other blog

Jumatatu, 19 Oktoba 2015

POSTED BY MABERE GODLUCK EAGLEFM... KATIKA SPORT


Mshambuliaji wa Barcelona, Neymar da
Silva Santos Junior (wa pili kushoto)
akiwania mpira na beki wa Rayo Vallecano
Nacho (kushoto) na kiungo Diego Llorente
wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Hispania
uliozikutanisha timu hizo kwenye Uwanja
wa Camp Nou, Barcelona. Barca ilishinda
5-2. Picha na AFP
Madrid, Hispania. Real Madrid na
Barcelona zimeng’ang’ania kileleni
mwa La Liga wakati Cristiano Ronaldo
akiweka rekodi Real ikishinda 3-0 dhidi
ya Levante, huku Neymar akifunga bao
manne wakati Barca ikichapa Rayo
Vallecano 5-2.
Real imeutumia vizuri uwanja wake
Bernabeu, wakati Ronaldo akivunja
rekodi ya Raul akifunga mabao 324
katika misimu yake saba aliyocheza
kwa miamba hiyo ya Hispania.
Barca ilitumia vizuri wenyeji wake,
huku safu yao ya ulinzi ikionyesha
kupwaya na kuhitaji uwezo wa binafsi
wa Neymar kusawazisha kutoka
nyuma kabla ya kuifunga Rayo
iliyocheza soka zuri la kushambulia
kwenye Uwanja Nou Camp.
Miamba hiyo ya Hispania
inayosumbuliwa na majeruhi sasa
zinaongoza ligi zikiwa na pointi18
katika michezo nane, huku Real
ikiongoza kwa tofauti ya mabao.
Villarreal iliyokuwa ikishikiria usukani
kwa muda, imeporomoka hadi nafasi
ya tatu, kabla ya mechi yake ya jana
dhidi ya Celta Vigo, wakati Atletico
Madrid inayoshika nafasi ya tano
itacheza na Real Sociedad.
Marcelo alifunga bao la kwanza la Real
katika dakika 27, wakati alipobadilisha
pasi na Ronaldo na kupiga shuti
lililompata kipa Ruben wa Levante.
Ronaldo alifunga bao la pili dakika tatu
baadaye kwa shuti la mbali lililojaa
wavuni , na kumaliza ukame wake wa
kutokufunga katika michezo minne
iliyopita ya ligi.
Naye Jese akiingia akitokea benchi
aliifunga bao la tatu dakika nane kabla
ya filimbi ya mwisho na kuhakikishi
ushindi 3-0, wakati Real ikijiandaa na
mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa
Kundi A dhidi ya Paris St Germain.
Barca yatakata
Barca ilimkosa nyota wake Lionel
Messi na nahodha wake Andres
Iniesta, wakati Javi Guerra alipofunga
bao la kuongoza kwa Rayo katika
dakika15.
Ivan Rakitic na Luis Suarez awali
alishindwa kumfunga Tono wakati
alipokutana uso kwa uso na kipa huyo
wa Rayo, lakini Barcelona ilisawazisha
dakika 22, kupitia Neymar kwa
mkwaju wa penalti.
Mbrazil huyo amechukua jukumu la
kuibeba timu hiyo baada ya
kukosekana kwa Messi, alidondoshwa
tena kwenye eneo la hatari dakika 13
na kufunga penalti yake ya pili.
Neymar alifunga bao la tatu dakika 69
na kupachika la nne dakika 70 kufanya
matokeo kuwa 4-1, magoli hayo
yanamfanya Neymar kuwa mchezaji
mwingine wa Barca mbali ya Messi
kufunga idadi hiyo ya magoli tangu
Samuel Eto’o alivyofanya hivyo 2008.
Neymar alitegeneza bao la tano kwa
kupiga krosi nzuri iliyomaliziwa na
Suarez na kuhitimisha kalamu hiyo ya
mabao 5-2.
Jozabed alitumia vizuri kutumia
udhaifu wa mabeki wa Barca kufunga
bao la pili kwa Rayo katika dakika ya
86.
“Neymar amekuwa katika kiwango
kizuri tangu kuanza kwa msimu huu,”
alisema Luis Enrique. “Wakati
anapoingia katika eneo la hatari
hakuna wa kumzuia.”
Sevilla inayojiandaa kucheza na
Manchester City katika Ligi ya
Mabingwa Jumatano, imelazimishwa
sare 1-1 na Eibar, wakati Valencia
ikipata ushindi mnono wa mabao 3-0
dhidi ya Malaga.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni