other blog

Jumatatu, 19 Oktoba 2015

MWADADA NOREEN KAHAYA...EAGLEFM


Msanii wa muziki wa Reggae, Jhikolabwino
Manyika 'Jhikoman' akipiga gitaa mbele ya
waandishi wa habari muda mfupi baada ya
mkutano ulioongelea tamasha la 'Karibu
Music Festival 2015'. Kulia ni Meneja
Uvumbuzi wa Serengeti Breweries
Limited, Attu Mynah. Picha na Said Hamis
Dar. Wadau wa muziki nchini, Afrika
Mashariki na dunia nzima kwa ujumla
watapata fursa kujumuika pamoja na
kubadilishana uzoefu wa kazi zao
katika tamasha la pili la muziki
maarufu kama ‘Karibu Music Festival’
litakalofanyika mapema mwezi ujao
huko Bagamoyo.
Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya
‘Fahari ya Tanzania’ linalennga kukuza
muziki wa Kiafrika na kuonesha
tamaduni za Kiafrika kwa dunia nzima
kupitia jukwaa la muziki
litakalokutanisha wanamuziki kutoka
sehemu mbalimbali duniani.
Akizungumza na waandishi wa habarI
leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari
Maelezo mwakilishi wa Karibu Music
Festival, Ernest Biseko alisema
Tamasha hilo mwaka huu
litahudhuriwa na wanamuziki
wakubwa akiwemo mkongwe Papa
Wemba, Sarabi Band, H-Art The Band,
Yuzzo & Frontline Band.
Biseko alisema kuwa, wasanii toka
Tanzania ni pamoja na Jhiko Manyika
(Jhikoman) na band yake ya
Afrikabisa, Tomgwa Ensembe, mshindi
wa shindano la vipaji la BSS mwaka
2008, Misoji Nkwambi, Ze Spirit, Isha
Mashauzi, Damian Soul na bandi yake,
Juma Nature, Msafiri Zawose na band
yake.
“Pamoja na kwamba lengo kubwa ni
kukuza muziki wa Kiafrika na
tamaduni zake pia tunataka liwe
tamasha pekee Afrika Mashariki
kukuza uchumi na kuleta maendeleo
kwa watu wake ndio maana biashara
na maenesho ya bidhaa mbali mbali ni
sehemu ya tamasha hili,” alisema
Biseko.
Naye mwakilishi wa wanamuziki
watakaoshiriki katika tamasha hilo,
Jhikolabwino Manyika maarufu kama
Jhikoman ambaye pia ni msanii
maarufu wa miondoko ya Reggae
nchini alisema mashabiki wa muziki
watarajie kuona wasanii wote
wakitumbuzia bila kutumia CD
‘playback’.
Jhikoman alisema kuwa kupitia
tamasha hilo anatarajia kupata nafasi
ya kujifunza kutoka kwa bendi
nyingine jinsi ya kukuza kazi zao na
kudumisha urafiki utakaoleta manufaa
katika kazi yake.
Tamasha hilo litaanza kwa matembezi
kuashiria uzinduzi wake na pia
kutakuwa na mafunzo mbali mbali
yenye mlengo wa kuwasaidia wadau
wa muziki kufahamu mambo mbali
mbali kwenye maswala ya kiutawala
na jinsi ya kujitangaza, mambo ya hati
miliki, ngoma za asili, kupiga ngoma,
na mengineyo.
Kiingilio katika tamasha hilo ni
Sh2,500 kwa watoto, watu wazima
watakaonunua tiketi zao kabla ya
tamasha itakua ni Sh 5,000 na kwa
wale watakaonunua getini itakua Sh
7,000 na kwa watu maalumu (VIP)
tiketi zitauzwa kwa Sh 30,000.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni