other blog

Jumanne, 22 Septemba 2015

Sport man RIZIK MALYA leo amekuandalia Martial aing’arisha Man United Mabao mawili ya kinda Anthony Martial na jingine la Juan Mata jana yaliiwezesha Manchester United


Martial alichukua mpira kutoka upande wa
kushoto akakimbia nao kuelekea kwenye
boksi na kumpiga chenga beki mzoefu
kwenye ligi, Martin Skrtel kabla ya
kufunga bao maridadi kabisa.
London, England. Mabao mawili ya
kinda Anthony Martial na jingine la
Juan Mata jana yaliiwezesha
Manchester United kushinda mabao
3-2 dhidi ya Southampton kwenye
mchezo mgumu wa Ligi Kuu England.
Kwa ushindi huo, Man United
imefikisha pointi 13 na kushika nafasi
ya pili ikiwa nyuma ya Man City
ambayo ipo kileleni ikiwa na pointi 15,
huku West Ham ikiwa katika nafasi ya
tatu ikiwa na pointi 12.
Katika mchezo huo uliofanyika
kwenye Uwanja wa St Mary’s, wenyeji
Southampton walitangulia kupata bao
kupitia kwa Graziano Pelle, kipindi cha
kwanza.
Kipindi cha pili, Martial aliyejiunga na
klabu hiyo siku ya mwisho ya usajili,
Septemba 2 kwa ada kubwa akitokea
AS Monaco ya Ufaransa, alifunga
mabao hayo mawili na Mata kuongeza
jingine, huku Pelle akifunga pia la pili
katika mchezo huo.
Mapema, Tottenham au Spurs iliilaza
Crystal Palace kwa bao 1-0 katika
mchezo wa mapema saa 9.30 alasiri
kwenye Uwanja wa White Hart Lane.
Nayo Liverpool ilizuiwa na Norwich
City na kutoka sare ya bao 1-1 katika
mchezo mwingine wa Ligi Kuu kwenye
Uwanja wa Anfield.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni