada ya kuteuliwa na
Halmashauri Kuu ya Uchaga.
Maadhimisho ya kwanza ya mwaka
1952 yalitanguliwa na uchaguzi wa
Halmashauri ya Wachaga wote
kuanzia kwenye ngazi ya Uchili
(kijiji), Umangi ( uchifu wa eneo) na
mwisho ngazi ya baraza kuu.
Sherehe ziliadhimishwa mjini Moshi
ambako Wachaga wote pamoja na
wageni waalikwa kutoka mataifa
mbalimbali walikusanyika katika
Viwanja vya Halmashauri ya Uchaga
(sasa ni makao makuu ya
Halmashauri ya Wilaya ya Moshi,
[Kilimanjaro District Council-KDC])
kushuhudia sherehe kubwa na yenye
kusisimua sana.
Jumba la Makumbusho
Upo umuhimu mkubwa wa kuhifadhi
historia ya Wachaga kama
kumbukumbu sahihi kwa vizazi vya
sasa na vijavyo.
Pia, ipo haja kwa majengo ya
Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
pamoja na Ikulu yakarejeshwa kwa
Wachaga ili yageuzwe kuwa majengo
ya kuhifadhi kumbukumbu ya kabila
hilo.
Katika majengo haya patahifadhiwa
nyaraka zote za Chaga Council
ambazo baadhi zimeshaanza
kutoweka, kutahifadhiwa pia
shughuli za mila na kiutamaduni
tangu enzi ya karne ya 18.
Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
haina budi kutafuta eneo la kujenga
majengo mapya badala ya kuyatumia
ya kihistoria.
*Mallya ni mchambuzi wa masuala
ya maendeleo ya jamii na
mwandishi wa kitabu cha
Wamarangu na Maendeleo. -0754
390 402, email:
exaudmalya@yahoo.co.uk au kimarioerasmi@gmail.com

NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MAJI WA BARIADI MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 12 OKTOBA 2015..wa hombolo mtapewa kipaumbele kwenye utendaji mitaa..POSTED BY ERASM KIMARIO A.K.A WASONGA MROMBO

HALMASHAURI YA MAJI WA
BARIADI
TANGAZO LA KAZI
Mkurugenzi wa Halmashaya Maji
wa Bariadi anatangaza nafasi za
kazi themanini na moja (81).
Maombi ya kujaza nafasi tajwa
hapa chini yanakaribishwa
kutoka kwa mtanzania yeyote
mwenye sifa zilizotajwa katika
tangazo hili.
Nafasi zinazotangazwa ni kama
ifuatavyo:-
1. MTENDAJE WA MTAA III
(NAFASI 73)
Ngazi ya Mshahara: TGS B
SIFA ZA MWOMBAJI
• Awe amehitimu Elimu ya
Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
• Aliyehitimu mafunzo ya
Astashahada/cheti katika moja ya
fani zifuatazo:- Utawala, Sheria,
Elimu ya Jamii, Usimamizi wa
Fedha, Maendeleo ya Jamii na
Sayansi ya sanaa kutoka chuo
cha Serikali za Mitaa Hombolo,
Dodoma au chuo chochote
kinachotambuliwa na serikali.
MAJUKUMU
• Kuratibu na kutekeleza Sera
na Sheria zinazotekelezwa na
Halmashauri.
• Kuishauri kamati ya
maendeleo ya Mtaa kuhusu
Mipango ya Maendeleo katika
Mtaa.
• Kusimamia utekelezaji wa
Sheria ndogo na sheria
zinazotumika katika Mtaa.
• Kusiamia ukusanyaji wa
mapato ya Halmashauri.
• Kutekeleza na kusimamia
shughuli za maendeleo katika
Mtaa.
• Kusimamia ulinzi na usalama
wa raia na mali zao.
============
2. MAENDELEO YA JAMII
MSAIDIZI III (NAFASI 3)
Ngazi ya mshahara: TGS B
SIFA ZA MWOMBAJI
• Awe amehitimu Elimu ya
Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
• Aliyefuzu mafunzo ya
Stashahada (Diploma) kwenye
fani ya Maendeleo ya Jamii
kutoka vyuo vya Maendeleo ya
Jamii au vyuo vingine
vinavyotambuliwa na serikali.
MAJUKUMU
• Kuratibu shughuli za
maendeleo ya jamii katika mtaa
zikiwemo za wanawake na
watoto.
• Kuhamasisha na
kuwawezesha wananchi kupanga
na kutekeleza kazi za
maendeleo.
• Kuwezesha jamii kubuni,
kupang, kutekeleza na
kusimamia miradi ya
maendeleo.
• Kusaidia kuunda vikundi vya
kijamii na kimaendeleo.
===========
3. MSAIDIZI WA
KUMBUKUMBU DARAJA LA II
(NAFASI 5)
Nafasi 3 Msaidizi wa
kumbukumbu masijala ya
kawaida.
Nafasi 1 Msaidizi wa
kumbukumbu masijala ya Ardhi.
Nafasi 1 Msaidizi wa
kumbukumbu masijala ya Afya.
Ngazi ya mshahara: TGS B
SIFA ZA MWOMBAJI
• Awe amehitimu Elimu ya
Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI).
• Aliyefuzu mafunzo ya cheti
cha utunzaji kumbukumbu katika
mojawapo ya fani za masijala ya
kawaida, Afya na Ardhi.
MAJUKUMU
Msaidizi wa kumbukumbu
masijala ya kawaida
• Kutafuta kumbukumbu/
majalada yanayohitajiwa na
wasomaji
• Kuweka kumbukumbu (barua,
nyaraka nk.) katika majalada.
• Kuweka majalada katika
makundi.
• Kudhibiti upokeaji,
uandikishaji wa kumbukumbu/
Nyaraka.
• Kuweka kupanga
kumbukumbu sehemu ya
kuhifadhia.
Msaidizi wa kumbukumbu
masijala ya Ardhi
• Kushughulikia madai/
malalamiko ya hati za viwanja na
kutunza kumbukumbu zake.
• Kutunza kumbukumbu za
cadastral surveys na mahesabu
yake.
• Kuandaa nakala za cadastral
site plans.
• Kutunza miongozo ya ramani
na viwanja.
Msaidizi wa kumbukumbu
masijala ya Afya
• Kutafuta kumbukumbu/
majalada yanayohitajiwa na
wasomaji.
• Kushughulikia mapokezi ya
wagonjwa wa ndani na nje.
• Kukusanya kukagua na
kuhifadhi taarifa mbalimbali za
wodi za wafonjwa
SIFA NYINGINE ZA JUMLA
i. Mwombaji awe raia wa
Tanzania.
ii. Awe na umri wa kati ya
miaka 18 na 40.
iii. Maimbi yake yaambatishwe
picha (passport size) na vielelezo
vya sifa zake.
iv. Cheti cha kuzaliwa
kinambatishwe pia.
Maombi yote yatumwe kwa njia
ya posta kwa anuani ifuatayo:-
Mkurugenzi
Hlmashauri ya Mji
S.L.P 526
BARIADI
Mwisho wa kupokea maombi ni
tarehe 12.10.2015 saa tisa na
nusu alasiri.
Source: Mwananchi 21st
September, 2015

Ijumaa, 18 Septemba 2015

Hizi ni baadhi ya huduma za kimtandao tigo, voda, airtell.

*152*00# kuhakiki taarifa ya usajilli kadi ya mpiga kura ..............
.... mfano.................. KADI IMESAJILIWA
Jina: ERASMI ONORY KIMARIO
Jinsia: M
Kuzaliwa: 21/07/1993
Kituo: SHULE YA MSINGI MFORO
Kata: MARANGU KITOWO
Wilaya: WILAYA YA ROMBO
Jimbo: ROMBO
Mkoa: KILIMANJARO

*106# ..hii ni kuangalia taarifa ya usajili wa laini yako.


*150*00# ..wote hii mnafahamu...Mpesa vodacom.

*150*60#..hii ni airtell money...

*150*01#..hii ni tigopesa..inalipa

*149*01# ...kwa vifurushi vyote voda... voda mnarahisisha

*148*60# ...kupata vifurushi vyote airtell ...

*149*44#... niwezeshe..kopa vifurushi, dakika na bando. Airtell pekeee

*148*01#..kwa huduma zote za vifurushi tigo..


Sasa huduma zote tajwa hapo juu ni bure kama ukitozwa piga 100

Pia kuna sababu ya kuchagua tigopesa......... inalipa

JAMAN HAYA MASHAMBA KWANI TUTAKUFA NAYO.. ROMBO HII NI AIBU

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania,
Said Mwema
KATIKA hali isiyo ya kawaida Jeshi la
Polisi wilayani Rombo,limelazimika
kusimamia shughuli ya mazishi
baada ya kundi la watu wanne
kuzuia mwili wa marehemu Gaspar
Evarist (18) aliyefariki kwa ajali ya
pikipiki usizikwe shambani kwake
kijiji cha Muriae, wilayani Rombo.
Mkuu wa Polisi wilayani hapa, Ralph
Meela alisema kuwa vurugu hizo
zilisababishwa na mama wa
marehemu huyo na watoto wake
wakitaka mwili huo usizikwe kwenye
shamba la baba yake mzazi bali
wakauzike sehemu nyingine.
Akifafanua zaidi Meela alisema
chanzo cha mzozo huo ni baba wa
marehemu kufariki miaka mingi
iliyopita na hivyo waliokuwa
wakizuia mwili huo walidhani kuwa
endapo marehemu atazikwa hapo
shamba hilo litakua la kwake na
hivyo watakosa urithi.
Alisema katika vurugu hizo
zilisababisha uharibifu wa mali,
kwani wahusika walivunja msalaba
wa jumuiya pamoja na kumzuia
padre kuendesha ibada ambaye
ndugu walimtishia na hivyo
kuondoka kuepuka vurugu hizo.
Baada ya polisi kufika waliwakamata
watuhumiwa na kisha kusimamia
mazishi hayo.
Wakati huo huo mtu mmoja
aliyefahamika kwa jina la
Lewanga Kimario (23) mkazi wa kijiji
cha Mrere Mashati wilayani Rombo
amefariki dunia baada ya kujinyonga.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Rombo,Ralph
Meela amethibitisha kutokea kwa
tukio hilo. Meela alisema kuwa tukio
hilo lilitokea Juni 25, mwaka huu
majira ya saa 9:00 alasiri katika Kijiji
cha Mrere Mashati.
Meela alisema kuwa mwili wa
marehemu ulikutwa ukiwa
umening’inia juu ya paa la nyumba
yake.
Aidha alisema kuwa chanzo cha kifo
hicho bado hakijajulikana. Kwa
mujibu wa baba mzazi wa
marehemu, Thomas Kimario alisema
kabla ya tukio marehemu alikua
akisumbuliwa na malaria kali na
hivyo inaweza ikawa ndio sababu ya
kifo chake.

Waandishi wa habari tuna kazi mwaka huu.. nccr mageuzi waanxa upinzanu dhidi ya ukawa shuka nayo..

Ajali nyingine tena tanga..yaua wawili ..huko lushoto


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Zuberi
Mwombeji
Lushoto.Watu wawili wamefariki
dunia na wengine 15 kujeruhiwa
baada ya basi walilokuwa wakisafiria
kuacha njia na kupinduka katika Kijiji
cha Longoi Kata ya Mtae wilayani
Lushoto jana majira ya saa 11.00 jioni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,
Zuberi Mwombeji alisema leo kuwa
ajali hiyo imelihusisha gari la Kampuni
ya Shambalai ambalo lilikuwa likifanya
safari zake kutoka Dar es salaam
kuelekea Mtae ambapo lilipinduka na
kuingia kwenye korongo.
Kamanda Mwombeji amesema abiria
waliofariki katika ajali hiyo miili yao
imeshatambulliwa ambapo mmoja ni
mkazi wa Mtae na mwingine ni mkazi
wa Vuli.
Aidha Kamanda Mwombeji alieleza
kuwa chanzo cha ajali hiyo bado
hakijafahamika ila ubovu wa barabara
pia unaweza kuwa umechangia kwa
ajali hiyo.
Majeruhi wa ajali hiyo akiwemo
dereva wa basi hilo, Sadiki Ayoub
mkazi wa Mlalo wamelazwa katika
Hospitali ya Wilaya ya Lushoto kwa
matibabu zaidi na hadi leo hali zao
zinaendelea vizuri huku wengine
wakipewa ruhusa.
Ingawa dereva wa basi hilo
amejeruhiwa katika ajali hiyo lakini
yupo chini ya uangalizi wa jeshi la
polisi kwa ajili ya kuho

Majambazi ya kenya yauawa arusha...soma zaidi...




Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha
Liberatus Sabas
Arusha. Majambazi wane, wakiwemo
raia watatu wa Kenya wameuwa na
polisi mkoani Arusha baada ya
kuhusika kufanya matukio mbalimbali
ya ujambazi wa kupora silaha pamoja
na fedha.
Akizungumza na waandishi wa habari
mkoani hapa, Kamanda wa polisi,
Liberatus Sabas amesema kuwa
majambazi waliouwawa watatu ni
raia wa Kenya ambapo bado majina
yao kamili hayajajulikana huku raia
wa Tanzania ametambulika kwa jina la
Sixtus Alfredy.
Kamanda Sabas amesema kuwa ,polisi
walianza kujibu majibizano hayo ndipo
walipofanikiwa kuua majambazi
watatu ambao walikutwa na
vitambulisho vitatu vya Jamhuri ya
Kenya vyenye majina ya Simon Githinji
Kariuki,Bonifas Mwanmgi Mbulu,
Thadeo Kamau Njuguna na
kitambulisho kimoja cha UN-ICTR
chenye jina la Chacha John Marwa.
Vitambulisho vingine walivyokutwa
navyo ni leseni ya udereva iliyotolewa
Kenya yenye jina la Thadeo Kamau
Njuguna , kadi ya Benki ya Equity
Master Card yenye jina la Simon
Githinji pamoja na kadi ya Benki ya
Cooperative yenye jina la Thadeo
Kamau Njuguna , simu tano aina ya
Nokia , Tecno na Sumsung.
Amesema kuwa, majambazi hao
watatu kila mmoja alikutwa na bastola
pamoja na risasi , mabegi matatu
meusi ambapo baada ya kuyafungua
walikuta bunduki aina ya AK 47 mbili,
SMG moja, bastola tatu, magazine nne
za SMSg, risasi 85 za SMG na AK 47 na
risasi nyingine 28 za bastola.
Kamanda Sabas amesema kuwa, tukio
hilo lilitokea jana Septemba 17 mwaka
huu majira ya saa 3:30 usiku katika
maeneo ya Chekereni wilayani
Arumeru ambapo polisi walipata
taarifa za kiintelejensia toka Agosti 19
mwaka huu juu ya kuwepo kwa kundi
la majambazi wanaotoka nchi jirani ya
Kenya na kuja hapa nchini kwa nia ya
kufanya uporaji kwa kushirikiana na
majambazi wenzao wa hapa nchini.
Alisema miili ya marehemu wote
imehifadhiwa katika Hopsitali ya Mkoa
ya Mount Meru huku jeshi la polisi
likiendelea na uchunguzi zaidi wa
kuwatafuta watuhimiwa wengine
waliotoroka katika tukio hilo na
kubaini mtandao wa majamba

Alhamisi, 17 Septemba 2015

Jk aagiza haraka nyayo za laitole zifukuliwe


Arusha. Rais Jakaya Kikwete, ameagiza
Idara ya Mambo ya Kale kwa
kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro (NCAA), kuharakisha
kufukua nyayo za kale za Laitole ili
kuvutia watalii na kuongeza pato la
nchi.
Rais Kikwete alitoa agizo hilo juzi,
wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi
wa jengo la kisasa la ghorofa 15
linalomilikiwa na NCAA jijini Arusha.
Alisema anashangazwa na uongozi wa
NCAA na idara hiyo kuchukua muda
mrefu kufukua nyayo hizo za
bianadamu wa kwanza kutembea kwa
miguu, ambazo zipo katika eneo la
Laitole Nyayo.
“Kinachotakiwa pale ni kufukuliwa
nyayo na kujengwa jengo la kisasa la
vioo ambalo, litazuia jua na maji
kuingia.
“Pia litadhibiti mabadiliko ya hali ya
hewa ili kutoharibu nyayo hizo, watalii
wakifika Ngorongoro, wataziona
badala ya kuonyeshwa zilipofukiwa,”
alisema Rais Kikwete.
Akizungumza baada ya kuweka jiwe la
msingi, Rais Kikwete alipongeza
uongozi wa Ngorongoro kuwezesha
mradi huo mkubwa wa kitega uchumi.
Awali, Mwenyekiti wa Bodi ya
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro,
Balozi Mwanaidi Maajar alisema ujenzi
wa jengo la kitega uchumi utagharimu
Sh42.3 bilioni.
Alisema ujenzi huo ulianza Novemba
2013 na utakamilika Novemba 2016 na
hadi sasa ghorofa tatu zimejengwa.
Maajar alisema tayari mkandarasi
amelipwa kiasi cha Sh10.2 bilioni ili
kuendelea na ujenzi huo na kwamba
kila mwezi zinatarajiwa kujengwa
ghorofa mbili. Alisema mkandarasi wa
jengo hilo ni Kampuni ya kimataifa ya
CATIC Engineering Limited na
anaendelea vizuri na ujenzi.IMEEANDALIWA NA DENNIC LYAMUYA MTU WA KIRUA

Jumanne, 15 Septemba 2015

Ajali mbaya ya basi la metro litokalo tarakea to dar, iliyotokea handeni yaua warombo watano na wengine 39 kujeuriwa vibaya


Handeni.Watu watano wamekufa hapo
hapo na wengine 39 kujeruhiwa baada
ya basi la kampuni ya Matro
walilokuwa wakisafiria kutoka Rombo
kwenda Dar Es Salaam kuacha njia na
kupinduka katika Kijiji cha Manga
kata ya Mazingara wilayani Handeni.
Akithibitisha taarifa hizo Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Tanga, Zuberi
Mwombeji alisema kuwa ajali hiyo
ilitokea majira ya saa tano asubuhi leo
katika kijiji hicho na kudai kuwa bado
wanachunguza chanzo cha ajali ila
inaonyesha ilimshinda dereva na
kuacha njia.
Kamanda Mwombeji alisema maiti
watatu walitambuliwa na wengine
wawili hawajatambuliwa bado na
kuongeza kuwa majeruhi
walikimbizwa hospitali kwa matibabu.
Kamanda Mwombeji alisema dereva
wa gari hilo hakuweza kupatikana
ametoroka baada ya kutokea ajali
hiyo.WASONGA MROMBO NATOA POLE KWA WOTE WALIONUSURIKA NA AJALI HIYO NA PIA WOTE WALIOFIWA NA NDUGU ZAO ... MUNGU AWAZIDISHIE UVUMILIVU WAKATI WA KIPINDI HIKI KIGUMU...

Jumatatu, 14 Septemba 2015

Makala... story ya waziri ambaye alikuwa mchawi inaendelea hapa.. usikose nakala yako kwenye gazeti la ijumaa kila ijumaa kwa simulizi za kweli ... inaandaliwa na WASONGA MROMBO .. Mjinga wa rombo

ILIPOISHIA IJUMAA:
Waziri Meshack alishaniona , akatoka na
kuja kunilaki kwenye mlango wa gari.
“ Karibu mchungaji ,” akaniambia huku
akitabasamu.
Niliposhuka kwenye gari nilifuatana naye
hadi sebuleni mwake .
“ Karibu ukae ,” Meshack akaniambia .
Nilikaa katika kochi moja na yeye akakaa
kwenye lingine akinielekea mimi.
“ Nimeshukuru kuwa umeitikia wito
wangu, sijui nikupatie kinywaji gani ?”
Waziri Meshack akaniuliza .
“ Hapana. Sihitaji kinywaji chochote .
Asante sana. ”
SASA ENDELEA …
Waziri akanyamaza kimya kama vile
alikuwa akitafuta jinsi ya kuanza
kuniambia alichokuwa anataka kuniambia .
Zilipita kama sekunde nne au tano kisha
ghafla akasema .“ Mchungaji samahani
sana. Nilipaswa kukueleza niliyonayo
ofisini kwako lakini kwa vile wewe ni
mtumishi wa Mungu umekubali kuja
nyumbani kwangu kunisikiliza . Kwa hilo
nakushukuru sana. ”
Alinyamaza kidogo , akiendelea kufikiri
kisha akaendelea.
“ Binadamu ni binadamu si malaika ambao
hawatendi dhambi wala hawakosei.
Binadamu unaweza kumkosea Mungu na
hilo linawakuta watu wengi lakini Mungu
humpenda yule mkosefu anayejirudi,
akatubu dhambi zake. Na kutubu ni lazima
kuungama kama ambavyo mimi nataka
kufanya kwako wewe hii leo. ”
“ Umesema maneno ya Kimungu .
Nakubaliana na wewe kwa asilimia mia
moja kwamba kutenda dhambi ni
majaribu ya shetani . Lakini roho mtakatifu
anaweza kukuongoza ukafikia mahali
ukasema sasa narejea kwa Mola wangu.”
“ Ni kweli mchungaji . Sasa ninataka
kuungama makosa yangu na pia ninahitaji
maombi ili ile hatari ambayo ninaiona iko
mbele yangu isinisogelee tena .”
“ Sawa. ”
“ Kwanza nitaanza kukuelezea historia
yangu. Nimefahamika kwa Watanzania
baada ya kuwa waziri lakini maisha yangu
ya nyuma hayatambuliki. “ Mimi ni mzaliwa
wa Kijiji cha Mbogwe Wilaya ya Nzega
mkoani Tabora . Baba yangu Mzee
Shangwe (si jina lake halisi) alifariki dunia
nikiwa darasa la saba. Nikalelewa na babu
yangu Mzee Ngasa ( pia si jina lake halisi) .
Mzee Ngasa aliendelea kunisimamia
masomo yangu hadi nikaingia chuo kikuu .
Lakini wakati namaliza kidato cha sita,
babu yangu aliniita na kuniambia jambo
ambalo lilinishitua .
Ilikuwa usiku. Aliniita chumbani kwake ,
akaniambia .
“ Nataka kukueleza jambo zuri mjukuu
wangu. Naona sasa umekua mkubwa,
unapaswa kujua mambo ambayo yatakuja
kukuhusu sana .”
Aliponiambia hivyo , kidogo nilishituka.
Nikamuuliza.
“ Ni jambo gani hilo babu?”
“ Mjukuu wangu umezaliwa katika familia
ya wachawi,” akaniambia .
“ Nimezaliwa katika familia ya wachawi?”
“ Ndiyo .”
“ Ni nani na nani ni wachawi katika familia
yetu?”
“ Baba yako alikuwa mchawi na uchawi huo
nilimfundisha mimi babu yako. ”
Maneno ya Mzee Ngasa yalinikumbusha
mambo kadhaa ambayo nilikuwa nikiyaona
pale nyumbani siku za nyuma . Nilipokuwa
ninaingia chumbani mwa babu wakati
mwingine hukuta vitu visivyo vya
kawaida.
Kuna siku nilikuwa natafuta panga,
nikachungulia uvunguni mwa kitanda cha
babu nikashituka kukuta mkono wa mtoto
mchanga uliokaushwa na kuwa kama
kijiko. Pia nilikuta ngozi ya kichwa cha
binadamu ikiwa na nywele zake.
Kitu kingine nilichokiona hakikuwa cha
kawaida kwa babu, alikuwa akienda kulima
shambani kwake usiku . Hupenda
kuondoka nyumbani usiku wa manane na
kurudi wakati wa alfajiri. Nilipokuwa
namuuliza babu unakwenda wapi ananijibu
kuwa anakwenda shamba .
Hivi vitu vilianza kunitia shaka mapema
sana kuwa babu yangu hakuwa mtu wa
kawaida. Hivyo siku ile aliponiambia kuwa
yeye ni mchawi lilikuwa jambo ambalo
nilianza kulishuku tangu siku za nyuma .
Babu akaendelea kuniambia .
“ Nilidhani ningekufa kabla ya baba yako .
Nilikuwa nimemuandaa yeye kurithi
mfuko wangu wa uchawi lakini akatangulia
kufa yeye kabla yangu.”
Babu akanyamaza kidogo na kunitazama
usoni kwangu . Alipoona sikuwa
nimeshituka sana akaendelea kuniambia .
“ Baba yako nilimfundisha uchawi lakini
hakuwahi kutoa kitu . Sasa mimi nilitakiwa
nikutoe wewe nikakataa.”
“ Sijakuelewa babu. Umeniambia baba
yangu hakuwahi kutoa kitu na wewe
umetakiwa unitoe mimi. Hebu fafanua
hapo babu.”
“ Yeye aliwahi kula nyama za wenzake .
Ukiwa mchawi ni lazima umtoe kafara
mwanao au mtu wako wa karibu ili
mumle. Yeye hakuwahi kutoa kafara mtu
yeyote. Badala yake nikaambiwa mimi
nikutoe wewe…”
“ Yaani babu unitoe mimi niliwe na
wachawi?” nikamuuliza babu kwa
mshituko .
“ Lakini nimekataa. ”
“ Hata mimi nisingekubali upumbavu huo . ”
“ Pale unapotakiwa unakuwa huna ujanja
mjukuu wangu. Utaonekana umekufa .
Ukienda kuzikwa, usiku tunakwenda
kufukua kaburi tunakuchukua. ”
“ Kwa hiyo mnakula nyama za maiti?”
“ Mbona ni kawaida mjukuu wangu. Kwani
utajua kama ni nyama ya maiti? Ni nzuri
sana.”
“ Sasa ulipokataa kunitoa wakakuambia
nini?”
“ Kwanza unapotakiwa kutoa mtu wako
huwezi kukataa ila mimi nilitoa hoja
zangu . Nilisema kwamba wewe
nimeshakuandaa kuwa mrithi wangu na
katika familia yetu umebaki wewe peke
yako. Nikawaambia kwamba karibuni
utaoa mke na mtoto utakayezaa kwanza
ndiye tutamtoa . Hapo ndiyo
walinikubalia.”
Maneno ya babu yalinikumbusha ule
mkono wa mtoto mchanga nilioukuta chini
ya mvungu wa kitanda chake na ile ngozi
ya kichwa iliyokuwa na nywele. Kutokana
na maelezo yake niliamini kwamba ule
mkono ulikuwa wa maiti ya mtoto
iliyofukuliwa na ile ngozi yenye nywele
ilichunwa kutoka katika kichwa cha
marehemu ambaye pia alikuwa
ameshazikwa .
“ Sasa ili kuyasitiri maisha yako na ili
nionekane mkweli nataka nianze
kukufundisha hii kazi ili wewe uwe kama
mimi,” babu akaniambia .
Baada ya kuyatafakari maneno yake kwa
makini nilimwambia .
“ Sikiliza babu…”
Je, nini kitaendelea? Usikose Ijumaa
kwenye Gazeti la Ijumaa .
Je, nini kiliendelea ? Usikose kufuatilia
Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa .


USIKOSE KUTEMBELEA PAGE HII IJUMAA ILI KUPATA MWENDELEZO WA SIMULIZI HIYO.... ROMBO MPOOOO.....LIKE PAGE YETU YA FACEBOOK ... www.facebook.com/eaglefm97 uunganishwe na mamia ya warombo kwa maendeleo ya wilaya yetu ya rombo ... na kukomesha tabia ya kusengenywa kwamba tumeshindwa kazi ... tupia like yako sasa...

Makala... story ya waziri ambaye alikuwa mchawi inaendelea hapa.. usikose nakala yako kwenye gazeti la ijumaa kila ijumaa kwa simulizi za kweli ... inaandaliwa na WASONGA MROMBO .. Mjinga wa rombo

ILIPOISHIA IJUMAA:
Waziri Meshack alishaniona , akatoka na
kuja kunilaki kwenye mlango wa gari.
“ Karibu mchungaji ,” akaniambia huku
akitabasamu.
Niliposhuka kwenye gari nilifuatana naye
hadi sebuleni mwake .
“ Karibu ukae ,” Meshack akaniambia .
Nilikaa katika kochi moja na yeye akakaa
kwenye lingine akinielekea mimi.
“ Nimeshukuru kuwa umeitikia wito
wangu, sijui nikupatie kinywaji gani ?”
Waziri Meshack akaniuliza .
“ Hapana. Sihitaji kinywaji chochote .
Asante sana. ”
SASA ENDELEA …
Waziri akanyamaza kimya kama vile
alikuwa akitafuta jinsi ya kuanza
kuniambia alichokuwa anataka kuniambia .
Zilipita kama sekunde nne au tano kisha
ghafla akasema .“ Mchungaji samahani
sana. Nilipaswa kukueleza niliyonayo
ofisini kwako lakini kwa vile wewe ni
mtumishi wa Mungu umekubali kuja
nyumbani kwangu kunisikiliza . Kwa hilo
nakushukuru sana. ”
Alinyamaza kidogo , akiendelea kufikiri
kisha akaendelea.
“ Binadamu ni binadamu si malaika ambao
hawatendi dhambi wala hawakosei.
Binadamu unaweza kumkosea Mungu na
hilo linawakuta watu wengi lakini Mungu
humpenda yule mkosefu anayejirudi,
akatubu dhambi zake. Na kutubu ni lazima
kuungama kama ambavyo mimi nataka
kufanya kwako wewe hii leo. ”
“ Umesema maneno ya Kimungu .
Nakubaliana na wewe kwa asilimia mia
moja kwamba kutenda dhambi ni
majaribu ya shetani . Lakini roho mtakatifu
anaweza kukuongoza ukafikia mahali
ukasema sasa narejea kwa Mola wangu.”
“ Ni kweli mchungaji . Sasa ninataka
kuungama makosa yangu na pia ninahitaji
maombi ili ile hatari ambayo ninaiona iko
mbele yangu isinisogelee tena .”
“ Sawa. ”
“ Kwanza nitaanza kukuelezea historia
yangu. Nimefahamika kwa Watanzania
baada ya kuwa waziri lakini maisha yangu
ya nyuma hayatambuliki. “ Mimi ni mzaliwa
wa Kijiji cha Mbogwe Wilaya ya Nzega
mkoani Tabora . Baba yangu Mzee
Shangwe (si jina lake halisi) alifariki dunia
nikiwa darasa la saba. Nikalelewa na babu
yangu Mzee Ngasa ( pia si jina lake halisi) .
Mzee Ngasa aliendelea kunisimamia
masomo yangu hadi nikaingia chuo kikuu .
Lakini wakati namaliza kidato cha sita,
babu yangu aliniita na kuniambia jambo
ambalo lilinishitua .
Ilikuwa usiku. Aliniita chumbani kwake ,
akaniambia .
“ Nataka kukueleza jambo zuri mjukuu
wangu. Naona sasa umekua mkubwa,
unapaswa kujua mambo ambayo yatakuja
kukuhusu sana .”
Aliponiambia hivyo , kidogo nilishituka.
Nikamuuliza.
“ Ni jambo gani hilo babu?”
“ Mjukuu wangu umezaliwa katika familia
ya wachawi,” akaniambia .
“ Nimezaliwa katika familia ya wachawi?”
“ Ndiyo .”
“ Ni nani na nani ni wachawi katika familia
yetu?”
“ Baba yako alikuwa mchawi na uchawi huo
nilimfundisha mimi babu yako. ”
Maneno ya Mzee Ngasa yalinikumbusha
mambo kadhaa ambayo nilikuwa nikiyaona
pale nyumbani siku za nyuma . Nilipokuwa
ninaingia chumbani mwa babu wakati
mwingine hukuta vitu visivyo vya
kawaida.
Kuna siku nilikuwa natafuta panga,
nikachungulia uvunguni mwa kitanda cha
babu nikashituka kukuta mkono wa mtoto
mchanga uliokaushwa na kuwa kama
kijiko. Pia nilikuta ngozi ya kichwa cha
binadamu ikiwa na nywele zake.
Kitu kingine nilichokiona hakikuwa cha
kawaida kwa babu, alikuwa akienda kulima
shambani kwake usiku . Hupenda
kuondoka nyumbani usiku wa manane na
kurudi wakati wa alfajiri. Nilipokuwa
namuuliza babu unakwenda wapi ananijibu
kuwa anakwenda shamba .
Hivi vitu vilianza kunitia shaka mapema
sana kuwa babu yangu hakuwa mtu wa
kawaida. Hivyo siku ile aliponiambia kuwa
yeye ni mchawi lilikuwa jambo ambalo
nilianza kulishuku tangu siku za nyuma .
Babu akaendelea kuniambia .
“ Nilidhani ningekufa kabla ya baba yako .
Nilikuwa nimemuandaa yeye kurithi
mfuko wangu wa uchawi lakini akatangulia
kufa yeye kabla yangu.”
Babu akanyamaza kidogo na kunitazama
usoni kwangu . Alipoona sikuwa
nimeshituka sana akaendelea kuniambia .
“ Baba yako nilimfundisha uchawi lakini
hakuwahi kutoa kitu . Sasa mimi nilitakiwa
nikutoe wewe nikakataa.”
“ Sijakuelewa babu. Umeniambia baba
yangu hakuwahi kutoa kitu na wewe
umetakiwa unitoe mimi. Hebu fafanua
hapo babu.”
“ Yeye aliwahi kula nyama za wenzake .
Ukiwa mchawi ni lazima umtoe kafara
mwanao au mtu wako wa karibu ili
mumle. Yeye hakuwahi kutoa kafara mtu
yeyote. Badala yake nikaambiwa mimi
nikutoe wewe…”
“ Yaani babu unitoe mimi niliwe na
wachawi?” nikamuuliza babu kwa
mshituko .
“ Lakini nimekataa. ”
“ Hata mimi nisingekubali upumbavu huo . ”
“ Pale unapotakiwa unakuwa huna ujanja
mjukuu wangu. Utaonekana umekufa .
Ukienda kuzikwa, usiku tunakwenda
kufukua kaburi tunakuchukua. ”
“ Kwa hiyo mnakula nyama za maiti?”
“ Mbona ni kawaida mjukuu wangu. Kwani
utajua kama ni nyama ya maiti? Ni nzuri
sana.”
“ Sasa ulipokataa kunitoa wakakuambia
nini?”
“ Kwanza unapotakiwa kutoa mtu wako
huwezi kukataa ila mimi nilitoa hoja
zangu . Nilisema kwamba wewe
nimeshakuandaa kuwa mrithi wangu na
katika familia yetu umebaki wewe peke
yako. Nikawaambia kwamba karibuni
utaoa mke na mtoto utakayezaa kwanza
ndiye tutamtoa . Hapo ndiyo
walinikubalia.”
Maneno ya babu yalinikumbusha ule
mkono wa mtoto mchanga nilioukuta chini
ya mvungu wa kitanda chake na ile ngozi
ya kichwa iliyokuwa na nywele. Kutokana
na maelezo yake niliamini kwamba ule
mkono ulikuwa wa maiti ya mtoto
iliyofukuliwa na ile ngozi yenye nywele
ilichunwa kutoka katika kichwa cha
marehemu ambaye pia alikuwa
ameshazikwa .
“ Sasa ili kuyasitiri maisha yako na ili
nionekane mkweli nataka nianze
kukufundisha hii kazi ili wewe uwe kama
mimi,” babu akaniambia .
Baada ya kuyatafakari maneno yake kwa
makini nilimwambia .
“ Sikiliza babu…”
Je, nini kitaendelea? Usikose Ijumaa
kwenye Gazeti la Ijumaa .
Je, nini kiliendelea ? Usikose kufuatilia
Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa .


USIKOSE KUTEMBELEA PAGE HII IJUMAA ILI KUPATA MWENDELEZO WA SIMULIZI HIYO.... ROMBO MPOOOO.....LIKE PAGE YETU YA FACEBOOK ... www.facebook.com/eaglefm97 uunganishwe na mamia ya warombo kwa maendeleo ya wilaya yetu ya rombo ... na kukomesha tabia ya kusengenywa kwamba tumeshindwa kazi ... tupia like yako sasa...

Efm...yazindua rasmi kipindi na shindano la uhondo dar.. na mwanahabari wetu DENNIC LYAMUYA...




Wanahabari wakichukua tukio .
EFM radio kupitia kipindi chake kipya
kiitwacho Uhondo imendaa shindano la
Kanga kwa ajili ya wanawake wote
wasikilizaji wa redio hiyo .
Akizungumza na wanahabari leo kwenye
ofisi za Efm radio zilizopo Kawe , jijini Dar
es Salaam, Mtangazaji na mtayarishaji wa
kipindi hicho , Dina Marios amesema kuwa
lengo la shindano hilo amabalo linaanza
leo na kuishia Oktoba 5 mwaka huu , lina
lengo la kuwahamasisha wanawake
wakione kipindi hicho kuwa kimekuja kwa
ajili yao.
Alisema kuwa kipindi hicho kitaweza
kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na
njia nyingine kumwonesha mwanamke
namna nyingine ya kumkomboa badala ya
kukakaa nyumbnani . Faida nyingine ni
pamoja na wanawake kujifunza ujasiliamali
kupitia biashara ya khanga .
“ Mfumo wa shindano lenyewe utakuwa
kama ifuatavyo yaani wasikilizaji wa Efm
redio ambao ni wanawake wanakaribishwa
kushiriki shindano la kubuni maneno ya
khanga kupitia kipindi cha ‘ Uhondo’ na
maneno hayo yawe na neno ‘ UHONDO ’
kwa kutumia mfano Uhondo wa Ngoma
uingie ucheze ,” alisema Dina nakuongeza:
“ mshindi wetu atajinyakulia kitita cha
shilingi za kitanzania milioni moja,”
alisema.
Vile vile aliongeza kuwa shindano hilo
halitaishia hapo, kwani baada ya kupata
mshindi neno lake la ushindi
zitatengenezwa khanga zitakazoandikwa
neno hilo ikiwa ni hatua ya pili sasa ya
kumwezesha mwanamke kujikwamua
kiuchumi.
Hata hivyo , aliongeza kuwa baada ya
kutengenezwa khanga hizo, Efm kupitia
kipindi hicho , itatoa nafasi kwa wanawake
kutengeneza pesa na kujikwamua kwa
kuuza khanga hizo na mwanamke yeyote
hasa kwa mikoa ya Dar es Salaam na
Pwani atachukua khanga hizo na kuziuza
pasipo kulipia pesa yoyote ambapo kwa
kila doti moja ya khanga atapata asilimia
30 ya pesa .Alisema washiriki watapewa
mafunzo maalum kwa jili ya kuwawezesha
katika uuzaji wao.
( NA DENIS LYAMUYA/EFM)

NAFASI YA KAZI TANESCO MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 25 SEPTEMBA 2015

EMPLOYMENT OPPORTUNITIES
INTERNAL AND EXTERNAL
ADVERTISEMENT SYSTEM OPERATORS -
09 POSTS:
Tanzania Electric Supply Company
(TANESCO) is focusing on increasing the
outreach and service quality of its Energy
products for Tanzanians. Next to its
current passion as a leading provider of
electricity is to be more efficient
customer focused utility for Tanzania and
beyond. The Company has the largest
electricity generation, transmission and
distribution network in Tanzania. In order
to reach its goals, the Company is
investing heavily in its generation,
transmission and distribution network, its
business systems and human capital.
TANESCO now invites applicants who are
self-motivated, honest, hardworking and
committed individuals to fill the under-
mentioned positions for Transmission
Business Unit at Head Office and
Upcountry.
Specific attributes for the Positions to be
filled
All Candidates must:
• Demonstrate outstanding performance
track record;
• Demonstrate highest degree of
integrity;
• Possess good communication and
interpersonal skills;
• Be self-driven and capable of working
with minimal supervision;
• Be capable of delivering expected
results and ability to work under pressure
with tight deadlines.
• Must be computer literate.
============
JOB TITLE : SYSTEM OPERATORS - 09
POSTS
NEW CITY CENTRE
Reports To: Principal Grid Operation
Engineer
REF. NO. 01
POSITION OBJECTIVE
• Grid System monitoring to ensure that
a continuous and reliable flow of electric
power supply from generating plants to
various places of grid destination and
distribution points are maintained.
PRINCIPAL ACCOUNTABILITIES
• Collect all necessary initial technical
data in the daily log sheets and defect
register book.
• Issue permits to work, limitation of
access, sanction of test after proper
Isolation of equipment at switch yard
before people start working to ensure
highest safety standards are observed
and maintained all the times in order to
preserve life and property.
• Maintain close liaison with Grid
Control Centre (SCADA), Generating
plants stations and other grid substation
Operators to ensure smooth restoration
of power supply in case of System power
failure.
• Report a day recorded shift events to
System control Supervisor to ensure the
higher authority get informed for record
and action.
PROFESSIONAL AND MINIMUM
REQUIREMENTS
• FTC in Electrical Engineering or holder
of (Ordinary Diploma in Electrical
Engineering) NTA level 6 from a
recognized Institute OR
• Relevant Technical Vocational Training
(Trade Test) from recognized Vocational
Training Institutions.
• Working experience will be an added
advantage.
• Ability to work outside normal hours,
weekends and holidays to support “24/7”
real time operations.
REMUNERATION
An attractive compensation package
based on performance and commensurate
with the responsibility will apply to
successful candidates. All positions’ terms
of employment are performance based
contracts.
HOW TO APPLY
If you are a Tanzanian National and
interested in the position you should
apply by sending an application letter,
giving full details of previous work life
history, qualifications and include two (02)
work references. Application letters
should be marked ‘’Private and
Confidential addressed to:
SENIOR MANAGER HUMAN RESOURCES
TANESCO LTD UMEME PARK
P. O BOX 9024
DAR ES SALAAM
Application close date: 25th September,
2015
Source: Daily News 14th September, 2015

NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA BUSEGA MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 25 SEPTEMBA 2015

HALMASHAURI YA WILAYA YA
BUSEGA
TANGAZO LA KAZI
(Barua zote zipelekwe kwa
Mkurugenzi Mtendaji)
Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Busega
anapenda kuwatangazia
watanzania wote wenye sifa na
nia ya kufanya kazi katika
Halmashauri ya Wilaya ya Busega
kuomba nafasi zifuatazo:-
DRERVA NAFASI 3
SIFA/ELIMU/UJUZI
i. Awe na cheti cha kidato cha
nne (IV)
ii. Awe na Leseni dalaja la “C”
ya uendeshaji magari
iii. Awe na uzoefu wa
kuendesha magari kwa muda
usiopungua miaka mitatu (3) bila
kusababisha ajari.
iv. Awe na cheti cha majaribio
ya ufundi darafa la II.
KAZI NA MAJUKUMU
i. Kuendesha magari ya aina
zote katika Halmashauri.
ii. Kuhakikisha gari na vyombo
vyake vipo katika hali nzuri
wakati wote na kufanya
uchunguzi wa gari kabla na baada
ya safari ili kugundua ubovu
unaohitaji matengenezo.
iii. Kufanya matengenezo
madogomadogo katika gari.
iv. Kutunza na kuandika daftari
la safari (Log-Book) kwa safari
zote.
NGAZI YA MSHAHARA
Kianzio cha Mshahara TGOS A (1)
UMRI
Mwombaji awe na umre
usiopungua miaka 18 na usiozidi
miaka 45.
MAELEZO YA JUMLA
Maombi yote yawasilishwe
yakiwa yameambatanishwa na
CV pamoja na nakala za vyeti vya
kuhitimu elimu na mafunzo
(vyeti vinavoonyeshwa kiwango
cha ufaulu na sio (leaving
certificate).
MUHIMU
Muombaji anatakiwa atume vyeti
vyake halisi na halali kwani
uhakiki utafanyika katika vyuo
ulivyopitia na Baraza la Mitihani.
Udanyanyifu wowote ukibainika
hatua za kisheria zitachukuliwa.
Maombi yote yatumwe kwa
Mkurugenzi
Halmashauri ya Wilaya
S.L.P 157
BUSEGA
Mwisho wa kupokea maombi ni
tarehe 25/09/2015 saa 9:30
Alasiri.
Source: Mwananchi 11th
September, 2015

Haya sasa mashabiki wa soka mpoooo..kazi ya champions leage inaanza leo rasmi ... usikose kupata update ya matokeo yote hapa...


Msimu mpya wa michuano ya Ligi ya
mabingwa wa Ulaya kwa msimu wa
2015-2016 utaanza leo kwa nyasi za
Viwanja vinane kuwaka moto.
Katika kundi A, PSG itawaalika timu ya
Malmo Ff kutoka Sweden huku Real
Madrid, wakiwa wenyeji wa Shakhtar
Donetsk, mchezo utakaopigwa kwenye
Dimba la Santiago Bernabéu.
Katika kundi B PSV Eindhoven, ya
Uholanzi watakua wenyeji wa
Manchester United, toka Uingereza huku
mchezaji wa zamani kwa kikosi hicho
Memphis Depay, akirejea kucheza na
timu yake hiyo ya zamani. Mchezo
wingine wa kundi hili VfL Wolfsburg, ya
Ujerumani watashuka dimbani kuwakabili
CSKA Moscow, kutoka Urusi.
Michezo mingine itayopigwa leo hi ya
michuano hii.
Kundi C
Galatasaray na Atletico Madrid
Benfica na FC Astana
KUNDI D
Man City na Juventus
Sevilla na Borussia Monchengladbach

Jumapili, 6 Septemba 2015

Habari ya tanzia Mkuu wa chuo cha nothern highland aaga dunia

Aliyekuwa mkuu wa chuo cha ualimu nothern higland j. S. Kirenga ameaaga dunia ... bado chanzo hiki hakijatambua nini hasa kilichosababisha kifo chake .. tutakapo jua zaidi juu yA kifoo chake tutawahabarisha ... mkuu kirenga wana northen walikupenda lakini mungu amekupenda zaidi pumzika kwa amani kirenga....




Hapoo juu ni mkuu wa chuo cha northen ambaye kwa sasa ni marehemu ... poleni sana wananothern.. poleni sana crow nzima eagle room na eaglefm kutoka kwa wasonga mrombo mimi zina cha zaidi zaidi ya kusema kirenga tulikupenda lakini mungu ndiye mtengenezaji na mbomoaji pumzika kwa amani na tutakukumbuka milele.

Ijumaa, 4 Septemba 2015

Nyota watatu kuiua Nigeria watajwa Wakati timu ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’ ikijiandaa kuikabili Nigeria, wachezaji watatu au


Wachezaji hao ni Mbwana Samatta, John
Bocco na Thomas Ulimwengu.
Dar es Salaam. Wakati timu ya Taifa
ya Tanzania, ‘Taifa Stars’ ikijiandaa
kuikabili Nigeria, wachezaji watatu au
wanne wameonekana ndiyo
watakaoamua mechi hiyo mapema
endapo watacheza katika ubora wao.
Wachezaji hao, Mbwana Samatta, John
Bocco na Thomas Ulimwengu ndiyo
pekee wameshikilia mkononi roho za
Watanzania ili kuhakikisha wanaipa
ushindi wa mapema Stars.
Stars inaikabili Super Eagles ya
Nigeria Jumamosi katika mchezo wa
kuwania tiketi ya kucheza fainali za
Mataifa ya Afrika (Afcon) mwaka
2017. Timu hiyo ilirejea jana saa 9
alfajiri ikitokea Istanbul, Uturuki
ilikoweka kambi ya wiki moja
kujiandaa na mchezo huo dhidi ya
Nigeria utakaochezwa kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mchambuzi masuala ya soka, Joseph
Kanakamfumu aliliambia gazeti hili
jana kuwa mchezaji pekee anayeweza
kuamua mchezo huo kwa kuleta
matokeo mazuri ni Samatta.
Kanakamfumu alisema Samatta ndiye
atabeba matumaini ya Watanzania,
lakini kama ataamua kucheza mpira
kwa kiwango ambacho amekuwa
akikionyesha akiwa TP Mazembe.
Kwa upande wake, Ally Mayay
anawataja Samatta, Ulimwengu na
Mrisho Ngassa kama wachezaji
wanaoweza kuibeba Stars.
Alisema tatizo la Stars siyo ulinzi wala
kiungo, isipokuwa washambuliaji
ambao wanakosa umakini wa kutumia
nafasi zinazopatikana. Kulingana na
Nigeria ilivyo na kikosi imara cha
wachezaji wengi wanaocheza soka la
kulipwa nje ya nchi hiyo, Stars haiko
nyuma kwani inao wachezaji
inaowategemea kuleta furaha kwa
mashabiki.
Samatta, Ulimwengu wanaocheza soka
la kulipwa kwenye klabu ya TP
Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo (DRC), tayari wamewasili
nchini na Ngassa anayecheza soka ya
kulipwa Afrika Kusini akisubiriwa.
Enyeama ‘aiogopa’ Stars
Wakati huohuo, nahodha na kipa wa
Nigeria, Vincent Enyeama amejitoa
kwenye kikosi kitakachoivaa Taifa
Stars, Jumamosi.
Mtandao wa Supersport.com
umekariri vyanzo kutoka kambi ya
Super Eagles mjini Abuja ukieleza
kuwa kipa huyo mwenye miaka 33
amejiondoa kwa sababu za kifamilia.
Kujitoa kwa Enyeama kunaifanya
Super Eagles kumuita kipa Carl Ikeme
wa Wolves au Ikechukwu Ezenwa wa
Sunshine Stars.






Ewe mpenzi msomaji usipoteze kura yako mpe lowasa tupaate mabadiliko ya kweli ok,

Mke wa docta slaa afunguka kuhusu mumewe docta.... amesema slaa ni mnafiki na mtu mwenye tamaa .. huku aliwatekeleza watoto wake amestaafu upadre kwa sababu ya tamaa za mwili.. hafai kusikilizwa kbisaa ametuhadaa vya kutosha sote tumkatae..


Mbunge wa viti maalumu wa Chadema,
Rose Kamili akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu
kauli aliyoitoa aliyekuwa katibu mkuu wa
Chadema, Dk Willibrod Slaa . Kushoto ni
binti wa Dk Slaa, Emiliana Slaa na Linus
Slaa. Picha na Venance Nestory
Dar es Salaam. Kauli ya Katibu Mkuu
wa zamani wa Chadema Dk Willibrod
Slaa kuhusu hatma yake kisiasa
imeendelea kutikisa baada ya mke
wake wa zamani, Rose Kamili kuibuka
na kusema amesikitishwa na kauli
alizozitoa mume wake huyo
alipozungumza na waandishi wa
habari Septemba Mosi.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana,
Kamili alisema wakati Dk Slaa
anatangaza kung’atuka kwenye siasa
alisema amekuwa akila mihogo na
familia yake, jambo ambalo si la kweli.
Alisisitiza kuwa japokuwa mihogo siyo
chakula kibaya lakini watoto wake,
Elimiana na Linus Slaa hawakuwahi
kuishi kwa kutegemea chakula hicho
ingawa walitelekezwa na baba yao
tangu mwaka 2010.
Kamili ambaye pia ni mbunge wa
kuteuliwa wa Chadema, alisema Dk
Slaa aliwadanganya wananchi
aliposema kuwa haongei na mgombea
wa urais wa Chadema anayeungwa
mkono na Ukawa, Edward Lowassa na
Waziri Mkuu wa zamani Frederick
Sumaye kuwa siyo kweli kwa kuwa
amekuwa akiwasiliana na viongozi hao.
Alisimulia kuwa mwaka 1995 wakati
Dk Slaa alipoenguliwa na CCM
kugombea ubunge Jimbo la Karatu,
alikwenda nyumbani kwa Lowassa
kuomba ushauri.
“Lowassa alisema ‘mimi nakushauri
ujiunge na chama chochote’” alisema
Kamili na kuongeza kuwa marafiki
zake Dk Slaa nao walimshauri aingie
chama chochote.
“Mimi namshangaa anavyosema
haongei na Lowassa… hizo chuki
anazosema yeye kama padri mstaafu
zinatoka wapi?,” alisema Kamili.
Kuhusu Sumaye, Kamili alisema kuwa
wiki tatu zilizopita alipigiwa simu na
kiongozi huyo akimuulizia namba ya
Dk Slaa, baada ya kumtafuta kwenye
simu yake bila mafanikio.
“Aliniuliza mbona simu yake
haipatikani, nikampa akampigia
wakaongea,” alisema.
Mjini Bukoba, Askofu Msaidizi wa
Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius
Kilaini amesema anamshangaa Dk Slaa
kutoa tuhuma dhidi ya maaskofu kwa
kuwa aliwahi kuwa Katibu wa Baraza
la Maskofu na anajua wanavyofanya
kazi.
Akizungumza katika mahojiano
maalumu na Mwananchi mjini Bukoba,
Askofu Kilaini alisema Maaskofu
hawanunuliki na kanisa halifungamani
na upande wowote wa kisiasa huku
akidai huenda kauli hiyo ilimponyoka.
Kauli ya Askofu Kilaini imetolewa
ikiwa ni baada ya siku chache
zilizopita aliyekuwa Katibu Mkuu wa
Chadema, Slaa kutangaza kustaafu
siasa huku akiwatuhumu baadhi ya
maaskofu kupokea rushwa kutoka kwa
mmoja wa wagombea.
‘’Wanasiasa ni wachangiaji wazuri
katika hafla mbalimbali za kanisa
lakini hata siku moja huwezi kusema
maaskofu wamenunuliwa Kanisa
linashikilia maadili na kuombea amani
kwa Taifa,’’ alisema Kilaini
Pia Askofu Kilaini aliongeza kuwa
matamko kama yaliyotolewa na Dk
Slaa yanaweza kusababisha
mkanganyiko kwenye jamii, huku
akionya hatari ya dini kutumika
kwenye mijadala kuelekea Uchaguzi
Mkuu.
Aidha alirejea mwaka 2000 kuwa
baada ya vurugu kuanza kutokea
Zanzibar na wananchi kukimbia,
waliitana viongozi wa madhehebu yote
ya dini na kutoa tamko la pamoja
wakionya dini zisihusishwe kwenye
harakati za kisiasa.

Jumatano, 2 Septemba 2015

Ukawa wamjibu Slaa, wasema tuhuma alizotoa zinalipasua taifa Siku moja baada ya Dk Willibrod Slaa kuibuka na kuelezea kilichotokea wakati wa kumkaribisha


Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James
Mbatia
Dar es Salaam. Siku moja baada ya Dk
Willibrod Slaa kuibuka na kuelezea
kilichotokea wakati wa kumkaribisha
Edward Lwoassa Ukawa na hatimaye
kutangaza kuachana na siasa,
Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James
Mbatia amejibu tuhuma zilizotolewa
na Dk Slaa huku akitahadharisha kuwa
zinalenga kulipasua taifa.
Mbatia ambaye ni Mwenyekiti Taifa
wa NCCR Mageuzi amesema leo jijini
Dar es Salaam alipokuwa akizungumza
an waandishi wa habari kuwa mambo
yaliyozungumzwa Dk Slaa ikiwa ni
pamoja na kashfa zakuwatuhumu
viongozi wa dini kuhongwa na Lowassa
si yakweli na yanaweza kuligawanya
taifa.
Mbatia amesema kuwa Dk Slaa
angepaswa kutoa hoja zake na sio
kuwashambulia watu binafsi
wakiwemo viongozi wa dini.
‘’Mimi nilitegemea Dk. Slaa ataeleza
hoja zake, lakini hoja za kashfa za
kuwahusisha viongozi wa dini hasa
maaskofu ni hoja ambazo ni wazi
zimelenga kulipasua taifa’’ alisema
Mbatia.
Pia Mbatia amekiri kuwa Dk. Slaa
alishiriki katika mchakato wa
kumkaribisha Lowassa lakini katika
vikao vyote Lowassa hakuwahi kusema
atakuja na wabunge toka Chama Cha
Mapinduzi.
‘’ Katika kikao cha kujadili juu ya
kumpokea Lowassa tukiwa na viongozi
waandamizi wa Ukawa pamoja na
Lowasaa kilichofanyika tarehe 20
mwezi wa saba , Lowassa hajawahi
kutamka kuwa atakuja na wabunge 50
toka Chama cha Mapinduzi, wala
hakusema atakuja na wenyeviti wa
mikoa na wilaya’’
Akizungumzia suala la Dk. Slaa kudai
alipewa rushwa ya Sh500m ili kuzuia
ripoti ya Richmond isiingie bungeni,
Mbatia ameuliza kwanini Dk.Slaa
hakuripoti kipindi hicho na anakuja
kuongelea sasa.
“Nashangaa tangu sakata la Richmondi
litokee ni miaka saba hadi sasa, lakini
Dk. Slaa hakuwahi kusikika
akilizungumzia, na kwanini hakuripoti
kwenye vyombo vinavyohusika’’ alihoji
Mbatia.
Aidha Mbatia amevitaka vyombo vya
habari kuandaa midahalo maalum
ambayo itawahusisha viongozi wa
kisiasi ili kujibu mambo
wanayotuhumiwa

Alikiba, diamond, vanesa na kingwendu wapeta mashindano ya bingwa kenya... soma vitengo vilivyopo kwenye mashindano hayo hapa...


Miongoni mwa wasanii wa Tanzania
waliotajwa kuwania tuzo hizo ni pamoja
na Diamond Platnumz, Alikiba, Vanessa
Mdee, Joh Makini, Ommy Dimpoz, Lady
Jaydee na wengine.
Kwa mara ya kwanza Bongo5 imetajwa pia
kuwania kipengele cha Bingwa
Entertainment Site of the Year.
Hii ni orodha kamili ya majina:
Bingwa New Artist Of The Year
Amos & Josh
Sosuun
Timmy
Dufla
Renee
Papa Denis
Bingwa Showbiz Personality Of The Year
Larry Madowo
Churchill
Willis Raburu
Buddha Blaze
Sheila Kwamboka
Chris Kirubi
Bingwa Kenya DJ Of The Year
Dj Genius
DJ Lita
Dj Pierra
Dj Cross Fade
DJ Flash
DJ Ace
Bingwa Best Video Of The Year East Africa
Nerea (Amos & Josh & Sauti Sol)
Fimbo Ya Tatu – Grand Pa
Papa Denis
Jamaican Girl – Wyre
Wale Wale – Chameleone
Chekecha – Alikiba
Bingwa Video Director Of The Year East
Africa
Young Wallace (KE)
Enos Olik (KE)
Adam Juma (TZ)
Super Star (UG)
J Blessing (KE)
Sammy Dee (KE)
Bingwa Come Back of the year
Octopizzo
Abbas
DNA
Wakimbizi
Wahu
Nyota Ndogo
Bingwa Showbiz Magazine Of The Year
Pulse -Standard
Spice -People Daily
Buzz -Daily Nation
Word is -The star
Nairobian
Insider Magazine
Bingwa Entertainment Site Of The Year
Ghafla Kenya (KE)
SDE (KE)
Mpasho.com (KE)
Vibe Weekly (KE)
Bongo5.com (TZ)
Mseto EA (KE)
Bingwa Verse Of The Year
Sosuun in Fimbo Ya Tatu
Wyre in Fimbo Ya Tatu
Cannibal Welle Welle Remix
Gabu in Weka Weka
Mejja in Moto ya Kuotea Mbali
Rabbit in Dandia
Bingwa Song Of The Year
Nerea -Sauti Sol & Amos & Josh
Moto Wa Kuotea Mbali- Kansoul &
Nameless
Fimbo Ya Tatu
Dandia by Kristoff, Rabbit & Frasha
Huu Mwaka by Jaguar
Lover Bahati
Bingwa EAST AFRICAN SONG Of The Year
Nerea Sauti Sol
Wale wale Jose Chameleone
Chekecha Alikiba
Fimbo Ya Tatu Grand Pa Records
Nasema Nawe Diamond ft Hadija
Love Letter Irene Ntale
Bingwa EAST AFRICAN Artist Of The Year
Jose Chameleone
Eddy Kenzo
Diamond
Alikiba
Wyre
Sauti Sol
Bingwa radio Of The Year
Radio Citizen
Radio Maisha
Ghetto radio
One FM
Kiss 100
Q FM
Bingwa East African Dj Of The Year
Creme de la Creme (KE)
Joe Mfalme (KE)
Kriss Darling (KE)
Kaytrixx (KE)
Choka (TZ)
Shira (UG)
Bingwa EAST AFRICAN Record Label Of
The Year
Ulopa Ngoma (KE)
Pacho Entertertainment (KE)
Mainswith Productions (KE)
Grand Pa Records(KE)
Swags Avenue (UG)
MJ Records (TZ)
Bingwa MC East African
DNG (KE)
Jalango (KE)
Kriss Darling (KE)
Shaffie weru (KE)
Dr Mitch Egwang (UG)
Shaa (TZ)
Bingwa Collabo Of The Year
Hello Avril featuring Ommy Dimpoz
Fimbo Ya Tatu Grand Pa
Moto ya Kuotea Mbali Kansoul
Dandia Kristoff, Rabbit, Frasha
Wele Wele Remix
Barua Kwa Rais Jaguar & Sudi Boy
Bingwa Stage Performer Of The Year
Kenrazy
Wyre
Size 8
Willy Paul
Juliani
H_art The Band
Bingwa Tv Show Of The Year
Mseto East Africa Citizen
Arena 254 K24
Bassline KTN
Live on Blast (Kiss Tv)
Club One KBC
Crossover NTV
Bingwa RADIO Presenter Of The Year
Mzazi William Tuva – Citizen
Rashid Abdala – QFM
Addele Anyango Kiss 100
Tina Korosho & Zulekha Radio Maisha
Allan Wakori & Nzula Makasi – Milele
Mwalimu Rachel Homeboyz Radio
Bingwa Radio Show
Mambo Mseto – Citizen Radio
Konnect – Radio Maisha
Bangaiza – Milele Fm
One drive – One Fm
Keeping It Kenyan – Kiss 100
The Source – Home Boyz Radio
Bingwa Legendary Awards
Fred Obachi Machoka
Leonard Mambo Mbotela
Catherine Kasavuli
Mr Sugu (TZ)
Chameleon (UG)
The Mushrooms
Bingwa Company Of The Year For
Supporting Local Talent
Sports Pesa
Safaricom
Coca Cola
Carnivore
EABL
Airtel Kenya
Bingwa Song Writer Of The Year
Mapepo – Visita
Nerea – Sauti Sol
Barua Kwa Kais Jaguar & Sudi Boy
Itakua Ngori- Kele Takatifu
Huu Mwaka- Sudi Boy & Jaguar
Kenty MOG & Mr Vee in Subira
Bingwa East African Comedian Of The
Year
Professor Hamo
Wilbroda
Jalango’
Owago Nyiro
Salvador (UG)
Kigwendu (TZ)
Bingwa Ever Relevant Artist Of The Year
Wyre
Rufftone
Nameless
Kenrazy
Size 8
Amileena
Bingwa Showbiz Writer Of The Year
Stevens Muendo- Pulse
Manuel – People
John Muchiri – Buzz Nation
Grace Kerongo – The Star
Uncle Chim- Mpasho
Sheila Kimani- SDE
Bingwa Artist Of The Year Kenya
The Kansoul
Shida Mbili
Sauti Sol
Rabbit (Kaka Sungura)
Jaguar
Willy Paul
Bingwa Artist Of The Year Uganda
Jose Chameleone
Bebe Cool
Eddy Kenzo
Bobi Wine
Cindy Janyu
Irene Ntale
Bingwa Artist Of The Year Tanzania
Diamond
Lady Jay Dee
AliKiba
Ommy Dimpoz
Vanessa Mdee
Joe Makini
Bingwa Artist Of The Year South Sudan
Silver X
Coozos Clan
Mary Boyori
Queen Zee
Dynamiq
Emmanuel Jal
Bingwa Artist Of The Year Rwanda
Knowles
Barbara Panther
Tom Close
King James
Dr Claude
Urban Boys
Bingwa Dialect Artist Of The Year
Ken Wamaria
Mike Rua
Lady Maurine
Joseph Shisia
Lilian Rotich
Mzee Ngala
Bingwa Lifestyle Award Of The Year
Fundi Frank (KE)
Nomadic Muhoho Kenyatta (KE)
Nairobi Me (KE)
Binti Africa(TZ)
Sylvia Awori (UG)
Bingwa Album Of The Year Kenya
Vanity- Daddy Owen
Lion- Wyre
LDPC – Octopizzo
Legend of Kaka – Rabbit
Amileena – Amileena
Mwanaume Ni Effort- Calvo

Jumanne, 1 Septemba 2015

Watanzania .. tuamini tunachokiamini .. maneno ya mtu mmoja yasitupotoshe lowasa anatosha .. na inaonekana dhana ya kufeli alikuwa nayo slaa wakati akiwa mlezi wa ccm B na sasa tumepata kiboko atakayetengeneza chadema ya kweli yeye inamuuma padre na siasa wap na wap ..........


Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA,
Dr. Slaa akiwa kwenye mkutano na
waandishi wa Habari katika ukumbi wa
Hoteli ya Serena.
Slaa: Watanzania wana kiu ya
kujua kwanini amekuwa kimya
kwa muda mrefu sasa licha ya
harakati za kisiasa kuendelea.
Muda utakaotumika ni saa moja,
hakuna muda mrefu sana.
Ameamua kufanya hayo kwa kuwa
imefika mahali ukweli lazima
usemwe na upotoshwaji
ukomeshwa. Namna pekee ya
kufanya hivyo ni kutoka
hadharani na kuusema ukweli.
Sote tunafahamu kuwa hana tabia
ya kuchenga mambo, mengi
yamesemwa na watu tofauti,
kwenye mitandao, magazeti na
viongozi wake!
Hana ugomvi na kiongozi yoyote,
kwa kuwa siasa sio ugomvi. Kama
binadamu wa kawaida hana chuki
wala hasira na binadamu
mwingine yoyote!
Iwe wazi kuwa katika Taifa kuna
misingi ambayo inaongoza taifa.
Inapofika mahali taifa
linaongozwa kwa msingi ya
propaganda na upotoshwaji
matokeo yake ni vurugu kubwa
katika taifa. Yeye amekataa hayo
yote!
Anasema kuwa YEYE hakuwa
likizo kama inavyosemwa na
viongozi wake! Atafafanua kwa
kifupi!
Kilichotokea ni kuwa aliamua
kuachana na siasa, tarehe 28 Julai
2015, majira ya saa tatu usiku,
baada ya kuona yanayofanyika
ndani ya chama chake
hayamridhishi.
Mtangulizi wa shuguli ambaye
anatoka kwenye kampuni ya
mahusiano ya umma
anamtambulisha Dr. Willibrod
Slaa.
Anasema kuwa kwa muda mrefu
Slaa amekuwa alama ya harakati
za ukombozi dhidi ya makucha ya
mkoloni mweusi.
anaongeza kuwa Dr. ataongea kwa
muda kisha kuruhusu maswali
kutoka kwa waandishi,
anamkaribisha!
Kinachosemwa ni kuwa Dr. Slaa
alishiriki tangu mwanzo kwenye
mchakato. Anasema ni kweli
alishirii kwenye majadiliano,
akaweka msingi na msimamo
wako. Kuna wakati wengi
wanashinda kutokana na wingi
wao, wewe unayeamini katika
misingi inabidi uachie ngazi.
Azam TV wameanza matangazo
kupitia kipindi chao cha KITUO
CHAKO CHA UCHAGUZI, wako LIVE
sasa... Bado uchambuzi wa safari
ya Kisiasa ya Dr. Willibrod Slaa
unaendelea.
Tumepelekwa moja kwa moja
kutoka Hoteli ya Serena
Mtangulizi wa shuguli ambaye
anatoka kwenye kampuni ya
mahusiano ya umma
anamtambulisha Dr. Willibrod
Slaa.
Anasema kuwa kwa muda mrefu
Slaa amekuwa alama ya harakati
za ukombozi dhidi ya makucha ya
mkoloni mweusi.
anaongeza kuwa Dr. ataongea kwa
muda kisha kuruhusu maswali
kutoka kwa waandishi,
anamkaribisha!
==========================
Slaa: Watanzania wana kiu ya
kujua kwanini amekuwa kimya
kwa muda mrefu sasa licha ya
harakati za kisiasa kuendelea.
Muda utakaotumika ni saa moja,
hakuna muda mrefu sana.
Ameamua kufanya hayo kwa kuwa
imefika mahali ukweli lazima
usemwe na upotoshwaji
ukomeshwa. Namna pekee ya
kufanya hivyo ni kutoka
hadharani na kuusema ukweli.
Sote tunafahamu kuwa hana tabia
ya kuchenga mambo, mengi
yamesemwa na watu tofauti,
kwenye mitandao, magazeti na
viongozi wake!
Hana ugomvi na kiongozi yoyote,
kwa kuwa siasa sio ugomvi. Kama
binadamu wa kawaida hana chuki
wala hasira na binadamu
mwingine yoyote!
Iwe wazi kuwa katika Taifa kuna
misingi ambayo inaongoza taifa.
Inapofika mahali taifa
linaongozwa kwa msingi ya
propaganda na upotoshwaji
matokeo yake ni vurugu kubwa
katika taifa. Yeye amekataa hayo
yote!
Anasema kuwa YEYE hakuwa
likizo kama inavyosemwa na
viongozi wake! Atafafanua kwa
kifupi!
Kilichotokea ni kuwa aliamua
kuachana na siasa, tarehe 28 Julai
2015, majira ya saa tatu usiku,
baada ya kuona yanayofanyika
ndani ya chama chake
hayamridhishi.
Kinachosemwa ni kuwa Dr. Slaa
alishiriki tangu mwanzo kwenye
mchakato. Anasema ni kweli
alishirii kwenye majadiliano,
akaweka msingi na msimamo
wako. Kuna wakati wengi
wanashinda kutokana na wingi
wao, wewe unayeamini katika
misingi inabidi uachie ngazi.
Baada ya Edward Lowassa
kukatwa na CCM Dodoma,
Mshenga wake alimpigia simu na
kuuliza nini kifuate baada ya
tukio la dodoma. Akamuambia
wawasiliane na mwenyekiti
Freeman Mbowe, Gwajima nae
akafika kwenye kikao hicho.
Msimamo wa Slaa ni kuwa ni
lazima kumsikiliza mtu kabla ya
kuamua nini cha kufanya.
chadema ni cham cha siasa na
hakiwezi kumkataa mtu yeyote
kujiunga na chama.
Wakaweka vijana kuchunguza nini
wanataka hao wanaotaka
kujiunga na chama!
Slaa akataka kwanza Lowassa
atangaze kutoka kwenye chama
chake alichopo, kisha atangaze
anakwenda kwenye chama gani.
Atumie nafasi hiyo ya mkutano
huo ajisafishe na tuhuma zote
ambazo amekuwa akituhumiwa
na watu.
Chadema ni cham ambacho kwa
muda mrefu kimejijenga kwa
msingi, na ni lazima wapokee mtu
ambaye hawezi kukichafua chama
chao.
Lowassa hakutangaza kujitoa,
wala kujisafisha hadi kwenye
mkutano ambao uliandaliwa na
chadema. Slaa hakuhudhuria ule
mkutano.
Kwenye kila jambo kuna jambo la
kuzingatia. Mtu anayejiunga
popote anakuja kama mtaji au
kama mzigo? Lowassa anakuja
chadema kama asset au liability?
Ijulikane, suala sio urais! Mpaka
siku hiyo Slaa hakuwa amechukua
fomu ya Urais kwenye chama
chake. Slaa hakuwa anamzuia
Lowassa kugombea urais
chadema. Alitaka mgombea
mwenye sifa na uwezo wa kukitoa
Chama cha Mapinduzi.
Hakutamka popote kuwa anataka
kugombea, hata 2010
hakugombea, aliombwa
kugombea! Urais wake binafsi
hauwezi kuikomboa nchi bila
mchango wa jamii nzima.
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Suala la adha Lowaasa ni msizo au
mtaji halikujibiwa hadi siku ya
mkutano tajwa. Wakataka kujua
anapokuja anakuja na akina nani,
ni wafuasi wa aina gani; vijana wa
bodaboda, vijana wasio na ajira
au watu waliosombwa tu, au
wanakuja kwenye mapambano?
Jibu lilikuwa ni kuwa tungepata
wabunge 50 na wenyeviti wa CCM
mkoa wasiopungua 22, wenyeviti
wa CCM wilaya 88. Slaa akakiri
kuwa kama ni hivyo kutakuwa na
tetemeko (la kisiasa).
Wakahitaji majina ya hao
waliotajwa kwa kuwa walikuwa
kwenye mchakato wa kupitisha
majina kwenye chama. KAtibu
mkuu makini huwezi kuchukuwa
watu usiowajua. Hakuna jina
nililopewa mpaka tarehe 25.
Tarehe 25 wakamfata na
kumuambia aitishe Kamati Kuu
ya chama. Akakubali lakini
akatahadjharisha kuwa hajapata
majina na hajapata jibu kuwa
Lowassa ni asset au liability.
Lakini akaitisha kikao kwa kuwa
ni jukumu la kikatiba la katiba.
Mwenyekiti akapiga simu,
anasikia kuwa hajaridhika. Tangu
2004 Slaa hajawahi kugombana na
mwenyekiti wake, isingekuwa
sawa kama wangetofautiana
kwenye kikao rasmi.
Wakakutana na Mwenyekiti,
Gwajima, Lissu na wakajadiliana
mpaka saa 9 mchana. Maneno
kuwa alikuwa anakubaliana na
mpango huo tangu mwanzo SI
KWELI!
Mkutano ukashindikana. Wdau
wakasema waende nyumbani kwa
Lowassa, Slaa akakataa wakaenda
Kamati kuu.
Kikao kikafanyika hadi saa 12
jioni. Ikaundwa kamati ndogo ya
kumshawishi Slaa. Akakataa!
Akaandika barua ya kujiuzulu kwa
kamati, Prof. Safari akaichana
barua yake. Akaandika barua
nyingine kwa Makamu-Zanzibar,
makamu akamuambia kuwa haya
mambo yamepangwa,
asijisumbue!
Wanasema siasa ni mchezo
mchafu, yeye anaaamini kuwa
siasa ni sayansi! Asubuhi ya
kesho akaandika barua,
wasichojua ni kuwa kujiuzulu
hakuhitaji barua. Maneno
yakazuka kuwa Slaa hajaandika
barua!
Upotoshwaji ukaendelea kuwa
Slaa atazungumza na waandishi
wa habari, wengine wakasema
amefungiwa, amefungiwa na
mkewe na kadhalika! Ukweli ni
kuwa alikuwa na Lissu, Gwajima
na Mbowe tangu asubuhi.
Maamuzi aliyoyafanya yanatokana
nadhamiri yake!
Josephine nae ni mwanaharakati,
ana sababu ya kuwa na uchungu.
Alipigwa mwaka 2011 wakati
wengine walijificha! Propaganda
hizo tumeshazisoea!
Kama kuna mwenye ushahidi wa
propaganda hizi aje, audited
report zipo! Josephine halipwi na
chama! Watu wanasema kuwa Slaa
analipwa mil. 7, yeye ameendelea
kula mihogo na maharage kama
walivyoahidi mwaka 2010.
Wana uchungu na harakati!
Kikubwa katika harakati ni
credibilty, jina la chama
kilichojengwa kwa muda mrefu
kisichafuliwe kwa namna yoyote!
Mwanasiasa yoyote hataki
kuchaguliwa, na Slaa nae hataki
kuchaguliwa!
Wanasema kuna maslahi mapana
ya taifa, ni nani anayapima?
Lazima kuwe na kipimo cha
kuapima hayo maslahi badala ya
kutegemea mtazamo wa mtu!
Anafafanua suala la liability sasa!
Wamekuwa waongo kwa kuwa
hakuna kipengele hata kimoja cha
madai ya Slaa kimetekelezwa.
Alisema wabunge waje kabla ya
kura ya maoni ya CCM, kuja
baada ya hapo ni kutafuta
kichaka cha kujificha!
Watanzania wameijenga Chadema
kwa damu yao, rasilimali zao!
Watu hawawezi kukimbilia
kirahisi wakati sio wasafi,
akiwemo Sumaye na wengine.
Nani hajua kama Sumaye ni
fisadi? Kwa muda mrefu Slaa
haongei na Sumaye kwa kuwa
alimtuhumu kwa ufisaidi.
Sumaye ni mtu ambaye
wanahabari walidai kuwa Sumaye
alisema kuwa atahama chama
endapo Lowassa atateuliwa, leo
akageuka!
Leo anamsafisha Lowaasa,
dhambi haisafishwa kwa dhambi.
Anakumbusha jina la Mr. Zero
(jina la utani la Sumaye).
Chama kimepokea makapi, na
katibu alitahadharisha kuwa
chama hakipokei makapi! Hakuna
ambaye alijitoa kwa hiari, wengi
walikuja baada ya kukatwa.
Wenyeviti wengi ni mzigo,
akiwemo Msindai.
Anangoja ajibu amlipue hadharani
kwa kuwa alikuwa mwenyekiti wa
kamati ya bunge hesabu za
serikali z mitaa.
Siku aliyoambiwa aitishe kamati
kuu aliuliza majina, akaambiwa
anakuja chizi! Chizi ni nani, hata
nyie hamumjui! Anaitwa chizi kwa
kuwa ni mwizi wa kura ndani ya
CCM.
Kuna haja gani ya kushindana
kama tunampango wa kuiba kura
pia. Wakamtaja Guninita, nani
asiyemjua udhaifu wake? Hawezi
kuandika hata ukurasa mmoja wa
ripoti, amehama vyama mara
kadhaa!
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Viongozi wa Chadema wamepata
kigugumizi, waseme nani
ameongeza thamani kwenye
chama?
Najua maneno ya kuwa ni lazima
kuiondoa CCM kwanza hata
ikibidi tuweke mkataba na
shetani, mimi ni padre wa Kanisa
Katoliki! Kuwaondoa CCM kwa
namna yoyote hakuleti
maendeleo. CCM itaondolewa kwa
program siriaz, sio kutumia watu
wale wale!
Lazima tujue nini kilifanya
Watanzania waamini chadema,
kwa kuwa waliamini wana misingi
isiyoyumba na uadilifu. Leo
tunasimamia uadilifu?
Wanasema mwenye ushahidi
aende mahakamani. Kama
tusingewatuhumu Mramba na
Yona wasingefikishwa kizimbani.
Chadema imefungwa mdomo kwa
kisingizio cha ushahidi!
Ni bora kukaa kimya kuliko
kupotosha. Anasema nukuu ya
biblia kuhusu wapotoshaji!
Inapofika mahali unapoambiwa
hakuna mwenye dhambi ni
makosa, dhambi haisahihishwi
kwa dhambi nyingine! CCM
wamekuwa waoga, wamewalea
watu hawa kwa muda mrefu!
Kwa Wafrika choo ni neno baya,
kwa wazungu choo ni rest room!
Choo cha Kitanzania huwezi
kukihamisha ndani ya chumba
cha kulala na ukakiita choo,
huwezi kulala kwa kuwa kitanuka,
tena zaidi!
Ufisadi ilikuwa ajenda iliyowapa
umaarufu CHADEMA, leo
wamewachukua. Waanweza kuwa
na ujasiri wa kukemea ufisadi?
Mwaka 2008 Slaa alikuwa bungeni
wakati wa sakata la Richmond,
anafahamu kwa uzuri
anachokimaanisha. Bahati mbaya
waandishi hawasomi makaratasi,
na wabunge wa CCM pia.
Lowassa hatuhumiwi kwa habari
ya Richmond pekee!
Lowassa aliambiwa na Slaa aache
kulalamika, atangaze uhalali au
uharamu wa Richmond, anamtaka
aseme hao 'wakubwa' ni akina
nani? Ni afadhali sifa yake
iharibike kuliko kusema uongo.
Ni aheri kupotea kwenye siasa za
dunia kuliko kusimamia uongo!
Msingi wa kwanza wa Richmond:
Ili uelewe ni lazima urudi kwenye
taarifa ya Kamati ya Mwakyembe,
Slaa alifuatwa asubuhi ya siku ile
kupewa rushwa, anashuru Sitta na
Mwakyembe wajitokeze!
Akamuuliza mtoa rushwa kama
anatoa m.500 kwa mbunge,
atakuwa nazo ngapi? Aliwaambia
Sumaye na Lowassa kuwa rushwa
ni jambo linaloanzia kifuani
kwanza. Mwanzo wa jambo hili ni
taarifa ya Baraza la Mawaziri la
10.2.2006. Kamati ya mwakyembe
iliangalia faili la kikao kile kisha
kuandika ripoti!
Suala hili lilianzia wakati wa
utawala wa mkapa kutokana na
dharura ya umeme nchini,
wakawasiliana na kampuni moja
ya Amerika Kaskazini kwa suluhu
ya muda mfupi ya umeme.
Serikali ya Kikwete ikapokea lile
suala. Wakaruhusu mpango
uendelee, ila kwa kufuata sheria.
Hiyo ilikuwa kauli ya Baraza la
Mawaziri!
Wakati auala lile linaamuliwa,
Lowassa alikuwa Waziri Mkuu! Na
ndie mwenye mandate ya
maamuzi ya Serikali, iweje leo
akane kuhusika?
Taarifa ya Mwakyembe
inapotoshwa! Taarifa ilitaka
Waziri Mkuu ajipime, au bunge
limjadili na kumchukulia hatua.
Lowassa akakimbia kwa kuwa
alijua Bunge lingemfukuza kazi!
Waliioomba tenda walikuwa 26,
waliorudisha walikuwa 8. Kamati
ya Tathmini ikaona hakuna
anayefaa hata mmoja! Waziri
Msabaha akaagiza taarifa ile
ifutwe na tathmini ifanyike upya,
mara ya kwanza, ya pili, ya tatu
na ya nne. Jeuri wa Msabaha
ilitoka wapi?
Baraza likaamua baadaye tenda
iliyopewa kwa kampuni ya kwanza
ifutwe! Lowassa alishiriki!
TANESCO wakatoa ushauriwa wao,
Mamlaka husika ikatafute
internatonal tender ya kununua
turbine!
Lowassa akaingilia mchakato
dakika za mwisho, akamuagiza
katibu muhtasi wake!
Kwanini Lowassa, kwa kuwa
anagombea urais, rais
asiyeaminika hawezi kuchaguliwa!
Lowassa alishawahi kumuita Slaa
kuhusu habari ya Meremeta, na
kumuambia kuwa taarifa yake
inaiaibisha Serikali! Kampuni ya
jeshi imewahi kutengeneza gari,
imehujumiwa na wahuni.
Akamtaka Lowassa amuambie ni
nani aliyehusika?
Akamuita mwingine kwnye
Speaker lounge. Slaa akamuambia
kuwa yeye ni fisadi kichwani,
rohoni mpaka...!
Tunamsifia Lowassa kuwa
an=taleta maji wakti jimbo la
Lowassa halina maji na ufisadi
mkubwa umefanyika kwneye
jimbo hilo. Mnazungumzia shule
za kata wakati wakati hamjua
zimeanza wapi?
Slaa anataja nafasi alizowahi
kushika Afrika. Uamuzi wa
kujenga shule za kata ulifikiwa
mwaka 90 huko Thailand, mpango
huo ukaitwa Education for All, sio
MMES kama unavyoitwa leo!
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Anasoma barua ya Ibrahim
Msabaha kwa Flugence Kazaura,
mkurugenzi wa bodi wa TANESCO!
Mpango ulikuwa kuondoa suala la
umeme mikononi mwa tanesko
kwa kuwa imeshindwa kutekeleza.
Ugomvi wake na Masha ni kwa
kuwa Lowassa alimlaumu Masha
kuingilia mchakato wa serikali,
akawekewa kinasa sauti
chumbani.
Waziri Mkuu haruhusiwi na sheria
kuingilia mchakato wowote wa
tenda.
Kwenye kampuni nane
zilizowasilisha maombi ya zabuni,
Richmond ni kampuni iliyokuwa
mbovu. Ilikuwa ni kampuni ya
steshenari, sio umeme!Wakadai
wana ushirikiano na kampuni
nyingine ya umeme, kampuni
hiyo ikakataa kujihusisha na
Richmond, wala kuzalisha na
majenereta!
Bill Clinton aliwai kukutwa na
kashfa, walitaka kumchukulia
hatua si kwa sababu ya zinaa, bali
kwa kuwa alifanya uongo! Kwa
kuwa alidanganya umma! Hata
sheria za Tanzania zinakataza
kuongopa, hata kesi za uchaguzi
za Slaa zimethibitisha hilo.
Lowassa anadai yeye
alisimamisha tenda, Slaa
anaonesha uthibitisho wa hilo
kwa barua za Lowassa kwenda
kwa Msabaha zinazokanusha hilo,
'Anaisoma'! Waziri Mkuu
aliharakisha mchakato wa tenda,
tofauti na sheria ya PPRA. Barua
imeandikwa miezi mitatu baada
ya mkataba kusainiwa, kwa
maagizo ya Waziri Mkuu.
Tanesko ikaagizwa kusaini
mkataba ambao haikuhusika
kwenye kuujadili! Anaona aishie
hapo... Anaupigia chapuo
mdahalo wa Sitta na Mwakyembe,
anasema Lowaasa nae afike
kuondoa utata na kusema ukweli!
Chadema ni chama kilichotoa
matumaini kwa vijana wengi!
Isifike mahali tukawa washabiki
kama 2005 ambapo watu
waliahidiwa maisha bora,
wakajikaanga kutokana na
ushabiki! Anatoa ushahidi wa
kitakwimu wa mfumuko wa bei...
Slaa ana uchungu kuona chama
alichokijenga, kikifikia hatua ya
kusomba watu kwa mabasi na
malori kisha mkasema mafuriko
hayazuiliki! Hayuko tayari,...
Anakataa kuwa ZEZETA!
Ajenda ya Chadema ni nini,
ilikuwa ni rushwa! Wananchi
waliamini kwa kuwa msingi huo
ndio unakijenga chama!
Sehemu kubwa ya kilichosemwa
Jangwani ni ilani ambayo
ilishaandaliwa tayri, hakuna kipya
kilichosemwa. Kinachomuuma ni
chama makini kuwa kibovu zaidi
ya Chama cha Mapinduzi!
Hatuwezi kujenga maadili tukiwa
na watu wachafu, anaishi na
mwanamke bila kufunga ndoa
kwa kuwa Serikali ya CCM haitaki
afunge ndoa. Kesi yake ililetwa na
mawaziri, waandishi wa habari na
mtu kutoka IKULU. Ndoa
inafungwa na Mungu!
Scotland Yard iliamrisha Lowassa
achunguzwe, inakuwaje leo
tunamtetea? Huu ni ushabiki usio
na vielelezo, Slaa ana ushahidi!
Hakuna ulazima wa kwenda
mahakamani kwa kuwa kesi ya
rushwa ni jinai, ni kesi ya
serikali! Slaa au mwingine hana
locus ya kwenda mahakamani
kwa kesi ya jinai!
Mwakyembe alisema kesi ya jinai
haina mwisho (kama zilizyo za
madai).
chadema iliahidi kusafisha nchi
kwanza endapo itashika dola,
huku maendeleo yakiendelea!
Anasoma barua ya mchakato wa
Richmond kuwa DOWANS.
Kampuni imesajiliwa Costa Rica,
na mwenyekiti asiye na anuani,
simu wala jengo! Siku
iliyosajiliwa, mmiliki alisajili
makampuni mengine 99! Zaidi ya
hayo ana makampuni mengine
zaidi ya 50, DOWANS ni jina tu.
Kampuni haipo!
Dowans sio kampuni halisi huko
Kosta Rika, nchi nzima hakuna
kampuni yenye uwezo wa
kuzalisha umeme kwa kiwango
hicho!
Leo Lowaassa anatuambia
tufunge mdomo, huu ni udikteta!
Anakumbusha sakata lake na
Waziri Marmo...
Mabilioni ya fedha yanalipwa kwa
kampuni ambayo haipo!
Tunapenda ushabiki... Acha sifa
iharibike!
Anasema hataki kuingia kwenye
mambo ya Babu Seya! Vyuo vikuu
vinatumia kesi ya Babu Seya
kama case study. Mtoto mdogo
hawezi kutoa ushahidi
mahakamani, haki inapuuzwa kwa
kuwa mtoto hawezi kutoa
ushahidi!
Kesi ya Ulawiti rais hana
mamlaka nayo, anatoa wapi
kiburi cha kusema kuwa atamtoa?
Aliyeagiza polisi kuingia na polisi
kuingia na mbwa msikiti wa
mwembechai ni Sumaye, akiwa
waziri mkubwa. Leo hii ni mpiga
kampeni wa Lowassa! Leo
tunataka kura kwa namna yoyote!
Ni afadhali kutokuwa na rais wa
aina ya mtu huyu! anayesaka kura
kwa kusaka huruma za watu. Slaa
hayuko tayari kuona hilo
linatokea...
Anahitimisha kwa kusema
hajagusa chochote kuhusu ilani
wala mkakati!
Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Kama taifa tuna kazi kubwa ya
kuchambua vitu nje ya
shamrashamra, maneno matamu!
Tumeshaumwa na nyoka,
tusilaghaiwe na maneno ya watu
hawa tena!
Utendaji uliotukuka unapimwa
kwa utafiti, sio kwa ukasuku na
kunukuu maneno ya wanasiasa!
Lowassa alipokuwa Waziri Mkuu,
matatizo ya wakulima na wafugaji
yalikuwepo, alifanya nini?
Lowassa aliwahi kubadili mpaka
wa Monduli na Karatu na
kusababisha mgogoro!
Mkampenia wake, Sumaye
alisababisha matatizo ya ardhi
Mvomero, akipora ardhi ambayo
ilitakiwa yajengwe makao makuu
ya Mvomero! Mengine ya Sumaye
ameyaweka kiporo, hisa zake za
kampuni aziweke wazi kama
Sekretarieti ya Maadili
inavyotaka!
Kutotangaza mali kunatosha
kumtoa mtu ubunge! Sembuse
Urais?
==============================
=========================
Ukweli huwa una tabia ya
kuegemea upande, anasemea
speculation kuwa ameisema
chadema peke yake.
Anasema amestaafu siasa, hana
chama lakini bado anabaki kuwa
mtanzania, mtetezi wa wanyonge
na atabaki hivyo! Ataendelea
kuwatumikia watanzania kadiri
ya Mungu alivyomjalia vipawa!
Kama alivyoombwa kugombea
urais 2010!
Anaweza kuwatumikia Watanzania
bila kuwa na chama!
Anasema kuwa hajapata vitisho
kama alivyopata kipindi hiki,
inazidi hata wakati alipotangaza
List of Shame. Rostam ndiye
anafadhili kampeni za urais wa
Lowassa! Anamnukuu vitisho
vyake! anakiri kuwa maaskofu
wamehongwa, Rostam akiwa
anaona, m60-m300!
Anasema hatenda chama
chochote, anasisitiza! Amejitoa
rasmi siasa za vyama vya siasa...
Ataendelea kuwa msimamiaji wa
anachokiamini!
Anawataka watu aliowataja
watoke hadharani, anatoa baraka
za KIMUNGU kwa nchi na watu
wake!
MASWALI!
Swali: Unawammbia nini
Watanzania kuelekea uchaguzi, ni
rais yupi anafaa?
Amesema hana chama, hampigii
kampeni mtu yoyote! Amesema
anafanya uchambuzi wa madhara
ambayo taifa litapata endapo
watamchagua Lowassa, na kwa
kuwa na uzoefu nao kwa muda
mrefu!
Hataki kufanya kampeni yoyote.
Anawaelimisha Watanzania
kuacha ushabiki
utakaowagharimu! Ni watu
wachache wanoweza kumtaja mtu
kwa majina, kuna tofauti ya
wanaotaja ajenda tu na wanaotaja
majina.
Rostam alimuambia kuwa ana
dakika 5 za kuishi, apige magoti
na kusali! Aliweka roho yake
rehani kwa ustawi wa taifa
hili...Anakumbusha ya
Mwembeyanga na namna Usalama
wa Taifa walivyokuwa na tension.
Magazeti mengi yaliogopa hata
kuandika habari, isipokuwa
MWanaHalisi!
Swali: Siasa ingekuwa asset kama
angekuja na wabunge kadhaa.
Angekuja kama asset, mengine
yangesafishika?
Kulikuwa na vigezo viwili, ama
asset na liability, yaani hayo
madhambi yote aliyoyasema.
Baada ya hayo wangefanya
tathmini kama anapokelewa au
hapokelewi. Anatoa mfano wa
Shirikisho la Afrika Mashariki na
nchi zinazotaka kujiunga!
Swali: Waliopokelewa ni makapi.
Je wewe ulikuwa kapi 95?
Anauliza kama watu wanaamini
yeye alikuwa kapi? Tupime
vigezo... Makapi ni watu
waliokataliwa na watu wao baada
ya kuwa wabunge kwa muda
mrefu. CCM wakasema kuwa
hakuwa mwenzao: hakuwa
anahonga, hakuwa anapokea
rushwa na kadhalika!
Kuingia kwa tiketi ya Chadema
ulikuwa ukombozi kwake!
Swali: Umetangaza kustaafu siasa,
una kadi za vyama viwili.
Unazirudisha au unakaa nazo?
Watanzania tuelimika, kadi sio
uanachama. Kadi ni mali ya
mwanachama, unaweza kuichoma,
kuweka kumbukumbu au
vyovyote, sawa na kadi ya ndoa
ambayo hairudishwi hata kama
ndoa itavunjika. Tuulize maswali
ya kujenga.
Swali: Anaoneka baada ya kukosa
urais anamshambulia Lowassa!
Wapi Slaa alichukua fomu ya
Urais, hakuwa na nia na urais
wala hawezi kukasirika. Tuache
ushabiki, tuwe na mtiririko na
kuzingatia hoja! Mwandishi awe
msikivu sana... Ameeleza tangu
mwanzo, hana chuki wala ugomvi
na mtu yoyote!
Chama cha Mapinduzi kilishakuja
kumpa ofa kadhaa kuachia jimbo
la Karatu, akaweka sharti la
mkataba wenye sahihi za watu
watatu; Rais, Slaa na Yesu Kristo.
Swali: Kama wewe uliweza
kuhama, wengine nao hawawezi?
Dr. Slaa hakuwa na uchafu
wowote, tatizo halikuwa kuhama
chama, tatizo ni watu wa aina
gani wanahama chama?
Swali: Unahamasisha uwazi,
mbona wewe umemficha muovu
mmoja?
Silaha haziwekwi zote mezani,
amewaomba anaowatuhumu
wajitokeze!