other blog

Alhamisi, 12 Novemba 2015

NAFASI YA KAZI HALMASHAURIYA WILAYA YA NGORONGORO MWISHO WA KUTUMA MAOMBI TAR 20 NOVEMBA 2015

HALMASHAURIYA WILAYA YA
NGORONGORO
NAFASI YA KAZI
Halmashauriya Wilaya ya
Ngorongoro imepokea kibali cha
Ajira Mbadala chenye Kumb.
Na.CB.170/371 /01 /'H’/77 cha
Tarehe 01 Septemba 2015.
Mkurugenzi Mtendaji we
Halmashauri yo Wilaya ya
Ngorongoro anawetangazia
Wananchi wote wenye sifa
kutuma maombi ya kazi kwa
kuzingatia vigezo na maelezo
yaliyo kalika Tangazo hili.
DEREVA DARAJA II (NAFASI 01)
SIFA
• Awe na Elimu ya kidato cha
nne (lV).
• leseni daraja C ya uendeshaji
pamoja na uzoefu kuendesha
magari kwa muda usiopungua
miaka mitatu (3) bila kusababisha
ajali.
• Mwenye cheti cha majaribio yo
Ufundi daraja Ia II.
NGAZI YA MSHAHARA
Kwe kuzingolia viwango vya
mishahara vya Serikali ngazi yo
Mshahara yo TGOS A kwa mwezi.
Majukumu ya Kazi
• Kuendesha magari ya
Halmashouri.
• Kuhakikisha gari na vyamba
vyake vipo katiko hali nzuri wakati
wote na kufanya uchunguzi wa
gari baada ya safari ili kugundua
ubovu unaohitaji matengenezo.
• Kufanya matengenezo madogo
madogo katika gari.
• Kutunza na kuandika daftari To
salari "Logbook" kwa safari zote.
MASHARTI YA JUMLA KWA
WAOMBAJI
• Mwombaji awe Raia wa
Tanzania.
• Mwombaji awe na umri kati ya
miaka 18 hodi 40.
• Barua zoIe ziandikwe kwa
mkono no ziambatane na nyaraka
zifualaza:-
• Maelezo binafsi (CV)
• Nakala za vyeti kidato cha 4 au
6, na cheti cha kuzaliwa.
• Picha ndogo moja (Passport
size) ya hivi karibuni.
• Transcript, "Testimonial",
Provisional Result au statement of
Result havitakubaliwa.
JINSI YA KUTUMA MAOMBI
Barua zote ziwe na anuani ya
mwombaji na namba ya simu
(kama ipo na zitumwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji,
HaImaShauri ya WiIaya ya
Ngorongoro,
S.LP. 1,
LOLIONDO
Tareheyo Mwisho yo kupokea
maombi ni tarehe 20/11/2015 saa
tisa na nusu (9:30) alasiri.
John K. Mgalula
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
NGORONGORO

Jumamosi, 7 Novemba 2015

Walimu Manyara



Mwenyekiti wa Chama cha Walimu nchini
(CWT) mkoani Manyara, Qambos Sulle.
Mirerani. Walimu mkoani Manyara
wametakiwa kujipanga ili wapate
huduma za fedha kwenye Benki ya
Walimu ambayo imepata leseni.
Benki hiyo inatarajiwa kuanza
kuwahudumia walimu na wananchi
wakati wowote kuanzia sasa.
Mwenyekiti wa Chama cha Walimu
nchini (CWT) mkoani Manyara,
Qambos Sulle aliyasema hayo wakati
akizungumza kwenye siku ya mwalimu
ambayo ilifanyika katika Mji Mdogo wa
Mirerani wilayani Simanjiro juzi.
Qambos alisema walimu ni wengi na
mishahara yao inapopitia kwenye
benki nyingine huwatengeneza faida
wamiliki wa benki hizo, hivyo
wanapaswa kutumia benki yao ili
iwanufaishe.
“Benki yetu pindi ikishaanza shughuli
zake tutazungumza na Serikali ili tuwe
tunapitisha mishahara ya walimu,
kwani watumishi tutakaowaajiri
tutawalipa kupitia makato ya benki,”
alisema.
Alisema huu ni wakati sahihi kwa
walimu kufaidi matunda ya jasho lao
kwa kuwa kupitia benki hiyo
watajiongezea kipato na kufanya
shughuli nyingine za maendeleo.
Akizungumza katika siku hiyo ya
mwalimu, Katibu wa CWT wilayani
Simanjiro, Abraham Kisimbi alisema
walimu wanapaswa kushughulikiwa
mahitaji yao ili waweze kutekeleza
majukumu ipasavyo.
Katibu wa CWT mkoani Manyara, Nuru
Shenkalwa alisema kwa sasa walimu
wengi ni vijana ambao wanajua haki
zao na wanasoma hadi mitandao,
tofauti na walimu walioanza kazi
miaka ya 1980 wanaotarajia kustaafu.
“Walimu wengi wa zamani walikuwa
wanategemea kusoma magazeti mawili
yaliyokuwapo, lakini hivi sasa kuna
hadi mitandao, hivyo walimu vijana
wanatambua namna ya kudai haki zao
za msingi,” alisema Shenkalwa.

Magufuli afuta safari


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dk John Pombe Magufuli
Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dk John
Pombe Magufuli amefuta safari zote za
nje ya nchi kuanzia leo hadi hapo
maamuzi mengine yatakapotolewa.
Dk Magufuli ameagiza shughuli zote
zinazotakiwa kufanywa nje ya nchi
zifanywe na kusimamiwa na
mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania
nchi za nje.
Uamuzi huo wa rais ameutoa Ikulu
jijini Dar es Salaam katika kikao
kilichojumuisha watendaji
mbalimbali wa serikali wakiwemo
Makatibu wakuu, Manaibu Makatibu
wakuu, Gavana wa Benki Kuu na
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA).
Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu kwa
vyombo vya habari ruhusa ya safari
nje ya nchi inaweza kutolewa kwa
jambo la dharura ambalo hata hivyo
jambo hilo lazima lipate kibali cha
Katibu Mkuu Kiongozi.
“Badala yake rais ametaka ziara nyingi
zielekezwe kwenda vijijini ili
kuwawezesha watendaji kujua na
kutatua kero za wananchi” imesema
taarifa hiyo.
Katika kikao hicho, rais ameelekeza pia
mambo kadhaa ambayo watendaji hao
wanapaswa kuyasimamia, kuyawekea
mikakati na kuyapanga vizuri ili
yasimamiwe mara moja na Baraza la
Mawaziri atakaloliteua.
Mambo hayo ni pamoja na kuanza kwa
mikakati ya kuhakikisha wanafunzi
wote wanaanza kupatiwa elimu ya
bure kuanzia Januari mwakani.
Taarifa hiyo imetaja jambo la pili kuwa
ni suala la uratibu wa mikopo ya
wanafunzi wa elimu ya juu ambapo
ameagiza lifanyiwe kazi na mipango
yake ikamilike kwa ajili ya utekelezaji
mzuri zaidi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, rais
amemuagiza Kamishna wa TRA
kusimamia kwa makini zoezi la
ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha
kero ndogo ndogo zinazowakabili
wananchi zinaanza kushughulikiwa
mara moja.
Ameitaka TRA kukusanya mapato toka
kwa wafanya biashara wakubwa na
wakwepa kodi bila kuogopa mtu wala
taasisi yoyote na kusisitiza kuwa
hakuna mwenye mamlaka ya
kubatilisha maamuzi hayo zaidi yake.
Dk Magufuli ametaka usimamizi
mzuri katika suala la manunuzi ya
umma ambalo amesema limekuwa
likitumika vibaya na kuwa mwanya
wa maofisa wasio waaminifu kuiibia
serikali kwa kuongeza bei za bidhaa
na huduma tofauti na bei halisi ya
manunuzi.

Prof Jay: Vijana ndiyo

Mbunge mteule wa Jimbo la Mikumi,
Joseph Haule, maarufu Profesa Jay
Mbunge mteule wa Jimbo la Mikumi,
Joseph Haule, maarufu Profesa Jay
amesema vijana ndiyo watakaoleta
mabadiliko nchini.
Akizungumza mwanzoni mwa wiki hii,
Profesa Jay, ambaye ni mbunge mteule
wa Jimbo la Mikumi kwa tiketi ya
Chadema, alisema vijana wanatakiwa
kujituma ili kuwa chachu ya
mabadiliko katika taifa lao.
Alisema jambo hilo wanatakiwa
kulifanya sasa bila kujali itikadi za
vyama vyao.
Profesa Jay, ambaye alipata umaarufu
kutokana na kibao chake cha kisiasa
cha “Ndio Mzee”, alisema kukaa
vijiweni na kulalamika hakuwezi kuwa
suluhu ya matatizo yao, hivyo
wakijituma kufanya kazi kwa pamoja
watawezesha Taifa kusonga mbele.
Profesa Jay alisema kuwa na malengo
ni njia mojawapo itakayomwezesha
kijana kujitambua na kujituma katika
kile anachokifanya, ili kutimiza
malengo aliyojiwekea kwa kipindi
mwafaka.
“Ukiangalia vijana maeneo ya vijijini
wanakuwa na malengo ya kuhakikishe
wanafanya mambo kadhaa kama
‘kujenga nyumba yangu ya kuishi
ndipo nioe mke’. Hii ni tofauti na
vijana wengi wa mijini. Naamini hata
wao wakiweka malengo Taifa litasogea
mbele kutoka hapa tulipo,” alisema
Profesa Jay.
Alieleza kuwa kijana yeyote anayeona
ana uwezo wa kufanya mabadiliko
anatakiwa kufahamu kuwa siasa
imeisha na huu ni wakati wa kufanya
kazi.
Alisema kwa sasa mabadiliko ni lazima
ili kuyavuta maendeleo kwani ndiyo
kitu cha msingi zaidi, akibainisha
kwamba ni kwa vijana wote nchini na
si Mikumi pekee.
“Mimi ni kijana nimefikiria kufanya
kazi itakayowakwamua vijana wote
nchini, nathamini uamuzi na namna
walivyoniamini wananchi wa Mikumi
kwa kunipa nafasi niwaongoze, lakini
natambua uwapo wa vijana Tanzania
nzima,” alisema Profesa Jay.
Alisema anachoweza kufanya sasa ni
kuwasaidia wasanii wenzake
kuwasemea na kutafuta njia za
kuwakomboa.
Hata hivyo alisema licha ya kuingia
katika siasa hana mpango wa
kuachana na muziki.
“Wapo wachungaji ambao waliingia
katika siasa hawakuacha kuhubiri,
wapo wafanyabiashara ambao nao
waliingia huko hata nao hawakuacha
biashara zao, kwa upande wangu
siwezi kuacha nitaendelea kufanya
muziki mpaka mwisho wa maisha
yangu,” alisema Profesa Jay.

Ikulu kutamu kwa

Kuna sura inayokinzana katika eneo la
Afrika Mashariki na lile la Kati. Kuna
wakati wanasiasa wanabisha kwenye
eneo hilo. Pia, bado kuna mwangwi
unaosukuma juu ya kile kinachoitwa
‘mabadiliko ya nyakati’.
Wote wanaozunguka eneo hilo
wanavuta subira kujua hatma yake.
Hata hivyo, kwa Rais Paul Kagame wa
Rwanda ni kama vile tayari
amechochea gia. Anajiandaa kukoleza
moto gari lake ili asonge mbele zaidi.
Inawezekana wakati huu anawatupia
macho wenzake. Anaendelea
kuwakodolea tena anawasimanga
moyoni. Lakini bila shaka anaamini iko
siku watafaulu na hatimaye kufuata
mkondo wa kisiasa zake.
Wenzake wanaendelea kupingana
kuanzia kwenye vikao vya Bunge hadi
majukwaa ya wazi ya kisiasa.
Pia, wanaendelea kutumia mifumo
‘dhaifu’ ya kisheria kuendelea
kupenyeza ushawishi wao. Wana kiu
kubwa tena wanaendelea kuwajaza
hamasa wananchi ili waendelea
kusalia madarakani.
Mengi yanaendelea kujitokeza barani
Afrika. Mathalani, Rais Joseph Kabila
wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
(DRC), bado haamini kama atafaulu.
Jaribio lake la awali kulishawishi
Bunge kubadilisha Katiba ili awanie
muhula mwingine wa tatu wa uongozi
lilizua mzozo mkubwa na hata
kusababisha ‘vurumai na kujitokeza
harufu ya kutoweka kwa amani’.
Jaribio hilo sasa ameliweka kando
huku akiendelea kupima kina cha maji
kwa kijiti.
Wale wanaomjua wanasema kuwa Rais
Kabila anachanga upya karata zake.
Wanasema huenda akaibuka
‘kivingine’.
Wanasisitiza kuwa Rais Kabila bado
hajakata tamaa tena anasukumwa na
kile kilichojitokeza kwa Rais Kagame.
Rais Kagame ameidhinishwa na Bunge
kuendelea kuwania madaraka kwa
muhula mwingine wa miaka saba.
Pia, kuna wale wanaamini kuwa, Rais
Kabika inawezekana yupo kwenye
tafakuli kubwa.
Wanaamini kuwa huenda kiongozi
huyo akabadilisha mchezo na
kuwashinda wapinzani wake kwa
kutumia ‘mkakati mgumu’ uliotumiwa
na Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi.
Licha ya kuwa mazingira ya kisiasa
kwa nchi hizo mbili yanabeba sura
mbili zinazotofautiana lakini siasa
hupenda kuazima matukio. Siasa ni
harakati ya kuhodhi madaraka. Daima
siasa ni mchezo wa kuwinda dola.
Inavyoonekana Rais Kabila shauku
yake kubwa ni kufuata mkondo wa
jirani yake Rais Kagame.
Rais Kagame amefunguliwa mlango
kuendelea kusalia madarakani. Bunge
limeidhinisha marekebisho ya Katiba
na hivyo kumpa fungua wa kuendelea
kukalia kiti cha ‘enzi’ kwa utawala wa
Rwanda.
Wenyewe Rwanda wanamsifu
wakisema ni kiongozi aliyebeba
‘mkono wa chuma’.
Rais Pierre Nkurunziza amejitwalia
funguo. Amewapiga chenga wapinzani
wake na kuendelea kushikilia ufunguo
wa kusalia madarakani. Licha ya
kuandamwa na shinikizo kutoka
nyumbani hadi katika duru za
kimataifa, Rais Nkurunziza hakusita
kuendelea na mkakati wake. Aliusuka
mpango na kisha kuutekeleza na sasa
anaushikilia.
Analaumiwa na kushutumiwa na
wengi. Anakosolewa tena anabanwa na
wakubwa wa magharibi.
Hata hivyo, amepuuza hayo yote na
kuendelea na kile kinachotajwa na
wengi ‘ umwamba wa baadhi ya
viongozi wa Afrika kusalia madarakani
kwa kupindisha katiba zao’.
Tayari ameanza kuonja kile wengi
wanakiita joto la jiwe. Mkoloni wake
wa zamani, Ubelgiji ilikuwa nchi ya
kwanza kuuadhibu utawala wake.
Ubelgiji imesitisha baadhi ya misaada
ya maendeleo huku ukionya kuchukua
hatua zaidi katika siku za karibuni
iwapo ukandamizaji kwa makundi ya
wapinzani utaendelea.
Marekani imefuata mkondo. Rais
Barack Obama ametangaza kuing’oa
Burundi kutoka kwenye mikataba yake
ya kibiashara ya AGOA
inayoyawezesha mataifa ya Afrika
kuingiza bidhaa zao katika soko la nchi
hiyo bila ya kulipa kodi.
Mpango huo uliasisiwa wakati wa
utawala wa Rais Bill Clinton
anayetajwa ndiye aliyefufua upya
uhusiano wa karibu baina ya mataifa
ya Afrika na Marekani.
Rais Obama ambaye katika siku za hivi
karibuni amekuwa mstari wa mbele
kuwakosoa viongozi wa Afrika
wanaong’ang’ania kubakia
madarakani, alisema amechukua
hatua hiyo baada ya kushuhudia
kushuka kwa viwango vya demokrasia
katika taifa hilo.
Jinamizi la utamu wa madarakani bado
linaendelea kuzunguka. Rais Kagame
amefaulu kunyosha mstari tena kwa
wananchi wake.
Hata hivyo, wapinzani wake
wanalalamika kwa kile wanadai
kuandamwa na vitisho na wakati
mwingine kuwa hatarini kuuawa.
Ingawa amefaulu kushika ufunguo wa
kuendelea kusalia Ikulu kwa mkono
wa umma, lakini kivuli cha mwisho
wake bado kinatawaliwa na chenga.
Wengi wanaona kuwa, Rais Kagame
‘amejitengenezea’ maadui wengi
kuliko ilivyotarajiwa.
Hali kama hiyo inaanza kulinyemelea
taifa la Congo Brazzaville ambako Rais
Denis Sassou Nguesso ambaye wakati
fulani alipewa sifa kubwa kutokana
mchango wake wa kusaidia kutatua
migogoro ya Afrika. Inaelezwa kuwa
kwa sasa kiongozi huyo anageuka
kinyonga.
Ameanzisha mkakati wa kubadilisha
Katiba ya nchi hiyo ili awanie urais
katika muhula mwingine wa tatu.
Hata hivyo anakabiliwa na upinzani
mkali, lakini mwenyewe anasisitiza
kuwa lazima ajenda yake ipate
uungwaji mkono.
Japokuwa kila mwanasiasa huja na
mwonekano wake, lakini kwa walio
wengi wanahisi kuwa viongozi hao
wanajaribu kucheza kwenye utelezi
mkali huku wakiwa wamevalia suruali
yenye msumari pembeni.

Jumatatu, 19 Oktoba 2015

MWADADA NOREEN KAHAYA...EAGLEFM


Msanii wa muziki wa Reggae, Jhikolabwino
Manyika 'Jhikoman' akipiga gitaa mbele ya
waandishi wa habari muda mfupi baada ya
mkutano ulioongelea tamasha la 'Karibu
Music Festival 2015'. Kulia ni Meneja
Uvumbuzi wa Serengeti Breweries
Limited, Attu Mynah. Picha na Said Hamis
Dar. Wadau wa muziki nchini, Afrika
Mashariki na dunia nzima kwa ujumla
watapata fursa kujumuika pamoja na
kubadilishana uzoefu wa kazi zao
katika tamasha la pili la muziki
maarufu kama ‘Karibu Music Festival’
litakalofanyika mapema mwezi ujao
huko Bagamoyo.
Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya
‘Fahari ya Tanzania’ linalennga kukuza
muziki wa Kiafrika na kuonesha
tamaduni za Kiafrika kwa dunia nzima
kupitia jukwaa la muziki
litakalokutanisha wanamuziki kutoka
sehemu mbalimbali duniani.
Akizungumza na waandishi wa habarI
leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari
Maelezo mwakilishi wa Karibu Music
Festival, Ernest Biseko alisema
Tamasha hilo mwaka huu
litahudhuriwa na wanamuziki
wakubwa akiwemo mkongwe Papa
Wemba, Sarabi Band, H-Art The Band,
Yuzzo & Frontline Band.
Biseko alisema kuwa, wasanii toka
Tanzania ni pamoja na Jhiko Manyika
(Jhikoman) na band yake ya
Afrikabisa, Tomgwa Ensembe, mshindi
wa shindano la vipaji la BSS mwaka
2008, Misoji Nkwambi, Ze Spirit, Isha
Mashauzi, Damian Soul na bandi yake,
Juma Nature, Msafiri Zawose na band
yake.
“Pamoja na kwamba lengo kubwa ni
kukuza muziki wa Kiafrika na
tamaduni zake pia tunataka liwe
tamasha pekee Afrika Mashariki
kukuza uchumi na kuleta maendeleo
kwa watu wake ndio maana biashara
na maenesho ya bidhaa mbali mbali ni
sehemu ya tamasha hili,” alisema
Biseko.
Naye mwakilishi wa wanamuziki
watakaoshiriki katika tamasha hilo,
Jhikolabwino Manyika maarufu kama
Jhikoman ambaye pia ni msanii
maarufu wa miondoko ya Reggae
nchini alisema mashabiki wa muziki
watarajie kuona wasanii wote
wakitumbuzia bila kutumia CD
‘playback’.
Jhikoman alisema kuwa kupitia
tamasha hilo anatarajia kupata nafasi
ya kujifunza kutoka kwa bendi
nyingine jinsi ya kukuza kazi zao na
kudumisha urafiki utakaoleta manufaa
katika kazi yake.
Tamasha hilo litaanza kwa matembezi
kuashiria uzinduzi wake na pia
kutakuwa na mafunzo mbali mbali
yenye mlengo wa kuwasaidia wadau
wa muziki kufahamu mambo mbali
mbali kwenye maswala ya kiutawala
na jinsi ya kujitangaza, mambo ya hati
miliki, ngoma za asili, kupiga ngoma,
na mengineyo.
Kiingilio katika tamasha hilo ni
Sh2,500 kwa watoto, watu wazima
watakaonunua tiketi zao kabla ya
tamasha itakua ni Sh 5,000 na kwa
wale watakaonunua getini itakua Sh
7,000 na kwa watu maalumu (VIP)
tiketi zitauzwa kwa Sh 30,000.

MABERE GODLUCK SPORT EAGLFM..... Messi ajipa matumaini


Mshambuliaji wa Azam, Ramadhan
Singano ‘Messi’
Dar es Salaam. Mshambuliaji wa
Azam, Ramadhan Singano ‘Messi’
amesema kuwa hakatishwi tamaa na
kitendo cha kutopata nafasi kwenye
kikosi cha kwanza cha timu hiyo na
ana uhakika atapata nafasi hiyo ndani
ya kipindi kifupi kijacho.
Singano aliyejiunga na Azam msimu
huu akitokea Simba, amekuwa hana
nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha
timu hiyo kutokana na ushindani
mkubwa uliopo kwa washambuliaji
mbalimbali waliosajiliwa na klabu
hiyo.
Miongoni mwa washambuliaji
wanaowania namba naye ni, Kipre
Tchetche, John Bocco, Farid Mussa,
Didier Kavumbagu na Allan Wanga
walioifanya Azam iwe moja ya timu
zenye safu kali ya ushambuliaji
kwenye ligi.
Singano aliliambia gazeti hili jana
kuwa si jambo la kushangaza kwa
mchezaji kutopata nafasi ya kuanza
kwenye kikosi cha kwanza kwani ni
jambo inategemeana na matakwa ya
kocha.
“Mwenyezi Mungu ndiye kila kitu
katika maisha na yeye ndiyo
kampangia kila mwanadamu riziki.
“Nafurahia maisha hapa na ingawa
bado sijapata nafasi ya kucheza
kwenye kikosi cha kwanza mara.
Naendelea kufanya mazoezi na
naamini Mungu atanisaidia kupata
nafasi muda siyo mrefu,” alisema
Singano.

GODLUCK MABERE EAGLEFM ON SPORT...


Mshambuliaji wa Mbeya City, Haruna
Moshi ‘Boban’
Mbeya. Wakati Simba ikiibuka na
ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya
City, imebainika kuwa Wekundu hao
wa Msimbazi waliingia uwanjani
wakiwaza namna ya kumkaba kiungo
wao wa zamani Haruna Moshi ‘Boban’.
Simba waliingia mchezo wakiwaza
Boban angeingia na jipya gani,
baadaye waligundua kiungo huyo
hawatishi kwani ameongeza uzito kiasi
cha kushindwa kuendana na kasi ya
mechi huo uliochezwa Uwanja wa
Sokoine.
Hiyo ilikuwa mechi yake ya kwanza
kwa Boban ya Ligi Kuu Bara msimu
huu baada ya kuchelewa kujiunga na
kikosi hicho na alifanya mazoezi siku
moja kabla ya mechi hiyo na kocha wa
City, Meja Mstaafu Abdul Mingange
kuamua kumtumia.
Wachezaji waliowahi kucheza naye
Boban akiwa Simba, akiwamo kocha
msaidizi, Seleman Matola na nahodha
wa timu hiyo, Musa Hassan ‘Mgosi’
walimwelezea Boban kuwa ni mchezaji
mzuri, ila kwa sasa anahitaji kuongeza
juhudi katika mazoezi kwani
anaonekana kuwa mzito kutokana na
mwili wake kuongezeka uzito.
“Boban nimemwona, ni mchezaji
mzuri, kikubwa anachopaswa
kukifanya kwasasa ni kuongeza
mazoezi, maana amekuwa na mwili
mnene, ila kiuwezo bado anaonekana
yupo fiti na anaweza kukubadilishia
matokeo muda wowote,” alisema
Matola.
Naye Mgosi alisema, “namfahamu
Boban, si mchezaji wa kubezwa
unapocheza naye, anaweza kukuliza
muda wowote, ila kwa sasa bado
hajapata mchezaji ndani ya Mbeya
City ambaye anaweza kumwelewa kwa
haraka uchezaji wa Boban ama nini
anataka anapokuwa uwanjani.
“Boban siyo mchezaji wa
kukimbiakimbia, jinsi anavyocheza
ndivyo hivyo hivyo, anavyoweza
kukufunga bila kutarajia, ila
namshauri aongeze mazoezi apunguze
mwili na atawasaidia Mbeya City kama
watamtumia vizuri,” alisema Mgosi.
Kocha mkuu wa Simba, Dylan Kerr
naye alisema kuwa amepata taarifa za
Boban kuwa ni mchezaji hatari na
anapaswa kuchungwa katika mechi
hiyo japokuwa hajawahi kumuona
akicheza.
“Tunashukuru tumeshinda mechi hii
na kupata pointi tatu, Mbeya City siyo
timu mbaya na wamecheza kwa
kiwango cha juu, ila hawajapata bahati
ya kutufunga.”

GUDLACK MABERE ON SPORT. EAGLEFM... Ubonge ‘nyanya’ wamtesa Boban Wakati Simba ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City, imebainika kuwa Wekundu hao wa

POSTED BY MABERE GODLUCK EAGLEFM... KATIKA SPORT


Mshambuliaji wa Barcelona, Neymar da
Silva Santos Junior (wa pili kushoto)
akiwania mpira na beki wa Rayo Vallecano
Nacho (kushoto) na kiungo Diego Llorente
wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Hispania
uliozikutanisha timu hizo kwenye Uwanja
wa Camp Nou, Barcelona. Barca ilishinda
5-2. Picha na AFP
Madrid, Hispania. Real Madrid na
Barcelona zimeng’ang’ania kileleni
mwa La Liga wakati Cristiano Ronaldo
akiweka rekodi Real ikishinda 3-0 dhidi
ya Levante, huku Neymar akifunga bao
manne wakati Barca ikichapa Rayo
Vallecano 5-2.
Real imeutumia vizuri uwanja wake
Bernabeu, wakati Ronaldo akivunja
rekodi ya Raul akifunga mabao 324
katika misimu yake saba aliyocheza
kwa miamba hiyo ya Hispania.
Barca ilitumia vizuri wenyeji wake,
huku safu yao ya ulinzi ikionyesha
kupwaya na kuhitaji uwezo wa binafsi
wa Neymar kusawazisha kutoka
nyuma kabla ya kuifunga Rayo
iliyocheza soka zuri la kushambulia
kwenye Uwanja Nou Camp.
Miamba hiyo ya Hispania
inayosumbuliwa na majeruhi sasa
zinaongoza ligi zikiwa na pointi18
katika michezo nane, huku Real
ikiongoza kwa tofauti ya mabao.
Villarreal iliyokuwa ikishikiria usukani
kwa muda, imeporomoka hadi nafasi
ya tatu, kabla ya mechi yake ya jana
dhidi ya Celta Vigo, wakati Atletico
Madrid inayoshika nafasi ya tano
itacheza na Real Sociedad.
Marcelo alifunga bao la kwanza la Real
katika dakika 27, wakati alipobadilisha
pasi na Ronaldo na kupiga shuti
lililompata kipa Ruben wa Levante.
Ronaldo alifunga bao la pili dakika tatu
baadaye kwa shuti la mbali lililojaa
wavuni , na kumaliza ukame wake wa
kutokufunga katika michezo minne
iliyopita ya ligi.
Naye Jese akiingia akitokea benchi
aliifunga bao la tatu dakika nane kabla
ya filimbi ya mwisho na kuhakikishi
ushindi 3-0, wakati Real ikijiandaa na
mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa
Kundi A dhidi ya Paris St Germain.
Barca yatakata
Barca ilimkosa nyota wake Lionel
Messi na nahodha wake Andres
Iniesta, wakati Javi Guerra alipofunga
bao la kuongoza kwa Rayo katika
dakika15.
Ivan Rakitic na Luis Suarez awali
alishindwa kumfunga Tono wakati
alipokutana uso kwa uso na kipa huyo
wa Rayo, lakini Barcelona ilisawazisha
dakika 22, kupitia Neymar kwa
mkwaju wa penalti.
Mbrazil huyo amechukua jukumu la
kuibeba timu hiyo baada ya
kukosekana kwa Messi, alidondoshwa
tena kwenye eneo la hatari dakika 13
na kufunga penalti yake ya pili.
Neymar alifunga bao la tatu dakika 69
na kupachika la nne dakika 70 kufanya
matokeo kuwa 4-1, magoli hayo
yanamfanya Neymar kuwa mchezaji
mwingine wa Barca mbali ya Messi
kufunga idadi hiyo ya magoli tangu
Samuel Eto’o alivyofanya hivyo 2008.
Neymar alitegeneza bao la tano kwa
kupiga krosi nzuri iliyomaliziwa na
Suarez na kuhitimisha kalamu hiyo ya
mabao 5-2.
Jozabed alitumia vizuri kutumia
udhaifu wa mabeki wa Barca kufunga
bao la pili kwa Rayo katika dakika ya
86.
“Neymar amekuwa katika kiwango
kizuri tangu kuanza kwa msimu huu,”
alisema Luis Enrique. “Wakati
anapoingia katika eneo la hatari
hakuna wa kumzuia.”
Sevilla inayojiandaa kucheza na
Manchester City katika Ligi ya
Mabingwa Jumatano, imelazimishwa
sare 1-1 na Eibar, wakati Valencia
ikipata ushindi mnono wa mabao 3-0
dhidi ya Malaga.

POSTED BY PINDA ..EAGLEFM

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
Dar es Salaam. Waziri Mkuu Mizengo
Pinda, jana alitumia Ibada ya Shukrani
iliyofanyika katika Parokia ya
Hananasifu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar
es Salaam, kumshukuru Mungu kwa
kumwezesha kulitumikia Taifa kwa
zaidi ya miaka 15 na kuwaomba
Watanzania wamsamehe kwa
matamshi aliyoyatoa akiwa kiongozi,
huenda yaliwakwaza baadhi yao.
Pinda ambaye amekuwa Waziri Mkuu
kwa miaka minane na miezi tisa,
Waziri kwa miaka miwili na nusu na
Naibu Waziri kwa miaka mitano,
alisema anasikia fahari kumaliza
uongozi wake kwa furaha na amani.
Moja ya kauli tata zilizowahi kutolewa
na kiongozi huyo iliyozua sintofahamu
ni ile ya Juni 29, 2013 katika ukumbi
wa Bunge mjini Dodoma alipoviagiza
vyombo vya dola kuwashughulikia kwa
kuwapiga wale watakaokataa kutii
amri wakati wakifanya vitendo vya
uvunjifu wa amani.
Kauli nyingine tata ni ile ya mwaka
2009 baada ya kuwaeleza wanaoua
watu wenye ulemavu wa ngozi
(albino) pamoja na vikongwe hawana
budi kuuawa kwa kuwa wakisubiri
mahakama kuwahukumu, watakuwa
wanakosea.
“Katika ibada hii ya shukrani,
nimemuomba Mungu anisamehe kwa
matamshi niliyoyatoa nikiwa kiongozi
yanaweza kuwa yaliwaudhi watu bila
mimi kujua.
“Uwaziri Mkuu ni kazi ngumu yenye
changamoto nyingi. Nitakuwa mtu wa
ajabu nisipomshukuru Mungu kwa
uongozi wake katika kipindi chote
hicho tangu nikiwa naibu waziri hadi
kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu,”
alisema.
Pinda alisema katika utumishi wake
kwa umma amejifunza mambo mengi
lakini kikubwa zaidi ni kujua jinsi ya
kuishi na watu.
Katika hatua nyingine, Abate Thadei
Mhagama wa Abasia ya Hanga,
aliwataka waumini nchini wazidishe
maombi kwa kufunga na kuomba kwa
siku sita zilizobaki kabla ya kufanyika
kwa Uchaguzi Mkuu.
“Ninawaomba waumini wote tuzidishe
sala ili nchi iendelee kuwa na amani
na upendo, tumwombe Mungu pia
atuwezeshe kupata viongozi
aliowandaa kwa yeye kwa maana ya
rais, wabunge na madiwani,” alisema
Mhagama.
Alisema uchaguzi wa mwaka huu ni wa
aina yake kwani demokrasia imekuwa
miongoni mwa Watanzania.
“Sote ni mashahidi, tumeona kwenye
mikutano kila mgombea akija sote
tunajaa huko. Hii ni kwa sababu
hatujui yupi ni yupi, ndiyo maana
nasisitiza kuwa tumuombe Mungu
atuletee yule ambaye amemuandaa
yeye,” alisisitiza.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya
Baraza la Walei katika parokia hiyo,
Arbogasti Warioba alisema:
“Sote tunatambua kuwa kazi
aliyoifanya Waziri Mkuu Pinda ilikuwa
ngumu, misafara ilikuwa ni mingi na
wakati mwingine ilikuwa ya mwendo
mkali, lakini Mungu alimtetea na
kumlinda hadi leo yuko salama.
Tunakushukuru pia kwa ushirikiano
ulioendelea kutuonyesha wakati ukiwa
madarakani na tunakuombea uendelee
kuwa na ucha Mungu katika maisha
yako ya uraiani.”

POSTED BY VUMILIA NKYA A.K.A VEN DA CLASSIC....EAGLEFM... Magufuli: Asiyefanya kazi


Mgombea urais wa CCM, Dk John
Magufuli akihutubia mkutano wa kampeni
wilayani Misungwi, Mwanza jana. Picha na
Mpigapicha Wetu
Magu/Misungwi. Mgombea urais wa
CCM, Dk John Magufuli amewataka
wananchi kujipanga kufanya kazi kwa
sababu Serikali yake haitavumilia
watu wavivu.
Akihutubia mkutano wa kampeni
katika Uwanja wa Shule ya Msingi
Misungwi jana, Dk Magufuli alisema
hata vitabu vya dini vimeelekeza
kwamba asiyefanya kazi na asile, hivyo
wanaoahidi vitu vya bure
wanawadanganya Watanzania.
“Tujipange kufanya kazi, hata
maandiko ya vitabu vitakatifu
yanasema, asiyefanya kazi asile…
Misungwi nitaibeba kwa nguvu zangu
zote nikichaguliwa,” alisema.
Pia alisema nyumba za tembe ambazo
zinaahidiwa na wagombea wenzake
kwamba zitaondolewa ndani ya siku
100 ni uongo hivyo wasisikilizwe, bali
atakachofanya ni kuhakikisha bei ya
vifaa vya ujenzi inapungua na
ameanza na saruji.
Alisema anatambua kuwa wilaya hiyo
inakabiliwa na tatizo la maji na
kuwaahidi wananchi kulishughulikia
na wasimsumbue mbunge wao na
kwamba anapoahidi kutoa Sh50
milioni kila kijiji nchini watu
wanamshangaa lakini Serikali ina
fedha, nyingine zilikuwa zinatafunwa
na mafisadi.
“...Ndiyo maana baada ya kusikia
nimetangazwa mengine yakakimbia…
hivi sasa wanasema Serikali haijafanya
chochote wakati wengine wamezeekea
humu mpaka wakang’oka meno na
kuwekewa ya bandia, mbona
hawakuondoka muda wote?” alihoji Dk
Magufuli.
Mgombea huyo huku akichomeka
lugha ya Kisukuma kila mara, alisema
ujenzi wa barabara ya Usagara –
Kisema ukikamilika, malori yatakuwa
hayaruhusiwi kuingia katikati ya mjini
wa Mwanza. Aliahidi kufufua viwanda
vya kuchambua pamba ili kuleta
mabadiliko ya kweli.
Dk Magufuli aliahidi kufufua kilimo
cha pamba kwa kuhakikisha mkulima
anapata pembejeo na kunufaika na zao
hilo na kwamba, haiwezekani pamba
ilimwe Tanzania Ulaya wavae nguo
mpya halafu Watanzania waletewe
mitumba.
Hata hivyo, mgombea huyo akiendelea
kutoa ahadi sauti za wanawake
zilisikika zikimtaka kuzungumzia
samaki kazi ambayo ndiyo
wanayoitegemea kiuchumi, hivyo
akalazimika kutamka kuwa atafuta
ushuru unaoonekana kuwa kero.
“Nitafufua Chuo cha Kilimo Ukiriguru
na kutumia wataalamu wake
kuboresha kilimo cha pamba,”
alisema.
Mgombea ubunge Jimbo la Misungwi,
Charles Kitwanga alisema kuna sifa ya
Dk Magufuli ambayo haijatajwa nayo
ni ubunifu, kwani alianzisha mfuko wa
kujenga barabara kwa fedha za ndani
hali iliyowashangaza wafadhili.
“Hizi barabara tunazotaja kama siyo
yeye zisingekuwapo, mnakumbuka
wafadhili walikuwa wanakataa
kutukopesha, akaanzisha mfuko wa
kujenga barabara mpaka wafadhili
wanauliza fedha zitakapopatikana,
akawaambia tunazo,” alisema.
Kitwanga alimwomba mgombea huyo
kuwajengea hospitali ya wilaya na
kiwanda cha kusindika nyanya, zao
linalolimwa kwa wingi.
Akiwa Magu, Dk Magufuli alisema
endapo atachaguliwa, ataubadilisha
mji huo kwa kutatua kero sugu ya maji
na kujenga barabara zinazozunguka
mji huo. Alisema atatumia uwezo wake
wote kuhakikisha kilimo cha pamba
kinakuwa bora ili bei ya zao hilo
ipande na kuwanufaisha wakulima.
Akihutubia umati wa watu kwenye
Viwanja vya Sabasaba jana, Dk
Magufuli alisema: “Natambua kwamba
Magu shida yenu kubwa ni maji,
mmekuwa mkitaabika kwa muda
mrefu, huku Ziwa Victoria likiwa
limewazunguka.
“Kwa kutambua kwamba maji ni
muhimu kwa binadamu, hapa Magu
lazima mpate maji na tayari Kampuni
ya Cowi inafanya upembuzi yakinifu
kuhakikisha maji yanafika,
wakikamilisha tu suala la maji kufika
Magu niacheni mimi...”
Dk Magufuli alisema anataka kuona
Magu inabadilika na kwamba
ameahidi kujenga barabara
zinazozunguka mji huo na kuunganisha
wilaya jirani.
Alisema amezaliwa na kulima pamba
pamoja na kufuga, hivyo ni mtoto wa
mkulima na mfugaji na kwamba
atatumia uzoefu wake kuhakikisha bei
ya pamba inakuwa juu. “Nafahamu
kwamba bei ya pamba kwa sasa
imeshuka, lakini mimi ni mtoto wa
mkulima na mfugaji, pamba
naifahamu vizuri, nataka tutengeneze
mazingira mazuri kwa wakulima wa
pamba ili iwe bora,” alisema Dk
Magufuli.
Aliwataka wakazi wa mji huo, kula
fedha za watu wanaowahonga ili
wawachague, akisema hizo ni fedha
zao ambazo walizichuma kwa kutumia
ufisadi.
“Nyie mkipewa fedha kuleni, kwani
kula ni kwa mafisadi kulala kwa
Magufuli,” alisema na kuongeza kuwa
akichaguliwa, atakuwa rais wa watu
wote, kwa kuwa maendeleo hayana
chama.
Aliahidi kufuta ushuru ambao
umekuwa ukiwasumbua
wafanyabiashara ndogondogo
sambamba na kupunguza kodi za vifaa
vya ujenzi ili bei ya vifaa hivyo
ipungue na kuwawezesha wananchi
kununua na kujenga nyumba bora.
Imeandikwa na Aidan Mhando, Midraji
Ibrahim na Twalad Salum

POSTED BY RIZIKI MALYA EAGLEFM Lowassa: Nimejiandaa


Mgombea urais wa Chadema, Edward
Lowassa akihutubia mkutano wa kampeni
uliofanyika kwenye Uwanja wa
Rwandanzovwe, Nzovwe mjini Mbeya
jana. Picha na Emmanuel Herman
Mbeya/Mbarali. Mgombea urais wa
Chadema, Edward Lowassa amesema
amejiandaa na yupo tayari
kuwaongoza Watanzania akiwa rais wa
awamu ya tano.
Akizungumza kwenye Uwanja wa
Ruanda Nzovwe- Mbeya Mjini, Lowassa
alisema: “Ninatosha, nitumeni kwa
kura zenu… nipeni kura za kutosha
niwatumikie.”
Lowassa ambaye alisema anasikia deko
kutokana na wingi wa watu, alisema
misamaha ya kodi kwa sasa ni Sh1.6
trilioni na kwamba atahitaji Sh1.3
trilioni kati ya hizo kwa ajili ya elimu
itakayolipiwa na serikali kuanzia
chekechea hadi chuo kikuu.
Alirejea kusema kuwa katika serikali
yake hakutakuwa na michango ya
elimu, maabara wala madawati.
Akizungumza kabla ya kumkaribisha
Lowassa, Mwenyekiti wa Chadema,
Freeman Mbowe alisema viongozi
waliokuwa CCM akiwamo Lowassa,
wamejiunga na chama chao kwa kuwa
kina misingi imara.
Akizungumzia suala la upigaji kura,
alisema siku sita zilizobaki ni muhimu
kwa Watanzania kufanya uamuzi na
kusisitiza kuwa kuna kila sababu ya
kubakia kwenye vituo vya kura baada
ya kupiga kura huku akidai kwamba
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),
haiko huru.
Sumaye
Akihutubia mkutano huo, Waziri Mkuu
mstaafu, Frederick Sumaye alimtaka
Waziri wa Uchukuzi, Harrison
Mwakyembe kuwasomea wananchi wa
Mbeya, ripoti ya Richmond kuona
kama Lowassa anahusika.
“Lowassa hahusiki, alijiuzulu kwa ajili
ya kuwakoa wao na wao wanaendelea
kuilipa Richmond kwa mgongo wa
Dowans wakati Lowassa hayupo,”
alisema.
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph
Mbilinyi alisema tatizo kubwa kwa
wakazi wa jimbo lake ni maji hasa
katika vijiji vya Uyole na Mwakibete na
kusema kuna kila sababu ya kuvuta
maji kutoka Ziwa Nyasa hadi Mbeya ili
kukabiliana na tatizo hilo. Alisema
matatizo mengine ni hospitali na
huduma za afya akitaka wapatiwe
mashine za x-ray, CT Scan na umeme
wa uhakika.
Ilivyokuwa mchakamchaka
Kabla ya mkutano huo, Jiji la Mbeya
lilitawaliwa katika hekaheka za
mapokezi ya Lowassa kuanzia asubuhi
huku wakazi wakianza kufurika
kwenye uwanja huo tangu saa mbili
asubuhi.
Jiji lilitawaliwa na pilipika za
bodaboda na bajaji zenye bendera za
Chadema katika maeneo mengi
hususan Barabara Kuu ya Mbeya-
Zambia kuanzia Kabwe, Mwanjelwa,
Mafiati, Soweto na Mama John
ulikofanyikia mkutano huo.
Wafuasi wa mgombea huyo
walionekana wakirandaranda maeneo
mengi ya jiji hilo wakiwa wamevalia
sare za Chadema huku wakipiga deki
Barabara Kuu ya Mbeya - Zambia.
Muda mfupi kabla ya mkutano kuanza,
wafanyabiashara walifunga maduka
kwenda kusikiliza sera.
Wachuuzi wa vyakula na vinywaji
walihamishia biashara zao kwenye
mkutano huo tangu usiku wa kuamkia
jana na wengi walionekana kufurahia
uamuzi wao kutokana na biashara
waliyofanya.
Mmoja wa wauza chipsi, John Antony
alisema: “Aisee si unajua tena kufaa
kufaana, leo kuna neema kubwa kwetu
ndiyo maana leo tumehamishia
biashara yetu uwanjani.”
Mbarali
Katika mkutano wa Mbarali, wafuasi
wa CUF na Chadema walizua tafrani
wakati wakimsubiri Lowassa katika
Uwanja wa Mpira, Rujewa.
Tafrani hiyo ilizuka baada ya
mgombea wa CUF, Gamdust Haji
kufika na gari lake kisha kushuka na
wafuasi wanaomuunga mkono kwa
kumbeba juujuu na kumpeleka jukwaa
kuu, jambo ambalo liliwakera wafuasi
wanaomuunga mkono mgombea wa
Chadema, Liberatus Mwang’ombe na
kutaka kumuondoa kwa nguvu.
Polisi wazima rabsha
Baadhi ya mashuhuda walisema
kulikuwa na kundi la wafuasi
wanaomuunga mkono mgombea wa
CUF na kundi la mgombea wa
Chadema ambao walikuwa
wakilumbana huku kila upande
ukitaka mgombea wao ndiye anadiwe
na Lowassa kwa wananchi.
“Unajua hawa watu walishindwa
kuafikiana nani agombee ubunge
kupitia yale makubaliano yao Ukawa,
kitu ambacho kila chama kilisimamisha
mgombea wake,” alisema mmoja wa
wakazi wa Rujewa mjini, Athumani
Mwakitalima.
Akizungumzia suala hilo, Haji alisema:
“Ni kweli nimefanyiwa vurugu,
wamevunja vioo vya gari langu,
wakitaka niondoke kwenye mkutano
huo eti sina haki ya kushiriki na
kumsikiliza mgombea wangu wa urais.
Nimetoa taarifa polisi na kuna watu
wamekamatwa.”
Aliwalaumu viongozi wa kitaifa
walioambatana na Lowassa kwamba
hawakutaka kuuliza sababu za yeye
kutowapo mkutanoni hapo na badala
yake kumnadi Mwang’ombe akisema
hawakutenda haki.

POSTED BY DENIC LYAMUYA EAGLEFM


Dar es Salaam. Zimesalia saa 144 za
kampeni ambazo wagombea wa vyama
vyote vya siasa watazitumia kutupa
karata zao za mwisho wakilenga
kupata ushawishi wa mwishomwisho
na hatimaye kunyakua ushindi.
Saa hizo za majeruhi zimesababisha
wagombea urais wa CCM, Dk John
Magufuli, Edward Lowassa wa
Chadema na Anna Mghwira wa ACT –
Wazalendo kujikita katika mikoa “ya
kimkakati” na ile yenye wapigakura
wengi.
Dk Magufuli ndiye aliyefungua pazia la
kampeni Agosti 23 kwenye viwanja wa
Jangwani, Dar es Salaam na kufuatiwa
na Lowassa hapohapo Jangwani kabla
ya Mghwira kuzindua huko Mbagala.
Wagombea hao ambao
wameshazunguka mikoa yote nchini,
watazitumia siku sita zilizobaki kabla
ya siku ya kupigakura kujiwekea
mazingira mazuri ya ushindi.
Akizungumzia mikakati ya mwisho ya
kampeni, Kaimu Katibu Mkuu wa
Chadema, Salum Mwalimu alisema
mikoa yote nchini ni ya kimkakati kwa
chama hicho na Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa), huku akieleza jinsi
Lowassa atakavyohitimisha siku
zilizobaki.
“Kwa sasa, mgombea anaendelea na
mikutano ya kampeni mkoani Mbeya.
Akimaliza huko atarejea Dar es Salaam
kwa ajili ya kufunga kampeni ila
atapita katika mikoa ya Iringa na
Morogoro.
“Tupo katika hatua za mwisho, hivyo
tunaweza kuangalia pia ni wapi
mgombea wetu anaweza kwenda
ukiacha maeneo hayo,” alisema
Mwalimu.
Mjumbe wa kamati ya kampeni ya
CCM, January Makamba alisema
mgombea urais wa chama hicho
atazitumia siku sita zilizobaki kupita
majimbo ambayo aliyaruka katika
baadhi ya mikoa.
“Lengo letu ni kwenda kwenye
majimbo yote, hivyo siku hizi zilizobaki
atapita huko. Kuhusu wapi tutafunga
kampeni zetu tutatangaza siku yoyote
kuanzia leo,” alisema Makamba.
Lowassa jana aliendelea na kampeni
mkoani Mbeya huku Dk Magufuli
akiwa katika Wilaya ya Magu mkoani
Mwanza.
Mikoa ya kimkakati na yenye
wapigakura zaidi ya milioni moja kila
mmoja ambayo huenda wagombea hao
wakaitumia kunadi sera zao za
mwishomwisho ni Morogoro, Tabora,
Dodoma, Kagera, Tanga, Arusha, Mara,
Geita, Kilimanjaro, Kigoma, Shinyanga,
Ruvuma, Mtwara na Simiyu.
Mambo yasiyosikika
Akizungumzia ahadi za wagombea hao,
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama
vya Wafanyakazi (Tucta), Nicolaus
Mgaya alisema wagombea wengi wa
urais wanazungumzia kuongeza
mishahara wafanyakazi, lakini
wanasahau kuzungumzia jinsi
watakavyoongeza marupurupu ya
wafanyakazi hao.
“Hapa nazungumzia kodi ya nyumba,
fedha za usafiri na malipo ya likizo,”
alisema Mgaya alipoulizwa kuhusu
ahadi za wagombea.
Ardhi na Katiba
Pamoja na wagombea hao kuahidi
kutatua migogoro ya ardhi, mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine
(Sua), Profesa Damian Gabagambi
anaona jambo hilo halijatolewa
maelezo ya kutosha.
“Ardhi ni jambo ambalo halijapewa
kipaumbele kwa maana ya kupimwa
na matumizi yake kuidhinishwa na
kulindwa kisheria. Mwingiliano wa
matumizi ya ardhi ni moja ya matatizo
makubwa nchini,” alisema Profesa
Gabagambi.
Alisema wagombea hao hawajagusia
suala la Watanzania kupata Katiba
Mpya, ambayo mchakato wake
ulikwama kabla ya hatua ya Kura ya
Maoni.
“Suala la kusaidia wakulima kupata
masoko ya uhakika halijafafanuliwa
kwa kina wala jinsi ya kuanzisha na
kuendeleza viwanda vidogovidogo kwa
sababu ndiyo vinaajiri wananchi wengi
kuliko vikubwa, ambavyo kila
mgombea anasema atavianzisha
akiingia madarakani,” alisema.
Itikadi
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa
Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu
Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM), Profesa Penina Mlama
alisema hakuna aliyesema akishinda
ataongoza nchi kwa itikadi ipi.
“Tunajua kuwa Wamarekani
wanatumia mfumo wa ubepari na
Mwalimu (Julius) Nyerere alitumia
ujamaa, sasa hawa wa sasa
(wagombea) wanaamini mfumo upi?”
alihoji Profesa Mlama.
Ahadi za Lowassa
Lowassa amekuwa akitumia ahadi ya
elimu bure kuanzia msingi hadi chuo
kikuu kama silaha yake kuu ya kupata
kura kwa wananchi.
“Kipaumbele cha kwanza ni elimu, cha
pili ni elimu na cha tatu ni elimu,”
alisema Lowassa tangu kwenye
uzinduzi wa kampeni zake na
amekuwa akirudiarudia kuhakikisha
kinaeleweka.
Pia, katika mikutano yake mingi waziri
huyo mkuu wa zamani amekuwa
akizungumzia jinsi ya kutatua tatizo la
maji, ambalo linaonekana kuwa kubwa
sehemu nyingi licha ya baadhi kuwa
na vijito, mito na maziwa, akitoa mfano
wa jinsi alivyoshughulikia mradi wa
maji ya Ziwa Victoria, ambao unasaidia
wakazi wa mikoa ya Mwanza, Tabora
na Mara.
“Nitahakikisha maziwa na mito
mikubwa kama Kagera inatumika
kuondoa tatizo la maji,” alisema
Lowassa alipozungumza na wananchi
wa Nkenge, Kagera.
“Kama niliweza kutoa maji Ziwa
Victoria nitashindwa vipi kutoa maji
kutoka Ziwa Tanganyika ili wananchi
mpate maji ya uhakika?” alisema
Lowassa katika mkutano wake wa
kampeni uliofanyika katika Uwanja wa
Mwanga Community Centre, Kigoma.
Lowassa, ambaye amekuwa akiwaita
waendesha bodaboda, wamachinga na
mamalishe kuwa ni marafiki zake,
amekuwa akiahidi kuanzisha benki
maalumu ya kuhudumia wajasiriamali
wadogo.
“Tumetengeza ilani kiboko ambayo
ndani ya miaka mitano Tanzania yetu
itabadilika, lazima tupunguze tabaka
kati ya tajiri na maskini kwa uchumi
wa pamba, chai, dhahabu na gesi kwa
nini tushindwe? Mkitupa ridhaa na
Mungu akikubali, tutakwenda kasi na
tutakuwa na maendeleo,” alisema
Lowassa katika mkutano uliofanyika
mjini Makambako.
Ahadi za Dk Magufuli
Kete kubwa tano za mgombea wa CCM,
Dk Magufuli ambazo amekuwa
akizinadi takriban kila mahali
anapokwenda tangu alipozindua
kampeni zake ni pamoja na kufuta
utaratibu wa kuwakamata na
kuwatoza ushuru usio na tija
waendesha bodaboda na mama lishe
na kuwabana wafanyabiashara
wakubwa kulipa kodi.
Kutoka Mpanda Vijijini alikoanzia
kampeni za mikoani hadi maeneo
anayoyafikia sasa, Dk Magufuli
amekuwa akipata zaidi shangwe pale
anapowaahidi awananchi kutoa
mikopo ya Sh50 milioni kwa kina
mama na vijana kwa kila kijiji nchi
nzima ili kukuza ujasiriamali na
kusomesha watoto bure kuanzia
darasa la kwanza hadi kidato cha nne.
Amekuwa akianisha mikakati yake ya
kudhibiti ufisadi nchini akiahidi
kuanzisha mahakama maalumu ya
kuwafunga mafisadi, ahadi ambao
imeonekana kumbeba kiasi cha
kutoisahau kila anapofanya mikutano
yake.
Katika kipindi hicho cha takriban siku
58 za kampeni, Dk Magufuli ambaye ni
waziri wa ujenzi, amekuwa akiahidi
kuinganisha nchi kwa kujenga
barabara za lami katika kila mkoa na
hata katika miji mikubwa isiyo na
barabara hizo kwenye mitaa na wiki
iliyopita wakati kampeni zilielekea
ukingoni alisaini mkataba wa ujenzi wa
barabara za juu jijini Dar es Salaam.
Ahadi hizo kubwa zimekuwa
zikisindikizwa na mikakati ya kujenga
Reli ya Kati, ya Kusini kuanzia Bandari
ya Mtwara – Songea – Mbamba Bay
kupitia Mchuchuma na Liganga na ile
ya Kaskazini kwa kiwango cha
kimataifa.
Dk Magufuli ameahidi kuboresha
huduma za afya na kusambaza maji na
umeme vijijini ili usaidie kufanikisha
mkakati wa kuifanya Tanzania kuwa
nchi ya viwanda.
Mghwira wa ACT
Mpaka sasa mgombea urais wa ACT-
Wazalendo, Anna Mghwira amefanya
kampeni katika mikoa mbalimbali Bara
na Zanzibar na ahadi zake kubwa
zikiwa ni kumaliza tatizo la maji, ujenzi
wa barabara, viwanda, migogoro ya
ardhi na elimu.
Upatikanaji wa majisafi na salama
umeonekana kuwa tatizo kuu katika
maeneo karibu mengi aliyozunguka
kufanya kampeni zake. Akiwa kwenye
mikoa ya Kanda ya Kusini na Kaskazini
na Dodoma, Tabora na Pwani aliahidi
kuwa serikali yake itapambana
kuondokana na tatizo hilo, kwa haoni
sababu ya kuendelea hasa ikizingatiwa
kuwa Tanzania ni nchi yenye vyanzo
vingi vya maji.
Akiwa Ruvuma kwenye majimbo ya
Tunduru Kusini na Kaskazini,
mgombea huyo aliahidi kuimaliza kero
ya muda mrefu inayowakabili wakazi
wa Tunduru na vitongoji vyake ya
ukosefu wa barabara iliyodumu kwa
kipindi cha zaidi ya miaka 54 ya
Uhuru, kwa kuhakikisha
inatengenezwa kwa kiwango cha lami.
Alirudia ahadi hiyo akiwa Lindi,
Mtwara, Katavi, Kigoma, Rukwa,
Dodoma na Tabora akisisitiza kuwa
nchi haiwezi kuendelea ikiwa hakuna
barabara zinazoungana na barabara
kuu. Kuhusu viwanda, amekuwa
akihoji ni nani walioviua
vilivyokuwapo?
Akiwa katika mikoa ya Kusini, Mtwara
Lindi Ruvuma, aliahidi Serikali yake
itahakikisha inajenga viwanda vya
korosho ili kuondokana na uuzaji wa
korosho ghafi kunakoipunguzia
mapato Serikali. Katika mikutano yake
aliyoifanya Korogwe na Handeni,
Tanga alisema ACT itawajengea
viwanda vya kusindika matunda ili
kuongeza ajira na pato kwa serikali.
Akiwa Mbulu mkoani Manyara,
aliahidi kujenga kiwanda cha pareto
pamoja na viwanda vidogovidogo vya
usagaji wa mazao ya ngano, dengu na
mahindi yanayopatikana kwa wingi
kwenye maeneo hayo.
Maoni ya wananchi
Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo
Kikuu cha Ruaha (Ruco), alisema ahadi
hizo zinaonekana kuwa nzuri na kujibu
vilio vya wananchi lakini tatizo kubwa
linatokea katika utekelezaji wake
kutokana na mfumo mzima wa
kiuchumi.
Alisema rais yoyote atakayepita ili
atekeleze ahadi za elimu bure, afya na
maji bure atatakiwa kupambana zaidi
na mfumo wa uchumi wa dunia ambao
hauungi mkono sera hizo za kijamaa.
Mkazi wa Kigogo, Salim Juma alisema
ahadi za Dk Magufuli ni nzuri na kwa
utendaji zinaweza kutekelezwa lakini
tatizo lipo kwenye chama chake
ambacho kimekithiri ufisadi na hakipo
tayari kwa mabadiliko hivyo
kupunguza kasi ya utekelezaji.
Dar es Salaam. Zimesalia saa 144 za
kampeni ambazo wagombea wa vyama
vyote vya siasa watazitumia kutupa
karata zao za mwisho wakilenga
kupata ushawishi wa mwishomwisho
na hatimaye kunyakua ushindi.
Saa hizo za majeruhi zimesababisha
wagombea urais wa CCM, Dk John
Magufuli, Edward Lowassa wa
Chadema na Anna Mghwira wa ACT –
Wazalendo kujikita katika mikoa “ya
kimkakati” na ile yenye wapigakura
wengi.
Dk Magufuli ndiye aliyefungua pazia la
kampeni Agosti 23 kwenye viwanja wa
Jangwani, Dar es Salaam na kufuatiwa
na Lowassa hapohapo Jangwani kabla
ya Mghwira kuzindua huko Mbagala.
Wagombea hao ambao
wameshazunguka mikoa yote nchini,
watazitumia siku sita zilizobaki kabla
ya siku ya kupigakura kujiwekea
mazingira mazuri ya ushindi.
Akizungumzia mikakati ya mwisho ya
kampeni, Kaimu Katibu Mkuu wa
Chadema, Salum Mwalimu alisema
mikoa yote nchini ni ya kimkakati kwa
chama hicho na Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa), huku akieleza jinsi
Lowassa atakavyohitimisha siku
zilizobaki.
“Kwa sasa, mgombea anaendelea na
mikutano ya kampeni mkoani Mbeya.
Akimaliza huko atarejea Dar es Salaam
kwa ajili ya kufunga kampeni ila
atapita katika mikoa ya Iringa na
Morogoro.
“Tupo katika hatua za mwisho, hivyo
tunaweza kuangalia pia ni wapi
mgombea wetu anaweza kwenda
ukiacha maeneo hayo,” alisema
Mwalimu.
Mjumbe wa kamati ya kampeni ya
CCM, January Makamba alisema
mgombea urais wa chama hicho
atazitumia siku sita zilizobaki kupita
majimbo ambayo aliyaruka katika
baadhi ya mikoa.
“Lengo letu ni kwenda kwenye
majimbo yote, hivyo siku hizi zilizobaki
atapita huko. Kuhusu wapi tutafunga
kampeni zetu tutatangaza siku yoyote
kuanzia leo,” alisema Makamba.
Lowassa jana aliendelea na kampeni
mkoani Mbeya huku Dk Magufuli
akiwa katika Wilaya ya Magu mkoani
Mwanza.
Mikoa ya kimkakati na yenye
wapigakura zaidi ya milioni moja kila
mmoja ambayo huenda wagombea hao
wakaitumia kunadi sera zao za
mwishomwisho ni Morogoro, Tabora,
Dodoma, Kagera, Tanga, Arusha, Mara,
Geita, Kilimanjaro, Kigoma, Shinyanga,
Ruvuma, Mtwara na Simiyu.
Mambo yasiyosikika
Akizungumzia ahadi za wagombea hao,
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama
vya Wafanyakazi (Tucta), Nicolaus
Mgaya alisema wagombea wengi wa
urais wanazungumzia kuongeza
mishahara wafanyakazi, lakini
wanasahau kuzungumzia jinsi
watakavyoongeza marupurupu ya
wafanyakazi hao.
“Hapa nazungumzia kodi ya nyumba,
fedha za usafiri na malipo ya likizo,”
alisema Mgaya alipoulizwa kuhusu
ahadi za wagombea.
Ardhi na Katiba
Pamoja na wagombea hao kuahidi
kutatua migogoro ya ardhi, mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine
(Sua), Profesa Damian Gabagambi
anaona jambo hilo halijatolewa
maelezo ya kutosha.
“Ardhi ni jambo ambalo halijapewa
kipaumbele kwa maana ya kupimwa
na matumizi yake kuidhinishwa na
kulindwa kisheria. Mwingiliano wa
matumizi ya ardhi ni moja ya matatizo
makubwa nchini,” alisema Profesa
Gabagambi.
Alisema wagombea hao hawajagusia
suala la Watanzania kupata Katiba
Mpya, ambayo mchakato wake
ulikwama kabla ya hatua ya Kura ya
Maoni.
“Suala la kusaidia wakulima kupata
masoko ya uhakika halijafafanuliwa
kwa kina wala jinsi ya kuanzisha na
kuendeleza viwanda vidogovidogo kwa
sababu ndiyo vinaajiri wananchi wengi
kuliko vikubwa, ambavyo kila
mgombea anasema atavianzisha
akiingia madarakani,” alisema.
Itikadi
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa
Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu
Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM), Profesa Penina Mlama
alisema hakuna aliyesema akishinda
ataongoza nchi kwa itikadi ipi.
“Tunajua kuwa Wamarekani
wanatumia mfumo wa ubepari na
Mwalimu (Julius) Nyerere alitumia
ujamaa, sasa hawa wa sasa
(wagombea) wanaamini mfumo upi?”
alihoji Profesa Mlama.
Ahadi za Lowassa
Lowassa amekuwa akitumia ahadi ya
elimu bure kuanzia msingi hadi chuo
kikuu kama silaha yake kuu ya kupata
kura kwa wananchi.
“Kipaumbele cha kwanza ni elimu, cha
pili ni elimu na cha tatu ni elimu,”
alisema Lowassa tangu kwenye
uzinduzi wa kampeni zake na
amekuwa akirudiarudia kuhakikisha
kinaeleweka.
Pia, katika mikutano yake mingi waziri
huyo mkuu wa zamani amekuwa
akizungumzia jinsi ya kutatua tatizo la
maji, ambalo linaonekana kuwa kubwa
sehemu nyingi licha ya baadhi kuwa
na vijito, mito na maziwa, akitoa mfano
wa jinsi alivyoshughulikia mradi wa
maji ya Ziwa Victoria, ambao unasaidia
wakazi wa mikoa ya Mwanza, Tabora
na Mara.
“Nitahakikisha maziwa na mito
mikubwa kama Kagera inatumika
kuondoa tatizo la maji,” alisema
Lowassa alipozungumza na wananchi
wa Nkenge, Kagera.
“Kama niliweza kutoa maji Ziwa
Victoria nitashindwa vipi kutoa maji
kutoka Ziwa Tanganyika ili wananchi
mpate maji ya uhakika?” alisema
Lowassa katika mkutano wake wa
kampeni uliofanyika katika Uwanja wa
Mwanga Community Centre, Kigoma.
Lowassa, ambaye amekuwa akiwaita
waendesha bodaboda, wamachinga na
mamalishe kuwa ni marafiki zake,
amekuwa akiahidi kuanzisha benki
maalumu ya kuhudumia wajasiriamali
wadogo.
“Tumetengeza ilani kiboko ambayo
ndani ya miaka mitano Tanzania yetu
itabadilika, lazima tupunguze tabaka
kati ya tajiri na maskini kwa uchumi
wa pamba, chai, dhahabu na gesi kwa
nini tushindwe? Mkitupa ridhaa na
Mungu akikubali, tutakwenda kasi na
tutakuwa na maendeleo,” alisema
Lowassa katika mkutano uliofanyika
mjini Makambako.
Ahadi za Dk Magufuli
Kete kubwa tano za mgombea wa CCM,
Dk Magufuli ambazo amekuwa
akizinadi takriban kila mahali
anapokwenda tangu alipozindua
kampeni zake ni pamoja na kufuta
utaratibu wa kuwakamata na
kuwatoza ushuru usio na tija
waendesha bodaboda na mama lishe
na kuwabana wafanyabiashara
wakubwa kulipa kodi.
Kutoka Mpanda Vijijini alikoanzia
kampeni za mikoani hadi maeneo
anayoyafikia sasa, Dk Magufuli
amekuwa akipata zaidi shangwe pale
anapowaahidi awananchi kutoa
mikopo ya Sh50 milioni kwa kina
mama na vijana kwa kila kijiji nchi
nzima ili kukuza ujasiriamali na
kusomesha watoto bure kuanzia
darasa la kwanza hadi kidato cha nne.
Amekuwa akianisha mikakati yake ya
kudhibiti ufisadi nchini akiahidi
kuanzisha mahakama maalumu ya
kuwafunga mafisadi, ahadi ambao
imeonekana kumbeba kiasi cha
kutoisahau kila anapofanya mikutano
yake.
Katika kipindi hicho cha takriban siku
58 za kampeni, Dk Magufuli ambaye ni
waziri wa ujenzi, amekuwa akiahidi
kuinganisha nchi kwa kujenga
barabara za lami katika kila mkoa na
hata katika miji mikubwa isiyo na
barabara hizo kwenye mitaa na wiki
iliyopita wakati kampeni zilielekea
ukingoni alisaini mkataba wa ujenzi wa
barabara za juu jijini Dar es Salaam.
Ahadi hizo kubwa zimekuwa
zikisindikizwa na mikakati ya kujenga
Reli ya Kati, ya Kusini kuanzia Bandari
ya Mtwara – Songea – Mbamba Bay
kupitia Mchuchuma na Liganga na ile
ya Kaskazini kwa kiwango cha
kimataifa.
Dk Magufuli ameahidi kuboresha
huduma za afya na kusambaza maji na
umeme vijijini ili usaidie kufanikisha
mkakati wa kuifanya Tanzania kuwa
nchi ya viwanda.
Mghwira wa ACT
Mpaka sasa mgombea urais wa ACT-
Wazalendo, Anna Mghwira amefanya
kampeni katika mikoa mbalimbali Bara
na Zanzibar na ahadi zake kubwa
zikiwa ni kumaliza tatizo la maji, ujenzi
wa barabara, viwanda, migogoro ya
ardhi na elimu.

POSTED BY ERASMI KIMARIO EAGLEFM Washauri mambo matano




Dar es Salaam. Zikiwa zimebakia siku
sita kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi
Mkuu, Watanzania wameibua mambo
matano yanayoweza kuliepusha Taifa
na vurugu zinazoweza kutokea baada
ya uchaguzi.
Mambo hayo ni pamoja na uwazi wa
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),
pande zinazohusika kuheshimu sheria,
wagombea kuwa wakweli kwa wafuasi
wao, kukaa pamoja kuweka mwafaka
wa kitaifa na NEC kuwa huru.
Mambo hayo yametajwa kukiwa na
mvutano kati ya vyombo vya dola na
viongozi wa vyama vya upinzani
kuhusu suala la wananchi kukaa mita
200 au kwenda majumbani baada ya
kupiga kura.
Tayari Rais Jakaya Kikwete
ameshaagiza vyombo vya dola
kuchukua hatua kali dhidi ya watu
watakaokaidi agizo la kuondoka kituoni
baada ya kupiga kura.
Mbali na mvutano huo, juzi wilayani
Tunduma mkoani Mbeya mfuasi
mmoja wa CCM alimuua kwa
kumchoma kisu mwanachama wa
Chadema, kabla ya yeye kuuawa pia.
Viongozi kukutana
Kutokana na hali hiyo, mhadhiri
kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
(OUT), Emmanuel Mallya alishauri
viongozi wa vyama vyote
vinavyoshiriki uchaguzi huo wakutane
kujadiliana mambo ya kukubaliana
katika kipindi hiki kabla ya kufanyika
uchaguzi huo, Jumapili.
Mallya, ambaye ni Mkuu wa Idara ya
Sayansi ya Siasa chuoni hapo, alisema
kukutana kwa viongozi hao kutasaidia
kuwarejesha kwenye tafsiri ya
uchaguzi wa demokrasia badala ya
kuvutana kwa maslahi yao, hatua
inayoweza kuliathiri Taifa.
“Pili, uwazi wa NEC unahitajika zaidi
katika kipindi hiki, iwaeleze wagombea
kuweka mawakala waaminifu na
ijenge uhusiano mzuri na vyama,
taasisi za kiraia kwani dhamana ya
taifa ipo mikononi mwao na lazima
wanasiasa waongoze Taifa likiwa
salama na siyo walemavu,” alisema
Mallya.
Kufuata sheria
Profesa Gaudence Mpangalla wa Chuo
Kikuu cha Ruaha mkoani Iringa
alisema ili kuepuka vurugu ni
kuhakikisha sheria zinafuatwa.
Alisema ili kufuatwa sheria lazima
wanasiasa wajenge utamaduni wa
kuwa wakweli kwa wafuasi wao.
“Ushindani siyo vita wala uhasama
lakini inaonyesha kundi la vijana
limekosa uvumilivu na walitakiwa
kuelimishwa ukweli, watambue itikadi
zao haziwezi kuwa zaidi ya maslahi au
amani ya Taifa,” alisema Profesa
Mpangalla.
Uwazi wa NEC
Kwa upande wake, Profesa
Mohammed Bakari kutoka Idara ya
Sayansi ya Siasa, Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam(UDSM), alitaja jambo
jingine linaloweza kunusuru amani ni
uwazi wakati wa shughuli za NEC.
Alifafanua kuwa licha ya vyombo vya
dola kujitahidi katika ulinzi, wafuasi
wa vyama vya siasa wanakosa imani
na NEC baada ya kuwazuia wasisubiri
matokeo ya uchaguzi mita 200 kutoka
vituoni, suala ambalo ni tofauti na
maelekezo ya sheria inayowataka
kukaa umbali wa mita 200 kutoka
kituoni.
“Mwaka 2010 walijikusanya kusubiri
kura na waliondoka wakiwa
wameridhika na matokeo lakini kwa
nini NEC izuie na kauli ya Rais
inatumika kama agizo la Amiri Jeshi
Mkuu, kwa hivyo dola lazima itekeleze
wakati kauli zake nyingine
zimeonyesha upendeleo kwa chama
chake, hii ni hatari sana,” alisema.
Vijana waepuke kutumika
Mwenyekiti wa Mtandao wa
Wanawake nchini, Profesa Ruth Meena
aliwataka vijana kuepuka kutolewa
kafara na wanasiasa wenye maslahi
yao ya kuelekea Ikulu.
“Burundi ilipochafuka kina mama,
watoto na vijana ndiyo walioanza
kuumia na machafuko lakini viongozi
walikuwa kwenye ulinzi mkali kwa
hivyo lazima vijana wajitambue itikadi
zao haziwezi kuwa zaidi ya maisha
yao,” alisema.
“Lakini pia wanasiasa wote lazima
wajiandae kupokea matokeo, hakuna
aliyeshinda au aliyeshindwa hadi sasa
na uchaguzi ni sawa na mchezo wa
soka kwani lazima kuna mmoja
atashindwa na mwingine kushinda.”
Vyombo vya habari kutenda haki
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za
Kiislamu Tanzania, Sheikh Rajabu
Katimba alisema mbali na tahadhari
hiyo, Rais hatakiwi kutoa matamko
yanayokinzana na sheria zilizopo huku
vyombo vya habari vikitakiwa kutenda
haki.
“Kama ni haki ya kisheria kulinda kura
umbali wa mita 200 basi Rais Kikwete
anatakiwa kuheshimu hilo na
wananchi watamwelewa.”
“Lakini pia NEC inatakiwa
kuheshimiwa kwa sheria
inazosimamia, wafuasi wa vyama na
wagombea kujiepusha na kauli
zinazovunja sheria za uchaguzi na
mwisho kabisa vyombo vya habari
vitende haki katika kuripoti habari
zake,”alisema Katimba.

Jumatatu, 5 Oktoba 2015

Jifunze kinanda hapa mfano moyo funguka as written by wasonga mrombo


Moyo wangu funguka solfa on piano play try now...

Rais Kikwete ateua


Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete
Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete
amewateua wakuu wapya 13 wa wilaya
na kuwahamisha vituo vya kazi
wengine saba.
Walioteuliwa ni Shaaban Ntanambe
ambaye anakwenda Chato; Thabisa
Mwalapwa (Hanang), Richard
Kasesera (Iringa), Ruth Msafiri
(Kibondo) na Abdallah Njwayo
(Kilwa).
Wengine ni Asumpta Mshama
(Wanging’ombe), Mohammed Utaly
(Mpwapwa), Dauda Yasin (Makete),
Honorata Chitanda (Ngara), Vita
Kawawa (Kahama), Christopher
Ng’ubyagai (Mkalama), Hawa
Ng’humbi (Kishapu) na Mrisho Gambo
(Uvinza).
Wakuu wa wilaya waliohamishwa vituo
vya kazi ni Fadhili Nkurlu ambaye
anatoka Mkalama, kwenda Wilaya ya
Arusha, Wilson Nkambaku
anahamishiwa Arumeru, kutoka
Kishapu, Francis Miti ambaye
anahama Hanang kwenda Monduli na
Jowika Kasunga ambaye anahamia
Mufindi kutoka Monduli.
Wengine waliohamishwa ni Muhingo
Rweyemamu kutoka Makete kwenda
Morogoro; Hadija Nyembo anayehamia
Kaliua kutoka Uvinza na Benson
Mpesya ambaye anahamia Songea
Ruvuma kutoka Kahama.

Alhamisi, 24 Septemba 2015

Njia bora na sahihi kwa vijana kujiwekea akiba kwa sababu ya maisha ya kesho..hii hapa..imeandaliwa na mwandishi wa rombo wasonga mrombo


Taifa lenye akiba ya kutosha na
uchumi imara linakuwa na uwezo
katika kujiletea maendeleo na hata
kustahimili majanga yoyote
yanapotokea. Nguvu hiyo inatokana na
uwezo mkubwa wa akiba na mtaji
iliyowekezwa kwenye miradi
mikubwa.
Mtu kuweka akiba, ni muhimu sana
kama vile ilivyo kwa taifa. Saikolojia ya
matumizi ya fedha inaonyesha kuwa
mtu hupenda kutumia sasa kuliko
kusubiri baadaye ambapo ingeongeza
faida na thamani zaidi.
Fedha ni kitu ambacho kipo tu kwa
muda kama mtu aliyekuwa nayo sasa
akishindwa kuidhibiti leo, kesho
hatakuwa nayo. Suala mtambuka hapa
ni je, kwa nini niweke akiba au
niwekeze kwa jambo lingine?
Ningependa nizungumzie juu ya njia
mbalimbali za kuweka akiba ambapo
zikitumika zinaweza kukuletea faida
kwa karne hii, japo kiuhalisia kwa
Waafrika kuweka fedha ni tatizo sugu
kwa walio wengi. Hali kama hii
inatokana na uwezo mdogo wa
kudhibiti fedha kwa mitindo ya kisasa
na kibiashara pia. Elimu juu ya jambo
hili haijafika au haijakaa vizuri katika
upande wa ubongo iliyo wazi kwa
mazingira ya hapa nchini.
Zipo njia ambazo ni nzuri zikitumika
kwa kuweka akiba kwa faida
zitaongeza maendeleo ya wengi. Njia
hizo ni:
Moja, ni kununua fedha za kigeni.
Mara nyingi fedha za kigeni mfano
Dola za Marekani, Euro, Pound ya
Uingereza na fedha kutoka Bara la Asia
kama vile za Saudi Arabia, huwa
zinapanda thamani ukilinganisha na za
Tanzania.
Mfano, ulinunua Dola moja ya
Marekani Novemba, mwaka jana kwa
Sh1,300. Mwaka huu unaiuza kwa
Sh2,100. Ukipiga hesabu umepata
faida ya Sh800. Kama ulinunua Dola
10,000, leo hii ikiziuza una faida ya
Sh1 milioni, na kadhalika.
Mtindo wa kununua dola kwanza
unapunguza kubeba lundo la fedha
nyingi, inakuzuia kuitumia bila
sababu, hivyo kuendelea kuwa akiba,
kukulinda na kukuwezesha uwe na
faida pale mfumuko wa bei
unapoongezeka na inaweza kukusaidia
iwapo itakulazimu usafiri nje ya nchi.
Ukisafiri nje ya nchi itakufanya
usitumie fedha nyingi za kununua za
kigeni kwa gharama kubwa.
Pili, ni simu benki. Huu ni mfumo
ambao upo sana siku hizi eneo la
Afrika Mashariki. Siku hizi kampuni za
simu zimewezesha mtu kuweka akiba.
Huduma imeboreshwa zaidi kwa
kuweza kuzihamishia kwenye akaunti
za benki, kulipia huduma na bidhaa au
kuzitoa katika nchi nyingine kulingana
na aina ya fedha za eneo husika.
Hii inamuwezesha hata kama mtu
akiwa mbali na benki na kuwa na
uwezo wa kuokoa muda kwa kutumia
pesa alizoweka kwenye simu yake kwa
kuzitoa kwa wakala aliye karibu naye.
Vilevile, kwa kutumia simu waweza
kuvuta fedha kutoka kwenye akaunti
yako ya benki na kuziingiza kwenye
simu yako na kuwa huru kuzitoa ili
kuzitumia eneo lolote kwa kutumia
mawakala.
Siku hizi pia kwa kutumia akiba
kwenye simu unaweza kupata huduma
nyingine kupitia simu hiyo kama vile
kununua umeme, kulipia bili ya maji,
matibabu, king’amuzi na hata tiketi za
kuingia kwenye michezo ya soka au
tamasha. Mtu aweza kudunduliza
fedha kidogokidogo kwenye simu yake.
Tatu, kuweka akiba kwa kutumia benki
na taasisi nyingine za kifedha. Hii
husaidia sana kuhamasisha huduma za
kuweka akiba kwa malengo kama vile
kumsomesha mtoto au amana.
Uwekaji wa fedha za namna hiyo pia
huweza kusaidia kuwa na fedha za
kukabili dharura na kuwa na mitaji
mikubwa ya kibiashara na hatimaye
kuleta maendeleo makubwa
yaliyokusudiwa.
Nne, ni kumkopesha mtu na kurudisha
kwa riba. Siku hizi aina hii ya
ukopeshaji imeenea sana, hasa mijini
na vyuoni. Hii imetokana na watu
kuzidi kukua sana kiuelewa,
wamebadili mwelekeo kutoka
kumkopesha mtu pasipo riba hadi
kuwa na faida.
Watu wameerevuka na kufahamu
kuwa fedha ya mwezi au wiki hii ni
tofauti na ya mwezi au wiki lijalo.
Tatizo lililopo ni kwamba hakuna
maandishi ya kukopeshana kwa walio
wengi kwa sababu za kujali utu. Lakini
ukweli ni kwamba wanadamu wengi
wana tabia ya kubadilika. Kama huna
maandishi ya kukopeshana itakuwa
vigumu kupata fedha zako pale
anapokuwa si mwaminifu.
Tano, ni kuwekea bima mali zako na
biashara yako. Hii ni njia ambayo ni
muhimu sana maana hakuna mtu
anayeweza kuzuia majanga ambayo ni
ya asili au ya kawaida, hivyo bima
hasaidia sana siku ukipata ajali ya
biashara kwa kuibiwa au kuungua.
Sita, ni kununua vitu kama nyumba,
ardhi na vifaa vya gharama vyenye
kudumu muda mrefu. Hivi waweza
kuviuza baadaye kwa bei ya juu.
Maendeleo ya mtu mmojammoja ni
mafanikio ya taifa. Taifa lenye akiba ya
kutosha kwa kawaida linakuwa imara
na wananchi wenye akiba kwa njia
mbalimbali kama nilivyoorodhesha, ni
watu wenye maisha ya uhakika.
Dharura zote wanaweza kuzikabili na
hapa ndipo pia mitaji mikubwa ya
biashara inatokea. Kuweka akiba ni
jambo la msingi, tuanze leo kuweka
akiba. MPENZI MSOMAJI KAMA UMEGUZWA NA MAKALA HAYA TUANDIKIE KWENDA EMAIL HII kimarioerasmi@gmail.com

Haya libabu la arsenal hii Ndoa ya Arsene Wenger yavunjika Ndoa ya kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na mke wake, Annie iliyodumu kwa miaka mitano imevunjika


Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na
mkewe Annie
Strasbourg, Ufaransa. Ndoa ya kocha
wa Arsenal, Arsene Wenger na mke
wake, Annie iliyodumu kwa miaka
mitano imevunjika baada ya miezi
kadhaa ya uvumi.
Habari za kimahakama mjini
Strasbourg zilieleza jana kuwa wawili
hao wenye binti wa miaka 18,
wamekuwa hawaonekani pamoja
tangu mwaka 2013.
Wenger, mwenye umri wa miaka 65 na
mkewe, Annie 59 wamefikia mwafaka
wa kugawana mali.
Mara kadhaa, kocha huyo alikiri kuwa
shinikizo kubwa la kazi kwenye klabu
hiyo ya London Kaskazini
limesababisha matatizo kwenye ndoa
yake.
Nyaraka za kimahakama zilionyesha
kuwa wawili hao walitengana Juni
mwaka huu.
Hata hivyo, nyaraka hizo zimeeleza
kuwa si talaka kamili, bali
wametengana kisheria, jambo
linalomaanisha kuwa wana jukumu la
kuendelea kuwa pamoja.
Wawili hao walifunga ndoa Desemba
2010 baada ya uhusiano wa muda
mrefu, lakini wamekuwa si wenye
furaha kwa muda sasa.
“Wamegawana mali na rasilimali,
wamefikia mwafaka wa kutengana.
Mwaka 2008, kocha huyo alieleza
dhamira ya kuacha soka ili kuwekeza
nguvu kwenye ndoa.
Alisema: “ Miaka kumi iliyopita,
nilimweleza mke wangu (Annie),
‘Anipe miaka mitano zaidi katika soka
inatosha’, lakini hadi leo ninaendelea
na kazi.
“Ni vigumu kuwa na muda wa kutosha
kukaa pamoja kwa sababu ya ratiba
ngumu ya masuala ya soka. Kuna
wenzetu wanaondoka Jumatatu na
kurudi Ijumaa
“Ninasafiri kikazi, lakini tatizo si kiasi
gani cha muda ninaotumia mbali ya
familia yangu, bali ubora wa muda
ninaotumia na familia yangu.
“Nikizingatia hilo, kuna madhara.
Familia inakosa ubora wa huduma
wanazostahili nikiwa nyumbani, kwani
ninafikiria mchezo unaofuata.”
Aliongeza: “Mke wangu anapenda
kuangalia soka, anaona mechi za
Arsenal akiwa nyumbani . Siyo shabiki,
lakini anapenda michezo. Ni kwa kuwa
hakuwa na chaguo.”
-

Watu 41 wakamatwa kwa kutishia amani kwenye kampeni Watu 41 wakiwamo wanawake tisa wamekamatwa mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya vurugu katika


Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya,
Ahmed Msangi.
Mbeya. Watu 41 wakiwamo wanawake
tisa wamekamatwa mkoani hapa kwa
tuhuma za kufanya vurugu katika
maeneo mbalimbali wakati wa
kampeni zinazoendelea kuwanadi
madiwani na wabunge.
Kamanda wa polisi mkoani hapa,
Ahmed Msangi amesema hayo leo
alipozungumza na waandishi wa
habari kuhusu tathimini ya matukio ya
uchaguzi.
Amesema tangu kampeni zilipoanza
matukio 30 ya uhalifu yalifanyika
yakiwahusisha wanaume 32 na
wanawake tisa.
Amesema tukio moja kati ya hayo
lilimhusisha Aman John ambaye
amefikishwa kortini na kupatikana na
hatia iliyosababisha alipe faini ya
Sh30,000.
“Kesi nane kati ya matukio hayo zipo
mahakamani zikiwa katika hatua
mbalimbali lakini kesi tatu majalada
yapo ofisi ya wanasheria wa Serikali
wakati kesi zingine 19 zinapelelezwa,’’
amesema.
Amesema waliokamatwa
wametuhumiwa makosa mbalimbali
yakiwamo ya kuchana mabango ya
wagombea wa Urais, Ubunge na
Udiwani.
‘’Wengine wamekamatwa kwa makosa
ya kung’oa bendera, kuharibu mali,
kufanya fujo, kujeruhi, kuingilia
mkutano, kutishia kuua kupigana
hadharani na wizi’’ amesema kamanda
huyo

Kipindupindu chaendelea kunyonga watu dar.. Kipindupindu chaendelea kuua D’Salaam Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa ugonjwa wa kipindupindu imeongezeka na kufikia 17 baada ya


Watoto wakicheza katika jalala eneo la
Bugando Mwanza, mazingira ya namna hii
ni hatari kwa afya zao.
Dar es Salaam. Idadi ya watu
waliopoteza maisha kwa ugonjwa wa
kipindupindu imeongezeka na kufikia
17 baada ya watu wengine wawili
kupoteza maisha jana.
Hata hivyo, idadi ya watu
walioripotiwa kuugua ugonjwa huo
tangu ulipuke katika Jiji la Dar es
Salaam Agosti 17, imefikia 2,000.
Ofisa Habari wa Manispaa ya Temeke,
Joyce Msumba alisema kuwa jana
walipokea wagonjwa wapya saba na
kati yao, mmoja ameshafariki dunia.
Msumba alisema wagonjwa wengi
hawatoki katika Manispaa hiyo bali
wapo wanaotoka eneo la Buguruni
katika Manispaa ya Ilala na
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
mkoani Pwani.
Alisema tayari wameshatoa taarifa
kwa maofisa wa afya wa wilaya zao ili
wafuatilie hali katika familia zao.
Mganga Mkuu wa Manispaa ya
Kinondoni, Victorina Ludovick alisema
wamepokea wagonjwa wapya 31 idadi
inayofanya watu waliolazwa katika
kambi ya ugonjwa huo kufikia 38.
Dk Ludovick alisema wagonjwa wengi
wanatoka maeneo ya Buguruni,
Vingunguti, Jangwani, Ilala,
Mchikichini, Tabata na Kigogo.
Alisema kuendelea kusambaa kwa
ugonjwa huo kunatokana na wakazi
wengi wa maeneo hayo kutozingatia
kanuni za afya wanazofundishwa na
wataalamu.
“Magari ya matangazo yanapita katika
mitaa yao kila siku kutoa elimu na
kuwahamasisha kunawa mikono kwa
sabuni baada ya kutoka chooni,
kuchemsha maji ya kunywa na
kuzingatia usafi wanapoandaa
vyakula,” alisema Ludovick
Alisema maofisa afya wanaendelea na
kazi ya kukagua mazingira
wanayofanyia kazi wafanyabiashara
wa vyakula na matunda ili kuwabaini
wanaokiuka agizo la kuacha kufanya
biashara hiyo hadi ugonjwa huo
utakapokwisha.

Idd kwa waislamu wengine imewasababishia kifo Mamia ya mahujaji wafariki katika mkanyagano Makka Watu wasiopungua 717 wamekufa, huku wengine 816 wamejeruhiwa leo jirani na mji mtakatifu wa Makka


Watu wasiopungua 717 wamekufa,
huku wengine 816 wamejeruhiwa leo
jirani na mji mtakatifu wa Makka
walikokwenda kuhiji ikiwa ni sehemu
ya utekelezaji wa moja ya nguzo
muhimu katika Imani ya dini ya
Kiislamu, maofisa Saudi Arabia
wathibitisha.
Kwa mujibu wa Baraza la Taasisi na
Jumuiya za Kiiislam nchini, kati ya
mahujaji 2,000,000 waliokwenda Saudi
Arabia mwaka huu, 1,500 wanatoka
Tanzania.
Japokuwa Msemaji wa Baraza hilo,
Shekhe Rajabu Katimba amesema
hakuna vifo vilivyokwisharipotiwa hadi
sasa toka Makka, taarifa zisizo rasmi
kutoka huko zinasema Mtanzania
mmoja amekufa na mwingine
amejeruhiwa baada ya kutokea
mkanyagano.
Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji
la BBC, katika maafa hayo, mahujaji
wengine wasiopungua 816
wamejeruhiwa katika eneo la Mina.
Vifo hivyo vimetokea ikiwa ni siku
chache kupita baada ya kutokea jail
nyingine ambapo winchi lilianguka na
kuua watu 109 katika msikiti ambapo
kulikuwa kukifanyika ibada ikiwa ni
maandalizi ya kuelekea sikukuu ya leo.
Haya ni maafa makubwa zaidi kutokea
katika sikukuu ya Eid Al Hajj baada ya
kupita takribani miaka 25. Kwa mujibu
wa Kurugenzi ya Wizara ya Usalama
wa Raia nchini Saudi Arabia, maafa
hayo yametokea kati ya saa sita
(majira ya Afrika Mashariki) katika
makutano ya mitaa namba 204 na 223
wakati mahujaji hao wakipanda ngazi
kuelekea jengo la ghorofa tano ambalo
limeuzunguka mnara, maarufu kwa
jina la Jamarat Bridge. “Tukio hilo
limetokea baada ya mahujaji
kuongezeka ghafla wakielekea kwenye
mnara,” taarifa ya wizara iliongeza.

Jumatano, 23 Septemba 2015

Maaaajabu haya .. mtoto mwenye miguu minnee azaliwa rombo ..kijiji cha kitowo


Mpenzi msomaji haya ni maajabu ambayo huwa hutokea kwa nchi za wenzetu lakini leo nishtuka sana na habari hizi ambazo hazijathibitishwa.. ila chanzo kmoja kinasema kwamba mtoto huyo alizaliwa katika zahanati ya kasuruwa.. tarehe 21/03/2014 na hadi sasa mtoto huyo amehamishiwa daresalamu ambako wanaishi wazazi wake ila nyumbani kwao ni kitowo ... habari hizi hazijathibitishwa pindi zitakapo kuwa sawa mtapata hapahapa eaglefm endelea kutufuatilia ili upate ukweli.

