other blog

Alhamisi, 6 Agosti 2015

Wananchi wavamia Shamba la muwekezaji saa nane usiku wapanda migomba.


Mbunge wa Arumeru Mashariki,Joshua Nasari(kulia).(PICHA/LM)Na mwandishi wetuShamba la hekari 3500 linalomilikiwa na mlowezi eneo la Ndatu wilayani Arumeru limekuwa likitumiwa vibaya tofauti na inavyotakiwa,ambapo inasemekana kuwa mlowezihuyo amekuwa akiwakodishia wananchi kwa kulima mboga mboga na kuuza kuni kwa wenyeji.Kutoendelezwa kwa shamba hilo na muwekezajihuyo imechangia hasira kwa wananchi ambao wanandai kuwa eneo hilo nila kwa ambalo walikuwa wanalitumia tangu miaka ya1952 baada ya wanakijiji waeneo hilo kulidai kwa kumtuma marehemu Japhet Kirilo kwenda Umojawa mataifa kudai Ardhi hiyoiliyokuwa inamilikiwa na walowezi wa kikoloni ambapo hadil leo ardhi kubwa haijarudishwa kwa wazawa wa Meru.Historia hii imechangia wananchi kuingia katika shamba hilo la Karamu(Karamu Estate)majira ya saa nane na kuchukua hatua ya kupanda migomba na kuacha ujumbe kwa kutumia mabango.Kwa mujibu wa Mbunge waArumeru Mashariki Joshua Nasari amesema kuwa mgogoro huo sasa umekua ukifukuta na wao paoja na waziri kivuli waliitaka serikalikuingilia kati kutatuamgogoro huu ambao sasa umechukua sura nyingine baada ya baadhi ya wananchi kujichukulia sheria na kuingia ndani ya Shamba hilo na kupanda migomba.Mbali na hilo Nasari alisema kuwa mwanzo Shamba hilo lilikuwa likitumiwa kwa kilimo cha Kahawa lakini sasa limekuwa halitumiki na badala yake limekuwa likitumiwa kwa matumizi mengine tena kwa wananchi kukodishiwa kwa matumizi ya kibinadamu.Aliongeza pia hivi karibuni inadaiwa mlowezi huyo alikata sehemu ya ardhi hiyo na kuiuza kwa uongozi wa chuo cha Tumaini,tawi la Makumira na kwa baadhiya wageni kwa kile kinachodaiwa muda wa umiliki wake wa miaka 99 umekwisha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni