other blog

Jumatatu, 5 Oktoba 2015

Rais Kikwete ateua


Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete
Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete
amewateua wakuu wapya 13 wa wilaya
na kuwahamisha vituo vya kazi
wengine saba.
Walioteuliwa ni Shaaban Ntanambe
ambaye anakwenda Chato; Thabisa
Mwalapwa (Hanang), Richard
Kasesera (Iringa), Ruth Msafiri
(Kibondo) na Abdallah Njwayo
(Kilwa).
Wengine ni Asumpta Mshama
(Wanging’ombe), Mohammed Utaly
(Mpwapwa), Dauda Yasin (Makete),
Honorata Chitanda (Ngara), Vita
Kawawa (Kahama), Christopher
Ng’ubyagai (Mkalama), Hawa
Ng’humbi (Kishapu) na Mrisho Gambo
(Uvinza).
Wakuu wa wilaya waliohamishwa vituo
vya kazi ni Fadhili Nkurlu ambaye
anatoka Mkalama, kwenda Wilaya ya
Arusha, Wilson Nkambaku
anahamishiwa Arumeru, kutoka
Kishapu, Francis Miti ambaye
anahama Hanang kwenda Monduli na
Jowika Kasunga ambaye anahamia
Mufindi kutoka Monduli.
Wengine waliohamishwa ni Muhingo
Rweyemamu kutoka Makete kwenda
Morogoro; Hadija Nyembo anayehamia
Kaliua kutoka Uvinza na Benson
Mpesya ambaye anahamia Songea
Ruvuma kutoka Kahama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni