other blog

Jumatano, 29 Julai 2015

Boko harram wataisha asema buhari raisi wa nigeria...wasonga mrombo.


Msemaji wa rais wa Nigeria,Muhammadu Buhari,amesema amejipanga kupambana na kundi la kigaidi la Boko Haram kama litaendesha mashambulizi yake katika mipaka ya kimataifa.Msemaji huyo , Garba Shehu , aliiambia BBC kuwa tangu rais Buharia achaguliwe mwezi Mei amejipanga kutatua migogoro inayoikabili nchi hiyo tangu wananchi wa Nigeria wampe dhamana ya kuwaongoza. Cameroon, Chad na Niger wote wanashiriki katika kikosi kazi cha askari karibu elfu tisa , ambao wanatarajiwa kuwa tayari kwa mapambano mwezi ujao.Hata hivyo hapo jana kundi la wapiganaji wa Boko Haram walituma ujumbe kwa rais Buhariwakielezea kuwa wapo tayari kwa mazungumzo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni