other blog

Alhamisi, 24 Septemba 2015

Idd kwa waislamu wengine imewasababishia kifo Mamia ya mahujaji wafariki katika mkanyagano Makka Watu wasiopungua 717 wamekufa, huku wengine 816 wamejeruhiwa leo jirani na mji mtakatifu wa Makka


Watu wasiopungua 717 wamekufa,
huku wengine 816 wamejeruhiwa leo
jirani na mji mtakatifu wa Makka
walikokwenda kuhiji ikiwa ni sehemu
ya utekelezaji wa moja ya nguzo
muhimu katika Imani ya dini ya
Kiislamu, maofisa Saudi Arabia
wathibitisha.
Kwa mujibu wa Baraza la Taasisi na
Jumuiya za Kiiislam nchini, kati ya
mahujaji 2,000,000 waliokwenda Saudi
Arabia mwaka huu, 1,500 wanatoka
Tanzania.
Japokuwa Msemaji wa Baraza hilo,
Shekhe Rajabu Katimba amesema
hakuna vifo vilivyokwisharipotiwa hadi
sasa toka Makka, taarifa zisizo rasmi
kutoka huko zinasema Mtanzania
mmoja amekufa na mwingine
amejeruhiwa baada ya kutokea
mkanyagano.
Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji
la BBC, katika maafa hayo, mahujaji
wengine wasiopungua 816
wamejeruhiwa katika eneo la Mina.
Vifo hivyo vimetokea ikiwa ni siku
chache kupita baada ya kutokea jail
nyingine ambapo winchi lilianguka na
kuua watu 109 katika msikiti ambapo
kulikuwa kukifanyika ibada ikiwa ni
maandalizi ya kuelekea sikukuu ya leo.
Haya ni maafa makubwa zaidi kutokea
katika sikukuu ya Eid Al Hajj baada ya
kupita takribani miaka 25. Kwa mujibu
wa Kurugenzi ya Wizara ya Usalama
wa Raia nchini Saudi Arabia, maafa
hayo yametokea kati ya saa sita
(majira ya Afrika Mashariki) katika
makutano ya mitaa namba 204 na 223
wakati mahujaji hao wakipanda ngazi
kuelekea jengo la ghorofa tano ambalo
limeuzunguka mnara, maarufu kwa
jina la Jamarat Bridge. “Tukio hilo
limetokea baada ya mahujaji
kuongezeka ghafla wakielekea kwenye
mnara,” taarifa ya wizara iliongeza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni