other blog

Jumatatu, 19 Oktoba 2015

MABERE GODLUCK SPORT EAGLFM..... Messi ajipa matumaini


Mshambuliaji wa Azam, Ramadhan
Singano ‘Messi’
Dar es Salaam. Mshambuliaji wa
Azam, Ramadhan Singano ‘Messi’
amesema kuwa hakatishwi tamaa na
kitendo cha kutopata nafasi kwenye
kikosi cha kwanza cha timu hiyo na
ana uhakika atapata nafasi hiyo ndani
ya kipindi kifupi kijacho.
Singano aliyejiunga na Azam msimu
huu akitokea Simba, amekuwa hana
nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha
timu hiyo kutokana na ushindani
mkubwa uliopo kwa washambuliaji
mbalimbali waliosajiliwa na klabu
hiyo.
Miongoni mwa washambuliaji
wanaowania namba naye ni, Kipre
Tchetche, John Bocco, Farid Mussa,
Didier Kavumbagu na Allan Wanga
walioifanya Azam iwe moja ya timu
zenye safu kali ya ushambuliaji
kwenye ligi.
Singano aliliambia gazeti hili jana
kuwa si jambo la kushangaza kwa
mchezaji kutopata nafasi ya kuanza
kwenye kikosi cha kwanza kwani ni
jambo inategemeana na matakwa ya
kocha.
“Mwenyezi Mungu ndiye kila kitu
katika maisha na yeye ndiyo
kampangia kila mwanadamu riziki.
“Nafurahia maisha hapa na ingawa
bado sijapata nafasi ya kucheza
kwenye kikosi cha kwanza mara.
Naendelea kufanya mazoezi na
naamini Mungu atanisaidia kupata
nafasi muda siyo mrefu,” alisema
Singano.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni