other blog

Alhamisi, 24 Septemba 2015

Haya libabu la arsenal hii Ndoa ya Arsene Wenger yavunjika Ndoa ya kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na mke wake, Annie iliyodumu kwa miaka mitano imevunjika


Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na
mkewe Annie
Strasbourg, Ufaransa. Ndoa ya kocha
wa Arsenal, Arsene Wenger na mke
wake, Annie iliyodumu kwa miaka
mitano imevunjika baada ya miezi
kadhaa ya uvumi.
Habari za kimahakama mjini
Strasbourg zilieleza jana kuwa wawili
hao wenye binti wa miaka 18,
wamekuwa hawaonekani pamoja
tangu mwaka 2013.
Wenger, mwenye umri wa miaka 65 na
mkewe, Annie 59 wamefikia mwafaka
wa kugawana mali.
Mara kadhaa, kocha huyo alikiri kuwa
shinikizo kubwa la kazi kwenye klabu
hiyo ya London Kaskazini
limesababisha matatizo kwenye ndoa
yake.
Nyaraka za kimahakama zilionyesha
kuwa wawili hao walitengana Juni
mwaka huu.
Hata hivyo, nyaraka hizo zimeeleza
kuwa si talaka kamili, bali
wametengana kisheria, jambo
linalomaanisha kuwa wana jukumu la
kuendelea kuwa pamoja.
Wawili hao walifunga ndoa Desemba
2010 baada ya uhusiano wa muda
mrefu, lakini wamekuwa si wenye
furaha kwa muda sasa.
“Wamegawana mali na rasilimali,
wamefikia mwafaka wa kutengana.
Mwaka 2008, kocha huyo alieleza
dhamira ya kuacha soka ili kuwekeza
nguvu kwenye ndoa.
Alisema: “ Miaka kumi iliyopita,
nilimweleza mke wangu (Annie),
‘Anipe miaka mitano zaidi katika soka
inatosha’, lakini hadi leo ninaendelea
na kazi.
“Ni vigumu kuwa na muda wa kutosha
kukaa pamoja kwa sababu ya ratiba
ngumu ya masuala ya soka. Kuna
wenzetu wanaondoka Jumatatu na
kurudi Ijumaa
“Ninasafiri kikazi, lakini tatizo si kiasi
gani cha muda ninaotumia mbali ya
familia yangu, bali ubora wa muda
ninaotumia na familia yangu.
“Nikizingatia hilo, kuna madhara.
Familia inakosa ubora wa huduma
wanazostahili nikiwa nyumbani, kwani
ninafikiria mchezo unaofuata.”
Aliongeza: “Mke wangu anapenda
kuangalia soka, anaona mechi za
Arsenal akiwa nyumbani . Siyo shabiki,
lakini anapenda michezo. Ni kwa kuwa
hakuwa na chaguo.”
-

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni