other blog

Jumapili, 30 Agosti 2015

Soma droo ya uefa hapa katika mechi za makundi Man Utd yapeta, Arsenal kwa Bayern Arsenal imetupwa kwa Bayern Munich wakati Manchester United ikipewa vibonde katika mashindano ya


Mshambuliaji wa FC Barcelona, Lionel
Messi akipokea tuzo ya mwanasoka bora
wa Ulaya kutoka kwa rais wa UEFA,
Michael Platini (kulia) baada ya kumshinda
mpinzani wake Cristiano Ronaldo wa Real
Madrid jana wakati kwa kupangwa kwa
ratiba ya Ligi ya Mabingwa UEFA jijinin
Monaco.
Monaco, Ufaransa. Arsenal imetupwa
kwa Bayern Munich wakati
Manchester United ikipewa vibonde
katika mashindano ya Ligi ya
Mabingwa, huku Lionel Messi akitwaa
tuzo ya mwanasoka bora wa mwaka
wa Ulaya.
Katika ratiba hiyo iliyopangwa jana
jijini Monaco inaonyesha Arsenal
inakutana tena na Bayern kwa mara
ya tatu ndani ya misimu minne
mfululizo.
Gunners pia itacheza na Olympiakos
ya Ugiriki na Dinamo Zagreb ya
Croatia.
Manchester United imepangwa
kuchezwa na PSV Eindhoven mechi
itakuwa kimrudisha mshambuliaji
Memphis Depay kucheza na timu yake
ya zamani.
Chelsea imetupwa kwa Porto, klabu
ambayo Jose Mourinho alitwaa taji
lake la kwanza la mashindano hayo
2004.
Manchester City itawavaa mabingwa
wa Serie A, Juventus pamoja na
mabingwa wa Europa Ligi, Sevilla na
Borussia Monchengladbach.
Mabingwa watetezi Barcelona
wakipangwa katika Kundi E, pamoja
naza Bayer Leverkusen, Roma na
BATE.
Barca, ambao wametwaa taji hilo mara
tano katika hisoria ya timu hizo
wataanza utetezi wa nyumbani
wakisaka heshima mpya ya kuvunja
rekodi ya kulinyakua taji hilo mara
nyingi.
Juventus, ambao walicheza fainali ya
msimu uliopita dhidi ya Barca,
wamepangwa katika Kundi D,
sambamba na timu za Manchester
City, Sevilla na Borussia
Monchengladbach.
Katika Kundi A, mabingwa wa
Ufaransa, Paris Saint-Germain
wataumana na mabingwa wa
kihistoria barani Ulaya, Real Madrid
pamoja na timu za Shakhtar Donetsk
na Malmo.
Wakifuzu kwa kishindo katika hatua ya
makundi, Manchester United nao
wamerudi katika fainali hizo kwa kasi
baada ya kukosa mashindano hayo
kwa msimu mmoja.
Man United wametupwa katika Kundi
B wakiwa na timu za PSV, CSKA
Moscow na Wolfsburg ya Ujerumani.
Katika Kundi C, mabingwa wa Ureno,
Benfica watakuwa na mabingwa wa
zamani wa Hispania, Atletico Madrid,
Galatasaray na Astana.
Vinara wa Ligi Kuu England msimu
huu, Manchester City wamepangwa
kuanza mashindano hayo katika Kundi
D, ambalo pia lina timu za Juventus,
Sevilla na Borussia Monchengladbach.
Bayern Munich, ambao ni mabingwa
wa Ujerumani waliocheza fainali ya
Ligi ya Mabingwa 2012 dhidi ya
Chelsea, wamepangwa kuanza
kampeni za msimu huu katika Kundi F
pamoja na timu za Arsenal,
Olympiacos na Dinamo Zagreb.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu
England, wao wamepangwa katika
Kundi G, wakiwa na Porto, Dynamo
Kiev na Maccabi Tel-Aviv ya Israel.
Katika Kundi H, mabingwa wa Urusi,
Zenit, Valencia, Lyon na Gent. Ligi ya
Mabingwa Ulaya msimu huu
inatarajiwa kuanza mwezi ujao.
Katika hatua nyingine, mshambuliaji
wa kimataifa wa Argentina
anayeichezea Barcelona, Lionel Messi
amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa
Ulaya wa mwaka.
Messi ameibuka na ushindi katika tuzo
hiyo akiwabwaga wenzake wawili
Cristiano Ronaldo wa Real Madris na
mshambuliaji mwenzake wa Barca,
Luis Suarez.

By rizik malya ... Logarusic amrejesha Kenya Ivo Mapunda Kocha wa zamani wa Simba, Zdravko Logarusic amempa kibarua kipa wa zamani wa klabu hiyo, Ivo


Ivo Mapunda
Dar es Salaam. Kocha wa zamani wa
Simba, Zdravko Logarusic amempa
kibarua kipa wa zamani wa klabu hiyo,
Ivo Mapunda (pichani) kwa kukubali
kumsajili katika klabu yake, AFC ya
Leopards ya Kenya.
Mapunda aliliambia gazeti hili jana
kuwa muda wowote atasaini kuichezea
klabu hiyo ya Ligi Kuu Kenya baada ya
kutoswa na Wekundu wa Msimbazi.
Ivo, ambaye alidaiwa kuchukua Sh10
milioni za awali kwa ajili ya kusaini
mkataba mwingine na klabu hiyo
aliachana na klabu hiyo kwa madai ya
viongozi wa klabu hiyo kuwa aligoma
kusaini fomu za usajili.
Kipa huyo mahiri na mzoefu aliliambia
gazeti hili kuwa ameitwa na Logarusic
kwa ajili ya kufanya mazungumzo na
kisha kusaini mkataba.
“Logarusic alinifundisha wakati ule
nikiwa Gor Mahia na alivyokuja Simba
nami nikamfuata, kisha akaondoka na
kujiunga na AFC Leopards na ameniita
ili niende huko,” alisema.
Pia, Ivo aliwataka wachezaji nchini
kuwa makini na mikataba yao na kama
wanashindwa kujisimamia wenyewe
inafaa watafute watu wa karibu wa
kuwasimamia kwani viongozi wengi wa
klabu kubwa ni wajanja wajanja.
“Nawashauri wachezaji wawe makini
kwenye suala la mikataba, wawe
makini kuisoma vizuri mikataba yao
na kama wakishindwa watafute
wasimamizi wa karibu.
“Wachezaji wengi wamekumbana na
matatizo ya mikataba yao na hiyo
inatokana na kutoisoma vizuri
mikataba hiyo na kuielewa ndipo
usaini,” alisema.
Aliongeza: “Viongozi wengi ni wajanja
katika masuala ya mikataba, baadhi
yao siyo wa kweli na kuna masuala ya
bima na mengine muhimu kwenye
mikataba hawayafuti, wanachoangalia
ni kukutumia wakishakuchoka
wanakuacha na mchezaji ukiwa
mkweli kwao wanakuweka pembeni.”
“Mchezaji ukipata timu inakupa
maslahi mazuri iwe nje ya nchi au
hapa nyumbani wewe nenda tu
hakuna haja ya kujishauri kwani mpira
ni biashara.
“Using’ang’anie sehemu moja hata
kama haina masilahi kwako hata kama
unacheza nje na hakuna masilahi na
nyumbani kuna timu imekuita
inalikupa vizuri rudi,” alieleza.
Kuhusu kuachwa na Simba, alisema ni
mizengwe, lakini binafsi hajali kwani
hawezi kukosa timu ya kucheza.
“Kuna maneno mengi yametokea,
naamini ni mizengwe imesababisha
yote haya kwani iliamriwa tukae kikao
cha pamoja mwisho wa siku
nikaambiwa sina ushirikiano.
“Wakati naendelea kuuguza majeraha
kuna kiongozi wa Simba alitumwa
kuniletea fomu za usajili, lakini
hakunitafuta na baadaye nikasikia
amerudisha majibu kwa viongozi kuwa
sionekani na kamati ya usajili ikaamini
bila kuniita ili nijitetee.
Aliongeza: “Nilishangaa sionekani vipi
wakati mimi nipo kila siku na wengi
walifahamu kuwa ninaumwa, lakini
isitoshe hata huyo kiongozi
aliyetumwa kwangu sina mazoea naye
na hata kuhusu masuala ya mimi kuwa
majeruhi hakuwa anafuatilia sasa sijui
alikuwa na lengo gani la kurudisha
majibu kama hayo.”
Alisema hakuwa na haraka ya kusaini
mkata mpya wakati mkataba wake
umebaki miezi michache kwa sababu
alihakikishiwa kuwa ataendelea
kuitumikia timu hiyo msimu ujao.
“Sikuwa na haraka ya kusaini mkataba
mpya baada ya mkataba wangu kubaki
miezi michache kwa sababu sikuwa na
wasiwasi, waliniambia kuwa
wataendelea na mimi, hivyo sikuona
haja ya kusaini mapema kabla ya
mkataba wangu haujaisha na isitoshe
tayari walishanipa kiasi cha fedha,”
alisema kipa huyo aliyewahi kuichezea
pia Yanga miaka michache iliyopita na
baadae kwenda nje ya nchi.
-

Jumamosi, 29 Agosti 2015

Kikwete atahadharisha kauli za uvunjifu wa amani Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amesema baadhi ya kauli zinazotolewa


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya
Kikwete amesema baadhi ya kauli
zinazotolewa na Umoja wa Vyama vya
Upinzani (Ukawa), zinaashiria uvunjifu
wa amani pindi matokeo ya kura
yatakapoanishwa baada ya zoezi la
upigaji kura Oktoba 25 mwaka huu.
Rais Kikwete alisema baadhi ya kauli
hizo zimekuwa zikionyesha wazi
viashiria vya uvunjifu wa amani na
upotoshaji kwa kundi kubwa la vijana
ambao wanapiga kura kwa mara ya
kwanza.
Akizungumza wakati akizindua
Kampeni ya Mama Ongea na Mwanao
jijini Dar es Salaam Rais Kikwete
alisema;
“Wamediriki kusema wazi bila kificho
kwamba patakuwa hapatoshi, hizi ni
kauli zinazoashiria uvunjifu wa amani.
Tunachokisema CCM ushindi kwetu ni
lazima na tutashinda kwa kishindo na
kwenda nginja nginja mpaka Ikulu.”
Kikwete alisema CCM imejipanga
kuhakikisha inapata ushindi katika
Uchaguzi Mkuu ujao na kuongeza
kuwa ili kufanikisha hilo wamepanga
kikosi kazi ambacho kitatembea
nyumba kwa nyumba, chumba kwa
chumba, mtu kwa mtu ikiwa kwa sasa
tayari wameshaanza kufanya kampeni
zao kupitia mtandao ya simu za
mkononi.
Katika hafla hiyo ya kuzindua kampeni
hiyo inayoratibiwa na msanii wa
filamu na Miss Tanzania mwaka 2006,
Wema Sepetu, Rais Kikwete aliwataka
wanawake kaungalia mazuri yote
yaliyofanywa na Serikali ya CCM katika
kumuinua mwanamke.
-

Jumatano, 26 Agosti 2015

LASTECK ALFRED 0 Recomendar DESKTOP VIEW BACK TO TOP Pluijm: Yondani, Cannavaro igeni Kocha mkuu wa Yanga, Hans Pluijm amewataka mabeki Ligi Kuu wakiwamo wa klabu yake, Kelvin Yondani


Kocha mkuu wa Yanga, Hans Pluijm.
Dar es Salaam. Kocha mkuu wa Yanga,
Hans Pluijm amewataka mabeki Ligi
Kuu wakiwamo wa klabu yake, Kelvin
Yondani na Nadir Haroub ‘Cannavaro’
waige aina ya ukabaji wa beki wa
Azam, Pascal Wawa.
Alisema ukabaji wa nguvu na wa
kujiamini wa beki huyo raia wa
Ivory Coast ndiyo unaotakiwa kwa
sasa kwenye soka.
Alisema, “ Wawa (Pascal) ni beki
mahiri na anayetakiwa kuigwa na
mabeki wengine Ligi Kuu, lakini pia na
mabeki wangu Nadir Haroub
‘Cannavaro’ na Yondani (Kelvin) kwa
kuwa beki huyo anakaba kwa nguvu
wakati inapoitajika huku akijiamini.
“Wawa ana nguvu anazitumia nguvu
zake akijiamini na kujua wazi kuwa
anafanya kitu sahihi. Ukabaji wake
unafuata sheria za soka na hata
anavyofanya hivyo na wachezaji
kumlaumu basi ni wazi kuwa
wachezaji hawatambui kuwa anafanya
kazi yake inavyotakiwa.
“ Kizuri anachofanya ni kujiamini na
kujua sheria za soka, pia anatumia
nguvu akijua kuwa hajakosea wala
hatadhibiwa kwa kuwa anafanya kitu
sahihi na kwa muda mwafaka,”
alieleza kocha huyo.
Alisema kuwa ukabaji wa Wawa una
utofauti mkubwa na ule unaofanywa
na mabeki wengine Tanzania.
“Wawa anakaba kwa nguvu kwa
malengo na kujiamini, lakini mabeki
wengi ambao nimekuwa nikiona hapa
wanakaba kwa nguvu bila ya lengo la
kuisaidia timu kimpira zaidi
wanawaumiza wenzao, pia wanakaba
kwa nguvu bila kujiamini na chote
wanachokuwa wanafanya wanaona
kama vile wanakosea na mara nyingi
huwa wanajikuta wakipatwa na hofu
wanapokuwa wakikaba huku waamuzi
wakiwafuatilia kwa umakini,” alieleza.
-

Majambazi yauawa Mwanza Polisi mkoani hapa wamefanikiwa kuwauwa majambazi wawili baada ya kutupiana nao risasi kwa zaidi


Kamanda wa Polisi Mwanza, Charles
Mkumbo
Mwanza. Polisi mkoani hapa
wamefanikiwa kuwauwa majambazi
wawili baada ya kutupiana nao risasi
kwa zaidi ya dakika 10.
Majambazi hao ambao walikuwa
wanne wanadaiwa kutaka kufanya
uhalifu kwenye Kisiwa cha
Chembaya kilichopo katika Ziwa
Victoria juzi.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi
Mwanza, Charles Mkumbo majambazi
hao walikuwa wanatumia usafiri wa
pikipiki na kwamba walianza
kutupiana risasi na polisi baada ya
kubaini kuwa wanafuatiliwa na askari
waliopata taarifa dhidi yao.
Akizungumza na waandishi wa habari
leo, Kamanda amesema polisi walipata
taarifa saa 8:00 mchana juzi kutoka
kwa raia wema kwamba kuna kikundi
cha majambazi kinajiaanda kufanya
uhalifu Ziwa Victoria.
“Baada ya Polisi kupata taarifa hizo
walijipanga na kuweka mtego kwenye
eneo la mwalo wa Kisaka uliyopo
katika Kata ya Ilemela,” Kamanda
Mkumbo amesema na kuongeza:
Kwa mujibu wa jeshi hilo, silaha moja
aina ya Shotgun iliyofutwa namba na
kukatwa kitako na mtutu wake
zimepatikana baada ya majambazi hao
kupekuliwa walikutwa na riasi tano.
Kamanda Mkumbo amesema miili ya
majambazi hao imehifadhiwa katika
hospitali ya Rufaa Bugando, jijini
Mwanza.

Je unakumbuka haya mazuri ya lowassa... yaone hapa

Lowassa aendelea kuumbua vigogo
Ingawa Wahenga wana msemo
usemao mgeni njoo mwenyeji
apone kwa mabosi wa mkoa wa
Kigoma hali imekuwa tofauti
baada ya mgeni wao, Waziri
Mkuu Bwana Edward Lowassa
kuwaonjesha joto ya jiwe
hadharani.
Miongoni mwa walioonja
shubiri ya Waziri Lowassa
ni Mkuu wa Wilaya ya
Kigoma, Bw. John Mongella
ambaye bila kutarajia
alijikuta akikatizwa kusoma
ripoti yake yenye kurasa
zaidi ya 10 wakati ndiyo
kwanza amefika ukurasa wa
tatu.
Ripoti hiyo ilianza
kumchafua Waziri Mkuu pale
Mkuu huyo wa Wilaya
aliposema kuwa chanzo cha
kuzorota kwa kilimo cha
kahawa ni ukosefu wa
wataalam wa zao hilo.
Bw. Lowassa akasema hayo ni
mambo ya zamani asiyotaka
kuyasikia katika ziara yake
na badala yake anahitaji
kuona wakuu hao wa wilaya
wakionyesha kwa vitendo
uelewa wao baada ya kupigwa
msasa wa nguvu na Rais
Kikwete kwenye semina
elekezi iliyomalizika hivi
karibuni huko Arusha.
’’John huna taarifa,
afadhali twende kwenye
ziara’’, akasema Bw.
Lowassa na kuinuka
kuendelea na ziara.
Bosi mwingine aliyekumbwa
na kasheshe hilo ni Mkuu wa
wilaya ya Kibondo Luteni
Kanari John Mzurikwao
ambaye naye aliambiwa
ripoti yake ni mbovu.
Waziri Mkuu akazidi
kumuumbua mkuu huyo wa
wilaya kwa kusema kuwa
anashangazwa na utendaji
wake wa kazi kwa vile ni
tofauti kabisa na jinsi
anavyomfahamu.
Akasema inaonekana wakuu
hao wa wilaya hawakuambulia
kitu katika semina elekezi
iliyoendeshwa na Rais
Kikwete hivi karibuni
katika hoteli ya Ngurdoto
iliyopo nje kidogo ya Jiji
la Arusha.
’’Inaonyesha kuwa semina
ile haikueleweka wala
hotuba ya Rais aliyoitoa
mwishoni mwa mwezi uliopita
haikusikilizwa, ndio maana
mambo haya yanajitokeza’’,
akasema Bw. Lowassa.
Kana kwamba hiyo haitoshi,
Lowassa pia akamuibukia
Katibu Tawala wa wilaya ya
Kigoma, Bw. Martin
Mgongolwa na wakurugenzi wa
wilaya hiyo kwa kushindwa
kumsaidia mkuu wa wilaya na
badala yake wakamuandalia
hotuba iliyopitwa na
wakati.
Akasema Mkuu wa wilaya hiyo
bado ni mgeni na anahitaji
msaada wa viongozi wengine
wa wilaya ambao wana uzoefu
na maeneo yao.
’’Mnashindwa kuwasaidia
vijana hawa na mnataka sisi
tuwashambulie bure’’,
akacharuka Bw. Lowassa.
Waziri Mkuu yuko mkoani
Kigoma kwa ziara ya siku
tano akikagua miradi
mbalimbali ya maendeleo.

Simba waleta msenegal mwingine... 0 Recomendar DESKTOP VIEW BACK TO TOP Niang mmh! Mwingine aja Wakati Papa Niang akishindwa kuonyesha makali yake Simba ikilazimishwa suluhu na Mwadui, leo




Mshambuliaji mpya wa Simba, Papa Niang
Dar es Salaam. Wakati Papa Niang
akishindwa kuonyesha makali yake
Simba ikilazimishwa suluhu na
Mwadui, leo itampokea mshambuliaji
mwingine kutoka Senegal, Pape
Abdoulaye N’Daw anayetarajiwa kutua
jijini Dar es Salaam akitokea Dakar.
Macho na masikio ya mashabiki wa
Simba jana yalikuwa kwa Niang
aliyecheza mechi yake ya kwanza
Tanzania, lakini alishindwa kukata kiu
ya mashabiki wake waliojitokeza
kwenye Uwanja wa Taifa.
Niang aliyedumu uwanjani kwa dakika
45 tu za kwanza, mashabiki wa Simba
walipata tukio moja tu la kuhadithia
juu ya nyota huyo katika sekunde 36,
alipopiga krosi iliyomgonga mkononi
beki wa Mwadui, Joram Mgeveke na
mwamuzi kuamuru penalti.
Hata hivyo, wachezaji wa Mwadui
walimzonga mwamuzi ambaye
baadaye alikwenda kumuuliza msaidizi
wake na kuamua mpira huo utolewe
nje ya eneo la penalti, adhabu ambayo
haikuzaa matunda.
Niang, ambaye ni mdogo wa
mshambuliaji wa kimataifa wa zamani
wa Senegal, Mamadou Niang
alionekana bado hajawa katika
kiwango chake na kushindwa
kushirikiana vizuri na Mussa Mgosi
kabla ya kutolewa wakati wa
mapumziko na nafasi yake kuchuliwa
na Hamis Kiiza.
Katika kile kinachooneka Simba bado
inasaka wachezaji wa kuimarisha
kikosi chake, leo watampokea
mshambuliaji N’Daw mwenye miaka
21, kutoka Senegal.
N’Daw alikuwa akichezea katika klabu
ya Dinamo Bucuresti ya Romania kabla
ya kuvunja mkataba wake kutokana
na kushindwa kutimiziwa masharti
yake ya kimkataba kwa mujibu wa
wakala wake, Paul Michel wa kampuni
ya Siavuma Sports ya Afrika Kusini.
Paul alilimbia gazeti hili jana kuwa
N’Daw alikuwa na wakati mgumu
Dinamo na kuamua kurejea nyumbani,
Senegal ambako alijiunga na klabu ya
Niarry Tally aliyoifungia mabao saba
katika ligi ya nchi hiyo.
Paul, ambaye ni wakala wa kocha wa
Simba, Dylan Kerr alisema N’Daw
atamaliza tatizo la ufungaji la klabu
hiyo pamoja na kuonyesha kiwango
cha juu katika michezo ya ligi na
kimataifa.
“Ni mchezaji mzuri ambaye naamini
atamaliza tatizo lao la ufungaji,
tulikubaliana niwaletee mchezaji, ni
matumaini yangu watamsajili kwa
sababu ni mshambuliaji wa kiwango
cha juu,” alisema Paul.
Mmoja wa viongozi wa Simba alisema
N’Daw alitegemewa kufika nchini
mapema zaidi, lakini matatizo ya
kupata vibali vya kufanya kazi
yalimkwamisha.
“Tumesikia sifa zake, lakini tulitaka
kumuona akicheza, japokuwa umri
wake mdogo wa miaka 21,
unatushawishi kwamba atakuwa
msaada kwetu kwa muda mrefu,”
alisema kiongozi huyo.
Tegete, Nizar warejea Taifa
Katika mchezo huo wa kirafiki ambao
makocha wa timu zote mbili walitumia
wachezaji wengi, lakini kuingia kwa
wachezaji wapya wa Mwadui, Jerryson
Tegete na Nizar Khalfan kuliamsha
shangwe kwa mashabiki wa Yanga
waliojitokeza uwanjani hapo.
Mwadui ilipata pigo dakika 77, baada
ya kipa wake Shabaan Kado kuumia na
kutolewa nje kwa machela na nafasi
yake kuchuliwa na Jackson
Abdulazack.
Pamoja na mabadiliko hayo, timu zote
zilionekana kushindwa kuwa na
mipango sahihi ya kutegeneza pasi za
mwisho za kupata mabao.
-

Na katika mchezo eaglefm..Samata, Ngassa, Uhuru wachemsha Haikuwa wiki nzuri kwa washambuliaji kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samata, Mrisho Ngassa na Uhuru




Mbwana Samata
Dar es Salaam. Haikuwa wiki nzuri
kwa washambuliaji kimataifa wa
Tanzania, Mbwana Samata, Mrisho
Ngassa na Uhuru Selemani baada ya
klabu zao kupoteza katika michezo
yao.
Samata alishindwa kuisaidia TP
Mazembe kukwepa kipigo cha bao 1-0
kutoka kwa Al Hilal mchezo
uliofanyika Omdurman wa kusaka
kufuzu kwa nusu fainali ya Ligi ya
Mabingwa.
Kwa matokeo hayo Hilal inaongoza
Kundi A, ikiwa na pointi nane sawa na
Mazembe wakitofautiana mabao.
Wakati Samata akipata kipigo hicho
Ngassa alikuwa benchi kuishudia timu
yake ya Free States Stars ikipokea
kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa
mabingwa wa Ligi Kuu Afrika Kusini,
Kaizer Chiefs.
Katika mchezo wake wa kwanza na
Free State Stars, Ngassa alicheza
dakika 64 na kupata kadi ya njano
wakati timu yake ilipofunga bao 1-0 na
Mpumalanga Black Aces.
Hiyo ni mechi ya pili mfululizo kwa
Free States kupoteza tangu kuanza
kwa Ligi Kuu Afrika Kusini na sasa
inashika mkia kati ligi hiyo yenye timu
16.
Naye Uhuru Selemani hakucheza
wakati timu yake ya Jomo Cosmos
ilipolazimishwa sare 0-0 na Golden
Arrows katika mchezo wa Ligi Kuu
Afrika Kusini.
Hata hivyo, winga huyo wa zamani wa
Simba, Uhuru tangu asajiliwe Cosmos
bado hajaanza kuicheza timu hiyo
katika michezo ya Ligi Kuu.
-

Kipindupindu chaota mizizi Dar, Morogoro Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na ugonjwa wa kipindupindu uliolikumba jiji la Dar es




TAHADHARI: Wafanyakazi wa afya katika
kambi ya wagonjwa wa kipindupindu
iliyopo katika Zahanati ya Mburahati jijini
Dar es Salaam, wakifanya usafi katika wodi
hiyo juzi. Picha na Venance Nestory
Dar/Moro. Idadi ya watu waliopoteza
maisha kutokana na ugonjwa wa
kipindupindu uliolikumba jiji la Dar es
Salaam imeongezeka na kufikia saba
huku waliolazwa wakifikia 230 na
Mkoa wa Morogoro ukiwa na
wagonjwa 32 na mmoja kupoteza
maisha.
Akizungumza ofisini kwake jana,
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk
Seif Rashid alisema Wilaya ya
Kinondoni inaongoza ikiwa na
wagonjwa186 huku Ilala na Temeke
zikiwa na wagonjwa 22 kila moja.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Morogoro,
Nicolaus Chiduo alisema tangu Agosti
18, watu 42 wameugua ugonjwa huo,
na kutibiwa na sasa wamebaki 18.
Dk Rashid alisema wizara yake
imetengeneza kambi katika manispaa
zote tatu; Kinondoni ipo katika
Zahanati ya Mburahati, Ilala (Kituo
cha Afya Buguruni) na Temeke
(Hospitali ya Temeke).
Alisema kuwa wananchi wanaweza
kuwasiliana na mganga Mkuu wa Mkoa
kwa simu namba 0767300234, endapo
wataona mtu mwenye dalili za
ugonjwa huo ili ushauri utolewe jinsi
ya kumsafirisha.
“Naomba sekta nyingine kama maji,
elimu, mawasiliano, uchukuzi na ujenzi
tushirikiane kutokomeza ugonjwa huu
kwa kuwapatia wananchi elimu ya
ugonjwa huu,” alisema Dk Rashid.
Ofisa Afya Wilaya ya Kinondoni,
Mathias Kapizo alisema tayari
wameanza kuchukua sampuli za maji
kutoka kwenye maeneo yaliyoripotiwa
kutoa wagonjwa wengi ili kubaini
chanzo cha tatizo hilo.
Ofisa Uhusiano wa Manispaa ya
Temeke, Joyce Msumba alisema wilaya
hiyo ilipokea wagonjwa 25 waliokuwa
na dalili za ugonjwa huo ila sampuli
zilionyesha kuwa 22 hawakuwa na
ugonjwa huo.
Alisema wagonjwa watatu wa familia
moja ambao sampuli zao zilionyesha
kuwa wana vimelea vya ugonjwa huo,
hawakutokea katika wilaya hiyo, bali
Manzese na mmoja alipoteza maisha.
Morogoro
Kuhusu athari za kipindupindu
wilayani Morogoro, imeelezwa kuwa
mgawo wa maji katika maeneo mengi
ndicho chanzo kikuu cha kuongezeka
kwa idadi ya wagonjwa.
Akizungumza kwenye kambi ya
Sabasaba, Dk Chiduo alisema Idara ya
Afya imelazimika kufungia maeneo
yote ya baba na mama lishe hasa yale
yenye mkusanyiko wa watu na kuzuia
uuzaji wa vyakula ndani ya mabasi.
Maeneo yaliyopigwa marufuku
kufanya biashara ya vyakula ni Soko
Kuu la Morogoro, Soko la Mawenzi na
maeneo yote ya stendi ikiwamo ya
Msamvu.
Alitaja maeneo yaliyoathiriwa kuwa ni;
Kilakala, Kihonda, Chamwino, Mkundi,
Boma, Lukobe, Kiwanja cha Ndege,
Sua, Kididimo, Nanenane, Kichangani,
Mafiga, Mwembesongo, Polisi Line,
Mzinga, Mzumbe, Sultani, Mafisa na
Mazimbu. Aliwataka wananchi
kuzingatia usafi katika maeneo yao na
kuacha kukaa na kula katika maeneo
ya mikusanyiko kama misiba.
Akizungumza marufuku ya kuuza
chakula, mama lishe, Amina Salim
alisema kinachowaumiza ni mikopo
waliyochukua katika taasisi za fedha.
Kauli hiyo iliungwa mkono na Samson
Akida aliyesema: “Wengi wetu
tumekopa ili tufanye biashara, sasa
hapa tunajiuliza tutalipa na kurejesha
nini?”
Imeandikwa na Lilian Lucas na
Emma Kalalu.
-

NEC yaonya vyama vya siasa vitakavyokiuka ratiba za kampeni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu wa


Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi, Kailima Ramadhani
Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vyote
vya siasa vinavyoshiriki Uchaguzi
Mkuu wa Oktoba 2015, kuhakikisha
vinafuata na kuheshimu ratiba ya
uchaguzi waliyojiwekea.
Katika taarifa kwa njia ya video
iliyotumwa kwa vyombo vya habari,
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi, Kailima Ramadhani
amesema kuwa vyama vyote vilishiriki
katika kuandaa ratiba hiyo na kuwa
viliiridhia hivyo hawana budi
kuhakikisha wanaifuata.
“Tulikaa na vyama, mimi sikuamua hii
ratiba, wao walipendekeza na
wakakubaliana na wakatoa ratiba hii,
cha kwanza kabisa vyama vya siasa
wazingatie waliyoyaweka humu,”
alisema Kailima.
Aliongeza kuwa utaratibu huo upo kwa
mujibu wa Sheria ya Maadili ya
Uchaguzi ya 2015 na kuwa wakikiuka,
sheria itawakamata.
“Kwenye maadili (Sheria ya Maadili ya
Uchaguzi 2015) kuna eneo ambalo
vyama vya siasa na wagombea
wanakubaliana kuzingatia muda wa
kuanza kampeni na muda wa kumaliza
kampeni,” alisema.
Aliongeza kwa chama au wanasiasa
watakaokiuka wataitwa kwenye kamati
ya maadili na kuhojiwa na
wataadhibiwa kwa mujibu wa sheria.
Agizo hilo la NEC linakuja siku chache
baada ya CCM kuzindua kampeni zao
siku ya Jumapili katika viwanja vya
Jangwani jijini Dar es Salaam ambapo
shughuli hiyo ya uzinduzi ilihitimishwa
majira ya saa 12.34 jioni, ikiwa ni nusu
saa zaidi ya muda unaotakiwa
kisheria.

Polisi yamtahadharisha Lowassa staili ya kampeni zake Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemtahadharisha mgombea wa urais kwa tiketi ya




Mgombea wa urais kwa tiketi ya Chadema
Edward Lowassa akishuka kwenye moja ya
daladala .
Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Kanda
Maalum ya Dar es Salaam
limemtahadharisha mgombea wa urais
kwa tiketi ya Chadema Edward
Lowassa kuwa kampeni alizoanza kwa
kuyatembelea makundi kadhaa
zinaweza kutumiwa na maadui wa
kisiasa kumdhuru.
Hata hivyo, wanasiasa wametakiwa
kufuata ratiba ya kampeni kwa
kuzingatia mwongozo wa Tume ya
Uchaguzi (NEC) ili kulisaidia jeshi hilo
kukabiliana na vitendo viovu.
Onyo hilo limetolewa ikiwa ni siku ya
pili tangu Lowassa na mgombea
mwenza Juma Duni Haji walipoanza
kuwatembelea wananchi huku
wakitumia usafiri wa umma.
Kwa kutumia staili hiyo, leo Lowassa
akiwa na Duni Haji wametembelea
maeneo ya Tandika, Tandale na
Kariakoo jijini Dar.
Akizungumza na wanahabari leo jijini
Dar, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum
Dar es Salaam, Suleiman Kova
amesema ziara iliyofanywa leo
maeneo ya Swahili, Kariakoo
zimesababisha mikusanyiko isiyo ya
lazima na kusimamisha shughuli za
maendeleo.
Baada ya CCM kuzindua kampeni zake
mwishoni mwa juma lililopita viwanja
vya Jangwani, jijini Dar es Salaam,
Chadema nacho kinajiandaa kufanya
hivyo Agosti 29 maeneo hayohayo.
-

Jumanne, 25 Agosti 2015

NAFASI ZA

HALIMASHAURI YA WILAYA YA
MAKETE
NAFASI ZA KAZI
Mkurugenzi Mtendaji (Wilaya ya
Makete kupitia kibali cha ajira
mpya kilichotolewa na Katibu
Mkuu - Utumishi Kumb. Na.
CB.170/363/01 /1/36 anapenda
kuwatangazia wananchi wote
wenye sifa za kuajiriwa kuleta
maombi yao ya kazi kwa nafasi
zifuatazo:-
1. Mtendaji Wa Kijiji III -
NAFASI 20
Majukumu ya Kazi
• Kuwa Afisa Mashuhuli na
Mtendaji Mkuu wa Serikali ya
Kijiji
• Kusimamia ulinzi na usalama.
• Kusimamia utawala bora
katika Kijiji
• Kuwa katibu wa mikutano na
kamati zate za Halmashauri ya
Kijiji
• Kutafsiri na kusimamia sera,
sheria na taratibu zinazoongoza
Serikali ya Kijiji
• Kusimamia, kukusanya na
kuhiladhi kumbukumbu zote na
nyaraka za Kijiji.
Ngazi ya Mshahara
Kwa kuzingatia viwango vya
Serikali ngazi ya mshahara ya
TGS B kwa mwezi.
Sifa za Mwombaji
Mhitimu wa kidato cha nne au
sita waliohitimu mafunzo ya
cheti katika moja ya fani za
Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii,
Usimamizi wa fedha, Maendeleo
ya jamii au Sayansi ya Sanaa
kutaka Chuo cha Serikari za
Mitaa Hombolo, Dodoma au
Chua chochote
kinachotambuliwa na Serikali.
============
2. Afisa Maendeleo Ya Jamii
Msaidizi III- NAFASI 19
Majukumu ya Kazi
• Kuratibu shughuli zote za
Maendeleo ya jamii katika Kata
kwa kuzingatia jinsia.
• Kuhamasisha kuondokana na
mila/desturi potofu katika jamii.
• Kuelimisha jamii juu ya
kutekeleza masuala ya kijinsia
• Kuelimisha jamii kuhusu
masuala ya watoto .
• Kukusanya, kuchambua na
kuweka takwimu za Kata
zinazozingatia jinsia
zitakazotumika katika mipango
ya maendeleo.
• Kuhamasisha jamii juu ya
kutumia teknolojia rahisi na
sahihi.
Ngazi ya mshahara
Kwa kuzingatia viwango vya
Serikali ngazi ya mshahara TGS B
kwa mwezi
Sifa za mwombaji
Wahitimu wa kidoto cha nne au
sita waliohitimu mafunzo ya
cheti cha Maendeleo ya Jcmii
kutoka vyuo vinavyotambulika
na Serikali.
================
3. Msaidizi Wa Kumbukumbu
II -NAFASI 4
Majukumu ya Kazi
• Kutafuta kumbukumbu/
nyaraka/ mafaili yanayohitajika
na watumiaji
• Kupokea, kuandikisha na
kutawanya .barua au nyaraka
mbalimbali.
• Kupanga nyaraka mbalimbali
katika reki na makabati ya
kuhifadhia nyaraka.•
• Kuweka kumbukumbu (barua
na nyaraka) katika mafaili.
• Kushughulikia maombi ya
kumbukumbuku/nyaraka kutoka
ndani ya Halmashauri na taasisi
za nje ya Halmashauri.
Ngazi ya mshahara
Kwa kuzingatia viwango vya
Serikali ngazi ya mshahara ya
TGS B kwa rt1V>ezi.
Sifa za mwombaji
Wahitimu wa kidato cha nne au
sita waliohitimu mafunzo ya
cheti cha utunzaji wa
kumbukumbu katika fani za Afya,
Ardhi, Mahakama au Masjala
kutoka Chuo cha Utumishi wa
Umma, Dar es Salaam au Chuo
chochote kinachotambuliwa na
Serikali. -
==============
4. Katibu Mahsusi III -
NAFASI 7
Majukumu ya Kazi
• Kuchapa barua, taarifa na
nyaraka za kawaida
• Kusaidia kupokea wageni
kuwasikiliza shida zao na
kuwaelekeza sehemu
wanapoweza kushughulikiwa.
• Kusaidia kutunza taarifa za
matukio, miradi-waqeni, tarehe
za vikao na safari za Mkuu wake
kazini.
• Kusaidia kutafuta na
kumpatia Mkuu wake majalada
au nyaraka zinazohitajika kwa
shughuli za kiofisi.
• Kusaidia kupokea na
kuyasambaza majalada sehemu
zinazohusika
• Kusaidia kufikisha maelekezo
ya Mkuu wake wa kazi kwa
wasaidizi wake na pia kumpatia
mrejesho wa maagizo
yaliyotolewa.
Ngazi ya mshahara
Kwa kuzingatia viwango vya
Serikoli ngazi ya mshahara ya
TGS B kwa mwezi
Sifa ya Mwombaji
Wahitimu wa kidato cha nne au
sita waliohitimu mafunzo ya
cheti cha Uhazili ngazi ya III na
kupata Cheti katika Programu za
Windows, Microsoft Office,
Internet, E-mail na Publisher.
Aidha, woombo]i wawe
wamefaulu somo la Hatimkato ya
maneno BO [kwo dakika moja).
Masharti ya Ujumla
• Waombaji wote wawe ni raia
wa Tanzania
• Waombaji wote
waambatanishe nakala ya cheti
cha kuzaliwa
• Waombaji wote
waambatanishe na maelezo
binafsi (CV)
• Waombaji waambatanishe
picha 1 "Passport Size" ya hivi
karibuni na nakala za vyeti halisi.
• Transcript "Testmonials" na
"Provisional Results" au
Statement of Results
havitakubaliwa. .
• Mwombaji awe na urnri
usiozidi miaka 45 na usiopungua
miaka 18.
Maombi yatumwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya
Makete,
S.L.P.6,
Makete.
Maombi yawasilishwe kabla au
mnamo tarehe 31/08/2015 soa
9:30 A1asiri. Maombi
yatakayowasilishwa baada ya
tarehe na muda uliopangwa
hayatafanyiwa kazi.

Jumatatu, 24 Agosti 2015

Pingamizi dhidi ya Profesa Maghembe latupwa Msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo la Mwanga ametupilia mbali pingamizi zilizowekwa na mgombea ubunge


Waziri wa Maji ambae pia ni Mbunge wa
Mwanga ,Profesa Jumanne Maghembe.
Mwanga . Msimamizi wa uchaguzi wa
Jimbo la Mwanga ametupilia mbali
pingamizi zilizowekwa na mgombea
ubunge kwa tiketi ya Chadema, Henry
Kileo dhidi ya wagombea wenzake
wawili.
Kileo aliweka pingamizi dhidi ya
Waziri wa Maji na mbunge
anayemaliza muda wake, Profesa
Jumanne Maghembe (CCM) na
Mgombea wa NCCR-Mageuzi,
Youngsaviour Msuya ambaye ni
wakili kitaaluma.
Kwa mujibu wa Kileo, wagombea hao
hawakuwa wamewasilisha tamko
rasmi la kisheria lililotolewa mbele ya
hakimu mkazi wa Wilaya ya Mwanga
na pia, hawakuwa wamedhaminiwa na
vyama vyao.
Kileo alidai mihuri iliyogongwa katika
fomu zao ni ya katibu wa wilaya
badala ya ofisi ya wilaya. Pia, alidai
kuwa picha ya Profesa Maghembe
haikupigwa ndani ya miezi mitatu.
Hata hivyo, msimamizi wa uchaguzi wa
jimbo hilo, Jamhuri William ametupilia
mbali sababu hizo akidai kuwa
kumbukumbu alizonazo ofisini kwake
wagombea hao wamedhaminiwa na
vyama vyao.
Alisema hatua ya Msuya kutoa tamko
mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya
ya Moshi haimuondolei sifa ya
kuteuliwa mgombea na pia, haoni
tatizo kwa Profesa Maghembe kula
kiapa Mahakama ya Mwanzo. “Masuala
yanayohusu mihuri ya chama
inategemea na muundo wa uongozi na
utendaji katika chama husika. Hakuna
kosa kwa katibu wa wilaya kugonga
muhuri wake,” alisema msimamizi
huyo.
William alifafanua kuwa suala la umri
wa picha ya Profesa Maghembe halina
uthibitisho na kwamba, malipo ya risiti
ya tamko rasmi siyo mojawapo ya
sharti la uteuzi wa mgombea ubunge.
Baada ya kutupwa kwa pingamizi lake,
Kileo aliliambia gazeti hili jana kuwa
atakata rufaa kwa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) akipinga uamuzi huo
wa msimamizi kuwa haukutenda haki.
Kileo alisema mathalani katika
uchaguzi wa Serikali za Mitaa
uliofanyika mwaka jana, baadhi ya
wagombea wa Chadema walienguliwa
baada ya fomu zao kugongwa muhuri
na katibu wa wilaya.
-

Magufuli afungua pazia la kampeni, ataja vipaumbele 25 Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amefungua pazia la kampeni za chama hicho kwenye Viwanja


Mgombea urais wa CCM, Dk John
Magufuli akihutubia wafuasi wa chama
hicho waliofurika katika Viwanja vya
Jangwani, Dar es Salaam wakati wa
uzinduzi wa kampeni za chama hicho jana.
Picha na Edwin Mjwahuzi
Dar es Salaam. Mgombea urais wa
CCM, Dk John Magufuli amefungua
pazia la kampeni za chama hicho
kwenye Viwanja vya Jangwani katika
tukio lililohudhuriwa na maelfu ya
wananchi, huku akieleza mambo 25
atakayoyafanya iwapo Watanzania
watamchagua kuwa Rais wa Awamu ya
Tano.
Huku akitumia maneno: “Mimi kazi
tu”, “Tanzania ya Magufuli ni ya
viwanda”, Dk Magufuli aliyetumia
dakika 53 kueleza sera zake, kuanzia
saa 11.40 hadi 12.33 jioni alisema
Watanzania wanataka kitabu kipya cha
mabadiliko na yeye na mgombea
mwenza, Samia Suluhu ndiyo
wanaoweza kuyaletea.
Mgombea huyo wa urais wa CCM
aliahidi kuanzisha mahakama
maalumu ya kusikiliza kesi za rushwa
na ufisadi, kumaliza tatizo la
wanafunzi wa elimu ya juu kukosa
mikopo, kuhakikisha mama lishe
hawabughudhiwi, kusimamia haki za
wasanii, kulinda Muungano na
usalama wa nchi.
Aliahidi kutoingilia utendaji kazi wa
Bunge na Mahakama, kuheshimu
mawazo ya vyama vingine vya siasa,
kuimarisha vyombo vya ulinzi na
usalama, wafanyabiashara wadogo na
wakubwa wote kulipa kodi, kuendeleza
kilimo, mifugo, uchimbaji wa madini,
majisafi na elimu bora.
Nyingine ni kusimamia nishati ya gesi,
ujenzi wa barabara, reli, kuboresha
sekta ya utalii, kuimarisha uwekezaji,
kuwasaidia walemavu na kusimamia
uhuru wa habari.
Mkutano huo ulioanza rasmi saa 9.30
alasiri ulihudhuriwa na viongozi
mbalimbali wa Serikali na CCM,
wakiongozwa na Mwenyekiti wake,
Rais Jakaya Kikwete na marais
wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na
Benjamin Mkapa. Wengine ni Waziri
Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba na
Salim Ahmed Salim.
Ahadi alizotoa
Mgombea huyo alitoa ahadi
mbalimbali ikiwamo ajira akisema:
“Ninataka Watanzania wapate ajira,
kazi ya Serikali itakuwa kukusanya
kodi tu. Viwanda vinaweza
kutengeneza ajira kwa asilimia 40 hasa
kwa vijana wanaohitimu vyuo
mbalimbali nchini.”
Kuhusu ubinafsishaji, alisisitiza: “Kuna
viwanda vilibinafsishwa sasa wahusika
wasipoviendeleza wajiandae
kuvirudisha haraka.”
Mbali na kurejesha viwanda
vilivyobinafsishwa, alisema akipewa
ridhaa hiyo atahakikisha chini ya
uongozi wake, anajenga viwanda vingi
vipya, akiainisha vile mahsusi kwa
shughuli za kilimo, mifugo, kusindika
nyama na madini.
Alitaja kipaumbele kingine kuwa ni
kilimo na kwamba atahakikisha sekta
hiyo ambayo ndiyo mhimili wa uchumi
inaendelezwa.
“Tutaleta vitendea kazi, pembejeo na
vifaa vingi vya kisasa na vya kutosha
kwa wakulima… kama nilivyosema
hapo awali, tutajenga viwanda kwa
ajili ya wakulima pia.
Mbunge huyo wa zamani wa Chato
alisema pia kipaumbele kingine katika
Serikali yake ni kuhakikisha kuwa
wananchi wa mjini wanapata majisafi
na salama kwa asilimia 95 na wananchi
wa vijijini wanapata maji kwa asilimia
85.
Kuhusu afya alisema: “Tutahakikisha
tunakuwa na vituo vya afya, zahanati
na hospitali katika maeneo mbalimbali
kwa sababu tunaamini maendeleo ya
kweli hayawezi kupatikana kama
wananchi hawana afya bora.”
Kipaumbele kingine ni mikopo kwa
wanafunzi wa elimu ya juu akisema
watakuwa wanapata mikopo kwa
wakati bila kuchelewa na kwamba
watajikita pia katika kujenga hosteli
kwa wanafunzi wa vyuo.
“Mishahara ya walimu na wafanyakazi
wote tutaishughulikia. Hata madereva
haki zao za msingi lazima ziangaliwe,”
alisema huku akishangiliwa na wafuasi
wa chama hicho.
Mgombea huyo alisema anafahamu
kero ya msongamano wa magari katika
Jiji la Dar es Salaam na kwamba
maendeleo ya kweli yatapatikana
kama changamoto hiyo itafanyiwa
kazi.
“Tutaunganisha mikoa yote kwa
barabara zenye viwango vya lami na
pia tutajenga barabara za juu saba
jijini hapa,” alisema Magufuli.
Alisema akipewa ridhaa hiyo
itashughulikia suala la reli kwa
kujenga reli ya kisasa kwa viwango vya
Standard Gauge” na kuboresha
bandari na usafiri wa anga.
Kuhusu maliasili, alisema ni
kipaumbele katika Serikali yake
endapo akipewa ridhaa ya kuongoza
nchi huku akieleza kukerwa na
ujangili... “Ninapata shida sana
ninapoona meno ya tembo yanauzwa
Ulaya halafu unaambiwa yanatoka
Tanzania… sasa unajiuliza yanapitaje?”
Alisema ili kushughulikia suala hilo
atahakikisha watendaji wa sekta hiyo
wanaboreshewa masilahi yao ili
wachangie mapato ya nchi.
Aliahidi Serikali yake kuwa rafiki wa
wawekezaji na kwamba italinda
masilahi ya wafanyabiashara.
Mgombea urais huyo aliahidi kuwa
atalinda uhuru wa habari na atafanya
kazi na waandishi wa habari siyo tu
wakati wa kipindi cha kampeni, bali
hata baada.
Katika ahadi zake, Dk Magufuli
hakuwaacha wasanii, alisema
atahakikisha wanapata hakimiliki na
kuhakikisha wao pamoja na
wanamichezo wanaanzishiwa mfuko
kwa ajili ya kuwasaidia k

Tazama taarifa zetu za habari mtandaoni bonyeza link yetu hapo chini..

Jumapili, 23 Agosti 2015

Ni kumbukumbu nzito sana ambayo inaniumuza akili na kunipa maumivu ya moyo ....nioombeeni ndugu zangu..


Je unafahamu kua
Leo unajiombea mwenyewe. Kesho utaombewa?
Leo unatembea mwenyewe. Kesho utabebwa?
Leo unaoga mwenyewe. Kesho utaogeshwa?
Leo unaswali mwenyewe. Kesho Utaswaliwa?
Umejiandaa vipi? n kulala katika tumbo la ardhi?
Umejiandaa vipi?
na kukabiliana na maswali ya Malaika wa Kaburini, Au
Umejisahau na mapambo ya dunia bac ni tukio ambalo sintosahau pale ninapotazama kaburi la mpendwa wangu shangazi yangu .. Fabiola kimario aliyefariki dunia tarehe 4/8/2015 tegemezi pekee la maisha yangu
... nikikumbuka huwa nawasa kisha machozi yananito amini usiamini mungu yupo na anafanya kazi yake cha msingi weka roho yako safi kila wakati maana hujui saa wala dakika wa siku atakayokuja malaika kkuchukua... Amen..

Jumamosi, 22 Agosti 2015

Kaseja atua Mbeya, Ivo asaka timu nje Wakati dirisha la usajili likifungwa jana usiku, kipa Juma Kaseja amesaini mkataba wa miezi sita


Kipa Juma Kaseja (kushoto) akikabidhiwa
jezi na kiongozi wa Mbeya City. Katikati ni
Tippo Athuman akishudia tukio hilo.
Dar/Mbeya. Wakati dirisha la usajili
likifungwa jana usiku, kipa Juma
Kaseja amesaini mkataba wa miezi sita
wa kuichezea Mbeya City, huku
mwenzake Ivo Mapunda akitangaza
kusaka timu nje ya nchi.
Makipa hao wa zamani wa Taifa Stars,
Kaseja na Ivo msimu uliopita hakuwa
mzuri kwao kutokana na kuingia katika
migogoro na klabu zao, Yanga na
Simba.
Kaseja alikaa nje ya soka kwa muda
mrefu kutokana na kuwa na mgogoro
na klabu yake ya zamani Yanga
uliohusisha masuala ya kimkataba.
Mgogoro huo ulipelekea Yanga
kumpeleka Kaseja katika Makahama ya
Kazi, Kitengo cha Usuluhishi hata
hivyo bado kesi hiyo inaendelea, lakini
haimzuii kipa huyo kujiunga na timu
yoyote ili kuokoa kipaji chake.
Hata hivyo, juzi usiku Kaseja alisaini
mkataba wa miezi sita kuitumikia
Mbeya City katika msimu huu wa Ligi
Kuu unaotarajia kuanza Septemba 12.
Msemaji wa Mbeya City, Dismas Ten
alisema kusajiliwa kwa kipa huyo ni
kutokana na mapendekezo ya kocha
Juma Mwambusi aliyeuambia uongozi
wao kuhusu ubora wa kipa huyo.
‘’Ni kweli tumenasa kipa mwenye
uzoefu wa hali ya juu nchini na
amesaini miezi sita kwa ajili ya
kuitumikia Mbeya City,’’ alisema.
Aliongeza kuwa Kaseja bado yupo Dar
es salaam na muda wowote atatua
jijini Mbeya kwa ajili ya kuungana na
wachezaji wenzake kwa ajili ya
maandalizi ya Ligi Kuu.
Alisema vipimo vyote vya kiafya kwa
mchezaji huyo vimekamilika na
kwamba japo Kaseja amesaini mkataba
mfupi, lakini wana imani ataitoa
Mbeya City kutoka hapa ilipo na
kuifikisha katika hatua fulani.
Kocha Mwambusi alisema ameamua
kumuweka Kaseja katika kikosi hicho
kutokana na ubora wa kazi
anayoonyesha akiwa langoni.
“Kaseja ni kipa aliyekuwa akimvutia
wakati akiwa na timu mbalimbali
ikiwamo Yanga aliyokuwa akitumikia
misimu ya hivi karibuni na kwamba
ubora huo sasa atauonyesha akiwa na
Mbeya City.”
Wakati Kaseja akijikita Mbeya City,
swahiba wake, Ivo Mapunda wa Simba
alisema atarudisha fedha za usajili za
klabu hiyo na kuendelea na jitihada
zake za kwenda kucheza soka la
kulipwa nje ya nchi.
Mapunda aliyeidakia Simba kwa
misimu miwili akitokea Gor Mahia ya
Kenya aliingia katika utata wa usajili
wake baada ya viongozi wake kudai
anadengua kusaini mkataba huku yeye
akipinga hilo na kudai kuwa hakuna
kitu kama hicho.
Uongozi wa Simba ulidai kuwa
umeamua kuachana na kipa huyo kwa
madai ni msumbufu na hataki kusaini
mkataba kwani kila walipomtaka
kufanya hivyo alionekana kama hataki
na wakati walishampa Sh 10 milioni
ingawa Ivo alisema kuwa yupo kila
siku na alikuwa anaumwa na viongozi
wanajua sasa anashangaa kuambiwa
hataki kusaini mkataba.
Kipa huyo aliliambia gazeti hili jana
kuwa soka la Tanzania lina mizengwe
na linahitaji uvumilivu mkubwa na
yote yaliyotokea kwake anamwachia
Mungu ana atarudisha fedha za usajili
alizochukua.
Alisema malengo yake ni kucheza soka
la kulipwa nje ya nchi ingawa hadi
jana kama kuna timu iliyokuwa
ikimuhitaji ilipewa ruksa ya kufanya
naye mazungumzo kabla ya dirisha la
usajili kufungwa jana usiku.
“Nitarudisha fedha zao za usajili,
ingawa kwa sasa malengo yangu ni
kucheza nje ya nchi, lakini sizizuii
klabu za hapa zinazonihitaji
kuzungumza na mimi ili kucheza kwa
muda mfupi wakati naangalia mipango
mingine ya kwenda nje.
Simba iliamua kuachana na Ivo baada
ya kumsajili kipa Vincent Angban
kutoka Ivory Coast , pia ilikuwa mbioni
kumsajili kipa mwingine wa JKU ya
Zanzibar, Abdulrahiman Mohammed,
lakini inao makipa wengine chipukizi
Manyika Peter jr na Dennis Richard.
-

Saa 48 hatari za Msenegali wa Simba Mshambuliaji mpya wa klabu ya Simba, Papa Niang kutoka Senegal ana saa 48 za kuthibitisha ubora


Mshambuliaji wa kimataifa wa Senegal,
Papa Niang akiwasili Uwanja wa Ndege wa
Julius Nyerere, Dar es Salaam jana tayari
kwa majaribio kwenye klabu ya Simba.
Picha na Said Khamis
Dar es Salaam. Mshambuliaji mpya
wa klabu ya Simba, Papa Niang
kutoka Senegal ana saa 48 za
kuthibitisha ubora wake, vinginevyo
ataondoka kama wengine
waliomtangulia.
Simba imepanga kumpa mkataba wa
miaka miwili kwa sharti la kuonyesha
kiwango cha kuridhisha kwenye
mchezo wa Jumatatu dhidi ya Mwadui
ya Shinyanga.
Kwa upande wake, Niang alisema jana
baada ya kuwasili nchini,” Nimekuja
kufanya kazi na kama ni majaribio
wasipoteze muda, najiona tayari
nimefuzu.
“Nimecheza soka Ulaya kwa miaka
minane na kwenye mashindano
makubwa kwanini nishindwe kucheza
hapa ?
Alijigamba kuwa yeye ni
mshambuliaji mwenye uwezo wa
kufunga mabao na pia anaweza
kutengeneza nafasi za mabao kwa
wenzake.
“ Mpaka sasa nina rekodi nzuri ya
ufungaji wa mabao nikiwa na klabu ya
Al Shabab ya Kuwait, nimefunga
mabao manane msimu huu.
Nimetengeneza mabao mengine 11 na
hii ni kutokana na nafasi niliyokuwa
nikipangwa ya nyuma ya
mshambuliaji wa kati.
“Sioni kama majaribio ni saizi yangu
kwa sababu ninajielewa na ninajua
uwezo wangu. Sijui kwanini Simba
wanapoteza muda,” alijinasibu.
Aliongeza, “ Ninacheza nafasi zote za
ushambuliaji. Kazi itakuwa kwa kocha
kuamua nicheze wapi, kimsingi,
nitafunga mabao nikiwa kokote.
Anipange kama mshambuliaji wa
pembeni, iwe kulia au kushoto
atafurahi, lakini akiniweka katikati
atanipenda zaidi.”
Wakala wa mchezaji huyo, Massouka
Ekoko , raia wa Cameroon alisema, “
Niliambiwa Simba inahitaji mfungaji,
lakini pia mchezaji anayeweza
kumudu kufunga akitokea kushoto au
kulia mwa kiwanja na Niang
nimemleta kwa kuwa najua
atawasaidia. “
Tayari, uongozi wa klabu hiyo
umemwachia jukumu kocha Dylan
Kerr kuamua mchezaji mmoja wa
kigeni atakayetemwa kwenye kikosi
hicho endapo Niang atafuzu na kusaini
mkataba.
Msenegali huyo aliwasili Dar es Salaam
jana tayari kufanya mazungumzo ya
awali na uongozi wa klabu hiyo kabla
benchi la ufundi la timu hiyo kuamua
kumpima uwezo kwenye mchezo wa
kirafiki dhidi ya Mwadui ili
kujiridhisha kabla ya kumpa mkataba.
Rais wa Simba, Evance Aveva
aliliambia gazeti hili jana kuwa
mchezo wa Jumatatu dhidi ya Mwadui
inayonolewa na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’
ndiyo utaamua kama Niang atabaki
Simba msimu huu, ama la.
Aveva alisema kocha Kerr ndiye atatoa
uamuzi wa mwisho baada ya mchezo
huo na endapo ataridhika na kiwango
chake atapewa mkataba wa miaka
miwili.
Endapo Niang atafuzu, Simba
italazimika kupunguza mchezaji
mmoja wa kigeni ili kubaki nao saba
kama kanuni za TFF zinavyoelekeza.
Hata hivyo, Aveva alisema jukumu hilo
wamelikabidhi kwa kocha wao na
baada ya mchezo wa Jumatatu atatoa
msimamo wake.
Wachezaji wa kigeni waliopo Simba ni
Emery Nibomana na Kelvin
Ndayisengaa ( Burundi), Justice
Majabvi (Zimbabwe) , Hamis Kiiza,
Simon Sserunkuma na Juuko Murshid
(Uganda) na kipa Vincent Angban,
raia wa Ivory Coast.

‘Utatu’ huu kumaliza mechi Azam, Yanga Baada ya tambo za muda mrefu kuhusu ubora wa vikosi vyao, Azam na Yanga zina silaha hatari tatu

Dar es Salaam. Baada ya tambo za
muda mrefu kuhusu ubora wa vikosi
vyao, Azam na Yanga zina silaha hatari
tatu kila moja zinazoweza kumaliza
mechi mapema.
Mbinu za makocha Hans Pluijm na
Stewart Hall kwa dakika 90 zinaweza
kutuliza mizuka ya mashabiki wao
wakati timu zao zinapofungua msimu
wa Ligi Kuu.
Katika mchezo huo, Yanga italazimika
kuwa makini na washambuliaji watatu
wa Azam, John Bocco, Kipre Tchetche
na chipukizi Farid Mussa wanaoweza
kubadili matokeo wakati wowote.
Ukuta imara wa Azam ambao
haujaruhusu bao kwenye mechi zaidi
ya kumi ukiwa chini ya Serge Pascal
Wawa, Aggrey Morris, Said Morad
unatakiwa kuwa makini, kuwachunga
Donald Ngoma, Simon Msuva na Amissi
Tambwe, ambao wamekuwa chaguo la
kwanza Yanga, ingawa pia anaweza
kutumika Malimi Busungu.
Yanga na Azam zimekuwa na upinzani
zinapokutana kwenye mchezo wa Ngao
ya Jamii, Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam, zina na kumbukumbu ya
matokeo ya sare ya 0-0 kwenye
mchezo wao wa mwisho, robo fainali
ya Kombe la Kagame, ambao
uliamuliwa kwa penalti 5-3 zilizoipa
ushindi Azam.
Timu hizo zinakutana mara ya tatu
mwaka huu, baada ya awali kwenye
mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Azam
iliishinda Yanga 2-1, kisha zikakutana
kwenye mashindano ya Kagame na
Azam kushinda kwa penalti 5-3.
Hata hivyo, Azam haina rekodi nzuri
dhidi ya Yanga kwenye mechi za Ngao
ya Jamii, mara mbili timu hiyo
imepoteza kwa kufungwa bao 1-0,
mwaka juzi na pia 3-0 mwaka jana.
Kurejea uwanjani kwa nahodha Nadir
Haroub ‘Cannavaro’, Tambwe na
Ngoma waliokuwa majeruhi tangu
timu yao (Yanga) ilipokuwa kambini
Mbeya kumempa ahueni kocha Pluijm
anayeona kikosi chake kuwa
kiimekamilika.
Pluijm ambaye hupenda kutumia
mifumo ya 4-3-3 au 4-4-2, alisema
wako kamili na hawana hofu leo,
watalipa kisasi cha penalti 5-3 za
Kombe la Kagame. Kocha wa Azam,
Stewart Hall, hupenda kutumia
mfumo wa 3-5-2, amekiri kuwa mechi
itakuwa ngumu.
-

Unachopaswa kufanya siku ya uchaguzi Dar es Salaam. Tanzania inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25, mwaka huu. Baadhi ya wananchi


Jaji Damian Lubuva, Mwenyekiti NEC
Dar es Salaam. Tanzania inaelekea
kwenye Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25,
mwaka huu. Baadhi ya wananchi hasa
vijana waliofikisha miaka 18 hivi
karibuni hawajawahi kushiriki kwenye
uchaguzi wowote na uchaguzi huu ni
wa kwanza kwao.
Vijana hawa na watu wengine,
wanahitaji kujifunza au kukumbushwa
juu ya mambo ya kufanya siku ya
uchaguzi ili kufanya zoezi la upigaji
kura kuwa lenye mafanikio na
kuepusha uvunjifu wa sheria
unaoweza kumweka mtu matatani.
Kwa bahati mbaya, elimu kwa
mpigakura haitolewi mara kwa mara
kwa wananchi mpaka nyakati za
uchaguzi. Hata wakati huo ukifika,
baadhi ya watu hasa wale wa hali ya
chini, hawafikiwi na elimu hiyo.
Elimu kwa mpiga kura bado
inahitajika ili kila mwananchi afahamu
haki na wajibu wake katika mchakato
mzima wa uchaguzi. Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (Nec) ndiyo yenye jukumu la
kutoa elimu hiyo kwa kushirikiana na
wadau wengine.
Hata hivyo, zoezi hili linakabiliwa na
changamoto ya uhaba wa rasilimali za
kufanikisha utoaji wa elimu kwa
wapigakura. Vilevile, hakuna chombo
maalumu cha kuratibu na kusimamia
utoaji wa elimu ya uraia.
Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian
Lubuva anasema changamoto kubwa
wanayokabiliana nayo ni pamoja na
uhaba wa Asasi za kiraia zinazotoa
elimu kwa wapigakura na kuwafikia
wananchi wote nchi nzima.
Jaji Lubuva anasema Tume imejipanga
vizuri kuhakikisha kwamba elimu
inawafikia wapigakura nchi nzima.
Anasema watatumia vyombo vya
habari vikiwamo vinavyomilikiwa na
taasisi za dini ili kuwafikia wananchi
haraka zaidi.
Zingatia haya siku ya uchaguzi
Mkurugenzi wa uchaguzi – Nec,
Kailima Kombwey anafafanua mambo
muhimu ambayo mpigakura anatakiwa
kufanya siku ya uchaguzi bila kuathiri
masharti ya sheria za uchaguzi na
kanuni zake.
Wahi kituoni
Anasema jambo la kwanzana la msingi
ni kuwahi asubuhi katika kituo cha
kupigia kura. Kombey anasema
wananchi wanatakiwa kufika vituoni
kuanzia saa moja asubuhi wakiwa na
vitambulisho vyao vya kupigia kura.
Anasema kila mpigakura anatakiwa
kujua kituo atakachopigia kura na
kuhakiki kama jina lake lipo kwenye
orodha ya wapigakura kwenye kituo
husika.
Panga foleni
Kombey anabainisha kuwa watu
watapanga foleni kuingia chumba cha
kupigia kura na vituo vitafungwa
kuanzia saa 10 jioni. Anasema
watakaokuwa kwenye mstari baada ya
muda huo wataruhusiwa kuendelea
kupiga kura mpaka watakapomaliza.
“Tunasisitiza wananchi wajitokeze kwa
wingi ili wawachague viongozi wao.
Kupiga kura ni jambo la muhimu kwa
maendeleo ya Taifa letu.
Wasipojitokeza basi wasilaumu
kiongozi atakayechaguliwa na
wengine,” alisema Kombwey.
Mkurugenzi huyo anasema katika
uchaguzi wa mwaka 2010,
waliandikisha watu milioni 20 lakini
waliojitokeza kupiga kura walikuwa
chini ya milioni 10. Kwa hiyo,
anasisitiza zaidi kujitokeza kupiga
kura siku hiyo.
Usivae sare za chama
Jambo la pili, mpigakura asivae nguo
yenye nembo au alama yoyote ya
chama cha siasa kwenye kituo cha
kupigia kura. Kufanya hivyo ni kukiuka
taratibu za uchaguzi na mtuhumiwa
anaweza kushitakiwa kwa kuhujumu
mchakato wa upigaji kura.
Kombey anafananisha jambo hilo na
akufanya kampeni siku ya kupiga kura,
jambo ni kinyume na kanuni. Kwa
hiyo, fulana, kofia, bendera au kanga
au nguo yoyote inayovaliwa na chama
chochote haitakiwi kwenye eneo la
kupigia kura.
“Tunatoa muda wa kampeni ili
wanasiasa na vyama vyao wajinadi
kadri wanavyotaka lakini siku ya
uchaguzi siyo siku ya kufanya
kampeni, ni kinyume cha kanuni za
uchaguzi,” anasema mkurugenzi huyo.
Anaendelea kubainisha kuwa Tume
kupitia kifungu cha 124 (a) cha sheria
ya taifa ya uchaguzi ya mwaka 1985
ilianda maadili ya uchaguzi ambayo
yamefanyiwa mabadiliko madogo
mwaka huu na kukubaliwa na vyama
vyote.
Wahusika wakuu katika maadili haya
ni Tume ya Uchaguzi, Serikali,
wagombea na wanachama wote wa
vyama vya siasa. Kombwey anasema
wadau hawa kwa pamoja wana wajibu
wa kufanya uchaguzi huru na wa haki.
Usilete ushabiki
Jambo la tatu, wapigakura wasilete
ushabiki kwenye vituo vya kupigia
kura. Mambo ya ushabiki ni pamoja na
kuongelea matokeo ya uchaguzi kabla
hayajatangazwa na mamlaka husika
zilizokasimiwa jukumu hilo.
Mkurugenzi huyo anafafanua kwamba
jambo hilo linajenga hisia tofauti
miongoni mwa wapiga kura na
linaweza kusababisha vurugu endapo
matokeo yatakuwa kinyume chake.
Anabainisha kuwa kura ni siri ya
mpigakura mwenyewe.
“Sitarajii kuona watu wakitengeneza
makundi ya kujadili mwenendo wa
uchaguzi kwenye vituo. Hiyo ni sawa
na kampeni siku ya uchaguzi,
hatutaacha ufanyike kwa sababu
utaharibu mchakato wa uchaguzi,”
anasema.
Ukipiga kura nenda nyumbani
Jambo la nne, mwananchi akimaliza
kupiga kura aende nyumbani kusubiri
matokeo kutangazwa. Kuendelea
kukaa kwenye vituo vya kupigia kura
kunasababisha msongamano usio wa
lazima.
Kombwey anasema hakuna haja ya
kukaa kwenye vituo vya kupigia kura
kwa ajili ya kulinda kura kwa sababu
tayari mawakala wa vyama vya siasa
wapo kwa ajili ya kuangalia mwenendo
mzima wa uchaguzi.
“Ile dhana ya kutaka kulinda kura
zisiibiwe ndiyo inayosababisha vurugu
kwenye vituo. Hizo ni hisia tu, hakuna
wa kuiba kura kwa sababu kuna
mawakala wanaowakilisha vyama
vyao,” anasema.
Tume ina jukumu la kutangaza
matokeo
Anasema jukumu la kutangaza
matokeo ya urais ni la Tume ya
uchaguzi. Tume pia imekasimisha
jukumu la kutangaza matokeo ngazi ya
kata kwa msimamizi msaidizi wa kata
na ngazi ya jimbo kwa msimamizi wa
halmashauri.
Kombwey anasema kuna baadhi ya
watu wanatishia kutangaza matokeo
endapo Tume itachelewa kufanya
hivyo. Anasisitiza kuwa kufanya hivyo
ni kinyume cha utaratibu kwa sababu
hakuna mtu mwenye jukumu hilo zaidi
ya Nec.
Anasema Nec imejipanga kutangaza
matokeo ya urais ndani ya siku tatu
kwa sababu watatumia Mfumo wa
Kusimamia Matokeo (RMS) ambao
utawawezesha kupokea, kujumlisha na
kutangaza matokeo.
Licha ya kutakiwa kisheria kutangaza
matokeo hayo ndani ya siku saba, Nec
imebainisha kwamba mfumo huo
utasaidia kuongeza kasi ya ukusanyaji
wa matokeo kutoka sehemu mbalimbli
nchini.
Mabadiliko ya sheria
Jaji Lubuva anasema mabadiliko
makubwa ya sheria ya uchaguzi
yalifanyika mwaka 2010, mwaka huu
sheria hiyo haijafanyiwa marekebisho
isipokuwa kanuni za uchaguzi
zimerekebishwa ili kuleta ufanisi
katika uchaguzi ujao.

‘Mpishi wa filamu za Bongo Movie aliyeweka kapuni’ shahada ya uhandisi Mtunzi na mwongozaji wa filamu maarufu za Bongo Movie, Daniel Leonard Manege ametangaza kuachia


tunzi na mwongozaji wa filamu maarufu
za Bongo Movie, Daniel Leonard Manege.
Dar es Salaam. Mtunzi na mwongozaji
wa filamu maarufu za Bongo Movie,
Daniel Leonard Manege ametangaza
kuachia filamu mpya akilezeza kuwa
atatumia mfumo tofauti wa masoko ili
kuhakikisha filamu hiyo iitwayo “Safari
ya Gwalu” inawafikia wananchi katika
ubora unaotakiwa.
Manege ambaye ameandika filamu
nyingi maarufu zinazosisimua
watazamaji nchini, alisema kuwa
atatumia taaluma na uzoefu alionao
wa miaka minne sokoni kuhakikisha
anaziba mianya yote ya uharibifu
dhidi ya kazi yake.
Mwongozaji huyo aliyehitimu Shahada
ya Uhandisi wa Viwanda na Utawala
kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
(UDSM), alisema ametumia zaidi ya
Sh20 milioni kutayarisha filamu hiyo
mpya ambayo mwigizaji mkuu ni Gabo
Zigamba na kwamba inamzungumzia
kijana aliyekwama kimaisha ambaye
aliamua kurudi shule ya msingi ili
apate elimu.
“Nimeshaandika filamu nyingi
zilizofanya vizuri sokoni na kujitwalia
tuzo nyingi za filamu hasa kwenye
tamasha la Ziff kila mwaka. Lakini
Safari ya Gwalu’ ni filamu yangu ya
kwanza kuiandaa. Niliamua kumtumia
Gabo kwenye filamu hii kwa sababu
alifanya vizuri katika Filamu ya Bado
Natafuta. Hiyo pia niliiandika mimi.
Kwa mujibu wa muswada wa Filamu
ya Safari ya Gwalu, niliona Gabo
anafaa na amefanya ilivyotakiwa.”
alisema Manege.
Alisema mapenzi yake katika tasnia
hiyo yalimfanya afikirie ni namna
atakavyofanya ili kuibadilisha fani
hiyo, akieleza kwamba kwake hakuna
hasara kuacha taaluma aliyosomea na
kuingia katika uwanja wa filamu.
“Filamu yangu ya kwanza kuiandika na
ikaingia sokoni na kupendwa ni; “U Me
and Him”, ilikuwa chini ya Jacob
Steven (JB), iliigizwa pia na JB
mwenyewe, Kajala, Cloud 112,”
alisema.
Alisema akiwa na JB alitunga filamu
nyingi, ikiwemo; Bado Natafuta;
Shkamoo Mzee; Nipende Monalisa; Dj
Benny; Nakwenda kwa Mwanangu na
nyinginezo.
Manage alibainisha kuwa kwa sasa
ameashandika filamu zaidi 10 na zote
zipo sokoni, ambapo alifanya kazi na
waigizaji mbalimbali akiwamo kama
Dk Cheni, Steve Nyerere, Wema
Sepetu, Gabo, Shamsa Ford na
wengineo.
Hata hivyo alisema licha ya kukaa kwa
muda mrefu katika tasnia hiyo,
hajawahi kufikiria kuwa mwigizaji bali
anatamani abadili mfumo wa masoko
katika tasnia hiyo.
“Nilikuwa naota ndoto za kuja kuwa
mkombozi wa tasnia hii, nashukuru
zimeanza kutimia kwa kuandika
filamu zilizokubalika, kujenga mtandao
wa masoko na hata ubora filamu
zenyewe. Nilijua siwezi kuwa
mwigizaji ila kuikuza tasnia.
“Unajua tasnia ya filamu imekuwa
ikikosa waandishi na , hivyo
wasomi tunatakiwa kuunganisha
nguvu katika sekta ya sanaa nchini
kwa kuwa filamu ni sekta pekee
inayoingiza kiasi kikubwa cha fedha
maeneo mengi ulimwenguni pia ni
muhimu sasa tusifikirie kuajiriwa
muda wote,” alisema Manege.

Nafasi ya kazi diamondi motors limited

NAFASI ZA KAZI UNIVERSITY OF BAGAMOYO MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 15 SEPTEMBA 2015

UNIVERSITY OF BAGAMOYO
vacancies
The University of Bagamoyo
wishes to recruit suitably
qualified candidates in the
Faculty of Computing and
Information Systems to fill the
following vacant posts;
1. Assistant Lecturers (5
posts- 3 Part time and 2
Permanent)
Qualifications:
• Master of Science holders in
areas of Network and Security,
Big Data Analytics and
Management Information
Systems
• Working experience of
Minimum of 3 years in related
industry.
• A teaching experience will be
an added advantage
Main Duties and Responsibilities:
(i) Carries out lectures, seminars,
tutorials and practicals for both
undergraduate and postgraduate
programmes;
(ii) Sets, invigilates and mark
examinations;
(iii) Supervises field work of both
undergraduate and postgraduate
students;
(iv) Conducts research and
publishes results;
(v) Carries out consultancy;
(vi) Organizes and participates in
relevant workshops and
conferences;and
(viii) Performs any other
relevant duties assigned by
superiors.
================
2. Lecturer (2 Posts- Part
Time)
Qualifications
• PHD Holders in areas of
Network and Security, Big Data
Analytics and Management
Information Systems.
• Working experience of
Minimum of 5 years in the
teaching profession/ Research
Main Duties and Responsibilities
(i) Carries out lectures, seminars,
tutorials and practicals for both
undergraduate and postgraduate
programmes;
(ii) Sets, invigilates and mark
examinations;
(iii) Supervises field work of both
undergraduate and postgraduate
students;
(iv) Conducts research and
publishes results;
(v) Carries out consultancy;
(vi) Organizes and participates in
relevant workshops and
conferences;
(vii) Guides junior staff in
lecturing and conducting
seminars and tutorials; and
(viii) Performs any other
relevant duties assigned by
superiors.
Remuneration
Competitive remuneration
according to the packages of the
University of Bagamoyo
Mode of Application:
Interested candidates should
send their applications letter
enclosing updated CV and copies
of the relevant certificates to
the:
The Vice Chancellor
University of Bagamoyo
P. O Box 75254
Dar es Salaam
Application Deadline:
Applications closes on 15th
September 2015, Only
shortlisted candidates will be
notified for interview.

NAFASI ZA KAZI MBEYA UNIVERSITY OF SCIENCE AND TECHNOLOGY MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 6 SEPTEMBA 2015

MBEYA UNIVERSITY OF
SCIENCE AND TECHNOLOGY
EMPLOYMENT OPPORTUNITIES
– RE ADVERTISED
Mbeya University of Science and
Technology invites applications
from suitably and competent
persons to fill vacancies that
exist in the Academic
Departments of the University.
1. ASSISTANT LECTURER (60
POSTS)
Qualifications and Personal
Attributes Required
Holders of Masters Degree in
the field of Mathematics/
statistics, Communication skills,
mechanical, Civil, Architecture,
Mining Engineering, Computer
Science/Engineering, Food
Science, Law, Procurement,
Electrical & Electronics,
Telecommunication, Information
and Communication Technology
and Science with Education from
recognized Institution.
Holders of Masters of Education
who has undergraduate degree
majored in Bachelor in Science
fields.
A minimum GPA of 3.8 out of 5
in the First degree with a
minimum score of B+ in the
relevant subject and G.P.A of
4.0 out of 5 at Masters Level is
required.
Excellent English, written and
oral communications skills.
Knowledge in Computer
application packages.
Key Responsibilities
• Teaches both Undergraduate
and Postgraduate students.
• Carries out lectures, conducts
tutorials, seminars and practicals
for undergraduate programmes;
Prepares and present case
studies.
• Conducts and publish/
disseminate research results.
• Recognizes students having
difficulties intervene and provide
help and supports.
• Participates in consultancies
and community services under
supervision.
• Attends workshops,
conferences and symposia.
• Performs any other duties as
assigned by Supervisor.
Salary Scale: PUTS 2
================
2. TUTORIAL ASSISTANT (6
POSTS)
Qualifications and Personal
Attributes Required
Holders of Bachelor Degree with
GPA of 3.8 out of 5 or
equivalents and must have
scored at least B+ in the fields
of Biology, Automotive
Engineering, Computer Science
and Chemical processing
Excellent English, written and
oral communications skills;
Knowledge in Computer
application packages.
Key Responsibilities
Understudies senior members,
including attending lectures and
seminars, tutorials and practical
training; Conducts tutorials,
seminars and practicals;
Assists in research, consultancy
and outreach activities; Performs
any other duties as assigned by
Supervisor.
Salary Scale: PUTS 1
===============
3. INSTRUCTOR II (9 POSTS)
Qualification and Personal
Attributes Required
Holder of Bachelor Degree /
Advanced Diploma or equivalent
qualification in Architecture,
Computer, Civil, Mechanical,
Mathematics, Science with
Education and Communication
Skills.
Excellent English, written and
oral communications skills
Demonstrates the potential of
being good Instructor
Key Responsibilities
• Teaches up to NTA level 6
and may assist teaching in higher
NTA levels; Administers
examinations for NTA 6
Students.
• Conducts examinations and
submits results.
• Conducts and supports
research and consultancy works;
Prepares learning resources;
• Supervises and assists junior
staff and
• Performs any other duties as
assigned by Supervisor
Salary Scale: PTSS 10
===============
4. TECHNICIAN (2 POSTS)
Qualification and Personal
Attributes Required
Holder of Ordinary Diploma (NTA
6) or equivalent qualification in
Mechanical and Mining. Excellent
English, written and oral
communication skills
Knowledge in Computer
application packages.
Key Responsibilities
• Carries out specified tasks
related to laboratory practical,
student projects, research,
consultancy and services under
close supervision.
• Assists in the repair and
maintenance of laboratory/
workshop facilities; Assists
senior staff in relevant fields of
laboratory/workshop operations;
Assists in students projects and
practical research and
consultancy work.
• Performs any other duties as
may be assigned by Supervisor.
Salary Scale: PGSS 6
=================
5 NURSING OFFICER II (2
POSTS)
Qualification and Personal
Attributes Required
Holder of Bachelor Degree in
Nursing or its equivalent from a
recognized institution plus
successful completion of
Internship and is registered with
Tanzania Nurses and Midwives
Council. Possession of Computer
skills is an added advantage.
Excellent English, written and
oral communications skills.
Key Responsibilities
• Provides high quality nursing
care using appropriate nursing
process.
• Assesses patient’s condition,
plan, implement, and document
and evaluate individualized care
using appropriate nursing model
and according to the hospital
nursing policy.
• Ensures all drugs and other
treatments are given to the
patients as prescribed and
observe any adverse condition.
• Maintains a professional
friendly atmosphere and create
a dignified environment.
• Follows hospital policy in
respect of custody and
administration of all drugs, with
special observation to Dangerous
Drugs Act (DDA).
• Maintains personal contact
with patients, their relatives and
visitors to enhance the patient’s
quality of life, dignity and the
good standing of the hospital.
• Ensures the safe care and
custody of patients’ property in
accordance with the hospital
policy.
• Reports any accident/
incident, loss or theft to the
Senior Graduate Nursing Officer
and complete necessary
statements promptly.
• Maintains Health and Safety
at work by ensuring that
infection prevention and control
principles are followed
• Performs any other duties as
assigned by Supervisor
Salary Scale: PMGSS 5
=================
6 CLINICAL OFFICER II (1
POST)
Qualification and Personal
Attributes Required
Holder of Form IV or VI
certificate plus a Diploma in
Clinical Medicine from a
recognized institution Excellent
English, written and oral
communications skills.
Knowledge in Computer
application packages.
Key Responsibilities
• Makes proper diagnosis of
disease, Prescribes treatments,
Treats wounds,
• Gives First Aid to MCH
problems, Gives anesthesia
during operations Attends
general outpatient clinics.
• Protects patients and
employees by adhering to
infection – control policies and
protocols, medication
administration and storage
procedures and controlled
substance regulations.
• Documents patient care
services by writing and keeping
patients records
• Maintains patient confidence
and protects operations by
keeping information confidential.
• Ensures operation of
equipment by completing
preventive maintenance
requirements, following
manufacturer’s instructions,
calling for repairs, maintaining
equipments inventories,
evaluating new equipment and
techniques.
• Performs any other duties as
may be assigned by Supervisor
Salary Scale: PMGSS 2
================
7 HEALTH LABORATORY
TECHNOLOGIST II (2 POSTS)
Qualification and Personal
Attributes Required
Holder of Certificate of
Secondary Education who have
successfully completed three (3)
years Diploma in Health
Laboratory from recognized
Institutions
Possession of Computer skills is
an added advantage
Excellent English, written and
oral communications skills
Key Responsibilities
• Performs various tests in
clinical laboratory.
• Assist to diagnose and
prevent all ailments and perform
all tests with help of automated
laboratory instruments.
• Analyze all test results and
maintain records of all results,
documents same according to
required quality control
procedures and evaluate all data
to ensure accuracy in same.
• Monitor performance of all
instruments, assist to calibrate
all laboratory instruments and
documents all results.
• Maintain records of all repairs
and maintenance work
performed on equipments
Performs any other duties as
assigned by Supervisor.
Salary Scale: PMGSS 2
===============
8 ESTATE OFFICER I (1 POST)
Qualification and Personal
Attributes Required
Holder of Bachelor Degree in
the fields of Electrical and
Electronics from recognized
Institutions.
Excellent English, written and
oral communications skills.
Knowledge in Computer
application packages.
Key Responsibilities
• Supervises maintenance and
cleaning of University properties
and grounds Examines bills of
quantities.
• Follow – up of title deeds and
acquisition of land Prepares
budgets for minor maintenance
works.
• Performs any other duties as
may be assigned by Supervisor
Salary Scale: PGSS 7.2
NB: GENERAL CONDITIONS
i. All applicants must be Citizens
of Tanzania
ii. Applicants must attach an up
– to – date /current Curriculum
Vitae (CV) having reliable contact
postal address, e-mail address
and telephone numbers.
iii. Applicants should apply on
the strength of the information
given in this advertisement.
iv. Applicants who are currently
employed should channel their
applications through their
employers.
v. Applicants must attach their
detailed relevant certified copies
of Academic certificates:
- Postgraduate/Degree/
Advanced Diploma/Diploma/
Certificates.
- Postgraduate/Degree/
Advanced Diploma/Diploma
Transcripts.
- Form IV and Form VI National
Examination Certificates.
- Computer Certificate.
- Professional Certificates from
respective boards (if any).
- One recent passport size
picture and birth certificate.
vi. Form IV and Form VI results
slips are strictly not accepted
vii. Testimonials, Partial
transcripts and results slips will
not be accepted.
viii. Presentation of forged
academic certificates and other
information in the CV will
necessitate legal
action.
ix. Applicants who have/were
retired from the Public Service
for whatever reason should not
apply.
x. Applicants should indicate
three reputable referees with
their reliable contacts.
xi. Certificates from foreign
Universities should be verified
by Tanzania Commission for
Universities (TCU).
xii. Women are highly
encouraged to apply.
xiii. Only short listed candidates
will be informed on the date of
interview
xiv. Application letters should be
written in English.
xv. Dead line for application is
6/09/2015, at 3:30p.m.
xvi. Application letters should be
posted to the following address;
THE VICE CHANCELLOR
MBEYA UNIVERSITY OF SCIENCE
AND TECHNOLOGY
P.O.BOX 131
MBEYA

Ijumaa, 21 Agosti 2015

Fahamu ukweli kuhusu freemason na jinsi ya kujiunga...

Ndugu mpenzi msomaji ..karibu katika makala haya kuhusu freemason .. leo nimebahatika kukutana na aliyewahi kuwa mkuu wa freemason africa mashariki sir andy chande ... shuka na hii



WANACHAMA WA FREEMASONS
DUNIANI: Duniani kote sasa
hivi kuna wanachama milioni
tatu laki tano wa
freemasons na wanachangia
dola za kimarekani zaidi ya
milioni 400 kwa ajili ya
misaada kila mwaka, yani
kwa siku ni zaidi ya dola
milioni moja kusaidia afya,
elimu vilevile wajane wa
wanachama wa freemasons
wanasaidiwa ambapo pia
ukiumwa na ukiwa na shida
yeyote kuna msaada wa bure
unapatiwa nakumbuka hata dr
Charles Matwali alipoumwa
sana, tulimpeleka uingereza
kwa matibabu.

JINSI YA KUJIUNGA NA FREEMASONS:
Ili kujiunga ni lazima uwe
na umri wa miaka 21, ni
hiari kujiunga na pia uwe
unamwamini Mungu haijalishi
ni Mungu gani, watu ambao
hawamuamini Mungu
hawaruhusiwi kuwa
Freemasons, na lazima uwe
mtu mkweli.
Ni lazima familia yako
ikubali pia wewe kujiunga
na freemasons kwa sababu
freemasons hawatokubali
kujiunga kwako kukufanye
uwe masikini kutokana na
kutoa misaada.
Unapotaka kujiunga ni
lazima upeleke maombi yako
kwa mtu unaemfahamu ambae
yuko Freemasons, au kama
hujui mtu unaandika barua
baada ya hapo utapewa
nakala za kusoma na kuelewa
na kamati ya kukuruhusu
kuingia kwenye freemasons
itakupeleleza wewe na
familia yako, na pia
watakutembelea nyumbani
kuongeana mkeo au mumeo au
familia.
Inaweza kuchukua mwaka
mmoja na nusu au mwaka
kuruhusiwa kujiunga na
freemasons baada ya
kupeleka maombi, ambapo
hapo ni kukubaliwa tu,
baada ya hapo ili uwe
freemason kamili kuna vyeo
vitatu ambavyo tunaviita
degrees ambavyo ni lazima
uvikamilishe jambo ambalo
linaweza kuchukua zaidi ya
miaka miwili.
.
BAADA YA KUJIUNGA: Pia
unatakiwa kujifunza vitu
vingi na kuvihifadhi
kichwani kama vile maneno
ya kusema wakati unafanya
ibada za freemasons kwa
sababu tukiwa pamoja
tunavyozungumzia sifa za
kuwa binadamu kamili
unaweza ukafananisha na
ibada ya kanisani.

KUHUSU FREEMASON YA UINGEREZA:
Acha nizungumzie Freemason
ya Uingereza ambayo mimi ni
mmoja wao, Makao makuu yako
London kwenye barabara
inaitwa great queen street,
Mkuu wa Freemasons
Uingereza ni binamu yake
malkia Elizabeth ambae
tunamuita Grandmaster.
Kazi zote zinazofanyika na
Freemasons zinaendeshwa
kutoka kule, kwa mfano mv
bukoba ilivyozama nilipiga
simu kule kuomba msaada
wakatuma pound elfu 10
ingawa na sisi hapa tuna
kitengo chetu cha misaada
ambayo kilichangia, maamuzi
ya misaada mikubwa yanatoka
Uingereza.
Kuna mahoteli ya freemasons
Uingereza, Scotland na
Ireland na katika nchi
zilizokua za kisovieti
zamani, tuna mahoteli
duniani nzima ambapo kama
upo kwenye freemasons ya
Dar es salaam unaweza
kuhudhuria vikao kwenye
yeyote kati ya hizo hoteli
duniani tunazomiliki ambazo
zinatumika pia kama kumbi
za mikutano yetu ili mradi
wawe na uthibitisho kwamba
wewe ni mmoja wetu.
Watu wengi huwa wanasema ni
taasisi inayofanya mambo
yake kwa siri lakini ukweli
ni kwamba siri pekee
iliyopo ni jinsi
nitakavyokutambua kama wewe
ni mmoja wetu, vingine
vyote viko wazi na
vinapatikana hata kwenye
internet na unaweza kwenda
kwenye maduka ya vitabu
kote afrika mashariki hata
uingereza ukapata nakala
zote za freemasons ikiwemo
hata maneno tunayosema
tukifanya ibada zetu.
Kwa afrika Mashariki makao
makuu ya freemasons yako
Nairobi Kenya kwa sababu
aliechukua nafasi yangu
yuko Nairobi na pia makamu
wake yuko Nairobi, Kuna
majumba 50 ya freemasons
Afrika Mashariki Ingawa
makao makuu yako Nairobi,
jumba la Dar es salaam
linajitegemea lenyewe na
tunafanya miradi yetu na
kusajili watu wetu
hapahapa, hatuingiliwi na
ofisi ya Nairobi, maamuzi
yetu yanafanyika hapa hapa.
Hapa ni Freemasons Hall Dar es salaam
ambapo Sir Chande anasema kuna
masonic lodge nne Dar es s

FREEMASONS WANAPOKUTANA : Huwa
tunakutana saa 12 jioni na
kutoa ripoti ya
tulivyovifanya tangu
mkutano wa mwisho, kuhusu
misaada tuliyotoa,
wanachama wanaoumwa, na
nani wa kwenda kumtembelea
au kama kuna mwananchama
mpya wa kumuapisha, kama
hayupo tunajadiliana kuhusu
mambo tofauti yanayotuhusu
isipokua siasa na dini,
tunakula pamoja na kila mtu
anaondoka.

MNAKUTANA MARA NGAPI?
Inategemea kama tawi la
Uingereza tulikua
tunakutana mara mbili kwa
mwaka, la huku ambalo ndiko
nilikoapishwa tulikua
tunakutana mara 11 kwa
mwaka lakini siku hizi ni
mara kumi, wengine
wanakutana mara 5,
inategemea na kazi za
kufanya, mfano labda
wanachama wa kuapisha ni
wengi . Ibada inafanyikaje?
.
Ibada inaanza wakati vikao
vinaanza, inahusisha mara
nyingi kitu ambacho
kinafanana na ibada
kanisani, mara nyingi
inahusika kumuweka
mwananchama mpya kwenye
mstari na mtazamo mmoja na
aliowakuta na kwenye ibada
huwezi kuvaa unavyotaka,
lazima uvar suti na tai
isipokua nchi kama India
ambao hawavai tai.
Ukiwa mwanachama unapewa
maswali ambayo ukiyajibu
vizuri kwa muda wako
unaweza kupandishwa cheo na
inachukua muda kufikia
degree ya tatu, tukiwa
kwenye vikao mwenyekiti
anaitwa Master na anao
wasaidizi wawili, kwenye
ibada mwenyekiti anakaa
mashariki, msaidizi mmoja
ana kaa mbele yake
akimtizama na wa pili
anakua anasaidia kwa
shughuli nzima
inayoendelea.
Kuna mwingine ambae ndio
muongozaji wa sala na
wakati tukisali, Mungu
tunamuita Fundi mkuu
aliyeumba sayari zote hiyo
inahakikisha kwamba uwe
Musilamu au mkristo
tunakwenda sambamba.

ISHARA ZINAZOTUMIKA FREEMASONS
.
.
Kuna alama ya Compass
inayotumika kuonyesha
mwelekeo kwa mishale yake,
kuna ruler na pembe nne
ambavyo ni vitu
vinavyotumika kwenye ujenzi
ila vinaweza kutumika
kufundisha kuhusu maisha,
na ndio vinatumika hivyo
wala sio kuhusu kitu
kingine.
Tukifanya ibada zetu au
kumkubali mtu kuingia
freemasons lazima avae
pajama au mavazi
yanayotumika kulalia usiku,
na haruhusiwi kuwa na pesa
mfukoni, kuvaa saa au cheni
ishara ya kuwa yeye ni
masikini kama alivyozaliwa.
Uchawi, kuabudu shetani na
mambo kama hayo watu
wanayosema kwamba
freemasons ndio
inajihusisha na hivyo vitu
ikiwemo kutoa uhai ndugu,
ni waongo, hawana ujuzi wa
kutosha, nakumbuka pia rais
Moi aliunda kamati maalum
kuchunguza uchawi na
waabudu shetani na tuliitwa
nikaenda kuwaeleza kwa muda
wa karibu saa na nusu
kuhusu freemasons, ingawa
hawakuja kutupa ripoti
kamili waliyopeleka kwa
rais moi, walituambia
kwamba wamekubali maelezo
yetu na ingekua bora kama
tungekua tunaeleza zaidi
watu wajue na tusiwe
wasiri.

FAIDA ZA KUWA FREEMASONS:
Hakuna faida za kupata pesa
kama wengi wanavyoambiwa
kwamba ukiwa freemasons
unapewa mihela, faida za
kuwa freemasons ni pamoja
na kuongeza idadi ya
marafiki na kuongeza
knowledge (ufahamu) Faida
nyingine labda ni kama
ukitoa tenda kama
unaanzisha kiwanda na
umetoa tenda ya kazi,
ukiona mmoja wa freemasons
yuko kwenye list ya
walioomba tenda utampa
kipaumbele kwa sababu
unamfahamu na ni kama
ndugu.
Hakuna utoaji wa kafara
kama inavyosemekana na pia
hakuna uhusiano kati ya
freemasons na agano la
kale.


MAMA MZAZI WA KANUMBA KUHUSU
KANUMBA KUWA FREEMASON:
Mama mzazi wa Marehemu
mwigizaji Steven Kanumba
alisema siku kadhaa baada
ya Kanumba kufariki kuna
kijana alikuja nyumbani na
kumwambia mama kwamba yeye
(kijana) ndio alimsaidia
Kanumba kujiunga na
Freemasons miaka kadhaa
iliyopita hivyo alikwenda
nyumbaniili wazungumze na
mama, mama Kanumba
alimfukuza hapohapo na
kumwambia mwanae hajawahi
kuwa freemason na
akamwambia akirudi tena
atamwitia polisi.
.
MISTARI YA JAY Z KWENYE WIMBO WA
FREEMASON WA RICK ROSS.
Watu wananisingizia mambo
ya kishetani, uvumi unaenea
sehemu zote, nipishe huyu
ni Mungu anafanya mambo
yake, najua mnaniogopa
Sijui wa kumwamini sala ya
maria inafanya kazi.
Mnanisingizia vitu vingi
vya kishetani lakini bado
mnapandisha sauti kubwa
mkisikiliza muziki wangu,
hizo stori zote hazina
msingi, mniache Mungu
anafanya kazi yake.
Mungu ndio injinia hapa,
asiefanya fanya dhambi
atupe jiwe la kwanza
angalieni sura zenu kwenye
vioo mnavyoonekana, Sio
kwamba mimi ni Freemason,
nilipitia tu mambo mengi
sana na Mungu anisamehe
manake nisingefika nilipo
bila kufanya dhambi,
nimeosha sura yangu kwa
maji matakatifu hii rozari
yenye shanga, tena shanga
za diamond ni uthibitisho
kwamba Mungu alinisamehe.
Mi ni mkali, acha kutazama
kwenye sahani yangu… sema
tu unatamani nilichonacho .

RIPOTI YA CNN AUGUST 2010 KUHUSU
FREEMASON:
Baadhi ya maseneta wa
majimbo kadhaa ya Marekani
walikiri kuwa ni wanachama
wa Freemason ambapo
ilifahamika kwamba Marais
12 waliowahi kuiongoza
Marekani walikua wanachama
wa Freemason ambapo pia
watu 9 kati ya waliosaini
hati ya uhuru wa Marekani
walikua freemason akiwemo
George Washington.
Sir Andy Chande akifanya interview na
Gerald Hando wa Clouds Fm.
Kuna idadi kubwa ya watu
waliohitaji kufahamu
Freemason ni nini baada ya
taarifa kuenea kwamba
Freemason ni dini ya
kishetani na watu wengi
maarufu wamo humo wakiwemo
viongozi wa nchi na mastaa
wengine kama Jay Z,
Rihanna, Beyonce, Kanye
West, Celine Dion na hata
hapa Tanzania june 2012
magazeti ya udaku
yaliwataja wasanii kama
Diamond Platnums na
Jackline Wolper kwamba wamo
humo lakini wasanii wenyewe
walikanusha.
Clouds TV/Radio kupitia kwa
mtangazaji Gerald Hando
ilipata nafasi ya kufanya
mahojiano na Sir Andy
Chande ambae aliwahi kuwa
kiongozi mkuu wa Freemason
Afrika Mashariki kwenye
nchi za Tanzania, Uganda,
Kenya na Seychelles.
Yafuatayo hapo chini ni
maelezo aliyoyatoa.
ALIKOANZIA SIR CHANDE: Sir
Chande: Alifika Tanzania
mwaka 1950, alihamia Dar es
salaam 1953 na kukutana na
watu wengi wa bandarini,
shirika la reli na
mashirika mbalimbali
aliyofanyia kazi na
alikutana na watu wengi
ambao walikua wanahudhuria
vikao vya freemasons,
akaanza kuuliziaulizia na
akajifunza mambo kadhaa
kuhusu hao watu.
Kwa wakati huo, hao watu
hawakua huru kuzungumzia
Freemasons kama anavyofanya
chande sasa hivi, haswa
kabla ya vita ya pili ya
dunia.
Sir Chande anasema wakati
huo Freemasons ilikua
imegawanywa kwenye makundi
tofauti, katika
mahospitali, shule, na
mashirika mbalimbali na
kulikua na kundi maalum la
freemasons kwa ajili ya
matajiri na wafanyakazi
wakubwa wa serikali,
ukiangalia vizuri wengi wao
walikua wazungu na baadhi
ya wahindi.
Kundi la kwanza lilikua
linaongozwa na watu wa
Scotland, makundi mawili
yaliyofata yalikua
yanaongozwa na waingereza
na kundi la nne lilikua
linaongozwa na wahindi
ambalo kundi la nne ndilo
Chande alilojiunga nalo
nalo, ilimchukua miaka
miwili kukubaliwa kujiunga
na freemason, aliapishwa
rasmi rasmi mwaka 1954
akiwa na umri wa miaka 28,
kumbuka kwamba masharti ya
kujiunga na freemasons ni
lazima uwe na umri kuanzia
miaka 21.
Baada ya hapo ndipo
alipoanza kupenda
Freemasons ambapo pia
alipanda cheo na kupewa
nafasi ya kuongoza kundi au
tawi la freemasons katika
nchi nne ambazo ni Kenya,
Tanzania, Uganda na sychels
na akajiunga na miradi
tofauti ya freemasons
nchini uingereza yakiwemo
mahoteli ya kifahari pamoja
na kupewa jukumu la kujenga
hoteli mpya ya freemasons
nchini Ghana kwenye mji wa
Khumasi ambayo ni ya
kifahari sana.
Hoteli nyingine ya kifahari
alisimamia ujenzi wake iko
Zambia. Sir Andy Chande kwa
sasa ni mstaafu wa
freemasons, 2005 alistaafu
kuwa kiongozi wa Freemasons
Afrika Mashariki baada ya
kuifanyia kazi kwa miaka
19, kwa sasa haudhurii
mikutano ya hizi nchi za
Afrika Mashariki lakini
anahudhuria mikutano ya
Uingireza kwa sababu bado
anafanya kazi na baadhi ya
mashirika Uingereza .

Kanye west, Jay Z na Rihanna.
FREEMASONS NI NINI? Ni taasisi
ambayo ilianzishwa miaka
350 iliyopita katika njia
ambayo haikua rasmi ikaja
kuhalalishwa miaka 300
iliyopita, hatujui vizuri
ilianzishwa vipi ila
inaaminika walikua wajenzi
wanaojenga mashule,
makanisa, wakati ule
kulikua hakuna miji mikubwa
kama sasa wala mahoteli, na
wao walikua wakiishi pamoja
na familia zao na wakihama
wanahama pamoja,
wakaanzisha miradi ya
kujenga hoteli ndogo ndogo
ili kusaidiana kama wajenzi
na kujikwamua kiuchumi,
wakawa wanafundishana..
yani kama una ujuzi
unamsaidia na mwenzako
kujua.
Anasema “Freemasons sio
dini na tukikuta wewe ni
mkristo tunakushinikiza
ukristo wako, kama wewe ni
mhindu unabaki kuwa mhindu,
lakini freemasons orijino
ilianzishwa na wakristo
nchini Uingereza na baadae
ikahamia Ulaya, Marekani,
Australia na India
Freemasons ikaja kuwa kubwa
sana”
NCHI ZA AFRIKA AMBAZO FREEMASON
NI KUBWA: Kwa nchi za Afrika
Freemasons imekuja kuwa
kubwa kwenye nchi kama za
Nigeria na Ghana pia Sierra
Leone, kwanza aliyewahi
kuwa rais wa nchi hiyo
Daudi Jawala alikua mmoja
wetu. Freemasons ilianza
mwaka 1646 alafu ikaja kuwa
rasmi mwaka 1717 lakini
kabla ya hapo katikati
ilikua inafanywa kimya
kimya.
KAZI ZINAZOFANYWA NA FREEMASON
Kazi zinazofanywa sasa hivi
na Freemasons ni kufundisha
wanachama wake kuhusu
majukumu yao kwa
mwenyemwezi Mungu, kwa nchi
yako, familia, na nchi
unayofanyia kazi hata kama
ni ugenini, na kutoa
misaada.

Rihanna.
WANACHAMA WA FREEMASONS
DUNIANI: Duniani kote sasa
hivi kuna wanachama milioni
tatu laki tano wa
freemasons na wanachangia
dola za kimarekani zaidi ya
milioni 400 kwa ajili ya
misaada kila mwaka, yani
kwa siku ni zaidi ya dola
milioni moja kusaidia afya,
elimu vilevile wajane wa
wanachama wa freemasons
wanasaidiwa ambapo pia
ukiumwa na ukiwa na shida
yeyote kuna msaada wa bure
unapatiwa nakumbuka hata dr
Charles Matwali alipoumwa
sana, tulimpeleka uingereza
kwa matibabu.
JINSI YA KUJIUNGA NA FREEMASONS:
Ili kujiunga ni lazima uwe
na umri wa miaka 21, ni
hiari kujiunga na pia uwe
unamwamini Mungu haijalishi
ni Mungu gani, watu ambao
hawamuamini Mungu
hawaruhusiwi kuwa
Freemasons, na lazima uwe
mtu mkweli.
Ni lazima familia yako
ikubali pia wewe kujiunga
na freemasons kwa sababu
freemasons hawatokubali
kujiunga kwako kukufanye
uwe masikini kutokana na
kutoa misaada.
Unapotaka kujiunga ni
lazima upeleke maombi yako
kwa mtu unaemfahamu ambae
yuko Freemasons, au kama
hujui mtu unaandika barua
baada ya hapo utapewa
nakala za kusoma na kuelewa
na kamati ya kukuruhusu
kuingia kwenye freemasons
itakupeleleza wewe na
familia yako, na pia
watakutembelea nyumbani
kuongeana mkeo au mumeo au
familia.
Inaweza kuchukua mwaka
mmoja na nusu au mwaka
kuruhusiwa kujiunga na
freemasons baada ya
kupeleka maombi, ambapo
hapo ni kukubaliwa tu,
baada ya hapo ili uwe
freemason kamili kuna vyeo
vitatu ambavyo tunaviita
degrees ambavyo ni lazima
uvikamilishe jambo ambalo
linaweza kuchukua zaidi ya
miaka miwili.


BAADA YA KUJIUNGA: Pia
unatakiwa kujifunza vitu
vingi na kuvihifadhi
kichwani kama vile maneno
ya kusema wakati unafanya
ibada za freemasons kwa
sababu tukiwa pamoja
tunavyozungumzia sifa za
kuwa binadamu kamili
unaweza ukafananisha na
ibada ya kanisani.
KUHUSU FREEMASON YA UINGEREZA:
Acha nizungumzie Freemason
ya Uingereza ambayo mimi ni
mmoja wao, Makao makuu yako
London kwenye barabara
inaitwa great queen street,
Mkuu wa Freemasons
Uingereza ni binamu yake
malkia Elizabeth ambae
tunamuita Grandmaster.
Kazi zote zinazofanyika na
Freemasons zinaendeshwa
kutoka kule, kwa mfano mv
bukoba ilivyozama nilipiga
simu kule kuomba msaada
wakatuma pound elfu 10
ingawa na sisi hapa tuna
kitengo chetu cha misaada
ambayo kilichangia, maamuzi
ya misaada mikubwa yanatoka
Uingereza.
Kuna mahoteli ya freemasons
Uingereza, Scotland na
Ireland na katika nchi
zilizokua za kisovieti
zamani, tuna mahoteli
duniani nzima ambapo kama
upo kwenye freemasons ya
Dar es salaam unaweza
kuhudhuria vikao kwenye
yeyote kati ya hizo hoteli
duniani tunazomiliki ambazo
zinatumika pia kama kumbi
za mikutano yetu ili mradi
wawe na uthibitisho kwamba
wewe ni mmoja wetu.
Watu wengi huwa wanasema ni
taasisi inayofanya mambo
yake kwa siri lakini ukweli
ni kwamba siri pekee
iliyopo ni jinsi
nitakavyokutambua kama wewe
ni mmoja wetu, vingine
vyote viko wazi na
vinapatikana hata kwenye
internet na unaweza kwenda
kwenye maduka ya vitabu
kote afrika mashariki hata
uingereza ukapata nakala
zote za freemasons ikiwemo
hata maneno tunayosema
tukifanya ibada zetu.
Kwa afrika Mashariki makao
makuu ya freemasons yako
Nairobi Kenya kwa sababu
aliechukua nafasi yangu
yuko Nairobi na pia makamu
wake yuko Nairobi, Kuna
majumba 50 ya freemasons
Afrika Mashariki Ingawa
makao makuu yako Nairobi,
jumba la Dar es salaam
linajitegemea lenyewe na
tunafanya miradi yetu na
kusajili watu wetu
hapahapa, hatuingiliwi na
ofisi ya Nairobi, maamuzi
yetu yanafanyika hapa hapa.

na blog ya samsasali)
FREEMASONS WANAPOKUTANA : Huwa
tunakutana saa 12 jioni na
kutoa ripoti ya
tulivyovifanya tangu
mkutano wa mwisho, kuhusu
misaada tuliyotoa,
wanachama wanaoumwa, na
nani wa kwenda kumtembelea
au kama kuna mwananchama
mpya wa kumuapisha, kama
hayupo tunajadiliana kuhusu
mambo tofauti yanayotuhusu
isipokua siasa na dini,
tunakula pamoja na kila mtu
anaondoka.
MNAKUTANA MARA NGAPI?
Inategemea kama tawi la
Uingereza tulikua
tunakutana mara mbili kwa
mwaka, la huku ambalo ndiko
nilikoapishwa tulikua
tunakutana mara 11 kwa
mwaka lakini siku hizi ni
mara kumi, wengine
wanakutana mara 5,
inategemea na kazi za
kufanya, mfano labda
wanachama wa kuapisha ni
wengi . Ibada inafanyikaje?


Ibada inaanza wakati vikao
vinaanza, inahusisha mara
nyingi kitu ambacho
kinafanana na ibada
kanisani, mara nyingi
inahusika kumuweka
mwananchama mpya kwenye
mstari na mtazamo mmoja na
aliowakuta na kwenye ibada
huwezi kuvaa unavyotaka,
lazima uvar suti na tai
isipokua nchi kama India
ambao hawavai tai.
Ukiwa mwanachama unapewa
maswali ambayo ukiyajibu
vizuri kwa muda wako
unaweza kupandishwa cheo na
inachukua muda kufikia
degree ya tatu, tukiwa
kwenye vikao mwenyekiti
anaitwa Master na anao
wasaidizi wawili, kwenye
ibada mwenyekiti anakaa
mashariki, msaidizi mmoja
ana kaa mbele yake
akimtizama na wa pili
anakua anasaidia kwa
shughuli nzima
inayoendelea.
Kuna mwingine ambae ndio
muongozaji wa sala na
wakati tukisali, Mungu
tunamuita Fundi mkuu
aliyeumba sayari zote hiyo
inahakikisha kwamba uwe
Musilamu au mkristo
tunakwenda sambamba.
ISHARA ZINAZOTUMIKA FREEMASONS

Kuna alama ya Compass
inayotumika kuonyesha
mwelekeo kwa mishale yake,
kuna ruler na pembe nne
ambavyo ni vitu
vinavyotumika kwenye ujenzi
ila vinaweza kutumika
kufundisha kuhusu maisha,
na ndio vinatumika hivyo
wala sio kuhusu kitu
kingine.
Tukifanya ibada zetu au
kumkubali mtu kuingia
freemasons lazima avae
pajama au mavazi
yanayotumika kulalia usiku,
na haruhusiwi kuwa na pesa
mfukoni, kuvaa saa au cheni
ishara ya kuwa yeye ni
masikini kama alivyozaliwa.
Uchawi, kuabudu shetani na
mambo kama hayo watu
wanayosema kwamba
freemasons ndio
inajihusisha na hivyo vitu
ikiwemo kutoa uhai ndugu,
ni waongo, hawana ujuzi wa
kutosha, nakumbuka pia rais
Moi aliunda kamati maalum
kuchunguza uchawi na
waabudu shetani na tuliitwa
nikaenda kuwaeleza kwa muda
wa karibu saa na nusu
kuhusu freemasons, ingawa
hawakuja kutupa ripoti
kamili waliyopeleka kwa
rais moi, walituambia
kwamba wamekubali maelezo
yetu na ingekua bora kama
tungekua tunaeleza zaidi
watu wajue na tusiwe
wasiri.
FAIDA ZA KUWA FREEMASONS:
Hakuna faida za kupata pesa
kama wengi wanavyoambiwa
kwamba ukiwa freemasons
unapewa mihela, faida za
kuwa freemasons ni pamoja
na kuongeza idadi ya
marafiki na kuongeza
knowledge (ufahamu) Faida
nyingine labda ni kama
ukitoa tenda kama
unaanzisha kiwanda na
umetoa tenda ya kazi,
ukiona mmoja wa freemasons
yuko kwenye list ya
walioomba tenda utampa
kipaumbele kwa sababu
unamfahamu na ni kama
ndugu.
Hakuna utoaji wa kafara
kama inavyosemekana na pia
hakuna uhusiano kati ya
freemasons na agano la
kale.
MAMA MZAZI WA KANUMBA KUHUSU
KANUMBA KUWA FREEMASON:
Mama mzazi wa Marehemu
mwigizaji Steven Kanumba
alisema siku kadhaa baada
ya Kanumba kufariki kuna
kijana alikuja nyumbani na
kumwambia mama kwamba yeye
(kijana) ndio alimsaidia
Kanumba kujiunga na
Freemasons miaka kadhaa
iliyopita hivyo alikwenda
nyumbaniili wazungumze na
mama, mama Kanumba
alimfukuza hapohapo na
kumwambia mwanae hajawahi
kuwa freemason na
akamwambia akirudi tena
atamwitia polisi.


MISTARI YA JAY Z KWENYE WIMBO WA
FREEMASON WA RICK ROSS.
Watu wananisingizia mambo
ya kishetani, uvumi unaenea
sehemu zote, nipishe huyu
ni Mungu anafanya mambo
yake, najua mnaniogopa
Sijui wa kumwamini sala ya
maria inafanya kazi.
Mnanisingizia vitu vingi
vya kishetani lakini bado
mnapandisha sauti kubwa
mkisikiliza muziki wangu,
hizo stori zote hazina
msingi, mniache Mungu
anafanya kazi yake.
Mungu ndio injinia hapa,
asiefanya fanya dhambi
atupe jiwe la kwanza
angalieni sura zenu kwenye
vioo mnavyoonekana, Sio
kwamba mimi ni Freemason,
nilipitia tu mambo mengi
sana na Mungu anisamehe
manake nisingefika nilipo
bila kufanya dhambi,
nimeosha sura yangu kwa
maji matakatifu hii rozari
yenye shanga, tena shanga
za diamond ni uthibitisho
kwamba Mungu alinisamehe.
Mi ni mkali, acha kutazama
kwenye sahani yangu… sema
tu unatamani nilichonacho .
RIPOTI YA CNN AUGUST 2010 KUHUSU
FREEMASON:
Baadhi ya maseneta wa
majimbo kadhaa ya Marekani
walikiri kuwa ni wanachama
wa Freemason ambapo
ilifahamika kwamba Marais
12 waliowahi kuiongoza
Marekani walikua wanachama
wa Freemason ambapo pia
watu 9 kati ya waliosaini
hati ya uhuru wa Marekani
walikua freemason akiwemo
George Washington. IMEANDALIWA NA WASONGA MROMBO DJS