Jumanne, 22 Septemba 2015

Kwa vume kunani.. Liewig ajitetea Stand United kuchemsha Wakati uongozi wa Stand United ukiwakingia kifua mashabiki wa timu hiyo kwa kumfanyia vurugu


Kocha wa Stand United, Patrick Liewig
Dar es Salaam. Wakati uongozi wa
Stand United ukiwakingia kifua
mashabiki wa timu hiyo kwa
kumfanyia vurugu kocha, Patrick
Liewig mwenyewe amesema uwezo
wake hauwezi kupimwa kwa mechi
mbili.
Liewig ameiongoza Stand kushinda
mechi moja na kutoka sare mbili tangu
alipojiunga na timu hiyo alijikuta
kwenye wakati mgumu wa kutaka
kupigwa na mashabiki baada ya timu
yake kuruhusu kipigo cha mabao 2-0
dhidi ya Azam wiki iliyopita mjini
Shinyanga.
Akizungumza na gazeti hili jana,
Mfaransa huyo alisema anajiamini na
anaamini yeye ni kocha mwenye
uwezo huku akisisitiza asipimwe kwa
matokeo ya mechi mbili ambazo timu
yake imekwishapoteza tangu kuanza
kwa ligi.
“Nahitaji kupewa muda, timu ya Stand
inajengwa taratibu, mashabiki wawe
na subira endapo wanahitaji mafanikio
kwani naamini ushindi hupo,” alisema
kocha huyo kwa kifupi.
Mwenyekiti wa Stand United, Aman
Vicent alisema kitendo kilichofanywa
na mashabiki wao kinaweza kutokea
katika timu nyingine yoyote ni cha
kawaida katika soka.
“Unajua tulitarajia makubwa
ukizingatia kocha analipwa fedha
nyingi sasa kitendo cha kufungwa
mechi mbili mfululizo kiliwakasirisha
mashabiki na kulazimika kufanya kile
kilichotokea, lakini tumeyamaliza na
tunajipanga kwa mechi zijazo,”
alisema Vicent.
Liewig aliajiliwa kuinoa Stand kama
kocha mkuu miezi michache kabla ya
ligi kuanza, kocha huyo pia aliwahi
kuifundisha Simba huku akiacha
rekodi ya kuwaibua vijana kwenye
timu hiyo.
Naye Mchambuzi wa soka na kocha wa
zamani wa Taifa Stars, Mshindo Msolla
amemtetea kocha huyo raia wa
Ufaransa na kueleza kuwa hastahili
kulaumiwa hivi sasa kutokana na
matokeo ya timu hiyo imepata na
kusisitiza kuwa wachezaji wa timu hiyo
hakuwasajili yeye.
“Liewig hastahili lawama, timu
ameikuta tayari imesajiliwa hivyo
matokeo ya sasa yanawahusu uongozi,
wanachotakiwa kufanya kwa sasa ni
kumpa muda wa kuijenga timu hiyo na
itakapofika kipindi cha dirisha dogo
aachiwe afanye usajili wa wachezaji
anaowahitaji,” alisema Msolla.

Sport man RIZIK MALYA leo amekuandalia Martial aing’arisha Man United Mabao mawili ya kinda Anthony Martial na jingine la Juan Mata jana yaliiwezesha Manchester United


Martial alichukua mpira kutoka upande wa
kushoto akakimbia nao kuelekea kwenye
boksi na kumpiga chenga beki mzoefu
kwenye ligi, Martin Skrtel kabla ya
kufunga bao maridadi kabisa.
London, England. Mabao mawili ya
kinda Anthony Martial na jingine la
Juan Mata jana yaliiwezesha
Manchester United kushinda mabao
3-2 dhidi ya Southampton kwenye
mchezo mgumu wa Ligi Kuu England.
Kwa ushindi huo, Man United
imefikisha pointi 13 na kushika nafasi
ya pili ikiwa nyuma ya Man City
ambayo ipo kileleni ikiwa na pointi 15,
huku West Ham ikiwa katika nafasi ya
tatu ikiwa na pointi 12.
Katika mchezo huo uliofanyika
kwenye Uwanja wa St Mary’s, wenyeji
Southampton walitangulia kupata bao
kupitia kwa Graziano Pelle, kipindi cha
kwanza.
Kipindi cha pili, Martial aliyejiunga na
klabu hiyo siku ya mwisho ya usajili,
Septemba 2 kwa ada kubwa akitokea
AS Monaco ya Ufaransa, alifunga
mabao hayo mawili na Mata kuongeza
jingine, huku Pelle akifunga pia la pili
katika mchezo huo.
Mapema, Tottenham au Spurs iliilaza
Crystal Palace kwa bao 1-0 katika
mchezo wa mapema saa 9.30 alasiri
kwenye Uwanja wa White Hart Lane.
Nayo Liverpool ilizuiwa na Norwich
City na kutoka sare ya bao 1-1 katika
mchezo mwingine wa Ligi Kuu kwenye
Uwanja wa Anfield.

Matajiri watano kuibeba Chadema Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema chama chake kina watu watano wenye uwezo wa kiuchumi


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman
Mbowe (mwenye kipaza sauti) akiendesha
harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya
kampeni za chama hicho iliyofanyika Dar
es Salaam juzi. Picha na Said Khamis
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa
Chadema, Freeman Mbowe amesema
chama chake kina watu watano wenye
uwezo wa kiuchumi wanaoweza
kukisaidia chama hicho kuendesha
shughuli zake za kampeni, ikiwa ni
siku 32 kabla ya wananchi kupiga kura
Oktoba 25.
Lakini mwenyekiti huyo wa Chadema
amesema watu hao hawataki
kutangazwa majina yao kutokana na
kuhofia kufuatiliwa na vyombo vya
dola, akisema kitendo hicho ni cha
kushangaza kwa nchi huru kama
Tanzania.
Chadema, ambayo inashirikiana na
NLD, CUF na NCCR Mageuzi chini ya
mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa) iliandaa harambee
hiyo juzi kwenye ukumbi wa Mlimani
City kwa ajili ya kutafuta fedha za
kuchangia shughuli zao za kampeni
zinazoendelea kote nchini.
Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na
takriban watu 800, jumla ya Sh97
milioni zilikusanywa, ikiwa ni fedha
taslimu, michango kwa njia ya simu na
ahadi.
Baada ya kazi ya uchangishaji kuanza,
Mbowe alishika kipaza sauti na
kueleza michango mingine kutoka nje
ya ukumbi huo.
“Wakati tunaendelea na uchangiaji
hapa, nimepokea simu kutoka kwa
rafiki zangu watano wenye uwezo
mkubwa kiuchumi. Wameahidi
kuchangia harambee lakini wanaogopa
kujulikana kwa kuhofia mkono wa
serikali,” alisema mwenyekiti huyo.
“Inasikitisha Mtanzania mwenye uhuru
ndani ya Taifa lake anahofia kuchangia
safari ya mabadiliko kwa sababu ya
kuiogopa Serikali, wakati Serikali
iliyopo imejaa mafisadi wakubwa?
“Unaweza kuona hii ni Serikali ya
namna gani, lakini ningewaomba
niwatie moyo tu ndugu zangu wenye
nia ya mabadiliko, tuwe na ujasiri,
msiogope.”
Sheria ya Gharama za Uchaguzi,
ambayo mwaka huu imeweka kiwango
cha juu cha matumizi ya kila chama
kuwa Sh17 bilioni, inataka uwazi wa
vyanzo vya mapato na matumizi, lakini
ni nadra kwa wafanyabiashara kuweka
bayana michango yao kwa vyama vya
upinzani.
Chadema imekuwa ikinufaika na
michango ya fedha na mali kutoka kwa
mfanyabiashara maarufu nchini,
Mustapha Sabodo, ambaye amekuwa
akitangaza hadharani kila
anapokichangia chama hicho.
Alipoulizwa ni kiasi gani chama hicho
kimepanga kutumia kwenye uchaguzi,
Mbowe alisema ni vigumu kutaja.
“Uchaguzi ni dynamic
(unabadilikabadilika). Hesabu za siku
haziwezi kuwa sawa wakati wote. Kwa
mfano bango la kupinga bao la mkono,
inahitajika sana kwa wakati huu lakini
gharama inaweza kuwa nyingine
wakati wa kusambaza bango jingine,”
alisema Mbowe.
Mkurugenzi wa mipango na uchaguzi
wa CUF, Shaweji Mketo alisema kila
chama ndani ya umoja huo
kinajitegemea kwenye gharama za
wagombea wake kwa ngazi ya
majimbo na udiwani.
“Hakuna tathmini ya pamoja ya
Ukawa...taarifa za gharama kwa CUF
tutaziweka wazi baada ya kukamilisha
majumuisho ya taarifa zote kutoka
majimboni na ngazi ya madiwani,”
alisema Mketo.
Maoni ya wachambuzi
Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),
Dk Alexander Makulilo alisema hofu
kwa wafanyabiashara nchini
imekuwapo kwa muda mrefu.
Alisema ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa
mwaka 2010 iliyoandaliwa na Timu ya
Waangalizi wa ndani wa uchaguzi
mkuu (Temco) inaonyesha TRA
kulalamikiwa na wafanyabiashara kwa
kuchunguza wafanyabiashara
waliokuwa hawaiungi mkono CCM.
Suala la matajiri hao kutotaka majina
yao kutajwa pia lilimgusa
mwanaharakati wa mtandao wa TGNP,
Gemma Akilimali, ambaye alisema
haoni sababu ya kuhofia kuchangia
kwa uwazi ili mradi ni wasafi katika
biashara zao.
“Sabodo ni mfanyabiashara mkubwa
tu na amekuwa akiwachangia
Chadema na CCM waziwazi bila
kuficha na hatujaona lolote likimtokea.
Kwa hivyo hofu zao zinaweza
kutujengea maswali katika uwazi wa
shughuli zao. Hofu iko kwa utayari
wao katika kuchimbuliwa shughuli zao
au vyanzo vya mapato yao.”
Awali kabla ya uchangiaji huo kuanza,
mgombea urais wa Chadema na
Ukawa, Edward Lowassa aliwataka
waalikwa kutoogopa kuchangia
harambee hiyo kwa hofu ya
kufuatiliwa na Mamlaka ya Mapato
(TRA).
“Nawaomba msiogope kuchangia, mtoe
tu kwani mabadiliko haya yanawahusu
wale wanaoyapenda na wasioyapenda.
Tunahitaji mabadiliko haya yafanikiwe
kwa kila hali,” alisema Lowassa,
ambaye aliihama CCM mwishoni mwa
mwezi Julai na kuungana na Chadema
kudai mabadiliko.
“Nawapongeza sana kwa juhudi za
maandalizi yaliyofanyika leo, na inatia
matumaini ya kufanikisha.”
Maombi ya uchangiaji
Akifungua harambee hiyo, Mbowe
alisema mikoa iliyosalia ni mingi kwa
hivyo bado wanategemea zaidi
michango ya wadau katika kufanikisha
kampeni.
Mbowe alisema muda uliobakia ni wa
“vita ya lala salama”, ambayo inahitaji
bajeti ya kutosha ili kufanikisha kufikia
wapiga kura wengi watakaoshiriki
uchaguzi huo.
“Ukichangia harambee hii hautakuwa
umemchangia Mbowe au Lowassa, bali
utakuwa umechangia ufanikishaji wa
kufikia ndoto ya mabadiliko. Utakuwa
umechangia ukombozi wa akina mama
na vijana wa Taifa la Tanzania,”
alisema Mbowe.
“Tangu kuanza kwa kampeni hizi,
Ukawa tumekuwa tukisaidiwa na
Watanzania mbalimbali wenye nafasi
zao, wapo waliotoa usafiri wa magari
ya kufanyia kampeni. Kwa hivyo
tunahitaji sana mchango wako katika
kipindi hiki.”
Chadema pamoja na Ukawa zimekuwa
zikipambana sambamba na CCM
kwenye kampeni za urais na ubunge
na matumizi yao makubwa
yanaonekana kuwa katika gharama za
safari za wagombea, matangazo ya
redio na televisheni, matangazo ya
moja kwa moja ya mikutano yao ya
kampeni, posho za mawakala na vifaa
kama mavazi, bendera, vipeperushi na
mabango.
Akizungumza kwenye hafla hiyo,
mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James
Mbatia, ambaye ni pia ni mwenyekiti
wa NCCR-Mageuzi, aliwataka waalikwa
kuhakikisha wanashiriki kikamilifu
kuchangia harakati za mabadiliko ili
kufanikisha ndoto za kuwakomboa
Watanzania kutoka mikononi mwa
Serikali ya CCM.
Mwingine aliyezungumza na waalikwa
ni mgombea mwenza wa urais, Juma
Duni Haji, maarufu kwa jina la Babu
Duni, ambaye alikuwa kivutio kutokana
na vijembe na misemo anayotoa
wakati akiwa jukwani.
Duni alisema kutoa ni moyo na siyo
utajiri kwani wapo wenye fedha
nyingi, lakini hawana moyo wa utoaji.
Mzee wa Upako aibuka
Baada ya viongozi hao kuzungumza na
kuendesha harambee, Mchungaji
Anthony Lusekelo wa Kanisa la
Maombezi (GRC), Ubungo Kibangu,
alitaka watu kuwa tayari kukubali
matokeo yoyote kwa kuwa ushindi wa
Lowassa au mgombea wa CCM, Dk John
Magufuli utakuwa wa Watanzania
wote.
Baada ya kutoa kauli hiyo, waalikwa
walipiga kelele za kupinga kauli yake
lakini aliendelea kueleza msimamo
wake huku akiwatuliza.
“Tulia, tulia wewe unayepiga kelele,
siasa chafu hazifai na siasa siyo
kumchafua mtu,” alisema.
“Hakuna taasisi inayoweza kuzidi
nguvu ya umma, lakini niseme jambo
kwamba, kwa sasa tuna wagombea
wakubwa wawili ambao ni Dk
Magufuli na Lowassa. Yeyote
atakayeshinda itakuwa ni ushindi kwa
Watanzania, tusiweke nongwa. Mimi ni
kiongozi wa dini nisiyekuwa na itikadi
ya vyama, ninaishi na waislamu na
Wakristo, kwa hiyo ni sawa kwa yeyote
kati yao.”
Lusekelo alisema hana itikadi ya
chama chochote kile na Lowassa ni
rafiki yake kwamuda mrefu, lakini
endapo Dk Magufuli atashinda bado
itakuwa ni sawa kwake.
Mbowe alisema uchangiaji huo
unaendelea kufanyika kwa njia ya
akaunti maalumu za simu za mikononi
na kujaza fomu zilizoandaliwa kwa ajili
ya ahadi za wanachama ukumbini
hapo.